Title October 2021

Mshahara wa Mbwa ni upi? Kama tunavyousoma katika Kumbukumbu 23:18

Jibu: Tusome,

Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Neno “Mbwa” kama linavyotumika hapo, linamaanisha “Mwanaume anayejiuza mwili wake”, kwa lengo la kupata fedha, kama vile mwanamke anayejiuza anavyojulikana kama Kahaba, vivyo hivyo mwanaume anayejiuza alijulikana kama “mbwa”.

Na kujiuza huko kuko kwa namna mbili. Namna ya kwanza ni mwanaume anayejiuza kwa wanawake, na namna ya pili, ni mwanaume anayejiuza kwa wanaume wenzake (yaani Hanithi). Makundi haya yote mawili yanajulikana kama “mbwa” kibiblia.

Hivyo Mungu alikataza kwa mtu yeyote awe mwanamke au mwanaume anayejiuza mwili wake na kupata fedha, asizilete hizo fedha katika nyumba ya Mungu kama sadaka, kwaajili ya nadhiri, na si tu nadhiri bali pia kama sadaka!..kwani ni machukizo mbele zake.

Mithali 15: 8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.

Kwahivyo biblia inatufundisha kuwa Utakatifu ndio sadaka ya kwanza kwa Mungu wetu..Maana yake tusipokuwa watakatifu wa mwili na roho, na tukaenda kumtolea sadaka, huku hatutaki wala hatuna mpango wa kubadilika, bado ni wazinzi, bado ni waasherati, bado ni makahaba, bado ni wachawi, bado ni watu tuliojaa vinyongo na chuki..basi tujue kuwa sadaka ile tunayokwenda kuitoa ni machukizo makubwa sana kwa Bwana. Kwasababu kitu cha kwanza Bwana anachotafuta kwetu si PESA, wala SADAKA, bali anataka tuwe wakamilifu, anataka tupate Rehema..

Mathayo 9:13 “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”.

Bwana Yesu mwenyewe alitupa ushauri mzuri, wa namna ya kumtolea Mungu..kwamba tujitakase kwanza kabla ya kwenda kumtolea yeye, ili sadaka yetu ikubalike na iwe na matokeo. Na kujitakasa huko sio kujitakasa leo, na kesho kurudia yale yale..bali ni kule kwa badiliko la kudumu ndani yetu..

Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,

24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”.

Kinyume chake tukimtolea sadaka na huku hatuna mpango wa kuacha maisha yetu mabaya ya dhambi, tufahamu kuwa sadaka zetu hazitakubaliwa na zaidi ya yote hatutaurithi uzima wa milele..Na maandiko yanasema wazi kuwa waasherati na MBWA hawataurithi uzima wa milele.

Ufunuo 22:14 “Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya”

Bwana atubariki na kutujalia neema zake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

MTAWATUPIA MBWA NYAMA HIYO.

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?

Noeli ni nini, na je! Neno hili linapatikana katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NANI ALIYEKUPA MAMLAKA HII UYATENDE HAYA?

Ulishawahi kujiuliza hoja ya msingi shetani aliyotumia kumshitakia Yesu mpaka kufanikiwa kumpeleka msalabani ilikuwa ni ipi?

Tukilifahamu hilo tutaelewa ni wapi ibilisi anapandaa ili kuwaletea dhiki wakristo katika siku za mwisho.

Ukisoma biblia utaona Wakati ule wayahudi wanatafuta sababu nyingi sana za kumshitaki Bwana Yesu lakini hawakuziona, mpaka dakika za mwisho mwisho wakatokea na hoja nyingine moja, ambayo ilikuwa na mashiko sana kwao..

Na hoja yenyewe ilikuwa ni katika lile HEKALU.

Mathayo 26:59 “Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua;

60 wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi.

61 Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu.

Nataka ujifunze jambo moja, kulikuwa na kauli nyingi sana zenye makwazo ambazo wayahudi wangeweza kuzisimamia kumuulia Yesu, kwamfano alipowaita wao ni wa baba yao Ibilisi na sio Ibrahimu(Yohana 8:44). Kwa kauli kama hiyo kwamfano ingetosha tu kumfanya wamuue. Lakini sio hiyo ya  kusema “Bomoeni hili Hekalu nami nitalijenga ndani ya siku tatu…”

Ulishawahi kujiuliza, kwanini kauli hiyo ilipata nguvu?

Hilo ni jambo ambalo shetani alijaribu kulijenga tangu zamani za akina Zerubabeli katika ujenzi wa Hekalu, kama wewe ni msomaji wa biblia, utakumbuka kuwa kipindi wanalijenga Hekalu la pili, maadui zao (ambao hawakuwa wayahudi) waliomba waungane nao ili kulijenga hekalu la Mungu, lakini Zerubabeli na wenzake kwa ufunuo wa Roho, wakawakatalia, kwasababu walijua madhara yake yatakayokuja huko baadaye (Ezra 4:3)..

Lakini muda mrefu ulipopita mamia ya miaka, hekalu hilo lilichakaa, likawa kama limepitwa na wakati, kwa ujenzi wake. Hapo ndipo akatokea mtawala mmoja wa ki-Rumi aliyeitwa HERODE, Akaomba alikarabati hekalu lile,. Sasa wayahudi bila ya Kutaka kumuuliza Mungu, wakakurupuka wakamruhusu, hivyo Herode akaanza kulikarabati tena, akalijenga kwa fedha nyingi sana na kwa muundo wa kisasa.

Muda alioutumia kukarabati ulizidi hata muda uliotumika kujenga Hekalu lile, kwani Herode alitumia miaka 46 kulikarabati, (Soma Yohana 2:20 utaona), wakati wakina Zerubabeli walitumia miaka  isiyozidi 7. Na alifanikiwa kulipamba kweli kweli, mpaka wakati Fulani mitume wakaenda kumuonyesh Bwana uzuri wa jengo hilo jinsi lilivyopambwa vizuri.

Sasa kitendo kile kilikuwa na agenda ya ibilisi nyuma yake. Kwasababu alijua upo wakati Masihi atakuja, na ataingia katika hekalu lile na kuwafundisha watu sheria za Mungu, Hivyo akatumia nguvu zake nyingi sana kutafuta namna ya  kupalimiliki. Ndipo hapo akamwingia Herode, ambaye roho ya mpinga-Kristo ilikuwa nyuma yake, mtu ambaye alikuwa hana hata upendo na Mungu, na ndio maana wakati tu Kristo anazaliwa badala afurahie mwokozi kaja ulimwenguni, kinyume chake akatuma watu kwenda kumuangamiza, lakini cha ajabu ndio mtu huyo huyo aliyelikarabati Hekalu la Mungu.

Sasa kwasababu yeye ndiye aliyelitengeneza upya. Mamlaka yote ikahamia mikononi mwake kutoka kwa wayahudi, wayahudi wakawa hawana la kusema, hapo ndipo akaanzisha biashara kubwa kubwa sana , ndani ya hekalu, akalifanya pia kuwa kama eneo la kitalii, la watu kuja kushangaa uzuri wake.

Vilevile kukawekwa sheria kali, mtu yeyote akitaka kufanya jambo, au kuleta mfumo mpya ni lazima kwanza apokee kibali kutoka kwa HERODE, vinginevyo utaonekana kama ni muhalifu, na msaliti, ambaye anastahili adhabu ya kifo.

Kwahiyo, hakukuwa na mtu aliyeweza kufumbua kinywa chake, kukemea jambo lolote baya lililofanyika katika hekalu la Mungu takatifu, kwa hofu ya Herode na wayahudi. Hivyo hiyo ikaifanya  hali ikaendelea kuwa mbaya kupindukia hadi wakati Kristo anatokea dunia,

Ibilisi alijua kabisa, mwisho wa Siku Bwana Yesu, ni lazima aje aingie katika hekalu lake takatifu. Na kweli wakati ulifika akaingia, ndipo akasambaratisha  biashara zote, na shughuli zote zilizokuwa zinaendelea ndani ya Hekalu.

Wayahudi kuona vile, wakadhani maagizo hayo kapewa na Herode ndipo walipomuuliza…..

Luka 20:2 “wakamwambia, wakisema, Tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii?”

Na baada ya kugundua kuwa hakuyapokea Kwa Herode, hapo ndipo wakajua mtu huyu ni msaliti, na gaidi, anataka kutuletea harufu mbaya duniani, ili sisi tuonekane kama waasi, ni lazima tumuue.

Ndipo wakamshitakia kwa kitendo chake kile, na kauli ile.

Nachotaka tuone ni kwamba. Shetani anafahamu kuwa Kristo yupo mlangoni kurudi tena mara pili kulinyakua kanisa lake takatifu. Hivyo alichokifanya tangu kile kipindi cha mitume hadi sasa ni kujiingiza kwa siri , ili kujifanya kama analisaidia kanisa la Mungu..

Lakini lengo lake sio Kristo, na ndio maana utaona sasa, madhehebu mengi ya uongo, yamefanikiwa sana, lakini ukijaribu kuchunguza mifumo yao utaona ipo mbali sana na biblia.

Ukiuliza ibada za sanamu za kumwomba bikira Maria zipo wapi kwenye biblia, au kwenda toharani tunakupata wapi, utaishia kuonekana ni msaliti, na gaidi, msambaza, chuki. Shetani sikuzote hataki mfumo wake mbovu kuhojiwa.. Hataki kwasababu anajua pale sio mahali pake.

Leo hii, bado hajapokea nguvu kamili,za kuleta uharibifu kwa watu, wakati unafika atapokea nguvu ya kuleta mauaji kwa wale wakristo ambao UNYAKUO utakuwa umewapita. Atataka kuwaondosha wote asibakie mtu.

Je! Umeokoka ndugu yangu? Au bado unajisifia dini na madhehebu? Hautanyakuliwa kwa dhehebu lako zuri, utanyakuliwa kwa kukamilishwa katika wokovu, yaani kutubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, na kuishi katika utakatifu. Tubu leo kama hujatubu, Kumbuka wakati wowote Kristo anarudi.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kikoto ni nini?(Yohana 2:15)

UFUNUO: Mlango wa 11

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU

Je! Wokovu umekufikia?

Wengi wanasema wamepata wokovu lakini kiuhalisia wokovu bado haujawafikia.
Leo napenda tujifunze juu ya viashiria vinavyorhibitisha kuwa wokovu umetufikia, au umefika nyumbani kwetu.

Tusome habari za mtu mmoja aliyeitwa Zakayo, ambaye kupitia yeye tutajua kama wokovu na sisi umefika nyumbani kwetu au la!

Luka 19:1-10
“1 Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.

2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.

3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.

4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.

5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako.

6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha.

7 Hata watu walipoona, walinung’unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi.

8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.

9 Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.

10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea”.

Nataka tuuone huo mstari wa 8, ni kitu gani Zakayo alichokifanya kikamsababisha mpaka Mwokozi Yesu aseme.. “Leo Wokovu umefika nyumbani humu”

Na kitu chenyewe ndicho hicho tunachokisoma..huo mstari wa 8.

“8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.”

Umeona?..Zakayo alijiona yeye ni mwenye dhambi, na kutubu…lakini aliona toba ya midomo peke yake haitoshi, na ilihali mali nyingi alizonazo ni kutokana na kuwadhulumu watu..akaona aib mbele za Bwana na vile vile moyo wake ukamchoma.
Alichofanya alitoa nusu ya mali yake yote iliyo ya halali na kuwapa masikini, na zaidi ya yote, wale wote aliowadhulumu aliwarudishia mara 4,.

Maana yake ni kwamba kama kuna kiwanja alimdhulumu mtu, alimrudishia mara 4, maana yake viwanja 4..

Kama kuna fedha alimdhulumu mtu, alimrudishia mara 4..

Na huo moyo wa toba yenye matendo ndio Bwana aliokuwa anauhitaji.. Na Bwana ndio akamwambia maneno yale “Leo wokovu umefika nyumbani humu”

Hebu jiulize leo ndugu, tangu umempokea Yesu, vile vitu vya wizi ulivyoiba, umemrudishia mwenyewe?..au umetubu tu kwa mdomo na kuishia hapo, na kuendelea kuwa navyo?

Zile mali za dhuluma ulizozipata bado unafurahia kukaa nazo baada ya kuokoka?..Zakayo hakuona vyema kukaa nazo, aliona aibu mbele za Bwana na alipoziondoa na ndipo Wokovu ulipoingia nyumbani mwake.

Sisi tunaonaje raha kubakiwa na simu za wizi?, Kubakiwa na fedha za dhuluma, kubakiwa na heshima wa hila n.k
Bwana wetu hafurahiwi na toba za midomo tu!..bali na za matendo,

Tunapotubu ni lazima na maisha yetu yabadilike, hata watu wa nje waone kweli pale pana mtu aliyebadilika, watu wa nje hawashawishiki kwa maneno ya midomo tu, ndipo waamini kuwa tumebadilika..wanashawishika wanapoona umewarudishia vile ulivyowadhulumu.

Kadhalika hawatashawishika kusikia kuwa umetubu kwa mdomo huku mavazi yako na mwonekano wako ni bado ule ule wa kikahaba au kihuni.

Wakikuona bado unavaa nguo za kubana, bado unavaa vimini, bado unajipamba uso kama Yezebeli, haijalishi unahudhuria kanisani kila siku kiasi gani..bado watakuona wewe ni kahaba na muhuni tu.

Wakisikia umetubu lakini bado huyo mke uliye naye si wako ni wa mtu mwingine, huyo mume uliye naye si wako ni wa mtu mwingine, hawashawishiki hata kidogo..na zaidi ya yote Kristo hakujui.

Tunapotubu hatuna budi kuzaa matunda yanayotokana na toba zetu hizo..

Mathayo 3:8-10
“ 8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;

9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.

10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.

Je! Toba yako ina matunda?

Kama bado basi ni wakati wa kuanza upya, kama ni mwanamke baada ya kutubu weka mbali vipodozi vyote, kaa mbali na dhuluma na biashara haramu..na kama ni mwanamume ni hivyo hivyo, kuviondoa vyote ulivyovipata kwa dhuluma na kujitenga na udunia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.

Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

KUONGOZWA SALA YA TOBA

MAOMBI YA TOBA.

Sala ya Toba na Rehema.

Ni lazima mtu aongozwe sala ya toba ili awe ameokoka?

NGUVU YA MSAMAHA

Rudi nyumbani

Print this post

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

SWALI: Mtume Paulo alikuwa anamaanisha nini aliposema..”Wengine wanahubiri habari za Kristo kwa sababu ya husuda na fitina; na wengine kwa nia njema.”(Wafilipi 1:15)? Huko kuhubiri injili kwa husuda ndio kukoje?


JIBU: Ili kuelewa Paulo alimaanisha nini ni vema tukaisoma habari yote tokea juu..

Wafilipi 1:12-18

[12]Lakini, ndugu zangu, nataka mjue ya kuwa mambo yote  yametokea zaidi kwa kuieneza Injili;

[13]hata vifungo vyangu vimekuwa dhahiri katika Kristo, miongoni mwa askari, na kwa wengine wote pia.

[14]Na wengi wa hao ndugu walio katika Bwana, hali wakapata kuthibitika kwa ajili ya kufungwa kwangu, wamezidi sana kuthubutu kunena neno la Mungu pasipo hofu.

[15]Wengine wanahubiri habari za Kristo kwa sababu ya husuda na fitina; na wengine kwa nia njema.

[16]Hawa wanamhubiri kwa pendo, wakijua ya kuwa nimewekwa ili niitetee Injili;

[17]bali wengine wanamhubiri Kristo kwa fitina, wala si kwa moyo mweupe, wakidhani kuongeza dhiki za kufungwa kwangu.

[18]Yadhuru nini? Lakini kwa njia zote, ikiwa ni kwa hila, au ikiwa ni kwa kweli, Kristo anahubiriwa; na kwa hiyo nafurahi, naam, nami nitafurahi.

Waraka huu Paulo aliuandika akiwa gerezani..Sasa akiwa huko kifungoni kulizuka makundi mawili ya watu ambao walianza kuihubiri injili kama ile ile aliyoihubiri..

Kundi la kwanza lilikuwa na Nia njema kwa Bwana kama ile aliyokuwa nayo Paulo. Kuzihurumia roho za watu na kuifanya kazi ya injili kwa kujitoa kwa upendo bila kujali kama wanapata faida yoyote au la..

Lakini kundi la pili lilikuwa la tofauti..lilianza kuhubiri kwalengo la kumkomoa Paulo na kutaka kujionyesha kuwa na wao wana mamlaka kama yake..N hiyo yote ni kwasababu ya kukua na kujulikana sana kwa huduma ya Paulo ulimwenguni..Hivyo wivu ulipowajaa  wakatumia fursa ya kufungwa kwake kuhubiri injili kwa lengo la kumuonyesha Paulo hana chochote cha ziada kushinda wao. 

Na wengine wakawa wanahubiri huku wakimnenea habari mbaya ili tu kumzidishia vifungo vyake kwa maaskari.

Lakini cha ajabu ni kuwa taarifa hizo zilipokewa tofauti na Paulo..badala ya kuchukia ndio kwanza akafurahia..kwasababu hata kwa njia hiyo injili inahubiriwa na watu wanaokoka..

Ni jambo gani tunaweza kujifunza kwa Paulo na hao wahubiri injili kwa fitina..

Hiyo ni kuonyesha kuwa injili inaweza kuhubiriwa na mtu yeyote na ikaleta matokeo yale yale ya wokovu..hata sasa wapo wahubiri wengi wa uongo wanawavuta watu wa Kristo..lakini hilo haliwafanyi wao kupokelewa na Kristo siku ile ya hukumu..

Bwana Yesu aliliweka wazi hilo katika; 

Mathayo 7:21-23

[21]Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

[22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

[23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Hivyo tuwe makini na kuhubiri kwetu..Je Nia yetu ni kwa Bwana? au kwa lengo la kushindana na mtumishi fulani au mtume fulani au mchungaji fulani au nabii fulani…

Vivyo hivyo…Sisi kama wahubiri hatuna haja ya kurudisha mashambulizi pale tunapoona watumishi wa uongo wanashindana nasi..ikiwa injili wanayoihubiri ni ya kweli basi sisi tufurahie matunda kama alivyofanya Paulo..hayo mengine tumuchie Mungu atayahukumu mwenyewe siku ile..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Fitina maana yake nini kwenye biblia?

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?

Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Rudi nyumbani

Print this post

NINI TUNAJIFUNZA KWA THEOFILO MTUKUFU?

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia neno la Mungu wetu, ambalo ni taa iongozayo miguu yetu na Mwanga wa njia yetu.

Leo tutajifunza juu ya mtu mmoja aliyeitwa Theofilo, ambaye biblia haijaeleza habari zake kwa urefu lakini amehusika pakubwa sana katika kuieneza injili.

Lakini kabla ya kwenda kumtazama huyu Theofilo hebu tuweke msingi kidogo kwa kuelewa juu ya baadhi ya nyaraka za kwenye biblia.

Katika maandiko hususani agano jipya tunaona nyaraka kadhaa, zikiandikwa kwa watu fulani, ambazo hizo zimekuwa msaada hata kwetu sisi wa nyakati hizi.

Kwamfano tunaona waraka ambao Paulo alimuandikia Timotheo, au Tito au Filemoni…Nyaraka hizo zilikuwa zinawasaidia hao watu kuwajenga na kuwaimarisha katika utumishi wao, lakini tunaona Mungu aliziruhusu zienee na kusomwa na watu wengi hata mpaka wakati  wetu huu.

Hawa wakina Tito, Filemoni, na Timotheo hawakujua kuwa barua hizo walizotumiwa na Paulo zitakuja kusomwa na maelfu ya vizazi mbeleni..wao pamoja na Paulo hawakulijua hilo.

Ni sawa na wewe leo umwandikie Barua ndugu yako aliyeko mbali, lakini ipite miaka mingi sana huko mbele uje usikie hiyo barua uliyomuandikia inasomwa duniani kote..bila shaka utashangaa…Ndivyo ilivyokuwa kwa Paulo na hawa wakina Timotheo, Tito na Filemoni..waliandikiana barua wao kwa wao kwa lengo la kuimarisha utumishi wao.. lakini kumbe Mungu alikuwa ana malengo makubwa sana na hizo barua..

Hapa tumechukua mifano ya hawa watatu Timotheo, Tito na Filemoni kwasababu ndio wanaojulikana sana..

Lakini pia katika maandiko pia kulikuwa na mtu mwingine wa kipekee sana, ambaye hajulikani sana lakini alichangia pakubwa sana katika uandishi wa vitabu vya biblia.. mtu huyu si maarufu sana ukilinganisha na hawa wakina Timotheo..

Na mtu huyo si mwingine zaidi ya THEOFILO MTUKUFU.

Kama vile kulivyokuwa na waraka wa kwanza na wa pili Paulo aliomwandikia Timotheo, kulikuwepo pia na waraka wa kwanza na wa pili kwa Luka aliomwandikia huyu mtu anayeitwa Theofilo.

Wengi wetu hatujui kuwa kitabu cha Luka na cha Matendo ya Mitume, ni nyaraka maalumu kwa mtu Fulani, hazikulengwa kwa watu wote, au kwa kanisa kwa ujumla…bali zilikuwa ni barua maalumu kwa mtu Fulani ambaye ndiye huyu Theofilo, yaani maana yake ni kwamba kitabu cha Luka na Matendo ya Mitume.. kwa lugha nyingine kingeweza kuitwa Waraka wa Kwanza kwa Theofilo, na waraka wa pili kwa Theofilo..Kwasababu vitabu hivyo viwili vilikuwa ni waraka kwa Theofilo kama kitabu cha Timotheo wa kwanza na wa pili.

Sasa huyu Theofilo alikuwa ni nani?

Kwa ufupi ni kwamba huyu Theofilo, alikuwa ni mkuu fulani, ambaye inasemekana alikuwa Mrumi, na wala hakuwa myahudi. Alikuwa ni mtu mwenye cheo, lakini alikuwa ni mtu wa kipekee sana.

Kwani ulifika wakati akasikia habari zinazomhusu Yesu, na Mitume wake pamoja na Paulo. Lakini hakuwa na uhakika nazo, huku anasikia hichi kule anasiki kile n.k Kipindi anasikia hizo habari, tayari Bwana Yesu ameshaondoka na Mtume Paulo alikuwa ameshakuwa mzee sana, na Mitume walikuwa wameshatawanyika duniani kote..

Hivyo alichikifanya kwasababu alikuwa ni mtu mkubwa, na mwenye cheo, kwa hekima alikwenda kumtafuta mtu mmoja anayeitwa Luka ambaye alikuwa anatembea sana na Mtume Paulo katika safari zake.

Na lengo la kumtafuta huyu Luka ni ili apate taarifa za kutosha na uhakika wa mambo aliyokuwa anayasikia na kuambiwa na watu yamhusuyo Yesu na Mitume wake. Hivyo akamsihi na kumwomba amuandikie kwa waraka mambo yote, tukio moja baada ya lingine tangu kuzaliwa kwa Yesu, kupaa kwake na Matendo yake yote, pamoja na matendo yote ya Mitume.

Hatujui alimsapoti Luka kwa kiwango gani, kwaajili ya kuifanikisha hiyo kazi, lakini aliifanya kwa moyo.

Na Luka kwasababu alikuwa ni mmoja wa watu waliokuwa wanapenda Mungu na mwenye elimu kubwa ya ufalme wa Mungu, na hata ya kidunia,(kwani alikuwa ni Tabibu) alimuandikia huyu Mtukufu Theofilo, tukio moja baada ya lingine, tangu kuzaliwa kwa Yesu, mpaka kupaa kwake mbinguni, na hakuishia hapo tu..bali akaendelea kumwandikia habari za mitume wake aliowaacha baada ya kupaa kwake..

Akamwandikia matendo yao, jinsi walivyohubiri injili kwa nguvu za Roho na kufanikiwa kuanzia Yerusalemu mpaka mwisho wa dunia.. Na huko huko akamwelezea pia habari za Paulo jinsi alivyoipeleka injili kwa mataifa yote, safari zake na mafanikio yake yote.

Na Luka baada ya kukusanya taarifa hizo na kuziandika, ndipo akamtumia huyu Theofilo nyaraka hizo…Na nyaraka hizo ndizo tunazozisoma leo ambazo ni kitabu cha LUKA NA MATENDO YA MITUME.

Na bila shaka Theofilo baada ya kuzipokea nyaraka hizo mbili, aliridhika pakubwa sana, utata ukaondoka kichwani mwake na akamtukuza Mungu..na kuelewa na kupata uhakika wa mambo yote..

Hebu kwa ufupi tusome muhtasari wa nyaraka hizo Luka alizomwandikia Theofilo, na kisha tuende kutazama ni nini tunachoweza kujifunza kutoka kwa huyu mtu.

Luka 1:1 “Kwa kuwa watu wengi wametia mikono kutunga kwa taratibu habari za mambo yale yaliyotimizwa katikati yetu,

2 kama walivyotuhadithia wale waliokuwa mashahidi wenye kuyaona, na watumishi wa lile neno tokea mwanzo,

3 NIMEONA VEMA MIMI NAMI, KWA KUWA NIMEJITAFUTIA USAHIHI WA MAMBO HAYO YOTE TANGU MWANZO, KUKUANDIKIA KWA TARATIBU, THEOFILO MTUKUFU,

4 UPATE KUJUA HAKIKA YA MAMBO YALE ULIYOFUNDISHWA”.

Huo ni waraka wa kwanza wa Luka aliomwandikia Theofilo Mtukufu..waraka mwingine wa pili ni kama ufuatao..

Matendo  1:1 “ Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, THEOFILO, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha,

2 hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua;

3 wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu”.

Huo ni waraka wa pili wa Luka aliomwandikia huyu Theofilo.

SASA NI NINI TUNAJIFUNZA KWA THEOFILO?.

Kabla ya kujua ni nini tunajifunza hebu tafakari ni mambo mangapi mazuri na ya kujenga tunayoyapata ndani ya hivyo vitabu viwili vya LUKA na MATENDO YA MITUME?.

Kama wewe ni msomaji wa biblia utajua ni jinsi gani, vitabu hivyo viwili vilivyokuwa vya muhimu na vyenye mafunzo mengi ya kiimani.

Theofilo aliona si vyema kusikia habari za Yesu juu juu tu, alitaka kujua alizaliwaje, katika mazingira gani, ndugu zake ni wakina nani, alihubiri nini, kwa muda gani, na alikufaje, alifufukaje na yupo wapi sasa hivi..Pengine alitaka hivyo kwa ajili ya faida yake na ya watoto wake na ndugu zake..

Lengo ni ili asipelekwe pelekwe na kila upepo wa elimu uliozagaa huko na huko, ili asichukuliwe na upotoshaji unaomhusu Yesu na wanafunzi wake..Hivyo akamtafuta Luka ambaye alikuwa ni mwenye elimu nyingi, na mwanafunzi wa Imani ya kikristo, amwandikie kwasababu aliamini ndiye chanzo salama na sahihi cha taarifa kwa wakati huo.

Na Luka akatimiza kiu yake kwa kumtafutia habari hizo kwa urefu na kumwandikia zote.

Ndio maana hapo Luka unaona anamwambia “NIMEONA VEMA MIMI NAMI, KWA KUWA NIMEJITAFUTIA USAHIHI WA MAMBO HAYO YOTE TANGU MWANZO, KUKUANDIKIA KWA TARATIBU, THEOFILO MTUKUFU”

Na kama tulivyojifunza, huyu Theofilo hakuridhika kusikia habari za Yesu tu! Na matendo yake..bali alizidi kutamani kujua Matendo ya Mitume wa Yesu kwa urefu.. kwani alikuwa anasikia tu habari za Mitume wake juu juu, alikuwa anamsikia tu Paulo, lakini yeye akataka kujua huyu Paulo ni nani, ni jinsi gani alimpokea Yesu, safari zake zilikuwaje, ni nini aliyopitia akiwa safarini, hatua kwa hatua..na Luka akamwandikia habari zote hakuacha kitu!

Hebu jiulize kwa kupitia safari na maisha ya Paulo tunayoyasoma katika kitabu cha Matendo ya Mitume tumejifunza mangapi leo?, Bila shaka ni mengi sana.. tumejifunza kumbe katika safari ya imani kuna kupanda na kushuka, wakati mwingine kuna kupitia dhiki na vifungo n.k.

Hivyo Theofilo kwa kutamani kuyajua hayo, na kutafuta kwa bidii taarifa hizo za Bwana Yesu, imekuwa msaada na kwetu sisi pia.

Kadhalika na sisi tunajunza hayo hayo…

Kwamba hatuna budi kuwa kama Theofilo..kuhusiana na masuala ya ufalme wa Mbinguni..

 tunapotia bidii kutafuta kulijua Neno la kweli la Mungu, taarifa zile haziji kutusaidia sisi peke yetu, bali pia wengine, na hata vizazi vijavyo.. kwasababu kwa kutafuta huko..kutakuja kuwafaa wengine na kuwabariki wengine huko mbeleni, na kuwa kumbukumbu bora kwetu.

Unapoona Neno katika maandiko hulielewi kwanini usitafute kwa bidii kulijua na kisha kuliandika au kuwafundisha wengine au watoto wako kwa msaada wa wao?..Leo utaona halina maana lakini hujui Mungu kalikusudia nini mbeleni.

Pengine Theofilo aliutaka ule waraka kwa faida yake tu na watoto wake, kumbe Mungu alikuwa na mpango na huo waraka kwa mamilioni ya watu huko mbeleni. Hata sisi kuna mambo ambayo tunaweza kuyafanya sasa, tukidhani yanaishia hapa tu kumbe Mungu ana malengo nayo kuwa msaada kwa maelfu ya watu mbeleni..

Hebu jiulize ni taji kubwa kiasi gani alilonalo huyu Theofilo?.. ambaye hata hakuwa Myahudi?..

Siku ile atasimama na kumwambia Bwana kwa utafiti wake na bidii yake ya kutaka kujua habari za Kwake na Mitume wake, imekuwa Baraka watoto wake na ndugu zake, lakini Bwana atamwonyesha mabilioni ya watu katika vizazi vya mbeleni waliobarikiwa kwa jitihada yake hiyo..

Kwasasa huyu Theofilo hajui chochote kwasababu kalala, lakini siku ya ufufuo, ndipo atakapojua jinsi thawabu yake ilivyo kubwa..Na naamini kama angejua angetafuta pia habari nyingine nyingi ili apate taji bora zaidi.

Kwa bidii yake kitabu cha Luka na Matendo ya Mitume kimeweza kuwepo!.

Mathayo 8:11 “Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni”

Na sisi Bwana atujalie tufanye jambo ambalo litatusaidia sisi na vizazi vijavyo..

Marana atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?

Uchaji ni nini kama tunavyosoma katika 1Timotheo 2:10?

USIPUNGUZE MAOMBI.

Rudi nyumbani

Print this post