URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

Urimu na thumimu ni nini?


Katika Agano la kale Mungu alikuwa akitumia njia kuu tatu aidha kuwasilisha  ujumbe au leta majibu au kuthibitisha jambo..Njia ya kwanza ni manabii, njia ya pili ni ndoto, na njia ya tatu ni Urimu na thumimu.

Tunalithibitisha hilo katika kitabu cha 1Samweli 28:4  pale ambapo Mfalme Sauli alipokwenda kuuliza kwa Bwana kuhusu vita iliyokuwa inamkabili mbele yake dhidi ya wafilisti, Kama watashinda au La, lakini Bwana hakumjibu kwa njia yoyote kati ya hizo tatu..

1Samweli 28:4 “Nao Wafilisti wakakusanyika, wakaenda kufanya kambi huko Shunemu; naye Sauli akawakusanya Waisraeli wote, nao wakapiga hema katika Gilboa. 

5 Basi alipowaona hao majeshi ya Wafilisti, huyo Sauli akaogopa, na moyo wake ukatetemeka sana. 

6 Lakini Sauli alipouliza kwa Bwana, Bwana hakumjibu, wala kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa manabii”.

URIMU NA THUMIMU maana yake nini nini?

Urimu maana yake ni “Mianga” Na Thumimu “mikamilifu”..Haya Ni mawe 12 ya aina tofauti tofauti yaliyokuwa yamegundishwa katika ki-mfuko kidogo kilichokuwa kinakaa katika kifua cha kuhani mkuu. Hivyo ikiwa kuna jambo watu wanahitaji kupata uhakika kutoka kwa Bwana basi Mawe haya yalikuwa yanatoa mwanga Fulani unaoakisiana, kuthibitisha jambo hilo, Na hivyo kama jambo hilo sio sawa basi hayakutoa mwanga wowote. Urimu na Thimumu ilikuwa inatoa jibu la mwisho japo si mara zote ilikuwa inatumika.

Kwa mara ya kwanza urimu na thumimu inaonekana katika kitabu cha Kutoka 28:29-30

29 Na Haruni atayachukua majina ya wana wa Israeli katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu juu ya moyo wake, hapo atakapoingia ndani ya mahali patakatifu, kuwa ukumbusho mbele ya Bwana daima. 

30 Nawe utie hizo Urimu na Thumimu katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu; nazo zitakuwa juu ya moyo wa Haruni, hapo atakapoingia ndani mbele ya Bwana; na Haruni atachukua hukumu ya hao wana wa Israeli juu ya moyo wake mbele ya Bwana daima.

Soma tena..

Walawi 8:6 Basi Musa akawaleta Haruni na wanawe, akawaosha kwa maji. 

7 Kisha akamvika Haruni ile kanzu, na kumfunga mshipi, na kumvika joho, na kumvika naivera, na kumfunga huo mshipi wa kazi ya mstadi wa naivera na kumfunga naivera kwa huo mshipi. 

8 Kisha akamtia kile kifuko cha kifuani; akatia hizo Urimu na Thumimu katika hicho kifuko cha kifuani. 

9 Akamvika na kile kilemba kichwani mwake; na juu ya kilemba, upande wa mbele, akakitia kile kipande cha dhahabu, hiyo taji takatifu; kama Bwana alivyomwagiza Musa.

Ukipata tena nafasi Soma  Kumbukumbu 33:8, Hesabu 27:21..

Tunaona tena, wakati mfalme Sauli alipopishana na mwanawe kuhusu kuvunjwa viapo ambavyo alivyoweka, alitaka Mungu ahukumu katikati yao ni nani mwenye makosa, Hivyo alitumia Urimu na Thumimu kuomba uthibitisho huo.

1Samweli 14:41 “Kwa hiyo Sauli akamwambia Bwana, Mungu wa Israeli, [Kwani usimjibu mtumishi wako leo? Ikiwa dhambi i ndani yangu, au ndani yake Yonathani mwanangu, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, utoe Urimu; bali ukisema hivi, Dhambi i katika watu wako Israeli,] utoe Thumimu ,Basi Yonathani na Sauli wakatwaliwa,lakini watu wakapona”.

JE! URIMU NA THUMIMU iliendelea kudumu muda wote?

Wakati wana wa Israeli wanachukuliwa tena utumwani Babeli, na hekalu la Mungu kubomolewa, ndio ilikuwa mwisho wa kutumika kwa urimu na thumimu. Hata waliporudi na kujenga upya nyumba ya Bwana, kitendo hicho hakikuonekana kikitendekea tena katikati ya makuhani.

KATIKA AGANO JIPYA URIMU NA THUMUMI NI NINI?

Kama vile ilivyokuwa katika agano la kale, ili kuthitisha jambo ilikuwa ni lazima mawe yale yatoe mwangaza Fulani wa tofuati, vivyo hivyo katika agano jipya Urimu na thumimu yetu ni BIBLIA TAKATIFU. Kila Neno, kila ndoto au kila unabii, kabla haujapokelewa au kuaminiwa ni lazima kwanza uletwe kwenye biblia ambayo ndio Urimu na Thumimu yetu..Na unabii huo au ndoto hiyo kama haipatani na maandiko basi tunapaswa tuukate ufunuo huo haijalishi utaonekana unao uhalisia mkubwa kiasi gani.

Katika nyakati hizi za mwisho shetani anabuni njama mpya za kuwadanganya watu kila siku kwa kivuli cha Neno Ufunuo..Kila mmoja anasema nimefunuliwa..hata jambo ambalo linaonekana linakiuka misingi ya Imani ya kikristo mtu anasema amefunuliwa.. Ni kweli tunayahitaji mafunuo ili tuyaelewe maandiko, lakini kila ufunuo  ili ukubalike ni lazima upatane na Urimu na Thumimu yetu ambayo ni biblia.

Upotashaji uliopo.

Lakini utajiuliza mbona, nabii yule alipokutabiria hivi au vile ni kweli vilitokea kama vilivyo na leo  hii kakupa tena maagizo mengine uachane na mume wako au mke wako ukaoane na mwingine..Nataka nikuambie kama Neno la Mungu likiwa halijakaa vizuri ndani yako unaweza kumsikiliza ukadhani kuwa ni maagizo ya Mungu, ukamwacha mke wako ukaenda kuoa mwingine au kuoelewa na mwingine, kisa tu nabii kasema, na kisa tu alishakutabiria kipindi cha nyuma na jambo Fulani likawa ni kweli..

Lakini wewe kwa kukosa ufahamu wa kimaandiko, hujui kuwa unakwenda kuishi katika uzinzi, umeshachukuliwa na maji, kwasababu biblia inasema mtu amwachae mke wake na kwenda kuoelewa na mwingine azini..

Marko 10:11  “Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake;

12  na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini”.

Ndugu yangu embu soma maandiko haya upate picha halisi ya kitu  ninachokuambia..

KUMBU: MLANGO 13

1 Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, 

2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; 

3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote. 

4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye. 

5 Na yule nabii, au yule mwotaji wa ndoto, na auawe, kwa kuwa amesema yaliyopotoka juu ya Bwana, Mungu wenu, aliyewatoa katika nchi ya Misri, akakukomboa katika nyumba ya utumwa, apate yule mtu kukupotoa katika njia aliyokuamuru Bwana, Mungu wako, uiendee. Ndivyo utakavyouondoa uovu utoke katikati yako. 

Unaona? Tunapaswa kabla ya kupokea Neno lolote au unabii wowote, tuutazame je unakubaliwa na Urimu na thumimu yetu (yaani biblia) au La. Tukizingatia hayo tutakuwa tumejiweka katika nafasi nzuri ya kuzishinda kirahisi hila za shetani katika nyakati hizi za mwisho ambazo anazileta kupitia   manabii wake na walimu wake wa uongo, katika siku hizi za mwisho. Mfano tena mtu anaweza akaja akakwambia kata mti huu au ule, unasababisha vifo vya wababa katika familia au ngo’a ua hili au lile, linatunza majini, au usifuge paka, au njiwa wanatumiwa na wachawi n.k. .

Mafundisho ya uongo.

Yote hayo ni mafundisho au mafunuo yaliyotoka kuzimu ambayo hayana msingi wowote wa kimaandiko, Zaidi tu yanawafanya watu waishi Maisha ya woga na wasiwasi wakidhani kuwa vitu vya nje vinaweza kuathiri Maisha yao rohoni, na kusahau kuwa asili ya laana zote zipo rohoni pale mtu anapokuwa mbali na muumba wake, anapotenda dhambi ndipo anapokumbana na laana. Na mafunuo mengine mengi ya namna hiyo..

Leo hii umeshaijua urimu na thumimu yako(BIBLIA), Hivyo jambo lolote linapokujia lipime kwanza na maandiko.

Je! Umeokoka? Je unafahamu kuwa tunaishi katika kizazi ambacho dalili zote zinaonyesha kuwa tutashuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa YESU KRISTO?. Je! Una habari kuwa hili ndio kanisa la saba na la  mwisho lijulikanalo kama LAODIKIA tunaloishi(Ufunuo 3), na baada ya hili hakutakuwa na kanisa lingine mbeleni. Je! Unataarifa kuwa Israeli imeshachipuka, na hii neema siku si nyingine itarudi kwao na ikisharudi kule, upande wetu mlango wa neema utakuwa umeshafungwa?

Unaona tupo katika hatari kubwa kiasi gani..Unasubiri nini usiokoke..Usimpe Kristo Maisha yako.. Huu ulimwengu umekupa faida gani tangu uanze kutaabika nao, Lakini Kristo anakuahidi amani idumuyo isitoshe anakupa na uzima wa milele juu.. Hakuna mwanadamu yoyote anaweza kukuahidia mambo mazuri kama hayo.

Yeye mwenyewe anasema..

Mathayo 11:28  “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29  Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30  kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”

Unaona? Amekuahidi mizigo yako yote ataitua, yeye hasemi uongo, ukiwa utakuwa tayari tu kumpokea muda huo huo anaanza kufanya kazi ndani yako ya kukugeuza..Hivyo usifanya moyo wako kuwa mgumu, chukua uamuzi huo sasa..

Kama upo tayari kufanya hivyo kumpa Bwana Maisha yako…

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Na Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Zingatia hayo na Bwana atakuwa pamoja nawe. Vilevile Usiacha kutembelea Website hii  https://wingulamashahidi.org mara kwa mara ili ujifunze maneno ya uzima..

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Zile tunu (Dhahabu, uvumba na manemane) Mamajusi walizozitoa kwa Bwana (Mathayo 2) . ziliwakilisha nini?

Je! sisi ni wafalme na makuhani kwa namna gani?

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
6 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Jonas Emmanuel.
Jonas Emmanuel.
2 years ago

Mungu awabariki sana kwa masomo mazuri na yenye pumzi ya Mungu. Hakika nabarikiwa sana.

MUSSA NYEMBE SANYIWA
MUSSA NYEMBE SANYIWA
2 years ago

This is really a wonderful message ever. There has been an overwhelming mushrooming of the self-proclaiming prophets and prophetesses who claim to have been shown signs and all about people’s lives. I call them false messengers because their messages contradict the immutable God’s precepts. these are really messengers of devil behind the mask of Christianity.
I like the message and I encourage you to keep disseminating to other people to be saved. God bless you

Anonymous
Anonymous
3 years ago

Barikiwa sana kwa somo hili Mtumishi wa Mungu! Nimejifunza kwa Utukufu wa Mungu.