Risasi inayotajwa kwenye Ezekieli 27:12 ni ya namna gani?

Risasi inayotajwa kwenye Ezekieli 27:12 ni ya namna gani?

 Je! ni risasi hizi tunazozijua za bunduki, au ni risasi ya namna gani?.


Jibu: Katika biblia kuna maneno yaliyotumika ambayo yakiletwa katika nyakati zetu, yanabadilika maana kabisa.. kwamfano utaona Neno “fisadi” likitajwa katika biblia.. Maana halisi ya neno hilo sio “mtu anayedhulumu fedha za umma”.. Bali maana halisi ya neno hilo ni “mtu anayefanya uasherati uliovuka mipaka”.

Hali kadhalika kuna neno kama “Fedha”.. Neno hili kama lilivyotumika nyakati za kale ni tofauti na linavyotumika leo, Leo hii ukizungumzia Fedha, moja kwa moja akili zinakwenda katika “Hela” iwe ya noti au sarafu. . Lakini kiuhalisia maana halisi ya neno Fedha sio “Hela”.. Bali ni madini aina ya “Fedha” kama vile yalivyo madini aina ya dhahabu.. Hata pale katika maandiko Bwana aliposema Fedha na dhahabu ni mali yangu,(Hagai 2:8) hakumaanisha “Hela na dhahabu”… bali alimaanisha madini aina ya fedha, na madini aina ya dhahabu, ndio mali za Bwana. ..

Sasa kwanini madini haya ya fedha leo ndio yamegeuzwa maana na kuwa Hela/pesa?..kiasi kwamba hela yoyote leo inaitwa fedha.

 Ni kwasababu tangu zamani hata sasa malighafi inayotumika kutengenezea sarafu nyingi, ni madini hayo ya fedha.. utaona sarafu nyingi, kama zile za sh.10, au 20 au 500 hazijatengenezwa kwa chuma, wala dhahabu bali zimetengenezwa kwa madini ya fedha,..hivyo hiyo ikafanya Hela zote zijulikane kama fedha..siku hizi hata Noti zote zinajulikana kama ni fedha, jambo ambalo kiuhalisia sio sawa.

Na madini ya fedha yanaweza kutumika kwa matumizi mbalimbali sio tu kutengenezea sarafu, bali pia vyombo vya chakula, urembo n.k..isipokuwa tumizi lililo maarufu ni hilo la kutengenezea Sarafu.

Kwa mantiki hiyo hiyo pia kwa Neno “Risasi”. Leo hii ukitaja neno risasi moja kwa moja akili za wengi zinakwenda kwenye kile kipande kidogo cha chuma kinachotoka ndani ya bunduki.

Lakini kiuhalisia hiyo sio maana ya Risasi.. Risasi ni aina nyingine ya madini, ijulikanayo kwa jina hilo.. kama vile ilivyo fedha, dhahabu, almasi, chuma, shaba  n.k.. Vivyo hivyo kuna madini aina ya Risasi ambayo kwa lugha ya kiingereza yanaitwa “Lead”.

Na madini haya yajulikanayo kama Risasi yanamatumizi mengi mbali mbali kama vile Fedha ilivyokuwa na matumizi mbali mbali sio tu kutengeneza sarafu, bali pia vitu vingine.. Kadhalika madini haya ya Risasi matumizi yake ambayo ni maarufu leo hii ni kutengenezea hicho kisilaha kidogo kijulikanacho kama risasi leo… lakini hayo sio matumizi pekee ya madini hayo, bali ina matumizi mengine mengi ambayo ndio hasaa yaliyokuwa yanatumika enzi za zamani.

Nyakati za biblia madini hayo ya Risasi, yalikuwa yanatumika sana sana katika kutengenezea vyombo vya kupikia, na kuhifadhia vitu vya moto sana, kwasababu yalikuwa ni magumu kuyeyuka hata kwa moto mkubwa, madini ya chuma yanawahi kuyeyuka kabla ya Risasi, kadhalika madini haya yalitumika kwaajili ya maandishi, yalikuwa ni bora kwa kuhifadhi maandishi kwa muda mrefu, tofauti na mengine yote. (Ayubu 19:24).

Hivyo yalikuwa ni madini ya kibiashara sana enzi za zamani na hata sasa.. Nyakati hizi yamezidi matumizi mpaka kufikia kutengeneza vifaa vya kisilaha kama hizi risasi zinazotumika katika bunduki.

Katika biblia madini hayo yameonekana yakitajwa katika sehemu kadhaa..

Ezekieli 27:12 “Tarshishi alikuwa mfanya biashara kwako, kwa sababu ya wingi wa utajiri wa kila aina; kwa fedha, na chuma, na bati, na risasi, walifanya biashara, wapate vitu vyako vilivyouzwa”.

Unaweza kuyapata pia katika vitabu vifuatavyo… Hesabu 31:22, Yeremia 6:29 na Zekaria 5:7

Lakini katika roho sisi watu wa Mungu tunafananishwa na vitu hivyo vya thamani.. kama fedha, dhahabu, almasi n.k

Kama vile chuma na dhahabu ili viwe imara na ili ving’ae ni lazima vipitishwe kwenye moto, na watu wa Mungu waliookoka ili wawe wa thamani mbele za Mungu ni lazima wapitishwe kwenye moto (yaani majaribu mbali mbali).

Kadhalika ili risasi iwe bora ni lazima ipitishwe nayo kwenye moto.. Na sisi tunafananishwa na risasi za Bwana.. na matumizi makubwa ya risasi katika zama zetu hizi ni SILAHA, Kadhalika na sisi ni silaha za Bwana, dhidi ya majeshi yote ya adui..Ili tuwe imara hatuna budi kupitishwa katika moto.. Ndivyo maandiko yanavyosema…

Ezekieli 22:18 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli imekuwa taka za fedha kwangu; wote wamekuwa shaba, na bati, na chuma, NA RISASI, kati ya tanuu; wamekuwa taka za fedha.

19 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu ninyi nyote mmekuwa taka za fedha, tazama, nitawakusanya kati ya Yerusalemu.

20 Kama vile watu wakusanyavyo FEDHA, NA SHABA, NA CHUMA, NA RISASI, NA BATI, KATI YA TANUU, ILI KUVIFUKUTIA MOTO NA KUVIYEYUSHA; ndivyo nitakavyowakusanya ninyi katika hasira yangu, na ghadhabu yangu, nami nitawalaza huko, na kuwayeyusha.

21 Naam, nitawakusanya, na kuwafukutia moto wa ghadhabu yangu, nanyi mtayeyushwa kati yake”.

Je umempokea Yesu?.. je wewe ni dhahabu safi?, ni fedha safi?, ni Risasi safi kwa Bwana?.. kama bado unasubiri nini?..Unawezaje kuishi maisha ya namna hayo yasiyo na thamani yoyote mbele za Mungu..Mpokee Kristo leo, na ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, upate ondoleo la dhambi, na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, atakayekuongoza katika kweli yote.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?

APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

Fuawe ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 41:7

KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.

ONDOA TAKATAKA KATIKA FEDHA, NA CHOMBO KITATOKEA KWA MTAKASAJI.

Ufisadi una maanisha nini katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Fried-rich@son ofJESUS%
Fried-rich@son ofJESUS%
2 years ago

Amina mtume wa KRISTO, mafundisho ya NENO kama haya ndiyo yatazidi kutufanya tuwe na thamani mbele za BWANA YESU.

NURU yake izidi kutuangazia