UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?

UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?

Unamalizaje mwaka wako?.Unamtukazaje Mungu katika sikukuu hizi na mwisho wa mwaka wako?


Ilikuwa ni Disemba 24, 1964, jaribio la kwanza la wanasayansi la kusafiri kutoka katika obiti (muhimili) wa dunia na kuelekea katika obiti ya mwezi..Ni jaribio ambalo lilikuwa ni la kwanza na la hatari sana, kiasi kwamba ingetokea tu injini moja ya chombo cha wana anga hao kufeli basi watu hao ndio wangepotea milele katika anga za mbali..

Tukio hilo la kuondoka kwao lilishuhudiwa na dunia nzima siku hiyo, watu wakiwa na shauku ya kuona ni nini kitatokea, katika ziara hiyo ya masafa ya mbali ya anga, vyombo vyote vya habari vilikuwa wazi na televisheni zote wakizungumzia safari hiyo ambayo ilichukua takribani siku tatu kuifikia orbit ya mwezi,..Sasa wana anga hao wakiwa tayari wameshaingia katika obiti ya mwezi wakijiandaa kuizunguka mara 10 Wakiwa kule angani kuchukua picha za matukio kitendo cha kuishuhudia “Dunia kunyanyuka”..Sio “Mwezi kunyanyuka” kama tulivyozea huku kuona mwezi ukinyanyuka kutoka mashariki mpaka kufika angani..Wao walifika hatua hiyo ya kushuhudia na kuchukua video ambayo ipo mitandaoni hadi leo jinsi dunia inavyoonekana kwa mbali ikinyanyuka kutoka katika pembe za mwezi hadi juu kama vile mwezi unavyonyanyuka kutoka katika pembe za dunia..

Lakini sasa wana anga wale 3, wakiwa wanajiandaa kutoa ripoti hiyo..Walikatisha matangazo yao..wakiwa sasa kule kule angani wakaiambia Dunia maneno haya..

Nukuu.

“Wakati tunakaribia kushuhudia tukio hili kuu, timu yetu ya Apollo 8 tunao ujumbe tunataka tuwaambie watu wote mlio katika dunia.. Na ujumbe wenyewe ndio huu..

1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.

4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.

5 Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.

6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.

7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo. 8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.

9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.

10 Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.”

Walipomaliza kuisoma mistari hiyo ya kitabu cha Mwanzo 1:1-10 wote watatu, walifunga biblia zao kwa kusema maneno haya:

“Sisi kama timu ya Apollo 8, tunamalizia kwa kuwaambia muwe na usiku mwema, wenye amani, na Heri ya krisimasi, Mungu awabariki wote, wote mlio katika dunia nzuri.”

Mwisho wa Nukuu.

Ikiwa utapenda kusikia audio hiyo basi bofya link hii.>>

Maneno hayo yaliugusa moyo wa ulimwengu mzima kwa wakati ule.. Na kuwafanya watu wengi, wajifikirie mara mbili juu ya Maisha yao ya rohoni, ikiwa wanasayansi wanaukiri utukufu wa Mungu wakiwa maelfu ya kilometa mbali na dunia..Inatupasaje sisi?..

Watu wale waliporudi salama duniani, Habari zao zikavuma sana, ndio waliowekwa kuwa watu wa mwaka kipindi hicho..

Kama hiyo haitoshi mwaka mmoja baadaye..timu nyingine ya wanasayansi wa anga (Astronauts) iliyojulikana kama Apollo 11,nayo ya watu watatu, ilifunga safari nyingine tena, lakini awamu hii sio kama ile ya kwanza ya kuuzunguka mwezi, bali hii ilikuwa ni kutua kabisa mwezini kwa mara ya kwanza..

Safari ilianza July 20, 1969 na ilipofikia July 21 walikuwa wameshafika katika uso wa mwezi..muda mchache tu baada ya kutua, mmojawapo kati ya wale watatu aliitoa divai yake na mkate wake, aliyoichua kutoka kanisani mwao..akamwomba kamanda wake wasitishe matangazo yote kwa muda, jambo lisilo la kawaida aliashiriki meza ya Bwana akiwa kule mwezini..Na alipomaliza aliomba wasikilizaji wake wote duniani wasikilize anachowaambia..

Akausoma mstari huu kwa nguvu dunia nzima ikiwa inasikia..

Yohana 15:5 “Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote”.

Akafunga biblia yake..wakaendelea na shughuli za kule mwenzi Na Walipomaliza shughuli zao baada ya masaa kadhaa, wakawasha chombo chao, wakaondoka..Sasa akiwa wanauacha mwezi, huku wakiangalia magimba ya ajabu Mungu aliyoyaumba angani..huyu mwanaanga aliyeitwa Buzz Aldrin.

Akaifungua tena biblia yake, akasema ninao ujumbe bado kwa dunia yote…huku mamilioni ya watu duniani wakiwasikiliza akasoma tena mstari huu..

Zaburi 8:3 “Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota ulizoziratibisha;

4 Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie”

Haleluya!!..Kama ilivyo ada maneno hayo yaliigusa mioyo ya watu wengi duniani..wakisema ikiwa watu hawa wanafanikiwa katika mambo makubwa kama haya, Lakini bado hawaachi kuitangaza mauti ya Kristo, na utukufu wa Mungu..Inatupasaje sisi ambao hatujafika popote?

Kama ulikuwa hujui hawa ndio waliokuwa wanadamu wa kwanza na wa mwisho kutua mwezini..Lakini katika mafanikio yao hawakuacha kumtukuza Mungu..hawakuacha kuyatimiza maagizo Kristo aliyowapa kama wakristo pasipo kujali hali na mazingira..

Embu tujiulize Watu kama hawa Mungu ataachaje kuwafikisha mbali ikiwa wanaiadhimisha Krisimasi yao kwa kuutangaza utukufu wa Mungu, wanafunga mwaka kwa kuubariki uumbaji wa Mungu..

Hata wakiwa mwezini mahali ambapo hapana oxyjeni, kusikoweza kuishi kiumbe chochote mkristo huyu haachi kuishiriki meza ya Bwana, wanaithamini damu ya Emanueli iliyomwagika pale Kalvari kwa ajili yao miaka 2000 iliyopita..Na sisi Je tutapate kupona tusipouthamini wokovu mkuu namna hii..

Wewe na mimi hatujawahi kufika mwezini, hatujawahi kuona hata mambo makubwa na ya kustaajabisha, wala hatuna elimu ya juu na utajiri wa kuwafikia watu hawa na taifa lao, ambao kimsingi ndio wangepaswa wawe wakwanza kusema hakuna Mungu lakini kinyume chake katika mafanikio yao ndio wanaokuwa wa kwanza kumuhubiri Kristo..

biblia inatuambia…

Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu..”

Na wewe Je! Bado unafikiria kuumaliza mwaka wako bar, au guest? Au Disko? Au Casino? Au kwenye kumbi za starehe?…Kumbuka hawa ndio watakaotuhukumu siku ile.. Ni heri ukaufunga mwaka wako kwa Bwana na kusema kuanzia leo nimeamua kumfuata Kristo kwa moyo wangu wote.

Ukifanya hivyo kwa kumaanisha kabisa, atakupokea, ameahidi hivyo katika Neno lake kuwa yeyote aendaye kwake hatamtupa nje kamwe..(Yohana 6:37).Na yeye si mwongo mwongo kama sisi.

Unasubiri Nini tubu leo dhambi zako kabla ya kuingia mwaka huu mpya..Ukabatizwe katika ubatizo wa kimaandiko wa kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako, kisha Bwana akupe kipawa cha Roho wake Mtakatifu kukulinda na kukuongoza hadi siku ile ya mwisho wa Maisha yako kama unyakuo utakuwa haujapita..Usisieme mimi ni wa dini hii, au ile hivyo siwezi kuwa mkristo, wala usiseme mimi dhehebu langu ni hili, hivyo siwezi kuokoka..Wokovu ni mlango wa wazi kwa watu wote..na wokovu ni wa lazima! Kama tunapenda maisha.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Shalom.

Mada Nyinginezo:

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

SAA YA KIAMA.

CHAPA YA MNYAMA

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments