Hayawani ni nini katika biblia?

by Admin | 30 November 2020 08:46 am11

Mwanzo 3:14 “Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako”

Hayawani ni wanyama wa mwituni, ambao sio wa kufugwa…Wanyama wa kufungwa ni kama Kondoo, Mbuzi, Ng’ombe, Ngamia, punda n.k. Hawa wameumbwa mahususi kuishi na wanadamu, na kunyenyekea chini ya mikono ya wanadamu. Lakini wanyama wengine wote ambao kamwe hawewezi kujinyenyekeza chini ya uongozo wa wanadamu, na hivyo hawaishi na wanadamu bali mwituni kama simba, chui, nyati, fisi, mbwa-mwitu n.k Hao ndio wanaoitwa hayawani, ni wanyama wasiofugika.

Kwamfano Swala ni kama mbuzi tu, lakini huwezi kumfuga, kwanza akikuona atakimbia…kadhalika Nyati, ni kama ng’ombe tu, lakini huwezi kumfuga na kumtumikisha kama ng’ombe akikuona atatatufa kukudhuru, badala ya kukutii. Kama biblia inavyosema..

Ayubu 39: 9 “Je! Nyati atakubali kukutumikia? Au atakaa katika zizi lako?

10 Je! Waweza kumfunga nyati kwa kamba matutani? Au, yeye atayalima mabonde nyuma yako?

 11 Je! Utamtumaini kwa sababu ana nguvu nyingi? Au, utamwachia yeye kazi yako?

 12 Je! Utamtumaini kwamba ataileta mbegu yako nyumbani. Na kukusanya nafaka ya kiwanja chako cha kupuria?”.

Baadhi ya mistari katika biblia inayozungumzia juu ya hayawani ni pamoja Mwanzo 3:14, Mwanzo 31:39, Ayubu 35:11, Zaburi 50:10, Isaya 13:21, Isaya 23:13 n.k.

Lakini pia biblia imewafananisha Maadui wa Injili kama Hayawani wa mwituni. Maadui wa Injili ni pamoja na manabii wote wa uongo na waalimu wote wa uongo, ni pamoja na watu wote wanaoipinga injili ya msalaba. Wale Bwana Yesu aliosema katika Mathayo  7:15.

Mathayo  7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali”.

Hivyo manabii wote wa uongo ni hayawani ambao kazi yao kubwa ni kuingia katikati ya kundi la kulidhuru, hawa hawafugiki chini ya zizi la Mchungaji mkuu Yesu Kristo, ni wanyama wa mwituni katika roho, sio miongoni mwa kondoo wake.

1Wakorintho 15: 32 “Ikiwa, kwa jinsi ya kibinadamu, nalipigana na hayawani wakali kule Efeso….”.

Hali kadhalika, mtu yeyote ambaye kwa nje anaonekana ni mkristo, lakini kwa siri ni mtu anayefanya uchafu, biblia inasema huyo naye ni hayawani..

Tito 1:12  “Mtu wa kwao, nabii wao wenyewe, amesema, Wakrete ni waongo siku zote, HAYAWANİ WABAYA, walafi wavivu”.

Hivyo tujitahiti tusiwe wanyama wasiofugiga (hayawani) bali tuwe miongoni mwa kondoo wa Yesu. Na pia tujihadhari na hayawani wote wanaojigueza na kuwa mfano mfano wa kondoo wa Yesu, biblia imesema tutawatambua kwa Matunda yao.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

CHAPA YA MNYAMA

Roho za Wanyama zinakwenda wapi baada ya kifo? Je! Watafufuliwa?

FAHAMU MAJIRA ULIYOPO NA NINI UNAPASWA UWE NACHO.

KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/11/30/hayawani-ni-nini-katika-biblia/