Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.

SWALI: Mstari huu unamaana gani? Mithali 19:21 Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.


JIBU: Kila moyo wa mwanadamu, unamatamainio mengi, lakini uhalisia ni kwamba sio matamanio yote ni ya ukweli au yanania nzuri baadaye, kwamfano mtu atataka mali nyingi, lakini moyo wake unasema atakapopata nyumba kubwa na gari atawakomoa waliomdharau, atalipiza kisasi, atafanya anasa ,atatembea kwa majigambo, ataongeza Masuria.

Na  ndio maana mengi ya malengo kama haya yawezi kusimama kwa watoto wa Mungu, kwasababu yana hila nyingi nyuma yake. Mtume Yakobo aliliweka wazi jambo hili, ni kwanini wakati mwingine hatupokei majibu ya maombi yetu alisema..

Yakobo 4:2  “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! 3  Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”

Lakini kinyume chake anasema Shauri la Bwana ndilo litakalosimama. Maana yake ni kuwa Hekima ya Bwana inayopima  haya yote imaamua cha kutoa na kutokutoa. Hivyo si matamainio yako yote unayoyaona ni mema, basi yatakuwa mema pia mbele za Mungu, mengine yana udaganyifu mwingi. Ndio maana Yeremia 17: 9 inasema “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua”?

Hivyo tuombapo jambo ni busara kumalizia na kusema “Bwana mapenzi yako yatimizwe”.

Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala Mwangalie sana

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)

JIFUNZE KUDUMU UWEPONI MWA MUNGU.

Je ni kweli Yuda hakuwa na dhambi kwa kumsaliti Bwana, kwasababu tayari ilikuwa imeshatabiriwa?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Paston
Paston
9 months ago

NIUNGE KWENYE WHATSAPP NO. 0756 65 23 65.