Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

JIBU: Saumu ni neno lenye asili ya lugha ya “kiaramu” lenye maana ya “kujizua kufanya jambo/kitu fulani kwa ajili ya ibada”.

Hivyo pale mtu anapoacha kula kwa kipindi fulani, kwa ajili ya sala..Mtu huyo yupo katika saumu.au kwa jina tulilolizoea tunasema yupo katika mfungo.

Neno hilo utalipata katika vifungu hivi kwenye biblia..

Zekaria 8:19

[19]BWANA wa majeshi asema hivi, Saumu ya mwezi wa nne, na saumu ya mwezi wa tano, na saumu ya mwezi wa saba, na saumu ya mwezi wa kumi, zitakuwa furaha na shangwe, na sikukuu za kuchangamkia, kwa nyumba ya Yuda; basi zipendeni kweli na amani.

Yoeli 1:14

[14]Takaseni saumu, iteni kusanyiko la dini, 

Wazee na wakusanye wenyeji wote wa nchi; Waende nyumbani kwa BWANA, Mungu wenu, Na kumlilia BWANA,

Soma pia Yoeli 2:15.utaliona neno hilo.

Saumu ya kweli ni ipi?

Lakini pia tofauti na wengi tunavyodhani..kwamba saumu inayompendeza Mungu ni ile ya chakula tu..ni kweli hiyo anaitazama lakini sio kiini cha saumu anayotaka kuiona ndani ya mtu.. Saumu anayoipokea ni ile ya kufunga vifungo vya uovu na dhambi.

Isaya 58:3-8

[3]Husema, Mbona tumefunga, lakini huoni? Mbona tumejitaabisha nafsi zetu, lakini huangalii? Fahamuni, siku ya kufunga kwenu mnatafuta anasa zenu wenyewe, na kuwalemea wote watendao kazi kwenu.

[4]Tazama, ninyi mwafunga mpate kushindana na kugombana, na kupiga kwa ngumi ya uovu. Hamfungi siku hii ya leo hata kuisikizisha sauti yenu juu.

[5]Je! Kufunga namna hii ni SAUMU niliyoichagua mimi? Je! Ni siku ya mtu kujitaabisha nafsi yake? Ni kuinama kichwa kama unyasi, na kutanda nguo za magunia na majivu chini yake? Je! Utasema ni siku ya kufunga, na ya kukubaliwa na BWANA?

[6]Je! Saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira?

[7]Je! Siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako, na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani kwako? Umwonapo mtu aliye uchi, umvike nguo; wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe?

[8]Ndipo nuru yako itakapopambazuka kama asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako itakutangulia; utukufu wa BWANA utakufuata nyuma ukulinde.

Umeona? Hivyo na wewe ufungapo basi fahamu kuwa Mungu anatazamia kuona mageuzi makubwa ya maisha yako dhidi ya dhambi na kutenda haki. Usifunge tu kidini ili kutumiza sheria.Funga kwa lengo la kuwa mkamilifu mbele zake.

Vinginevyo unaweza ukafunga hata siku 40 usiku na mchana bila kula, kama Musa na Mungu bado akaona unafanya kazi bure.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Mafundisho

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Fried-rich@son ofJESUS%
Fried-rich@son ofJESUS%
2 years ago

Amina

Mtumwa BWANA; nimeinuka kwelii kwa fundisho hili. Hakika ndio maana paulo akesema hv; kol3:16

BWANA AKUBARIKI&KUITUNZA HUDUMA HII SIKUZOTE!