TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

Tumtolee Mungu vitu vinavyotugharimu hata kuhatarisha maisha…2Samweli 23:15 Daudi akatamani, akasema, Laiti mtu angeninywesha maji ya kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango!

Shalom, Jina la Bwana Yesu libarikiwe. Ni siku nyingine tumepewa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha tushiriki pamoja kujifunza maneno matakatifu ya Mungu.

Leo kwa ufupi tutaichunguza habari moja inayotoka katika  kitabu kile cha Samweli wa pili, sura ile ya 13, tunaona kuna wakati Daudi alipokuwa katikati ya vita vikali na wafilisti, wakati akiwa kule mafichoni katika pango moja lijulikanalo kama pango la Adulamu, alitamani maji ya Kisima kilichokuwa Bethlehemu Lakini wakati huo  mji wa Bethlehemu ambao ndio ulikuwa mji wa Daudi ulikuwa umezungukwa na wafilisti (Maadui zao), na ndipo walipokuwa wameweka kambi zao hapo.. Hivyo Daudi akiwa kule mabondeni biblia inatuambia alitamani sana maji ya kisima cha Bethelehemu kule maadui zake walipo, Hivyo watatu kati ya wale mashujaa wake 300 aliokuwa nayo waliposikia maneno yale ya Daudi, wao wenyewe kwa sirisiri  wakapanga mikakati ya kwenda kumletea Daudi maji ya kisima kile bila hata ya kumwambia..

Ndipo wakaanza safari kutoka katikati ya kambi ya Daudi, wakaondoka hivyo hivyo bila kujali wanakwenda kuingia katika kambi ya maadui zao, kwasababu ilikuwa ili kufikia Kisima hicho ni lazima upenye katikati ya wafilisti, lakini wao waliondoka hivyo hivyo, hatujui walitumia njama gani, lakini walidhubutu kuhatarisha Maisha yao, kwa hali na mali ili tu wafikie azimio lao, la kuchota maji yale ya Kisima kile na kumletea Daudi..

Halikuwa jambo rahisi ni sawasawa na wewe leo uone umewekewa simba 100 mbele yako, halafu nyuma yao kuna lulu unayopaswa ukaichukue, si jambo rahisi kibinadamu lakini hawa mashujaa watatu wa juu wa Daudi hawakujali hilo, walifanikiwa kweli kupenya katikati ya wale watu kisirisiri, na kuyachota maji yale ya Kisima cha Bethlehemu na kumletea Daudi…Lakini Daudi alipoona Maji yale, tunaona mwitikio wake ulikuwa ni kinyume na matazamio yao..tusome..

2 Samweli 23:13 “Tena, watatu miongoni mwa wale thelathini waliokuwa wakuu wakashuka, wakamwendea Daudi wakati wa mavuno mpaka pango la Adulamu, na kikosi cha Wafilisti walikuwa wamefanya kambi katika bonde la Warefai.

14 Naye Daudi wakati ule alikuwako ngomeni, na jeshi la Wafilisti wakati ule walikuwako Bethlehemu.

15 Daudi akatamani, akasema, Laiti mtu angeninywesha maji ya kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango!

16 Basi hao mashujaa watatu wakapenya jeshi la Wafilisti, wakateka maji kutoka kile kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango, wakayachukua, wakamletea Daudi; walakini yeye hakukubali kuyanywa, akayamimina mbele za Bwana.

17 Akasema, Hasha, Bwana, nisifanye hivi; je! Si damu hii ya watu hao waliohatirisha nafsi zao? Kwa hiyo hakukubali kuyanywa”.

“Hayo ndiyo waliyoyafanya wale mashujaa watatu”

Kama tunavyoona hapo, Daudi hakudhubutu kuyanywa maji yake.Kwa nje yalikuwa yanaonekana ni maji lakini kwa ndani Daudi aliyaona ni damu.. Na damu sikuzote huwa hainywewi, kwasababu damu inabeba uhai..Na uhai unazungumza..

Daudi aliona maji yale ni dhabihu tosha ambayo haistahili kutolewa kwake ili kwa Mungu tu peke yake. Na ndio maana alichokifanya ni kuyachukua yale maji na kwenda kuyamwaga mbele za Bwana.. kama vile damu imwagikayo kwa ajili ya dhabihu.

Hivyo tunaona badala maji yale kuenda tumboni mwa Daudi, yalikwenda moja kwa moja hadi katika madhabahu ya Mungu mbinguni..Na hivyo bila shaka kwa tendo lile si tu Mungu kuwarehemu wale watu kwa jicho la tofauti bali pia kuwapa ushindi dhidi ya maadui zao.

Habari hiyo inafunua nini katika agano  jipya tulilopo?

Daudi anamfunua Bwana wetu Yesu Kristo, kumbuka wale mashujaa wa Daudi walikithamini kiu cha Daudi hawakujali kuwa hata pale kulikuwa na maji mengi tu si angekunywa ya pale  kwanini atafute ya mbali, lakini wao hawakujali hilo..na hivyo wakawa tayari kuhatarisha Maisha yao kwa ajili tu ya kuishibisha kiu yake, Hivyo kwa tendo lile ikamfanya Daudi asiyanywe maji yale, bali kwenda kuyamwanga mbele za BWANA.

Kristo naye alipokuwa msalabani alisema ninaona KIU..Lakini wale askari hawakuithamini kiu yake..Vilevile hadi sasa Kristo anasema ninaona kiu, lakini wengi wetu tunaidharau kiu yake tunaona kama anataka kutuau huyu, kutufilisi, yeye si ana kila kitu iweje tena atuombe sisi maji, utasema ni wapi kwenye maandiko Yesu anasema nina kiu..ukisoma Mathayo 25 utaona  anawaambia wale watu aliowafananisha na mbuzi kuwa alikuwa na kiu lakini hawakumnyeshwa, vilevile na wale wengine ambao aliwafananisha na kondoo akiwaambia  nilikuwa nina kiu na mlininywesha..

Ni kweli tunamnywesha kila siku maji kwa matoleo yetu, lakini Je! Maji hayo tunaweza kuyageuza kuwa Damu?. Kiasi kwamba ashindwe kuyanywa na kuyamwaga mbele za Mungu mbinguni kama dhabihu?

Kristo anatazamia, tumtolee kilicho bora, bila kujali inatugharimu kiasi gani..bila kujali tutapoteza nini, au tunapata hasara kiasi gani baada ya hiki, na hiyo yote ni kwa faida yetu sisi wenyewe (anataka tumtolee Mungu vile vinavyotugharimu)….Na kwa kufanya hivyo..haitamfikia tena kama maji yakatayo kiu,.. bali sadaka yako itamfikia kama DAMU..kama uhai wako mwenyewe..

Ukiingia  gharama kubwa kumpa Kristo kitu Fulani  jambo ambalo mtu wa kawaida hawezi kufanya, ..mbinguni unahesabika ni kama umemwaga damu yako kwa ajili yake..Haijalishi hicho kitu ni kidogo kiasi gani, kinachojalisha ni gharama uliyoingia. Je ni kubwa kiasi gani..mbele za Mungu, Yule mwanamke aliyekuwa mjane, aliingia gharama kubwa kutoa kila alichonacho ingawa kwa nje ilikuwa ni senti mbili tu.

Mtu anayefanya hivyo  anapata thawabu kama tu aliyechinjwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu. Hivyo tumtolee Mungu vile vinavyotugharimu Zaidi. Ili tuvuke hata kiwango vya baraka tu za kimwilini bali mpaka zile za mashahidi wa Yesu.

Tumtolee Mungu wetu kwa wingi, naye atatujaza kwa vingi.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengin

Mafundisho mengine:

Tafadhali Share ujumbe huu na kwa wengine.


Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/tofauti-katika-ya-zaka-na-sadaka-ni-ipi/

SADAKA YA MALIMBUKO.

HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.

INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments