Nini maana ya “Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai?

Nini maana ya “Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai?

SWALI: Shalom naomba kufahamu maana ya huu mstari..

Luka 17:37 “Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai”.


JIBU: Kabla ya wanafunzi wa Yesu kumuuliza Bwana hilo swali “WAPI?”..Kuna maneno ambayo yalitangulia juu kidogo, ambayo tukiyasoma yatatusaidia kuelewa vizuri huo mstari ulimaanisha nini, embu tusome kidogo.

Luka 17:22 “Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione.

23 Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate”;

Ukisoma kwenye Mathayo imeeleza kwa undani zaidi, inasema..

Mathayo 24:23 “Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki.

24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.

25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.

26 Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki”.

Maneno hayo Yesu aliyatanguliza kama angalizo la nyakati za hatari zitakazotokea siku za mwisho, akiwaonya kwamba wengi watakuja wakiwavuta watu kwao wakiwaambia Kristo yupo huku au kule, kwa maneno yao ya ushawishi, wakijinadi, tuna hichi au kile, sisi tuna miujiza mikubwa, sisi tuna upako wa mafuta mabichi, sisi ni wataalumu wa tiba za kiroho, sisi tuna makanisa makubwa kuliko yote duniani n.k.

Hivyo Yesu kwa kulijua hilo kwamba litakuja kutokea akawapa tahadhari wanafunzi wake kwamba wasitoke kuwafuata, wasiwe wepesi kuwaendea, wabaki mahali walipo, wasiende popote, kwasababu watawapotosha..

Sasa katika mazingira hayo ya kutokwenda mahali popote ndipo wanafunzi wake mwishoni wakamuuliza swali, NI WAPI sasa patakuwa sahihi pa kwenda..au tutakwenda wapi?

Ndipo Yesu akawaambia palipo na mzoga ndipo watakaposanyika Tai.. Ikiwa na maana mahali palipo na chakula cha Tai ndipo watakapokuja hapo na kukusanyika..

Na kama tunavyojua ndege aina ya tai wanaouwezo wa kuona mbali sana, leo hii kama kuna mnyama kafa porini na angani hakuna ndege yoyote, ukikaa baada ya muda mfupi utawaona tai wengi wamekusanyika hapo.. utajiuliza wametokea wapi na wakati anga lilikuwa jeupe halina ndege hata mmoja? Ni kwasababu jicho la Tai huwa linaona chakula kutokea mbali sana. Tai anaona mahali ambapo wewe huwezi kumwona.

Ni kama tu vile, mahali Fulani pawe na kinyesi cha mnyama au mtu, dakika si nyingi utaona nzi wengi wamekusanyika, na utajiuliza wametoka wapi wadudu hao na mahali hapo ni porini..Jibu ni kwamba, Mungu kawaumbia uwezo mkubwa wa kunusa vitu vya asili yao, tokea mbali, na ndio maana utawaona hata kama eneo hilo limejificha namna gani, wataenda tu.

Vivyo hivyo na wana tai wa Mungu, Kristo kawawekea uwezo Fulani wa kujua chakula chao halisi kilipo haijalishi ni wapi walipo watakipata tu. Tai si kama kuku, ambaye anaona vya hapo chini tu, bali Tai anaona vya mbali sana. Vivyo hivyo na sisi kama ni wanatai, ni lazima tuwe wa kufuata kile chakula kilicho chetu tu..Si kila chakula cha kukikurupukia kisa kipo karibu na sisi, au kinavutia..

Bali tuwe na macho ya tai ya kujua chakula chetu kipo wapi..

Hizi siku za mwisho, usiwe wa kukurupukia kila aina ya mafundisho, au imani. Kristo ameshatuonya..

Tafuta chakula cha wakati wako unaoishi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
1 year ago

AMEN..

Mch mass kavumbi
Mch mass kavumbi
1 year ago

Leo tunatafakari neno toka MATHAYO 24:24-27

Anonymous
Anonymous
2 years ago

Amen mtumishi. Ubarikiwe Sana.