Title September 2021

Kwanini Mungu aliwaita Adamu na Hawa jina moja?

SWALI: Kwanini katika Mwanzo 5:2 tunasoma Mungu aliwaita Adamu na Hawa jina moja la Adamu..na sio mawili tofauti.?

Mwanzo 5:2

[2]mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki akawaita jina lao Adamu, siku ile walipoumbwa.


JIBU: Kumbuka siku Mungu alipowaumba wanadamu(mwanamke na mwanamume)..hàkuwaumba wote kwa pamoja..Bali alimuumba ADAMU peke yake..kisha hawa baadaye..ambaye  alikuja kuumbwa kutoka katika ubavu wa Adamu.

Hivyo wakati Mungu anatoa majina kwa viumbe vyake Hawa hakuwepo..Jina hilo alikuja kupewa na Adamu mwenyewe baadaye soma..

Mwanzo 3:20

[20]Adamu akamwita mkewe jina lake Hawa; kwa kuwa yeye ndiye aliye mama yao wote walio hai.

Kwahiyo  kwanini Mungu aliwaita jina moja ni kwasababu alipomuona  Hawa alimuona Adamu kwasababu ni zao lake..hivyo machoni pake hakuona mwanamke anastahili kuitwa kitu kingine tofauti na jina la Mume wake ..Ni sawa na wewe uone ‘sisimizi’ huwezi wala huioni sababu ya kumuita sisimizi wa kike jina tofauti na yule wa kiume..wote utawaita tu jina moja sisimizi..na ndivyo ilivyokuwa machoni pa Mungu kwa Adamu na Hawa.

Lakini Mungu alitaka kutufundisha nini kwa kuwaita vile?

Ikiwa wewe ni mwanamke fahamu kuwa ukishaolewa, Mungu hakuoni tena kama ni mtu tofauti na mumeo. Atakutambua kwa jina lake. Hivyo jifunze kumtii mumeo. Kwasababu yeye ndio kila kitu kwako kwa muda huo.

Vilevile wewe kama mume..mpende mke wako, kwasababu ule ni ubavu wako. Na ndio maana haitwi jina lingine zaidi ya hilo la kwako. Hata kama utajaribu kumuita kwa majina mengine lakini Mungu anamtambua kwa hilo jina lako. Hivyo jifunze kumpenda na kumuhudumia. 

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Je Mungu aliumba watu wengine kabla ya Adamu?

Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.

Mafundisho

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Raheli aliiba miungu ya Baba yake, (Labani) Mwanzo 31:19.

Ni kwanini Raheli afanye vile, ilihali Mungu alikataza ibada za sanamu?.


Jibu: Tusome,

Mwanzo 31:18 “Akachukua wanyama wake wote, na mali yake yote aliyokuwa ameyapata, na wanyama aliowapata katika Padan-aramu, ili afike kwa Isaka babaye katika nchi ya Kanaani.

19 Basi Labani alikuwa amekwenda kuwakata manyoya kondoo zake, na Raheli akaviiba vinyago vya babaye”.

Lengo la Raheli kuiba vinyago vya baba yake si kwasababu alikuwa anataka kwenda kuviabudu (yaani kuvifanya miungu yake) kama baba yake alivyofanya..

Hapana bali lengo la kufanya vile ni ili akaviharibu. Kwasababu hivyo ndio vimekuwa chanzo cha matatizo yote, (Kati ya Labani na Yakobo).

Ikumbukwe kuwa Raheli ndiye aliyekuwa mke wa ahadi wa Yakobo, na mara ya kwanza kabisa aliahidiwa kumchukua kutoka kwa Baba yake Labani, baada ya kutumika kwa miaka 7, lakini tunaona baada ya miaka hiyo ya utumishi kuisha…Yakobo hakupewa Raheli badala yake aliozwa Lea dada yake.

Mwanzo 29:25 “Ikawa, kulipokuwa asubuhi, kumbe! Ni Lea. Akamwambia Labani, Nini hii uliyonitenda?

26 Sikukutumikia kwa Raheli? Mbona umenidanganya? Labani akasema, Havitendeki hivi kwetu, kumtoa mdogo kabla ya mkubwa”

Ukiendelea kusoma mbeleni utazidi kuona visa Labani alivyokuwa anamfanyia Yakobo, mpaka Labani kufikia hatua ya kutaka kumfilisi Yakobo mali zake.

Mwanzo 31:36-42
36 Yakobo akakasirika, akagombana na Labani. Yakobo akajibu, akamwambia Labani, N’nini hatia yangu? Nayo ni nini dhambi yangu, hata ukanifuatia namna hii?

37 Umepapasa-papasa vyombo vyangu vyote; ni kitu gani ulichokiona cha nyumbani mwako? Kiweke hapa mbele ya ndugu zangu, na ndugu zako, wakaamue kati yetu.

38 Miaka hii ishirini nimekaa kwako; kondoo zako wala mbuzi zako wake hawakuharibu mimba wala waume katika wanyama wako sikuwala.

39 Kilichoraruliwa na hayawani sikukuletea, mimi mwenyewe nimetwaa hasara yake, wewe umekidai katika mkono wangu, ikiwa kilichukuliwa mchana, au ikiwa kilichukuliwa usiku.

40 Hii ilikuwa hali yangu; mchana jua likanipata, na baridi usiku, usingizi ukanitoka machoni mwangu.

41 Miaka hii ishirini nimekaa nyumbani mwako; nilikutumikia miaka kumi na minne kwa binti zako wawili, na miaka sita kwa wanyama wako, nawe umebadili mshahara wangu mara kumi.

42 Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Ibrahimu na Hofu ya Isaka, hangalikuwa pamoja nami, hakika sasa ungalinifukuza mikono mitupu. Mateso yangu na kazi za mikono yangu Mungu ameziona, akakukemea usiku huu”.

Sasa kwa mambo kama hayo na mengine mengi ni wazi kuwa Raheli aliamini miungu ya baba yake ndio chanzo cha matatizo yote (Au ndiyo inayompelekesha yeye kuwa hivyo alivyo, au kutoa maamuzi anatoyatoa, ya kusumbua Yakobo).

Hivyo siku anaondoka yeye na Yakobo, Raheli aliiba ili kwamba baba yake asiitumie hiyo ikamwaribu akili na kusababisha madhara zaidi kwa Yakobo na kwake yeye Raheli. Hivyo ikawa msaada kwa Labani baba yake na Yakobo.

Hiyo ndio sababu (Ni ili amponye baba yake)..Endapobaba yake angeendelea navyo mbali na kumharibu akili, vingemsababishia kuadhibiwa na Mungu.
Kwasababu wote wanaoabudu miungu, hawafiki mbali.

Hivyo Raheli aliiba ili akaiharibu.
Ndio maana hata baada ya kuiiba alienda kuikalia (Mwanzo 31:34-35). Sasa kwa mtu mwenye lengo la kwenda kuiabudu asingeikalia, hakuna mtu anayeweza kukalia mungu wake..(hata wote wanaoabudu sanamu, huwa wanaziheshimu hizo sanamu zao)..hawawezi kuzikalia kwa lengo lolote lile.

Na baada ya hapo hatuoni, Labani akimfuatilia wala kumsumbua tena Yakobo.
Ikifundisha kuwa kuna mazingira tutawaokoa watu kwa kuwanyakua kutoka kwenye hatari..kama Raheli alivyofanya kwa Baba yake.

Yuda 1:2 “na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”.

Maran atha

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MTI UANGUKAPO, PAPO HAPO UTALALA.

Nifanye nini ili niishi maisha ya ushindi siku zote?

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

 

Rudi nyumbani

Print this post

Waanaki ni watu gani katika biblia?

Waanaki ni jamii ya watu wakubwa na warefu waliotoka katika uzao wa mtu mmoja anayeitwa Anaki mtoto wa arba (Yoshua  15:13, 21:11)..Maana halisi ya jina hilo kulingana na lugha ya kuyahudi ni ‘MTU MREFU’ au ‘MWENYE SHINGO NDEFU’.

Watu hawa waliishi upande wa kusini mwa Israeli,  walikuwa ni wakubwa sana na wenye nguvu kuliko watu wengine wa kawaida walioishi ulimwenguni wakati ule.. vilevile walikuwa na nguvu kubwa za kivita, hakuna taifa lililoweza kushindana nalo.

Habari zao utazisoma sehemu nyingi sana katika biblia..lakini hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowaelezea.

Kumbukumbu la Torati 1:28

[28]Twakwea kwenda wapi? Ndugu zetu wameiyeyusha mioyo yetu, wakituambia, Wale watu ni wengi, ni warefu kuliko sisi; miji nayo ni mikubwa, imejengewa kuta hata mbinguni; na zaidi ya hayo huko tumewaona Waanaki.

Kumbukumbu la Torati 9:1-3

[1]Sikiza, Ee Israeli; hivi leo unataka kuvuka Yordani uingie kwa kuwamiliki mataifa yaliyo makubwa, na yenye nguvu kukupita wewe, miji mikubwa iliyojengewa kuta hata mbinguni,

[2]watu wakubwa, warefu, wana wa Waanaki, uwajuao, uliokuwa ukisikia wakitajwa hivi, Ni nani awezaye kusimama mbele ya wana wa Anaki?

[3]Basi jua siku hii ya leo kuwa BWANA, Mungu wako, ndiye atanguliaye kuvuka mbele yako kama moto uteketezao; atawaangamiza, tena atawaangusha mbele yako; ndivyo utakavyowafukuza na kuwapoteza upesi, kama alivyokuambia BWANA.

Soma pia Kumbukumbu 2:11, 21, Yoshua 11:21, 22, 14:12, 15….utaona habari zao.

Sasa wayahudi kulingana na desturi zao wanaamini watu hawa chimbuko lao lilikuwa ni kutoka katika  ule uzao wa Wanefili (majitu) yaliyokuwepo kabla ya gharika kushushwa ulimwenguni (Mwanzo 6:4). Na ndio uzao ule ule uliokuja kuonekana hadi wakati wa mfalme Daudi (Yule Goliati)

Lakini kwanini Mungu aliruhusu watu hawa wawepo duniani?..kwanini asingeumba tu watu wote walingane?

Ni kuonyesha kuwa hata sasa rohoni wapo watu ambao ni majitu (wana wa anaki) karibu katika nyanja zote ya maisha..Na lengo lao ni kuweka vitisho tu na kuogopesha, lakini kama vile watu wa Mungu walivyoweza kuwashida kwa kumtegemea Bwana..vivyo hivyo na watakatifu wa sasa wanaweza kuwashinda kwa kumtegemea Bwana YESU katika mapito yao.

Unapoona mataifa makubwa yenye  nguvu kubwa yanakuja kupigana na wewe uliye taifa dogo huna haja ya kuogopa maadamu Bwana yuko pamoja na wewe.

Ikiwa watu wenye nguvu wamekuzunguka kuupinga wokovu wako..wewe kama mkristo huna haja ya kutikisika maadamu Bwana yupo upande wako.

Kumbuka alichokifanya kwa Waanaki wa Yeriko ndicho atakachokufanyia na wewe ambaye uliyemwamini Yesu Kristo. Lakini kama upo nje ya wokovu fahamu huna tumaini, twewe  utakuwa kama panzi kwa kila adui  atakayetokea mbele yako, kukupinga. Na mwisho wa siku utakuwa ni mtu wa kuchukuliwa mateka tu daima..Lakini ya nini yote hayo yakukute katika ulimwengu huu wa dhambi, ni heri ukampa Kristo maisha yako leo akuweke salama. Hizi ni siku za mwisho Yesu yupo mlangoni kurudi. Tubu dhambi zako kwa mumaanisha kuziacha umgeukie Yesu akusemehe. Kwasababu hakuna tumaini lolote nje ya Kristo.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MUNGU HAONI SHIDA KUMUHAKIKISHIA MWOVU ULINZI.

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

UZAO WA NYOKA.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

Shalom ni Raheli yupi aliyekuwa anawalilia watoto wake?, na Watoto hao ni wakina nani? Na kiliwatokea nini?.. (Yeremia 31:15 na Mathayo 2:18).

Jibu: Tusome,

Yeremia 31:15 “Bwana asema hivi, Sauti imesikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake; asikubali kufarijiwa kwa watoto wake, kwa kuwa hawako”

Katika Unabii huo kuna vitu viwili vya kuzingatia navyo ni “Rama” na “Raheli”..Tukianza na Raheli, huyu kama inavyojulikana alikuwa ni Mke wa Yakobo..Na ndiye mke wa ahadi ambaye Yakobo alimpenda kuliko wengine wote.

Na “Rama” ni mtaa uliokuwa ndani ya mji wa Bethlehemu, ambao tutakuja kuona mbele kidogo ulitumika wapi kutimiza unabii huo wa Yeremia.

Sasa Raheli mke wa Yakobo, ni mwanamke aliyekufa mapema kabla kabla ya kuona hata Baraka za watoto wake (Yusufu na Benyamini), Na alikufa akiwa katika uchungu wa kuzaa Benyamini….. Na maandiko yanasema alipokufa alizikwa katika mji wa Bethlehemu…ambao ndio ule ule mji aliokuja kuzaliwa Bwana Yesu, miaka mingi baadaye.

Mwanzo 35: 19 “Akafa Raheli, akazikwa katika njia ya Efrathi, ndio Bethlehemu”.

Kwahiyo kwasababu Raheli, alikuwa ni mwanamke aliyemcha Mungu kuliko wake wengine wote wa Yakobo, na ndiye aliyekuwa mke wa ahadi, na alikufa pasipo kuziona Baraka za wanawe..hivyo kwasababu yake yeye, pale mahali alipokufa na kuzikwa, Bwana alipatukuza kwa heshima yake, na kupafanya kuwa mji atakaokuja kuzaliwa mwokozi wa ulimwengu, Yesu Kristo, miaka mingi baadaye..

Mika 5:2 “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”.

Na pia Mathayo 2:6 inazungumzia jambo hilo hilo..

Mathayo 2:4 “Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?

5 Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,

6 Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli”.

Kwahiyo Bethlehemu ulipata hadhi hiyo na neema hiyo kufuatia huyu mke wa Yakobo (Raheli). Hivyo Raheli ndio akawa kama nembo ya mji wa Bethlehemu katika roho. Kama vile Daudi alivyokuwa nembo ya mji wa Yerusalemu.

Sasa tukirudi kwenye huo unabii wa Yeremia unaosema..

Yeremia 31:15 “Bwana asema hivi, Sauti imesikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake; asikubali kufarijiwa kwa watoto wake, kwa kuwa hawako”

Wakati Yeremia anatangaza maneno haya, tayari Raheli alikuwa ameshakufa miaka mingi sana na kuzikwa hapo Bethlehemu, lakini kuna tukio la kipekee lilitokea katika mji wake huo aliozikwa.. Kwani wakati Nebukadneza anaiteketeza Yerusalemu, kwa kuwaua watu kikatili, watoto kwa wazee, wanaume kwa wanawake..lilibakia kundi dogo ambalo halikuuawa, badala yake lilifungwa na kupelekwa Babeli utumwani.

Sasa kituo kilichotumika kuwakusanya hao mabaki machache ambayo hayajauawa, tayari kwa kupelekwa utumwani.. kilikuwa ni huo mtaa mdogo ulioutwa “RAMA”, hapo Bethlehemu katika mji huo wa Raheli. Na baada ya kukusanywa na kufungwa kwa siku kadhaa, ndipo wakaondolewa na kuanza safari ya kupelekwa utumwani Babeli..

Yeremia 40:1 “Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, baada ya wakati ule Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, ALIPOMWACHA AENDE ZAKE TOKA RAMA, baada ya kumchukua hali ya kufungwa minyororo, pamoja na wafungwa wote wa YERUSALEMU NA YUDA, WALIOCHUKULIWA HALI YA KUFUNGWA MPAKA BABELI”.

Wakati wanaondoka, ile ahadi ambayo Mungu aliiahidi pale Bethlehemu kwaajili ya Raheli, ikawa inamlilia Mungu katika roho, pale mabaki ya wana wa Israeli walipokuwa wanaondolewa…na ahadi ile, ndio kama “Sauti ya Raheli”…kama vile “sauti ya damu ya Habili ilivyokuwa inamlilia Bwana kutoka katika ardhi, baada ya Kaini ndugu yake kumuua (Soma Mwanzo 4:10) ”

Yeremia 31:15 “Bwana asema hivi, Sauti imesikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake; asikubali kufarijiwa kwa watoto wake, kwa kuwa hawako”

Lakini ukiendelea kusoma utaona Bwana anatoa faraja, kuwa watoto wake watarudi tena (maana yake Israeli watarudishwa tena katika nchi yao kama mwanzo, Yeremia 31:16-17).

Sasa hiyo ni sehemu ya kwanza ya unabii huo, kwani wakati ulipofika kweli Israeli walirudishwa katika nchi yao, baada ya ile miaka 70 waliokaa utumwani Babeli.

Lakini wakati wa Bwana Yesu kuzaliwa, kuna jambo lingine tena lilitokea kama hilo hilo..likafanya unabii huo kujirudia tena..

Bwana alivyozaliwa huko Bethlehemu Herode alitafuta kumuua, lakini alishindwa kwani Mariamu na Yusufu waliondoka pamoja na mtoto kwenda Misri..na kumfanya Herode akasirike na kwenda kufanya mauaji katika ule ule mji wa Raheli, (Bethlehemu), kwani alianza kuua watoto wote walio chini ya umri wa miaka miwili, na kufanya sauti ile ile ya Raheli irudi, kama ilivyosikika wakati wa kwanza Israeli wanachukuliwa utumwani..

Mathayo 2:16 “Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi.

17 NDIPO LILIPOTIMIA NENO LILILONENWA NA NABII YEREMIA, AKISEMA,

18 SAUTI ILISIKIWA RAMA, KILIO, NA MAOMBOLEZO MENGI, RAHELI AKIWALILIA WATOTO WAKE, ASIKUBALI KUFARIJIWA, KWA KUWA HAWAKO”.

Sasa endapo tukio hilo lingetokea mahali pengine, au kwenye mji mwingine kama Yerusalemu..pengine asingetajwa Raheli  tena, pengine ingekuwa  Daudi au mtu mwingine, lakini kwasababu ni Bethlehemu, hakuna budi awe Raheli aliyekuwa kama nembo ya mji ule.

Hiyo inatufundisha nini?

Unabii wa Mungu unaweza kutimia zaidi ya mara moja..Neno la Mungu halina tarehe ya kuisha matumizi (expire date). Hapo tunaona unabii mmoja umetimia vipindi viwili tofauti..Kadhalika na nabii nyingine zote, hazina mwisho wa muda wa matumizi..Kwa nafasi yako unaweza kusoma (Hosea 11:1 na Mathayo 2:15), utaona jinsi unabii mmoja unavyoweza kutimia vipindi viwili tofauti.

Biblia inaposema kutatokea mpinga-Kristo siku za mwisho..hatuna kufahamu kuwa hilo neno tayari linatimia sasa hata kabla ya kumfikia huyo mpinga kristo mmoja aliyetabiriwa, maana yake, wapinga-kristo wapo hata sasa…

1Yohana 2:18 “Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho”.

Vile vile unabii wa Yuda kumsaliti Bwana, uliotabiriwa katika Zaburi 41:9, haukutimia kwa Yuda tu, ukaishia pale, hapana!.. bali pia unaendelea kutimia mpaka sasa. Sio kwamba Yuda alikuwa na bahati mbaya sana kuliko sisi..wala unabii huo hakuandikiwa yeye peke yake. Na kwamba ulishatimia juu yake na hauwezi kujirudia tena..

 Nataka nikuambie katika siku zetu hizi za mwisho watakuwepo watu wenye hatia kubwa ya kumsaliti Bwana kuliko hata Yuda, na watakuwa wametimiza hilo andiko la Zaburi 41:9. Hivyo hatuna budi kuongeza umakini katika Ukristo wetu, ili tusiwe sehemu ya kutimiza maandiko mabaya bali yale mazuri.

Luka 13:1 “Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichanganya damu yao na dhabihu zao.

2 Akawajibu akawaambia, Je! Mwadhani ya kwamba Wagalilaya hao walikuwa wenye dhambi kuliko Wagalilaya wote, hata wakapatwa na mambo hayo?

3 Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.

4 Au wale kumi na wanane, walioangukiwa na mnara huko Siloamu, ukawaua, mwadhani ya kwamba wao walikuwa wakosaji kuliko watu wote waliokaa Yerusalemu?

5 Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo”.

Mwisho kama bado hujatubu na kumpokea Yesu, fahamu kuwa hizi ni siku za mwisho, na Kristo yupo mlangoni kurudi..jiulize akija leo, atakukuta katika hali gani?..je tumaini lako ni nini?..ni mali?, ni mke? ni watoto? Au ni nini?…Bwana mwenyewe alisema… “Itakufaidia nini upate kila kitu halafu upate hasara ya nafsi yako”?

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?

KUJIFUNUA KWA YESU KWA PILI.

KWANINI NI YESU KRISTO WA NAZARETI?

JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

Rudi nyumbani

Print this post

EPUKA KUPELELEZA KILA KITU MUNGU ANACHOKUAHIDIA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, nakukaribisha katika kuyatafakari maneno ya uzima ya Mungu wetu, Karibu sana.

Jambo ambalo tunapaswa tuwe makini nalo, ni kuchunguza chunguza au kupeleleza peleleza ahadi ambazo Mungu anatuahidia katika maisha yetu. Sio kwamba kupeleleza ni kubaya, hapana, lakini matokeo ya kufanya hivyo ni kuwa tutakayokutana nayo  yatakuja kinyume na matazamio yetu, na mwisho wa siku tukavunjika mioyo, na kupelekea hata kumuudhi Mungu, hadi kughahiri kutupa alichotuahidia.

Ili kulielewa hilo, tusome mfano mmoja wa wana wa Israeli, ambao tunajua wao walipotoka Misri, Mungu aliwaongoza jangwani kwa muda mfupi sana, sasa wakati wanakaribia kuingia katika ile nchi ya ahadi ambayo Mungu aliwaahidia kuwa ni nchi yenye kububujika maziwa na asali, wao hawakutulia kwenda na Mungu mpaka dakika ya mwisho, badala yake, wakataka kuharakisha mambo.

Hivyo walichokifanya ni kumwendea Musa, na kumwambia, awapelekee watu wakaipeleleze ile nchi, waone kama ni kweli Mungu alichowaahidia ndicho kilichopo au la. Kumbuka agizo hilo Mungu hakuwapa, bali ni wao wenyewe waliliwaza, na kumwambia Musa, baadaye Mungu ndio akawapa ruhusu kwa kumwagiza Musa awafanyie hivyo, lakini Mungu hakuliagizo hilo jambo,.

Sasa kama wengi tunavyojua habari, ni kweli waliona uzuri wa ile nchi, wakakiri kabisa ni nchi nzuri yenye kuvutia, lakini hakukuwa na uzuri tu peke yake, bali kulikuwa  pia na vitisho vingine vingi sana nyuma yake, hadi ule uzuri wote ukafunikwa na hayo mabaya..Mambo yakawa kinyume chake, wana wa Israeli badala ya kufurahia kwa wema waliouona wakaomboleza kwa mabaya, na misiba, na vifo walivyoviona mule, jinsi wale watu walivyowakubwa sana, wenye nguvu, wenye teknolojia ya hali ya juu, wenye silaha kubwa za kivita. Lakini jambo hilo likamuudhi sana Mungu, hadi akawaapia kuwa wote waliotoka Misri watakufa, hawataiona hiyo nchi,  isipokuwa Yoshua na Kalebu tu.

Wakamsababishia hadi na Musa naye kukasirikiwa na Mungu, na yeye pia akaambiwa atakufa.

Kumbukumbu 1:22 “Nanyi mkanikaribia kila mmoja wenu, mkasema, Na tupeleke watu mbele yetu, ili watupelelezee nchi na kutuletea habari za njia itupasayo kuipandia, na za miji tutakayoifikia.

23 Neno hili likanipendeza sana; nikatwaa watu kumi na wawili, mtu mmoja wa kila kabila.

24 Nao wakageuka, wakapanda mlimani wakafika bonde la Eshkoli, wakalipeleleza.

25 Wakatwaa baadhi ya matunda ya nchi ile mikononi mwao, wakatuletea huku chini, wakatuletea habari tena, wakasema, Nchi hii anayotupa Bwana, Mungu wetu, ni nchi njema.

26 Lakini hamkukubali kukwea huko, mlihalifu neno la Bwana, Mungu wenu;

27 mkanung’unika hemani mwenu, mkasema, Ni kwa sababu Bwana ametuchukia, ndipo akatutoa katika nchi ya Misri, apate kututia katika mikono ya Waamori, ili kutuangamiza.”;…………..

34 Bwana akaisikia sauti ya maneno yenu, akaghadhibika, akaapa, akasema,

35 Hakika yangu hapana mmoja miongoni mwa watu hawa wa kizazi hiki kibaya atakayeiona nchi hiyo nzuri, niliyowaapia baba zenu kuwapa,

36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, huyo ataiona; nami nitampa yeye na watoto wake nchi hiyo aliyoikanyaga; kwa kuwa amemfuata Bwana kwa kila neno.

37 NA BWANA ALINIKASIRIKIA MIMI KWA AJILI YENU, akasema, Wala wewe hutaingia humo;

Sasa hiyo yote ni kutufundisha kuwa,  Sio kwamba Mungu anachukizwa na sisi, kupeleleza ahadi alizotuahidia, lakini hatari yake ni kuwa, zipo katikati ya uharibifu. Mungu huwa anaficha Baraka zake, katika mazingira ya kushangaza sana,wakati mwingine katika vifungo, na dhiki, na magonjwa, na taabu, na mateso. Na ndio maana anataka watu wake sikuzote waishi kuwa imani ya kumtegemea yeye tu.

Embu mwangalie Yusufu, alionyeshwa kuwa ndugu zake watakuja kumwinamia, sasa kama angeishi kwa kudhani jambo hilo litatokea katika raha sikuzote ghafla bin vuu.. Hakuna  kuuzwa na ndugu zake, hakuna kufungwa kwenye magereza ya mfalme miaka ya kutosha, hakuna kuwa mtumwa  wa mtu mwingine kwa muda mrefu, angeshamwacha Mungu siku nyingi sana.

Vivyo hivyo na wewe, uliyeokoka, Ahadi zote na Baraka zote ambazo Mungu aliahidi kwa wateule wake wote waliomwamini, zitakuja tu kwa wakati wake, Pengine Mungu alikuonyesha atakutumia katika viwango vingine vya kiutumishi, au atakupatia vya mwilini kama vile, fedha, nyumba, mali, n.k. Usichunguze chunguze ni lini, usifikiri fikiri mema tu muda wote, kuwa  hapo katikati (Neutral), mtegemee Mungu katika kila hali, kwasababu unaweza kumbana leo na mikosi, ukadhani Mungu hayupo na wewe, kumbe ndio njia ya kuelekea maono yako.

Bwana atusaidie tujue kutembea katika kanuni zake za kiroho.

Mungu akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Kwanini Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wasikisaze chakula?

WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.

Kwanini Paulo aungane na wale watu wanne wenye nadhiri?

UFUNUO: Mlango wa 17

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post

Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani.

SWALI: Ni kwa jinsi gani Paulo aliwiwa na Wayunani na wasio Wayunani, wenye hekima na wasio na hekima? (Warumi 1:14).


JIBU: Labda tuanze kusoma kuanzia juu kidogo mstari wa 13.

Warumi 1:13 “Lakini, ndugu zangu, sipendi msiwe na habari, ya kuwa mara nyingi nalikusudia kuja kwenu, nikazuiliwa hata sasa, ili nipate kuwa na matunda kwenu ninyi pia kama nilivyo nayo katika Mataifa wengine.

14 Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani, nawiwa na wenye hekima na wasio na hekima.

15 Kwa hiyo, kwa upande wangu, mimi ni tayari kuihubiri Injili hata na kwenu ninyi mnaokaa Rumi”.

Awali ya yote ni vizuri kujua maan a ya neno kuwiwa.. Neno kuwiwa maana yake “kudaiwa”

Kwahiyo Mtume Paulo alikuwa anajaribu kueleza ni kwa jinsi gani, ana deni kubwa la kuhubiri injili kwa makundi ya watu mbalimbali.

Na baadhi ya makundi hayo ndio hayo aliyoyataja..ambayo ni Wayunani na Wasio wayunani.

Sasa wayunani kwa lugha nyingine Ndio Wagiriki.

Wagiriki ndio kundi la watu lililokuwa linajulikana kuwa na akili nyingi enzi za kale.

Hekima nyingi ziligunduliwa huko Ugiriki, watu kama Plato, na Alexander ambao tunawajua sana leo kama wana filosofia wakubwa, walitokea huko Ugiriki.

Kwahiyo ni watu waliokuwa na hekima na elimu kubwa sana, nyakati hizo.

Hiyo ikawafanya mambo mengi wanayoyasikia kutoyabeba bila kuyafanyia uchunguzi wa kutosha..Maana yake ni kwamba walikuwa wanashawishika sana na hoja zinazotumia akili na hekima nyingi..kuliko hata zinazotumia ishara..

Kwa maana ishara kama miujiza mtu anaweza kuitengeneza na kudanganya, lakini jambo lolote ambalo limechambuliwa kwa hoja nyingi zenye akili na mashiko ni ngumu kupotosha..Hivyo walikuwa ni watu wasioshawishika kwa miujiza..

Kwamfano ukiwafuata na kufanya muujiza na kisha kuwaambia Yesu ni mwana wa Mungu, pasipo kuwaelezea kwa kina na elimu ya kutosha, si rahisi kukuamini ijapokuwa umeitenda ishara mbele yao.

Lakini ukafika na kuwaeleza ni kwa kina, na kwa elimu ya kiMungu, ambayo ina mantiki ndani yake..na ina hekima kuliko wanachokijua na kukiamini..basi ni rahisi wao kukuamini hata bila kufanya muujiza wowote…

Wapo watu ambao wanahitaji kuona miujiza ili waamini kama Wayahudi ambao Bwana aliwasema katika….

Yohana 4:48 “Basi Yesu akamwambia, Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa?”

Na wapo watu ambao hawahitaji kuona muujiza ndipo waamini, bali wanachotaka ni kupata hekima kwa kile unachowapelekea ndipo waamini mfano wa hao ndio hawa Wayunani (Wagiriki).

1 Wakorintho 1:22 “Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wayunani wanatafuta hekima”

Kwahiyo tukirudi kwenye swali letu, ni kwa namna gani Mtume Paulo alikuwa anawiwa na Wayunani na wasio wayunani.

Jibu ni katika kuipeleka injili. Alikuwa na deni kubwa sana la kuwafikishia injili, na mara nyingi alipojaribu kwenda alikuwa anapitia vipingamizi vingi.

Na Paulo alikuwa anatumia akili nyingi ili kuwavuta watu kwa Kristo, alipofika kwa Wayahudi waliokuwa wanata ishara, alizitumia hizo ili kuwavuta kwa Kristo..

Kadhalika alipofika kwa Wayunani ambao walikuwa wanataka hekima, hakuitumia miujiza kuwavuta, bali alitumia elimu sana ili kuwavuta..

Hivyo alikuwa anageuka kulingana na aina ya watu aliokutana nao..

1 Wakorintho 9:19 “Maana, ingawa nimekuwa huru kwa watu wote, nalijifanya mtumwa wa wote, ili nipate watu wengi zaidi.

20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.

21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria.

22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.

23 Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.

24 Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate”.

Hiyo inatufundisha nini sisi wakristo?.
Na sisi pia tunawiwa injili na makundi yote ya watu, tunawiwa injili na maskini na Matajiri, wenye elimu na wasio na Elimu, watu wakuu na watu wanyonge.

Wapo wengi wanaohubiri kwa masikini tu, wakiamini kuwa matajiri hawawezi kuwasikia…

Wapo wanaohubiri kwa kwa watu watu wanyonge tu, wakiamini kuwa watu wakuu hawawezi kuwasikia.

Kumbe kiuhalisia ni wao ndio wamekosa hekima ya kuwaendea…sio kila mtu ataamini kwa kuona ishara ya pepo kutoka. Wengine huna kuanzia huko walipo, hicho wanachokiamini..ukaanza kukifafanua kwa hekima za Roho, ndipo aamini.

Lazima tumwombe Roho Mtakatifu hekima ya jinsi ya kuipeleka injili ili tuyapate makundi yote.

Kwa kumalizia hebu, tuangalie jinsi Paulo alivyowapata baadhi ya watu wa Athene, ambao ni Wayunani..wakati fulani alipokwenda katika nchi yao..

Matendo 17:16 “Paulo alipokuwa akiwangojea huko Athene na kuona jinsi mji ule ulivyojaa sanamu, roho yake ilichukizwa sana ndani yake.

17 Basi katika sinagogi akahojiana na Wayahudi na waliomcha Mungu, na wale waliokutana naye sokoni kila siku.

18 Na baadhi ya Waepikureo na Wastoiko, wenye ujuzi, wakakutana naye. Wengine wakasema, Mpuzi huyu anataka kusema nini? Wengine walisema,Anaonekana kuwa mtangaza habari za miungu migeni, kwa maana alikuwa akihubiri habari za Yesu na ufufuo.

19 Wakamshika, wakamchukua Areopago, wakisema, Je! Twaweza kujua maana ya elimu hii mpya unayoinena?

20 Kwa maana unaleta mambo mageni masikioni mwetu, tutapenda kujua, basi, maana ya mambo haya.

21 Kwa maana Waathene na wageni waliokaa huko walikuwa hawana nafasi kwa neno lo lote ila kutoa habari na kusikiliza habari za jambo jipya.

22 Paulo akasimama katikati ya Areopago, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini.

23 Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua.

24 Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo, yeye, kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika hekalu zilizojengwa kwa mikono;
[25]wala hatumikiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji kitu cho chote; kwa maana ndiye anayewapa wote uzima na pumzi na vitu vyote.

26 Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao;

27 ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.

28 Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi alivyosema, Maana sisi sote tu wazao wake.

29 Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu.

30 Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu.

31 Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu.

32 Basi waliposikia habari za ufufuo wa wafu wengine walifanya dhihaka; wengine wakasema, Tutakusikiliza tena katika habari hiyo.

33 Basi hivi Paulo akaondoka akawaacha.

34 Baadhi ya watu wakashikamana naye, wakaamini; katika hao alikuwamo Dionisio, Mwareopago, na mwanamke mmoja jina lake Damari, na watu wengine pamoja na hao.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habarihizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Mataifa ni nini katika Biblia?

KWANINI TUNAOMBA KWA JINA LA YESU?

Tofauti kati ya kuungama na kutubu ni ipi?

JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.

Tofauti kati ya Myunani, Farisayo na Sadukayo ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Watu wajikatao ni watu wa namna gani? (Wafilipi3:1).

Tusome,

Wafilipi 3:1 ‘Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana. Kuwaandikieni mambo yale yale hakuniudhi mimi, bali kutawafaa ninyi.

2 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na WAJIKATAO’’.

3 Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili’.

Watu wanaojikata wanaozungumziwa hapo ni watu wa ‘Tohara’.. Yaani watu wanaofanya tohara, na hao si wengine Zaidi ya wayahudi.. limetumika neno ‘wajikatao’ kufuatia kitendo chenyewe cha Tohara, ambacho kilihusisha KUKATA sehemu ya nyama ya mbele ya viungo vya uzazi vya wanaume..

Wayahudi hawa wajikatao waliwashurutisha watu wa Mataifa, waliomwamini Mwokozi Yesu, kuwa nao pia wanapaswa watahiriwe kama wao, kulingana na Torati. Na kwamba kama hawatatahiriwa basi Mungu hatawakubali. Ikiwa na maana kuwa kigezo cha mtu kukubali wana Mungu ni kufanyiwa tohara ya mwilini.

Jambo ambalo sio kweli kwa kipindi hichi cha agano jipya.. Katika agano jipya, tohara inayokubalika na Mungu si ya mwilini tena, bali ni ya rohoni, katika mioyo yetu, ambayo tohara hiyo ni UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU.

Roho Mtakatifu anapokuja ndani yetu, baada ya kumpokea Yesu na kutubu, anachofanya ni kuondoa sehemu ya uovu iliyoongezeka katika roho zetu, kama vile tohara ya mwilini inavyoondoa sehemu ya nyama iliyoongezeka…

Kadhalika Roho Mtakatifu anaondoa kiburi kilichoshikamanika na sisi tangu kuzaliwa, anaondoa uongo ulioshikamanika na sisi tangu kuzaliwa, anaondoa tamaa mbaya, na kila aina ya dhambi.. na kutufanya kuwa kiumbe kipya.

Kwahiyo kama vile katika Agano la kale mtu yeyote ambaye hakutahiriwa katika Mwili hakuwa mtu wa Mungu, kadhalika katika agano jipya mtu yeyote asiyetahiriwa katika roho, (maana yake asiye na Roho Mtakatifu), maandiko yanasema huyo sio wa Mungu.

Warumi 8:9 ‘Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, HUYO SI WAKE’.

Kwahiyo Mtume Paulo, aliwaonya wakristo ambao si wayahudi, kuwa Kutahiriwa katika mwili (yaani kujikata) si tiketi ya kukubaliwa na Mungu, Maana yake yule mtu aliyetahiriwa katika mwili na yule ambaye hajatahiriwa wote mbele za Mungu ni kitu kimoja…

Wagalatia 6:15 ‘Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya’.

Warumi 2:29 ‘bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko; ambaye sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu’.

Hiyo inatufundisha kuwa tujitahidi kwa hali na Mali kuzaliwa mara ya pili, kwasababu Bwana Yesu alisema, mtu yeyote asipozaliwa mara ya pili na kuwa kiumbe kipya hawezi kuuingia ufalme wa mbinguni.

Na kuzaliwa mara ya pili ni kumwamini Yesu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi kwa maji mengi na kwa jina la Yesu, na kupokea Roho Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Mlima wa Mizeituni  unaumuhimu gani kwetu?

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

JIBU: Andiko ambalo linaonyesha kutengwa kwa mwanamke anapotokwa na damu au anapokuwa katika siku zake ni hili;

Mambo ya Walawi 15:19-33

[19]Mwanamke ye yote, kama anatokwa na kitu, na kitu chake alichokuwa nacho mwilini mwake ni damu, ataketi katika kutengwa kwake muda wa siku saba; na mtu ye yote atakayemgusa atakuwa najisi hata jioni.

[20]Na kitu cho chote akilaliacho katika kutengwa kwake kitakuwa najisi; na kila kitu ambacho akiketia kitakuwa najisi.

[21]Mtu ye yote atakayekigusa kitanda chake huyo mwanamke atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.

[22]Mtu ye yote atakayekigusa cho chote ambacho huyo mwanamke amekiketia atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.

[23]Kwamba ni katika kitanda, au cho chote alichokikalia huyo mwanamke, atakapokigusa kitu hicho, atakuwa najisi hata jioni.

[24]Na mtu ye yote atakayelala na mwanamke na unajisi ukawa juu yake, atakuwa najisi muda wa siku saba; na kila kitanda alichokilalia kitakuwa najisi.

[25]Na mwanamke kama akitokwa na damu yake siku nyingi, nayo si katika majira ya kutengwa kwake, au kama anatoka damu kuzidi majira ya kutengwa kwake; siku hizo zote za kutoka damu ya unajisi wake, atakuwa kama alivyokuwa katika siku za kutengwa kwake; yeye yu najisi.

[26]Kila kitanda akilaliacho katika siku zote za kutoka damu kitakuwa kama kitanda cha kutengwa kwake; na kila kitu atakachokilalia kitakuwa najisi, kama unajisi wa kutengwa kwake.

[27]Na mtu ye yote atakayevigusa vitu vile atakuwa najisi, naye atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.

[28]Lakini huyo mwanamke kwamba ametakaswa na kule kutoka damu kwake, ndipo atakapojihesabia siku saba, na baadaye atakuwa safi.

[29]Siku ya nane atajipatia hua wawili, au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani, mlangoni pa hema ya kukutania.

[30]Kuhani atamsongeza mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za BWANA, kwa ajili ya kutoka damu ya unajisi kwake.

[31]Ni hivi mtakavyowatenga wana wa Israeli na unajisi wao; ili wasife katika unajisi wao, hapo watakapoitia unajisi maskani yangu iliyo katikati yao.

[32]Hii ndiyo sheria ya mwenye kisonono, na ya mtu ambaye shahawa yake yamtoka, akawa na unajisi kwa hiyo;

[33]na ya mwanamke ambaye yu katika kutengwa kwake, na ya mtu ambaye ana kisonono, kama ni mtu mume, kama ni mtu mke, na ya huyo alalaye na mwanamke mwenye unajisi.

Kumbuka tunapaswa tujue kuwa si kila  jambo ambalo lilitendeka agano la kale, linatendeka vilevile hadi wakati wa agano jipya..mambo mengi yalikuwa ni kama kivuli tu kuwasilisha ujumbe wa rohoni kwa agano letu jipya…kwamfano kwenye suala la chakula utaona Bwana alikuja kurekebisha akasema kimwingiacho mtu hakimtii unajisi bali kumtokacho mtu kwasababu kinamtoka moyoni..hivyo chakula kwa namna yoyote hakiwezi kumfanya mtu amkosee Mungu kikilika kwa shukrani..lakini zamani kwamfano wanyama ambao walikuwa hawacheui(yaani hawawezi kurudisha tena chakula wanapokimeza) walijulikana kuwa ni najisi ikifunulia kuwa kwasasa rohoni wapo watu najisi ambao hawana tabia ya kucheua chakula cha kiroho wanacholishwa..yaani hawana muda wa kuyatafakari ya nyuma waliyofundishwa au waliyofanyiwa na Mungu,  Au kutendea kazi yale waliofundishwa.

Vivyo hivyo na suala la wanawake katika siku zao kwa kawaida damu kama damu haina shida lakini jiulize kwanini hiyo inayotoka katika viungo vya uzazi ilionekana ina unajisi..Hiyo ni kufunua kuwa uchafu unazoalika kutokana na zinaa ni unajisi mkubwa sana kwa mtu.

 Na ndio maana biblia inasema na malazi yawe safi.. (Waebrania 13:4)

Tunapaswa tuitunze miili yetu mbali na uasherati

Lakini haimaanishi kuwa ukitokwa na damu, wewe tayari ni najisi hapana kwasababu lile ni tendo linalokuja lenyewe halipangwi na mwanamke. Hivyo halimtoki rohoni mpaka likamtia mtu unajisi..Mungu alitumia mfano ule tu kuonyesha jinsi mambo yatokayo kule yasivyofaa(katika uzinzi)… Kwahiyo mwanamke akitokwa na damu au asipotokwa na damu hakumzuii yeye kumwomba Mungu wake au kumtumikia madhabahuni pake..

Anachopaswa kufanya ni kujiweka tu katika mazingira ya usafi na uangalifu.

Bwana akubariki.

Mada nyinginezo:

MATARAJIO YA KILA MWANADAMU DUNIANI NI YAPI?

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

UFUNUO: Mlango wa 17

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Rudi Nyumbani

Print this post

Katika biblia Madhehebu ya Wanazorayo yalikuwaje? (Matendo 24:5)

Tusome

Matendo 24:5 “Kwa maana tumemwona mtu huyu mkorofi, mwanzilishi wa fitina katika Wayahudi wote duniani, tena ni kichwa cha madhehebu ya Wanazorayo”.

Katika biblia kipindi ambacho Bwana Yesu yupo ulimwenguni, yalikuwepo madhehebu makuu mawili katikati ya wayahudi ambayo ni Mafarisayo na Masadukayo.

Matendo 5:17 “Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu,”

Tusome pia..

Matendo 15:5 “Lakini baadhi ya madhehebu ya Mafarisayo walioamini wakasimama wakisema, Ni lazima kuwatahiri na kuwaagiza kuishika torati ya Musa”.

Hayo ndiyo madhehebu mawili makuu, na yote yalikuwa yanaamini katika torati ya Musa, tofauti ilikuwa ni katika kuamini kiama..Mafarisayo waliamini kuna ufufuo lakini Masadukayo walikuwa hawaamini hayo.

Lakini baada ya Bwana kuondoka lilizaliwa dhehebu lingine ambalo nalo liliamini katika torati ya Musa, lakini lilienda mbele zaidi kuamini kuwa Yesu aliyetokea Nazareti ndiye Masihi.

Hivyo dhehebu hilo likaitwa dhehebu la Wanazorayo…kufuatia mji wa Nazareti ambao Bwana alilelewa…na yeyote aliyeishi Nazareti aliitwa mnazorayo..

Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo.”

Lakini je! madhehebu hayo yote, yalifanikiwa kumjua Kristo? 

Ukweli ni kwamba mitume wa Bwana Yesu, hawakuwa wafuasi wa madhehebu yoyote ya kidini yaliyokuwa wakati ule. Wala siku ile ya Pentekoste Roho Mtakatifu hakutua, katika mojawapo ya madhehebu hayo.

Bali alitua juu ya watu waliokuwa wamefanyika wanafunzi wa Bwana Yesu, sio kwa dini bali kwa kusikia na kuyatenda yote aliyoyafundisha. Hata sasa ndivyo Roho Mtakatifu anavyofanya juu ya watu.

Hatui kwenye madhehebu ya kidini, bali kwa watu waliomtii Kristo kwa kutubu dhambi zao.

Je umempokea Yesu maishani mwako na kujazwa Roho Mtakatifu?..kama bado hujampokea ni heri ukafanya hivyo sasa maana muda uliobakia ni mchache sana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.

Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

KWANINI NI YESU KRISTO WA NAZARETI?

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

Kwanini wakristo walipomuona Petro akigonga walisema “Ni malaika wake”?

JE CHANJO YA KORONA NI ALAMA YA MNYAMA?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini wakristo walipomuona Petro akigonga walisema “Ni malaika wake”?

SWALI: Kwanini wakristo wa kwanza waliposikia kuwa Petro kafunguliwa hawakuamini badala yake walitumia neno “Ni malaika wake”..kwanini wawaze vile au waseme vile?


JIBU: Tusome.

Matendo ya Mitume 12:11-17

[11]Hata Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi.

[12]Na alipokuwa akifikiri haya akafika nyumbani kwa Mariamu, mamaye Yohana, ambaye jina lake la pili ni Marko; na watu wengi walikuwa wamekutana humo wakiomba.

[13]Naye alipobisha kilango cha lango, kijakazi, jina lake Roda, akaja kusikiliza.

[14]Alipoitambua sauti ya Petro, hakukifungua lango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani akawaambia kwamba Petro anasimama mbele ya lango.

[15]Wakamwambia, Una wazimu. Lakini yeye akakaza sana, akasema ya kwamba ndivyo hivyo. WAKANENA,  NI MALAIKA WAKE.

[16]Petro akafuliza kugonga, hata walipokwisha kumfungulia wakamwona, wakastaajabu.

[17]Naye akawapungia mkono wanyamaze, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa katika gereza. Akasema, Kampasheni Yakobo na wale ndugu habari hizi. Akaondoka, akaenda mahali pengine.

Wayahudi tangu zamani hadi sasa wanaamini kuwa kila mtu anaye malaika mlinzi..Na malaika hawa wanaweza kuja katika maumbile tofauti tofauti..wanaweza kuja kwa sura ya mtu mwingine au kwa sura au sauti  ya yule mtu anayemlinda.

Vilevile tunaweza kulithibitisha hilo pia katika maneno ya Bwana aliyoyasema katika (Mathayo 18:10) Kwamba wapo malaika wanaosimama kwa ajili ya watu tangu wakiwa wadogo.

Sasa kulingana na hiyo habari ni kuwa Roda aliposikia sauti ya Petro, .hakuhangaika kuhakikisha kwamba yeye anayegonga ni Petro au la! bali aliamini moja kwa moja na kwenda kutoa taarifa ..Lakini alipowapelekea habari wale waliokuwa ndani haikuwa rahisi kwao kuamini moja kwa moja kama yule angeweza kuwa Petro. Kwasababu kutokana na mazingira Petro aliyofungiwa, ni ngumu kutoka kwani alikamatwa kwa amri ya mfalme, na vilevile alikuwa chini askari 16.

Hivyo jambo ambalo wangeweza kudhani ni kuwa malaika wake ndio amekuja kwa maumbile ya Petro au pengine kwa umbile lingine isipokuwa katumia sauti ya Petro labda kuwafariji au kuwapa taarifa juu ya kifo  chake.

Lakini  walipoona Petro anazidi kugonga mlango wakaenda kumfungulia, wakathibitisha kuwa kumbe alikuwa ni Petro na sio malaika wake.

Ni nini tunaweza kujifunza katika habari hiyo?

Ni karama ya Mungu kuwatuma malaika zake kutuhudumia.Lakini malaika hawa hawamuhudumii kila mtu tu ilimradi hapana bali ni watakatifu tu..ikiwa na maana kama wewe ni mwovu ujue kinachokulinda ni rehema za Mungu tu ili uendelee kuishi, lakini hakuna huduma yoyote unayoweza kupokea kutoka kwa malaika zake. Kinyume chake ni kuwa mapepo ndio walinzi wako.

Na ndio maana huwezi kuishi maisha ya raha au ya amani hata kama unazopesa zote ulimwenguni..ni kwasababu ufalme wa Mungu haupo wala hautembei pamoja na wewe. Ni heri ukatubu leo ukamkabidhi Yesu maisha yako. Naye atakuokoa na kuuleta ufalme wake wa mbinguni kutembea pamoja na wewe. Hapo ndipo utakapoona tofauti yako ya jana ambayo hukuokoka na leo ambayo umeokoka.

Na wokovu unakuja kwanza kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha na pili ni kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo na kupokea Roho Mtakatifu.

Hivyo kama utapenda kumpokea Kristo leo basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo wa kiroho bure. Kumbuka saa ya wokovu ni sasa na wakati uliokubalika ni leo.

+255693036618/ +255789001312

Bwana akubariki

Mada Nyinginezo 

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

TUSIRUHUSU MAMBO YA KUSUBIRISHA, YAVURUGE MUDA WETU NA MUNGU.

Mafundisho

Rudi Nyumbani:

Print this post