Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu aliwalenga mbwa na nguruwe tu , na si wanyama wengine katika mfano wa Mathayo 7:6?

Mathayo 7:6 “Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua”.


JIBU: Alitumia mfano wa wanyama hao wawili, kwasababu ya tabia zilizopitiliza za kutokujali walizo nazo, kwamfano Mbwa, ni mnyama wa kufugwa lakini bado ni mnyama asiyejali ni kitu gani anakula tofauti na wengine kama vile paka.. Na ndio maana anaridhika na vyakula vya majalalani au   makombo yaliyosalia ya majumbani, kama vile Bwana Yesu alivyosema katika…

Mathayo 15:26 “Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao”.

Vilevile ni heri ingekuwa anaishia kwenye makombo tu, lakini pia mbwa ni mnyama ambaye yupo tayari KUYALA MATAPISHI YAKE mwenyewe. Bila kujali kuwa ni uchafu ule. Sasa embu jiulize, kama hajali anachokula, atajali vipi, au atathamini vipi chakula kizuri unachompa?..Utadhani atakufurahia sana, kumbe mwenzako wala!!

Halikadhalika, na nguruwe naye. Ni mnyama wa kufugwa, lakini anapenda sana kukaa kwenye matope, jambo ambalo huwezi kuliona kwa kuku au mbuzi. Ni mnyama asiyethamini usafi hata kidogo. Sasa fikiria unaondoka, na kuchukua ile lulu yako ya thamani ambayo umeinunua kwa bei ghali, labda tuseme milioni 10, lulu ambayo unajua wanaovaa ni mamalkia tu au watu wenye uwezo, halafu unakwenda kumuogesha nguruwe wako vizuri na  kumvisha, lengo lako ni kutaka kumwona akipendeza.

Wewe unategemea nini kama sio kwenda kugaragara nayo kwenye matope,na kuikanyaga? Yaani ni heri hata ungemvisha punda, lakini sio nguruwe. Hivyo mbwa na nguruwe walitungiwa hata mithali yao tangu zamani, ambayo tunaisoma katika..

2Petro 2:22 “Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni”.

Ikifunua kuwa hata leo hii, wapo watu wenye tabia za wanyama hawa, ambao hawapaswi hata kidogo kupewa vitu vitakatifu (ikiwa na maana hawapaswi kupewa mambo ya ndani kabisa yamuhusuyo Mungu). Watu kama hawa hata ujaribuje kuwaeleza habari za Mungu, na uzuri wake, mambo ambayo pengine wewe uliyapata kwa mateso, na ulipoyapata ukayafurahia, ukadhani itakuwa sawa na kwao, ndugu utaishia tu kudharauliwa, kuchekwa, kukejeliwa, kutukanwa, na wakati mwingine kupigwa na kuudhiwa.

Hivyo wewe kama mkristo unapaswa uwe na hekima unapokutana na makundi ya watu wa namna hii. Ukishaona mtu anabishana na wewe kuhusiana na habari za Kristo, au anadhihaki dhihaki, tu wala usihangaike naye kumuhadithia maneno mengi, achana naye, kuwa kama mjinga kwake, nenda kwa Yule mwingine aliyetayari kusikia.. Kwasababu ukizidi kubishana na huyu mwishowe wewe ndio utakayeumia.

Hiyo ndio maana ya hiyo mithali, Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?

MTAWATUPIA MBWA NYAMA HIYO.

Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

UFUNUO: Mlango wa 18

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
faustin francis
faustin francis
1 year ago

Nafurahishwa na kubarikiwa na mafundisho yenu .Mungu awabariki

.