Tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu ni ipi?

Tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu ni ipi?

SWALI: Bwana Yesu asifiwe,.Naomba kufahamu tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu, maana nashindwa kuelewa, imesema tusihukumu. Je kwa mtu anayetenda dhambi kwa makusudi unapomlaumu ni sawa na kumuhukumu?

Luka 6:37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa”.


JIBU: Kuhukumu ni kitendo cha moja kwa moja kutoa/kuamua hatma ya mtu mwingine, Na hiyo inakuja pale mtu anapojiona yeye ni bora/mwema sana zaidi ya wale wengine, . Kwamfano mtu mmoja atamwona kahaba, au mlevi, au shoga barabarani na wakati huo huo atamwambia wewe ni ibilisi, mwana wa kuzimu, Au atakutana  na wapagani wanaabudu miungu yao mahali fulani, ataanza kuwanyooshea kidole na kuwaita makafiri wa motoni wale, bila hata kuwaambia kitu kingine chochote, kisa tu kawaona wanafanya matendo yasiyompendeza Mungu. Hapo tayari kashawahukumu.

Lakini Kulaumu ni kitendo cha kukosoa kila kitu, kwa lengo la kuonyesha kuwa  kitendo alichokifanya/anachokifanya Yule mwingine ni cha kupuuzi sikuzote, hakina maana. Na kwa kawaida watu wanaolaumu nao pia wanakuwa na fikra kwamba wao huwa hawakoseagi..Ingekuwa ni wamepewa fursa hiyo wangeitumia vizuri. (Wana tabia ya kujiona wao ni wakamilifu sikuzote)

Kwamfano lawama mara nyingi zinawakuta viongozi, Utakuta kiongozi, kafanya jambo fulani la kimaendeleo, lakini kwasababu mtu fulani anajiona yeye hawezi kukosea, ataanza kutoa kasoro, kwa kila kitu kilichofanywa hata kama ni kizuri, utasikia, kwanini zile pesa zisingetumiwa kwa hili au lile, kusingekuwa na matatizo haya na yale, hiyo ndio laumu. Kana kwamba yeye yupo sahihi wakati wote, hajawahi kufanya kitu akakosea.

Au mtu mwingine, labda mzazi wake ameshindwa kumtimizia haki yake ya msingi, pengine elimu, halafu amekuwa mtu mzima, akaona madhara ya kutopelekwa kwake shule. Sasa badala ajifunze “kuachilia” kama biblia inavyosema, achilieni, nanyi mtaachiliwa, yeye ataanza kuwalaumu wazazi  wake tangu ujana wake hadi uzee wake, kana kwamba walifanya makosa makubwa sana, Na kusahau kuwa yeye mwenyewe pia anayomakosa mengi, ambayo Mungu anayohaki ya kumlaumu kupitia hayo.

Vitendo vyote hivi Mungu havipendi. Kuhukumu pamoja na kulaumu, kwasababu na sisi Mungu atatufanyia hivyo hivyo siku ile ya hukumu, tusipobadilika, Na kwakweli Bwana atusaidie viondoke ndani yetu. Lakini pia tunapaswa tufahamu kuwa kuelezwa uhalisia wa mambo sio kuhukumiwa, jambo ambalo watu wengi wanatafsiri isivyosawa. Kwamfano mtu ni mlevi, halafu anaelezwa kuwa walevi wote biblia inasema wataenda jehanamu, akadhani hapo anahukumiwa.. Hapo haukumiwi, bali anaelezwa ukweli wa mambo. Kwamfano hata wewe ukimwona mtoto wako anacheza karibu na shimo, ukamwambia “watoto wanaocheza karibu na mashimo mwisho wao huwa ni kutumbukia na kufa”. Hapo hujahitimisha kuwa Yule mtoto ni wa kufa, lakini umemweleza uhalisia wa mambo. Hivyo na wewe unavyohubiriwa wazinzi wote watakwenda kuzimu, ujue kuwa hauhukumiwi, bali unaelezwa hatma ya maisha yako.

Unapoambiwa wanaojichubua miili yao wote na wanaovaa nguo za uchi uchi, hatma yao ni kwenye ziwa la moto. Hauhukumiwi wala haulaumiwi bali unahubiriwa hatma yako. Lengo la Yule mhubiri sio uende kwenye ziwa la moto bali utubu ili uikwepe hukumu.

Lakini mtu akikufuata na moja kwa moja akakwambia wewe ni ibilisi, au kafiri, au joka, au ajenti wa kuzimu, kana kwamba wewe huwezi kupokea neema yoyote kama ya kwake,. Huyo tayari ameshakuhukumu na biblia imekataza sana hilo, kwasababu anayejua hatma ya mtu ya mwisho ni Mungu na sio yeye. Lakini akikueleza matokeo ya ukafiri wako, hajakumukumu, zaidi kaonyesha upendo kwako.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

SI KWA UWEZA WALA KWA NGUVU BALI KWA ROHO YANGU, ASEMA BWANA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments