Je! ni sahihi kwa mkristo kujifukiza?

Je! ni sahihi kwa mkristo kujifukiza?

SWALI: Nina swali mtumishi. Je mkristo aweza kujifukiza katika kipindi hiki cha changamoto za kupumua. Biblia inasema nini juu ya hili. Je, neno hili kwenye Ayubu 5:3 inazuia kujifukizia?

Ayubu 5:3 “Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi; Lakini mara niliyalaani maskani yake”.

JIBU: Kujifukiza ni tiba mojawapo kama zilivyo tiba nyingine. Mtu mmoja anaweza kuumwa na akaenda kumeza dawa za hospitalini, na mwingine akaenda kuchemsha mwarobaini akanywa. Na wote wakawa wazima.

Jambo ambalo si sahihi, ni pale tiba hiyo inapotolewa “sadaka kwa sanamu” nikiwa na maana kuwa pale inapohusianishwa na uganga au Imani potofu ambazo mara nyingi zinaambatanisha na masharti Fulani ambayo hata hayana uhusiano wowote na hiyo dawa kwamfano labda utaambiwa unywapo sema maneno Fulani, au nenda kainywee makaburini, au usinywe mbele ya watoto wako, au unyapo hakikisha upo uchi n.k… Sasa hizo ndio Mungu amekataza kwasababu ni ibada za sanamu.

Lakini tukirudi kwenye huo Mstari wa Ayubu 5:3 haizungumzii mizizi hii tunayoifahamu kama dawa, hapana, bali habari hiyo inazungumzia jambo lingine kabisa jinsi wenye dhambi wanavyoweza kujiimarisha kiasi cha kukita mizizi chini, wakijiwekea hazina nyingi, na kujijengea maboma makubwa, lakini hata hivyo, Mungu atawalaani na kuziangamiza maskani zao. Ukianzia kusoma tokea mistari ya juu utapata picha kamili ya habari hiyo.

Hivyo, kwa mkristo kujivukiza, si makosa, lakini pia ni vizuri tukajua sababu ya magonjwa haya kulipuka ni nini. Mungu hajayaleta ili tuyatafutie tiba hapana, Bali haya ni mapigo kutoka kwa Mungu na hilo lipo wazi yanayotutambulisha kuwa sisi kama dunia tumemsahau yeye, na pia  tunaishi katika siku za mwisho sawasawa na maneno ya Yesu katika , (Luka 21:11).

Swali ni je! Umeokoka? Je Yesu yupo ndani yako? Kama jibu ni hapana, basi ujue upo katika wakati wa hatari sana. Na wewe upo ndani ya hiyo hiyo ghadhabu ya Mungu iliyoachiliwa wakati huu tunaoishi, Hivyo fanya uamuzi wa busara, mkaribishe Yesu maishani mwako katika dakika hizi za majeruhi tunazoishi, Kabla mabaya hayajakufikia.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/je-ni-vema-kwa-mkristo-kwenda-hospitali-au-kutumia-miti-shamba-anapougua/

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments