Je Adamu na Hawa, walikuwa hawafanyi mema kabla ya kula tunda?

by Admin | 26 September 2021 08:46 pm09

SWALI: Ni mema gani na mabaya gani, Adamu na Hawa waliambiwa watayajua?, Kwasababu Kama ni mema siwalikuwa wanayafanya hapo kabla?


JIBU: Ili tuweze kuelewa vizuri, tujifunze katika mifano ya kawaida ya maisha.

Haiwezekani mtu kujijua kwamba yeye ni mrefu kama hajakutana na mtu mfupi katika maisha yake..

Yeye siku zote atajiona yupo kawaida tu..lakini siku atakapokutana na aliowazidi kimo ndipo atakapojijua kumbe yeye ni mrefu.

Kadhalika haiwezekani kujijua kama kwasasa una afya kama hujawahi kupitiaga kuumwa…zaidi ya yote hutajua hata maana ya kuwa na afya ni nini.

Lakini siku ile utakapougua na hamu yote ya kula kupotea, ndipo utakapojijua kuwa kumbe siku kadhaa nyuma ulikuwa ni mwenye afya sana.

Vile vile haiwezekani kujijua kuwa unatenda wema kama hujawahi kuujua ubaya…

Wewe utakuwa unaufanya tu! Na kuona kawaaida, Lakini hutajua kama unachofanya ni kitu chema…siku utakapokuja kuuona ubaya, ukifanywa na mwingine..ndipo utakapojua kuwa kumbe wewe ulikuwa mwema. N.k

Sasa hiyo ni mifano tu ya kimaisha,Sasa tukirudi pale Edeni,jambo ni lile lile, Adamu na Hawa walikuwa wanatenda mema lakini walikuwa hawajijui kama wanatenda mema, mpaka siku walipofanya ubaya na kuona madhara yake.

Ndio maana Mungu aliwakataza Adamu na Hawa wasile yale matunda, maana yake wasiujaribu ubaya…kwasababu siku watakapoujaribu ndipo watakapojijua kuwa kumbe siku kadhaa nyuma walikuwa katika mema.

Maana yake watajujua kumbe walikuwa katika utakatifu..

Hiyo ndio maana ule mti ukajulikana kama ni mti wa UJUZI WA MEMA NA MABAYA …Na si mti tu wa UJUZI WA MABAYA..hapana! bali mema na mabaya.. kwasababu mambo hayo mawili yanakwenda pamoja…hayaachani…

Kadhalika na sisi tunapokuwa dhambini tunakuwa tunajiona tupo sawa na njia zetu hizo, Hatujioni kama tupo hatarini, wala matatizoni, tunaona ni kawaida maisha ndivyo yalivyo..

Lakini siku tunapompokea Yesu, na kuonja Mema.. ndipo macho yetu yanafumbuliwa na kuelewa kwamba kumbe maisha tuliyokuwa tunaishi yalikuwa ni maisha mabaya, yalikuwa yana kasoro nyingi, yalikuwa ni ya mateso, yalikuwa ya tabu na hatari…lakini tulipokuwa huko dhambini tulikuwa hatulioni hilo..

Na YESU KRISTO, Ndiye ule MTI WA UZIMA.
Kwamba kila atakayeonja matunda ya mti ule hatatamani tena mabaya..na macho yake yatafumbuliwa, na kujitambua na hivyo kujitenga mbali na dhambi..

Adamu na Hawa walipokula na kujijua kuwa wapo dhambini walitamani kurudi, lakini walishindwa kwasababu njia ilifungwa.

Lakini sasa njia imefunguliwa, ipo wazi na njia hiyo si nyingine zaidi ya YESU KRISTO.
Ni kwasababu gani leo unaona ulevi unaoufanya ni kawaida?..ni kwasababu bado hujampokea Yesu na macho yako kufumbuliwa..siku utakapoocha kipawa cha Roho Mtakatifu ndipo utajiona kuwa hizo pombe zilikuwa ni sumu, huo uasherati ulikuwa ni kitanzi na wala hauna raha yoyote zaidi ni mateso..

Ndipo utakapojua kuwa kumbe maisha ya chuki, vinyongo na visasi yalikuwa ni maisha ya shida.

Bwana leo anatuita wote..na anasema tuonje!..Maana yake tujaribu kula matunda hayo ya mti wa uzima, tuone kama tutatamani kubaki dhambini.

Zaburi 34:8 “Onjeni mwone ya kuwa BWANA yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini”.

Je! Umempokea Kristo?

Kama bado mlango wa kutubu upo wazi sasa, lakini hautakuwa hivyo siku zote. Mpokee Yesu leo akutue mizigo na utapata raha ambayo hujawahi kuipata.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu”

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JINSI EDENI ILIVYOKUWA.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

JIFUNZE KUELEWA MAANA YA KUOA/KUOLEWA KABLA YA KUINGIA HUKO.

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/09/26/je-adamu-na-hawa-walikuwa-hawafanyi-mema-kabla-ya-kula-tunda/