Kikuku/vikuku ni nini katika biblia?

Kikuku/vikuku ni nini katika biblia?

Vikuku ni vitu mfano wa bangili ambavyo vinavaliwa aidha mikononi au miguuni, kwa lengo la urembo. Tazama picha juu. Katika enzi za zamani vikuku vilivaliwa na jinsia zote, yaani wanaume na wanawake.

wanawake wanavaa vikuku miguuni

Katika biblia tunaona neno hilo likitokea mara kadhaa..

2 Samweli 1:10 “Basi, nikasimama karibu naye, nikamwua, kwa sababu nalijua hakika ya kuwa hawezi kupona baada ya kuanguka; kisha nikaitwaa ile taji iliyokuwa kichwani mwake, na kikuku kilichokuwa mkononi mwake, nami nimevileta hapa kwa bwana wangu”.

Na pia unaweza kusoma mistari ifuatayo binafsi iliyozungumzia juu ya vikuku Mwanzo 24:47, Isaya 3:19,  Ezekieli 16:11 na Ezekieli 23:42.

Lakini sio hilo tu, vikuku pia vilitumika katika kutengenezea mishikio ya masanduku. Kwa mfano utaona sanduku la Agano lilitengenezwa kwa vikuku katika pande zake za chini ili kuwezesha upitishaji wa zile fimbo zake, na kufanya ubebaji wake uwe mrahisi… Tazama picha chini.

vikuku katika sanduku la agano

Kutoka 25: 14 “Nawe tia hiyo miti katika vile vikuku vilivyo katika pande mbili za sanduku ili kulichukua hilo sanduku.

15 Hiyo miti itakaa katika vile vikuku vya sanduku; haitaondolewa.

16 Kisha tia ndani ya sanduku huo ushuhuda nitakaokupa”.

Lakini je! Katika agano tunaruhusiwa kuvaa vikuku?

Jibu ni la!. Mwanaume au mwanamke wa kikristo hapaswi kutoboa pua na kuweka hazama, hapaswi kujiharibu ngozi kwa kujichubua, hapaswi kuvaa vikuku katika mikono yake au miguu yake..Kwasababu miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu.

1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;

4  bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao”

Mwanamke anayevaa kikuku mguuni, anakuwa hana tofauti na kahaba. Matumizi ya vikuku yabaki katika kutengenezea masanduku na bidhaa nyingine lakini si kuivalisha miili yetu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Hazama ni nini katika biblia?(Ezekieli 16:12, Kutoka 24:47)

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments