KIMBIA! KIMBIA! KIMBIA!

KIMBIA! KIMBIA! KIMBIA!

Makanisa yanayohubiri injili ya mafanikio tu. Na kukwambia kuwa uthibitisho wa Mungu kuwa yupo na wewe, ni kuwa tajiri ...JIHADHARI NA HILO KANISA!

Makanisa yasiyohubiri toba ya msamaha na kuwafanya watu wajione ni kawaida kuishi na dhambi zao…JIHADHARI NA HILO KANISA!..Toba na msamaha ndio kiini cha Imani.

Makanisa yanayochanganya NENO la Mungu na siasa na vikundi vya kijamii, jambo ambalo huwezi kutofautisha jukwaa la siasa na kanisa, na makanisa yanayochanganya Neno la Mungu na mapokeo ya wanadamu….JIHADHARI SANA!

Makanisa yasiyohubiri utakatifu na kufundisha watu ukweli kulingana na Biblia…KUWA MWANGALIFU NA HILO KANISA..

Makanisa yanayohubiri ujumbe wa kutoa tu, na kuacha mafundisho ya adili kama upendo, utakatifu na imani,,,,JIHADHARI NA HILO KANISA KWA USALAMA WA MAISHA YAKO YA MILELE.

Kanisa lisilokufundisha wala kugusia kujiandaa kwenda katika unyakuo…KUWA MAKINI!

Kanisa lisiloruhusu karama za Roho kufanya kazi, kama uponyaji wa kiungu, unabii, lugha, miujiza n.k. jua hilo kanisa limekufa au lipo karibuni kufa. JIHADHARI NDUGU!

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada zinazoendana:


Mada Nyinginezo:

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU

KWANINI MUNGU ANAMPA NABII HOSEA MAAGIZO YA KUMUOA MWANAMKE KAHABA? (HOSEA 3)

KUTOKA 10:1 “BWANA ANASEMA ATAMPA FARAO MOYO MGUMU, ASIMTII, JE! HAPO BWANA ATAMHUKUMU FARAO KAMA MKOSAJI SIKU ILE?”


Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments