YAPO MAJIRA YA KUONJWA NA BWANA.

YAPO MAJIRA YA KUONJWA NA BWANA.

Bwana alisema…

Zaburi 34:8

[8]Onjeni mwone ya kuwa BWANA yu mwema; 

Heri mtu yule anayemtumaini.

Maana yake ni kuwa Mungu ametoa nafasi kwa kila mtu ambaye yupo mbali na neema  kuonja au kujaribu kwanza uzuri ulioko ndani yake kabla hajauingia moja kwa moja..kwamfano kujaribu kungalia kama ndani ya Kristo kuna furaha, au amani, au upendo n.k.

Na pale mtu anapoona kuwa ipo basi anawajibika kumuishia Mungu maisha yake yote, lakini kama hajaiona basi anaruhusiwa kughahiri uamuzi wake..Na Ukweli ni kwamba hakuna aliyemjaribu Kristo akatamani kutoka baada ya hapo.

Lakini sio sisi tu tunaonja vya Mungu.. Mungu naye pia anayotabia ya kutuonja sisi auminifu wetu na uelekevu wetu kwake kama tunakidhi kweli vigezo vya yeye kutupa moja kwa moja kile tulichomuomba…au kutukaribia moja kwa moja milele.

Sasa hatua kama hii ukishafikia tambua kuwa unapaswa ung’ang’ane kweli kweli kwasababu huwa hakiwi kipindi cha raha sana.

Tukirudi kwenye biblia…tunaona wana wa Israeli walipotoka Misri, Mungu alikuwa nao karibu katika kiila hatua waliyopiga, walichokitaka walikipata wala hawakuachwa bila majibu..mpaka wanavuka bahari ya shamu wote wakawa wanamwimbia Mungu na kumchezea kwa shangwe kwa jinsi alivyowatendea miujiza mikubwa..Hivyo hilo likamvutia Mungu sana..Mungu akashawishika kushuka atembee nao milele katika furaha na raha..

Lakini kabla ya yeye kufanya vile ilimpasa kwanza AWAONJE..aone kama ni kweli wamekidhi vigezo vya yeye kuwa Mungu wao au la.

Hivyo alichofanya ni kuwaacha siku tatu kwa Kiu kule janwani pindi tu walipovuka bahari ya shamu, jambo ambalo hawajawahi kulipitia kabisa maisha yao yote tangu walipoanza kutembea na Mungu.. 

Tusome…

Kutoka 15:22-25

[22]Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.

[23]Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.

[24]Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?

[25]Naye akamlilia BWANA; BWANA akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, AKAWAONJA HUKO.

Unaona mstari wa 25 inasema Mungu akawaonja huko.kama kweli walimpenda kutoka moyoni au ni kwa miujiza tu..au kwa mikate tu..au kwa mafanikio tu..

Lakini tunaona wana wa Israeli walinung’unika badala ya kujinyenyekeza..Hivyo Mungu hakuona ukamilifu ndani yao.akajua kumbe walimpendea kwasababu walipata  raha tu lakini sio kwasababu ni Mungu wao..Laiti wangejinyenyeza ni wazi kuwa tangu ule wakati na kuendelea wasingekaa kusikia kitu kinachoitwa shida au taabu au masumbufu…

Ndugu yangu..Mungu akidhamiria kushuka kwako moja kwa moja kukaa na wewe au kukupa kitu fulani ulichomuomba ni sharti kwanza AKUONJE..uaminifu wako kama alivyofanya kwa Ibrahimu kumtoa mwanae Isaka..Hiyo ndio kanuni yake ambayo wana wa Israeli walishindwa kuielewa..

Soma pia Kumbukumbu 8:1-3 utaona Bwana akilisisitiza neno hilo hilo..

Hivyo ndugu uliyeokoka..lijue jambo hilo, liweke akiba moyoni mwako. Kabla hujawa rafiki wa Mungu wa milele ni sharti kwanza akuonje..ukikidhi vigezo basi ndio kimekuwa chako milele.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

BIRIKA LA SILOAMU.

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

UFUNUO: Mlango wa 14

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments