Wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza

Wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza

SWALI: Naomba kufahamu kwanini mafuta yaliendelea kutumika wakati Yesu tayari alikuwa ameshakuja duniani?

Marko 6:12 “ Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu. 13  Wakatoa pepo wengi, wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza”


JIBU: Ndio, Bwana Yesu alikuwa na kanuni nyingi za kuwaponya watu, kuna wakati alitamka tu na mtu akapokea uponyaje wake, utakumbuka habari ya Yule mtu aliyepooza alimwambia jitwike kitanda chako uende nyumbani(Marko 2:1-9),  vilevile kuna wakati alimgusa kwanza mgonjwa, kisha akaponywa, utamkumbuka Yule mkoma,aliyemfuata na kumpigia magoti kumwomba amponye, maandiko yanasema akamgusa na kusema nataka takasika,(Marko 1:40-42). Vilevile Kuna wakati alitoa tu agizo la kutekelezwa na katikati ya agizo hilo, mtu anapokea uponyaji wake, ile habari ya wale wakoma 10, inatuthibitishia hilo,(Luka 11:17-19) na kuna wakati alitumia visaidizi, kama udongo, mate, kama ishara ya nje, ya mtu Yule kupokea uponyaji wake. Ukisoma habari ya Yule mtu ambaye alikuwa kipofu tangu kuzaliwa utali hakiki hilo nalo (Yohana 9:6).

Na hapa ndivyo ilivyokuwa aliwapa maagizo wanafunzi wake, Pale alipowaita na kuwatuma kwenda kuhubiri injili Ukisoma kuanzia mstari wa 7, Utaona aliwapa maagizo hayo ya kutoa pepo, na bila shaka na ya kuwapaka mafuta wote waliokuwa wagonjwa kwa jina lake.

Lakini hiyo haikuwa staili, kwamba kila mahali watakapokwenda wawe na chupa za mafuta, au maji, au udongo au chochote.

Hata sasa, hatupaswi kudhani Bwana hawezi kutuagiza tutumie kitu chochote cha asili kama ishara ya nje ya kuachilia uponyaji wake. La! Tusifikiri hivyo, Lakini hilo halipaswi lifanyike mara zote, au kama staili, kama inavyofanywa sasa, watu hawahubiri tena Neno la Mungu, kinachopigiwa kampeni ni mafuta na maji ya upako. Lakini mitume hawakufanya hivyo, ukisoma mstari wa 12, hapo anasema “Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu”. Umeona, Walijua jukumu lako kubwa ni kuwahubiria kwanza watu habari za dhambi zao. Na katika huduma hayo mengine yanafuata tena kwa uongozo wa Roho Mtakatifu.

Ni jambo linalosikitisha sasa, Jina la Yesu halitumiwi tena, shetani ameingilia eneo hili na kulivuruga, watu wakidhani hiyo ndio kanuni ya Mungu iliyobora ya watu kupokea uponyaji,  wamemgeuza kama mganga wa kienyeji ambaye yeye kazi yake ni kutoa tu miti-shamba lakini hajali hali ya mtu ya kiroho.

Wengine wanakimbilia lile andiko la Yakobo ambalo linasema,

Yakobo 5:14  “Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.

15  Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa”

Wanasahau kuwa kilichotangulia ni kuombewa kwanza..kuungamanishwa dhambi zake, kupatanishwa na Mungu, kisha ndio mafuta yafuate, kwa jina(agizo) la Bwana.

Tukikariri kwamba wakati wote tunapaswa tutumie chumvi kisa Elisha aliagizwa atupe chumvi kwenye chemchemi ya maji ili aondoe mapooza(2Wafalme 2:19-22), basi tukariri pia kitendo cha kulala juu ya maiti, kila tunapowaombea wafu ili wafufuke, kwasababu Elisha naye alifanya kitendo kama hicho(2Wafalme 4:32-34). Unaona, tutaonekana ni wachawi.

Ndugu, kuwa makini na staili za kisasa za uponyaji, ni makundi machache sana yanayoongozwa na Bwana kutumia vitu hivi vya asili katika kufanya huduma, na utaona havitumiki mara kwa mara au kila siku bali kwa mwongozo Fulani. Lakini ukiona mahali hapo ndio imekuwa staili, kimbia hapo Mungu hayupo hiyo ni ibada ya sanamu. Wana wa Israeli walimkosea Mungu hivyo hivyo, baada ya kuona Mungu amewaponya kwa kuitazama  ile nyoka ya shaba, Musa aliyoagizwa aiunde kule jangwani,  wao wakadhani Mungu sikuzote yupo katika sanamu ile, matokeo yake ikawa walipofika katika nchi ya ahadi wengine waliendelea kuiunda, wakiitazama ili kutatuliwa matatizo yao, ikawa ni chukizo kubwa sana kwao. Mpaka baadaye sana mfalme Yosia alipokuja kuivunja vunja, ndipo hasira ya Mungu ikaisha.(2Wafalme 18:1-5)

Hivyo usigeuze kitu chochote kuwa sanamu yako, kukitegemea hicho angali maisha yako yapo mbali na dhambi utakumbana na laana badala ya  baraka. Tumepewa jina la YESU hilo ndio mwanzo na mwisho. Vinginevyo vyote tusubiri kwanza uongozo wa Roho Mtakatifu, kama haupo, tuache.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

NEHUSHTANI (NYOKA WA SHABA).

Ni kwa namna gani Kristo analitakasa kanisa kwa Maji katika Neno? (Waefeso 5:26)

NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?

MAOMBI YA KUFUNGULIWA KIUCHUMI.

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?

VITA BADO VINAENDELEA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments