KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Cheo cha Mpinga-Kristo, kimeshafunuliwa Zaidi ya Karne moja iliyopita huko nyuma, nacho si kingine Zaidi ya cheo cha ki-PAPA, Wakati wa Mwisho utakapofika atanyanyuka mmoja atakayekikalia hicho kiti, ambaye atafanya mambo maovu na ya ajabu, yale yote yaliyotabiriwa katika maandiko matakatifu. Huyo bado hajafunuliwa kwasasa jina lake ni nani?… Lakini hatatoka pengine mbali na kiti hicho cha Kipapa..Lakini kwasababu tunajua majira na nyakati, kwamba hizi ni siku za mwisho, labda huyu aliyeko sasahivi ndiye!..au kama siye miongoni mwa wachache sana wanaokuja huko mbeleni atakuwa mmojawapo!…Huyo ndiye atakayeihimiza chapa! Huyo ndiye atakayeidanganya dunia kuwa ataleta amani! Lakini badala yake ataipeleka kwenye matatizo na kiama.. Na ndiye atakayetafuta kwenda Yerusalemu kwenye Hekalu litakalotengenezwa kule hivi karibuni kule Israeli aabudiwe pale kama Mungu (2Wathesalonike 2).

Vipo viishara vingi vinavyotuthibitishia utendaji kazi wake, katika kizazi chetu…lakini pia kipo kiashiria kimoja kikubwa sana! Cha kutufanya tuzidi kuwa macho na kufunguka fahamu zetu, kujua ni majira gani tunaishi.

Kiashiria hicho si kingine Zaidi ya Roho yake huyo Mpinga-Kristo kuwavaa watu(wanaojiita watumishi),

Leo hatutazungumzia, jinsi hii roho ilivyoyavaa makanisa pamoja na serikali..Bali tutaangalia ni jinsi gani imewavaa wanaojiita watumishi.

Zamani, kusikia Mtu anayejiita mtumishi wa Mungu, kuwa na walinzi wa pembeni (ma-bodyguards) ilikuwa ni jambo la kushangaza sana…Hata hivyo halikuwepo kabisa, kwasababu Bwana Yesu mwenyewe ambaye sisi tunamwita Bwana! Hakuwa na mabody-guards, wapo watu wanasema wale mitume walikuwa ma-bodyguards wake, huo sio ukweli, bodyguard huwa anatembea na silaha na kazi yake ni kumlinda Yule ili asidhuriwe anakuwa tayari hata kuua ili kwamba tu Yule anayelindwa akae salama, lakini Bwana hakuwaita mitume kwa kazi hiyo, ya kumlinda yeye, kinyume chake Petro alipojaribu kufanya hivyo kwa kumkata Yule mtu sikio alimkemea …Zaidi ya yote yeye mwenyewe alijitoa kwa hiyari yake kufa kwa ajili ya wengi, ingawa alikuwa na uwezo wa kuagiza malaika waje wampiganie lakini hakutumia uwezo huo, ili kwamba awe sadaka kwa wengine (soma Mathayo 26:51-54 )…

Na Neno lake linatuambia kama yeye alivyojitoa kwa ajili yetu na sisi pia tunapaswa tujitoe kwa ajili ya wengine. (1Yohana 3:16)

Lakini leo ni kinyume chake utaona Mhubiri anakwenda kuhubiri injili na Mabody-guards ambao wameandaliwa mahususi kumtetea yeye, na ndani ya kifuko yao wamebeba silaha..yote hiyo hataki kufa! au Anaogopa kufa!..Ukimgusia habari za kwenda kuhubiri bila bodygurds anapambana na wewe!..Leo malengo ya wahubiri wengi ni kununua Helikopta na ndege, ili hatimaye waziandike majina yao, na wajulikane dunia nzima, na hatimaye waonekane mbele ya vyombo vya habari ili wapate heshima duniani kote…

Sasa hiyo yote imetoka wapi? Na kwanini haikuwepo kipindi cha nyuma?

Jibu ni rahisi! Hiyo yote ni ile nguvu ya mpinga-Kristo mkuu imewavaa hawa watumishi!….Roho ya Mpinga kristo ndiye inayowafanya watafute fahari na ufalme katika dunia hii, sasa roho hiyo haijaanzia kwao, bali imeanzia kwenye kile cheo cha Mpinga Kristo mwenyewe, (yaani kiti cha upapa)…Papa ambaye anajulikana kama mhubiri maarufu, ndiye Mhubiri pekee aliye kinyume na Kristo, ambaye analindwa na JESHI! Linaloitwa “Swiss guards” linalomzunguka na kumlinda kila anakokwenda..Mabodyguard hao kabla ya kumlinda Papa, wanaapa kuwa tayari hata kuutoa uhai wao ili tu kumlinda Papa asife!…jambo ambalo Kristo aliye Bwana hakufanya, wala hakutamani kulindwa kwa namna hiyo…hivyo si ajabu leo kuwaona hawa wahubiri wengine wadogo wakifanya hayo hayo…wakiajiri mabodygurd kuwalinda hadi madhabahuni..ni roho ile ile ya mpinga-kristo ipo kazini.

Papa ana ndege yake maalumu inayoitwa “Alitalia Flight AZ4000” inayokaribiana sana kufanana na Ndege ya Raisi wa Marekani Airforce one… roho hiyohiyo imewavaa manabii wa uongo wanaozuka sasahivi, nao pia wanafanya juu chini kumiliki ndege kama ya Papa, lengo lao sio kutumia hizo kumuhubiri Kristo, bali kujihubiri wao wenyewe na ufahari wao.

Papa anaabudiwa na ana pete iliyopo mkononi mwake ambao maelfu ya waumini wa kikatoliki, wamkaribiapo ni lazima waibusu, mkononi mwake…roho hiyo hiyo imewavaa manabii wa uongo leo, wanatafuta kwa bidii kuangukiwa na kusujudiwa..na hata watu kuwapa heshima fulani kubwa ya kipekee…Na mambo mengine mengi Papa anayafanya yameshaanza kuonekana kwa wanaojiita wahubiri.

Ndugu tuonapo Mambo hayo yaliyo kinyume na Kristo, ambapo hapo kwanza yalikuwa yanafanyika na mtu mmoja tu Papa, lakini sasa yanafanyika na maelfu ya watu wanaojiita watumishi wa Mungu, ni wakati wa kunyanyua vichwa vyetu juu, kwasababu ule mwisho umekaribia sana..Ile roho ya mpingakristo imeshateka ulimwengu mzima…kinachosubiriwa ni unyakuo tu! Dhiki kuu ianze..Ni kama ugonjwa! Ulioanzia kichwani kama upele lakini sasa umeenea mwili mzima…hiyo ni dalili mbaya!

Tabia hii, ikishamalizika kusambaa, itamsaidia baadaye mpingakristo kufanya kazi yake kirahisi. Atakapoanzisha chapa, afanye kazi kirahisi kwasababu watakuwepo watu wengi watakaosapoti mambo anayoyafanya…Kwasasa yataonekana si ajabu tena.

Je umeokolewa? Na kama umeokoka una uhakika na wokovu wako? Biblia inasema

2 Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”

Ufunuo 3:20 “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”.

Bwana akubariki.

Tafadhali share na wengine


Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

MPINGA-KRISTO NI NANI?

CHAPA YA MNYAMA NI NINI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments