Category Archive Home

Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Swali: Katika 1Nyakati 21:5 tunasona waliohesabiwa kwa Israeli na Yuda jumla ni  askari 1,570,000 lakini tukirudi  katika 2Samweli 24:9 tunaona jumla ya  idadi ya askari waliohesabiwa walikuwa ni 1,300,000 kwa Yuda na Israeli, je biblia inajichanganya?.

Jibu: Turejee,

1Nyakati 21:5 “Naye Yoabu akamtolea Daudi jumla ya hesabu ya watu. Na hao wote wa Israeli walikuwa watu elfu mara elfu, na mia elfu, wenye kufuta panga; na wa Yuda watu mia nne na sabini elfu, wenye kufuta panga”.

Tusome tena…

2Samweli 24:8 “Nao walipokwisha kuzunguka nchi yote, wakaja Yerusalemu mwisho wa miezi kenda na siku ishirini. 

9 Naye Yoabu akamtolea mfalme jumla ya hesabu ya watu; nao walikuwa wa Israeli mashujaa wenye kufuta panga mia nane elfu; nao wa Yuda walikuwa watu mia tano elfu”.

Ni kweli katika mistari hii miwili, panaonyesha tofauti ya Askari waliohesabiwa, tunaona kitabu kimoja kinataja idadi ya juu sana, na kingine kinataja idadi ya chini, sasa swali ni je biblia inajichanganya?

Jibu ni la! Biblia haijichanganyi kwasababu ni kitabu kilichovuviwa na Roho Mtakatifu. Fahamu zetu zinaweza kujichanganya katika kuielewa biblia  lakini kamwe biblia haijawahi kujichanganya, hususani panapotokea habari moja kunukuliwa na waandishi wawili tofauti, kwasababu kama biblia itakuwa na makosa sehemu yoyote, basi kitabu kizima kitakuwa na mapungufu na hivyo hakiwezi kuwa kitabu kitakatifu.

Lakini mpaka Roho Mtakatifu aruhusu kidumu kwa nyakati zote na vizazi vyote ni wazi kuwa biblia yenye vitabu 66 ni maandishi matakatifu na ya kuaminiwa asilimia 100, kwaajili ya maarifa sahihi ya kiMungu, na haina makosa yoyote.

Sasa tukirudi katika hiyo habari tunayoisoma katika vitabu hivyo viwili (1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9) kila mwandishi alijaribu kunukuu aina ya askari waliohesabiwa..

Mwandishi wa kwanza wa kitabu cha 2Samweli 24:9 alinukuu idadi ya Askari ambao walikuwa ni MASHUJAA TU! Ambao idadi yao ilikuwa ni hiyo 1,300,000 Na Mwandishi wa pili wa kitabu cha 1Nyakati 21:5 alinukuu idadi ya Askari wote kwa ujumla (Waliokuwa mashujaa na wasio mashujaa)..ndio maana utaona idadi imeongezeka mpaka kufikia hiyo 1,570,000. Kwahiyo biblia haijichanganyi.

Ilikuwepo tofauti ya Askari wa kawaida na waliokuwa Mashujaa, waliokuwa mashujaa na wale waliokuwa wakongwe na wazoefu katika vita wenye uwezo mkubwa wa kupambana, kwamfano utaona Mfalme Uzia biblia inaonyesha alikuwa na Askari wa kawaida na waliokuwa mashujaa, waliozoea vita, wepesi na hodari wa vita.

2Nyakati 26:11 “Zaidi ya hayo Uzia alikuwa na jeshi la watu wa kupigana, waliokwenda vitani vikosi vikosi, sawasawa na hesabu walivyohesabiwa na Yeieli mwandishi, na Maaseya msimamizi, chini ya mkono wa Hanania, mmojawapo wa maakida wa mfalme. 

12 Hesabu yote ya wakuu wa nyumba za mababa, WATU MASHUJAA, ILIKUWA ELFU MBILI NA MIA SITA.

13 Na chini ya mkono wao kulikuwa na jeshi la askari, mia tatu na saba elfu, na mia tano, ambao walipigana vita kwa nguvu nyingi, kumsaidia mfalme juu ya adui”.

Je unaliamini Neno la Mungu?

Je unajua Bwana Yesu alisema kuwa ”Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni (Mathayo 7:19 )??”

Je ni matunda gani unayozaa?..Mazuri au mabaya..

Mathayo 7:17 “Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.

18  Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.

19  Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni”

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

USIZITEGEMEE NGUVU ZAKO KUKUSAIDIA!

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kanaani ililaaniwa (Mwanzo 9:20-25,) kwanini Mungu awapeleke wana wa Israeli katika nchi iliyolaaniwa?

Jibu: Turejee,

Mwanzo 9:20 “Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;

21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.

22 Hamu, BABA WA KANAANI, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. 

23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao. 

24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.

25 Akasema, NA ALAANIWE KAANANI; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake”.

Kumbuka hapo kwanza “Kaanani” halikuwa jina la Nchi, bali lilikuwa ni jina la ‘Mtu’. Na mtu huyo alikuwa ni mtoto wa nne (4) wa Hamu..

Mwanzo 10: 6 “Na wana wa Hamu ni Kushi, na Misri, na Putu, na Kanaani”.

Hatujui kwa undani mtoto huyu (Kanaani) alikuwa na tabia gani?..lakini ni wazi kuwa matendo yake yalikuwa kama ya baba yake Hamu, ndio maana akabeba laana ya moja kwa moja ya baba yake.

Sasa huyu Kanaani ndiye aliyelaaniwa na baadaye alikuja kuzaa watoto na uzao wake ukaitwa Uzao wa Kanaani, kufuatia jina la Baba yao, na walipotawanyika usoni pa nchi yote katika ule utawanyiko wa Babeli (Mwanzo 11:8-9) ndipo wakaenda kuishi mahali wana wa Israeli walipowakuta.

Kipindi wanaishi, ardhi ile ilijulikana kama nchi ya Wakanaani. Na kilichokuwa kimelaaniwa na Mungu si ile ardhi/nchi bali ni watu, (ambao ndio hao wakaanani)..ikiwa na maana kuwa hata kama wasingeishi katika ile ardhi na kwenda kuishi katika ardhi nyingine bado wangekuwa chini ya laana.

Kwahiyo wana wa Israeli wakati wanatoka Misri, Mungu aliwatoa Wakanaani kwenye ile ardhi na kuwaweka wana wa Israeli, kwasababu kilicholaaniwa katika Mwanzo 9:5 si ardhi bali ni watu, hivyo watu wanaweza kuondolewa na ardhi ikaendelea kutumika na wengine na ikawa nchi ya Baraka tu, ndio maana baada ya pale haikuitwa tena nchi ya wakanaani bali nchi ya Israeli.

Lakini swali ni je! Hawa Wana wa Hamu mpaka leo wamelaaniwa?.. Maana miongoni mwao kuna Kushi ambaye uzao wake ni watu weusi.

Jibu ni la! Kristo alikuja kuondoa laana zote pale Kalvari, na hivyo hakuna tofauti ya Myahudi na Mmisri, Mkushi na mwisraeli, mbele za Mungu… kama tumeokoka wote tunahesabiwa sawa mbele zake. Lakini kama hatutazaliwa mara ya pili kwa maji na kwa roho wote mbele zake ni kama tuliolaaniwa.

Wakolosai 3:10 “mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.

11  Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala mshenzi, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote”.

Waefeso 2:16  “Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba”

Je umezaliwa mara ya pili?..

Yohana 3:3  “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

4  Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5  Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu”.

Bwana Yesu anarudi!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Wakaanani walikuwa ni watu gani?

TUMEFANYA KAZI YA KUCHOSHA USIKU KUCHA.

NI KWANINI WATU WENGI WANASHINDWA KUMWELEWA MUNGU?

Moabu ni nchi gani kwasasa?

Je ni kweli Isaka alifarijika kwa kifo cha mamaye? (Mwanzo 24:67).

Rudi nyumbani

Print this post

Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule(Kutoka 12:4)

SWALI: Bwana yesu apewe sifa, Naomba kufahamu, Kwanini Wana wa Israeli walimuhifadhi mwana-kondoo siku nne kabla ya kuchinjwa katika sikukuu ya pasaka.Je Kuna ufunuo gani tunaweza kupata katika Tendo hilo (Kutoka 12:6)


JIBU: Tusome..

Kutoka 12:3-7

[3]Semeni na mkutano wote wa Israeli, mkawaambie, Siku ya kumi ya mwezi huu kila mtu atatwaa mwana-kondoo, kwa hesabu ya nyumba ya baba zao, mwana-kondoo kwa watu wa nyumba moja;

[4]na ikiwa watu wa nyumba ni wachache kwa mwana-kondoo, basi yeye na jirani yake aliye karibu na nyumba yake na watwae mwana-kondoo mmoja, kwa kadiri ya hesabu ya watu; kwa kadiri ya ulaji wa kila mtu, ndivyo mtakavyofanya hesabu yenu kwa yule mwana-kondoo.

[5]Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka mmoja; mtamtwaa katika kondoo au katika mbuzi.

[6]Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko lote la mkutano wa Israeli watamchinja jioni.

[7]Nao watatwaa baadhi ya damu yake na kuitia katika miimo miwili na katika kizingiti cha juu, katika zile nyumba watakazomla.

Bwana aliwapa agizo la kuwatenga wana-kondoo Kutoka katika kundi siku ya 10, Kisha  siku ya 14 kuchinja.

Maana yake ni kuwa sadaka/dhabihu Yao, ilipaswa itambilike mapema Kisha ikatengwa. Kama wangekaidi agizo hilo na kuchagua mwanakondoo siku Ile Ile ya kuchinja au hata siku moja kabla  ilikuwa ni kosa mbele za Mungu.

Kufunua nini?

Na sisi pia Bwana anapendezwa na dhahibu zenye maandalizi, ambazo zimetengwa mapema…Kwamfano unapokwenda ibadani jijengee desturi ya kumwandalia Mungu sadaka zako mapema..hata ikiwezekena siku kadhaa kabla..Kwa jinsi unavyoandaa mapema ndivyo inavyokuwa na utukufu mwingi zaidi..

Lakini pia Unahakikisha unaitenga kabisa na hesabu zako nyingine..(yaani haiguswi), mpaka siku ya kumtolea. 

Hiyo itaifanya sadaka Yako ipokelewe Kwa furaha na Mungu, kuliko kufikiria kumtolea Mungu muda huo huo wakati ulikuwa na nafasi ya kufanya maandalizi. Ndio ufunuo ulio nyuma ya agizo hilo la Pasaka.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Kwanini Kristo aitwe Mwana-kondoo. (Yohana 1:29)

Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?

TUUTAFUTE USEMI MMOJA. TUUJENGE MNARA WA MUNGU

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana Yesu ajulikane kama ‘Amina’ (Ufunuo 3:14)

Jibu: Turejee,

Ufunuo 3:14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye ‘ALIYE AMINA’, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu”

Neno Amina maana yake ni “Na iwe hivyo”.. Neno hili kwa lugha ya kiingereza ni “Amen” Hivyo Popote panapotajwa “Amina” au “Amen” maana yake ni “na iwe hivyo”.

Sasa kwanini Bwana Yesu ajitambulishe kwa neon hilo?..

Ni kuyatofautisha maneno yake na wengine! Kwamba maneno yake ni Thabiti.

Sasa ili tuelewe vizuri, turejee pale Bwana Yesu aliposema kuwa “Mimi ndimi Njia, na Kweli na Uzima, mtu haji kwa Baba ila kwa njia yangu mimi (Yohana 14:6)”.

Tukiunyambua huo mstari vizuri, tunapata sentensi mbili 1. Yeye ndiye Njia, 2. Mtu haji kwa Baba ila kwa njia yake yeye.

Hapo Bwana anajiita kuwa yeye “Njia” anajifananisha yeye na kitu kisicho na uhai..lakini anazidi kufafanua ni kwa jinsi gani yeye ni njia kwa kuendelea kusema… “mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye” ikiwa na maana kuwa, kwa maneno ya Yesu na maisha yake, tukiyafuata hayo tutafika mbinguni (hayo ndio njia)… Njia zipo nyingi, lakini zote hizo hazimpeleki mtu mbinguni, isipokuwa njia ya Yesu tu! Ambayo ni Neno lake.

Sasa tukirejea tena hapo Bwana aliposema yeye  ni “Amina” utaona mbele kidogo anaendelea kufafanua ni kwa namna gani yeye ni “Amina”.

Ufunuo 3:14  “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, SHAHIDI ALIYE MWAMINIFU NA WA KWELI, MWANZO WA KUUMBA KWA MUNGU”.

Anasema yeye ni Amina, Shahidi aliye mwaminifu, mwanzo wa kuumbwa kwa Mungu. Maana yake maneno yake ni hakika!, akisema amesema ni lazima iwe hivyo!.. Amina yake ni amina kweli.. wengine wanazo amina lakini zinaweza zisitimie kama walivyoseme. Lakini yeye (Yesu) maneno yake ni hakika!.. akisema basi ni lazima “ITAKUWA HIVYO KAMA ALIVYOSEMA” Ndio maana anaitwa Shahidi mwaminifu.. hajawahi kusema jambo halafu lisitimie..Ni mwaminifu kwa maneno yake siku zote.

Tusome,

Marko 13:31 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.

2Wakorintho 1:20 “Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin; Mungu apate kutukuzwa kwa sisi”.

Je umemtumainia huyu ambaye Maneno yake hayapiti?. Alisema “Aaminiye na kubatizwa ataokoka (Marko 16:16)” je unadhani kutakuwa na kanuni nyingine Zaidi ya hiyo?.. Alisema wadhalimu, na wachawi, na wazinzi, na walevi hawataurithi ufalme wa mbinguni, je unadhani anadanganya??..ni kweli itakuwa hivyo!, maneno yake kamwe hayapiti, Amina yake ni amina kweli..

Je umempokea Yesu?, je umebatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu?.. Kama bado basi tafuta kufanya hivyo mapema.

Maran atha?

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UAMINIFU NI KIGEZO KIKUBWA CHA KUTUMIWA NA MUNGU.

Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharabu

Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)

Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.

HUDUMA YA WALE MASHAHIDI WAWILI.

Rudi nyumbani

Print this post

NI KWANINI WATU WENGI WANASHINDWA KUMWELEWA MUNGU?

Je! Moyo wako upo kweli kwake?

Kuna kauli Bwana Yesu alisema kuhusiana na watu kumwelewa Mungu na uweza wake kwetu, alisema..

Mathayo 13:14  “Na neno la nabii Isaya linatimia kwao, likisema, Kusikia mtasikia, wala hamtaelewa; Kutazama mtatazama, wala hamtaona. 15  Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, WAKAELEWA KWA MIOYO YAO, WAKAONGOKA, NIKAWAPONYA”

Ametaja mambo makuu matatu,

  1. Kuona – Kwa macho
  2. Kusikia –kwa masikio
  3. Kuelewa – Kwa moyo

Hatua ya mwisho ambayo Mungu anatarajia, pindi anapomfundisha mtu, au kusema naye ni KUELEWA. Hivyo ataanza kwanza kwa kumwonyesha mambo kadha wa kadha, yatapita mbele yake, ataanza kusema na yeye kwa njia nyingi, aidha kwa wahubiri wake, au ndoto, au maono, au vitu vya asili, au kwa Neno lake, au kwa maisha yake mwenyewe.. Lakini  pamoja na njia zote hizo  bado mtu huyo anaweza asimwelewe Mungu, kama Moyo wako haupo kwake.

Jambo ambalo watu wengi hatujui, ni kwamba Mungu anazungumza na kila mmoja, Na kila mmoja anaonyeshwa maono mengi na Mungu, kila mtu ameshakutana na Mungu, aidha uso kwa uso au katika roho, haijalishi ni mwema au mwenye dhambi, Lakini ni wachache sana walioweza kuielewa sauti yake iliposema nao.

Ni kwasababu gani hawaielewi? Ni kwasababu inahitaji MOYO ili kuielewa, Na sio macho au sikio. Kama moyo wako haupo kwake, sahau kumwelewa Mungu anaposema na wewe kwa njia yoyote ile. Hata kama itakuja kwa dhahiri, bado hutamwelewa. Sauti yake kwako itakuwa ni ngurumo tu, kama ilivyokuwa kipindi kile Bwana Yesu alipokuwa anazungumza na makutano kuhusiana na ufalme wa mbinguni.

Yohana 12:28  “Baba, ulitukuze jina lako. Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena. 29  Basi mkutano uliosimama karibu wakasikia, walisema ya kwamba kumekuwa ngurumo; wengine walisema, Malaika amesema naye.30  Yesu akajibu, akasema, Sauti hiyo haikuwako kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu”

Ni kwanini iwe hivyo kwao? Ni kwasababu kilichowapeleka kwa Yesu sio wokovu wa Roho zao, au upendo wao kwa Mungu, kilichowapeleka kwake, ni miujiza, uponyaji, uzuri, mwonekano, mazingira, basi, hakuna jipya. Wakishapata walichokuwa wanakitafuta hao wanaondoka zao kuendelea na mambo yao ya dhambi ya sikuzote.

Ndio maana hakukuwa na hata mmoja ambaye aliyeelewa mifano yote Yesu aliyokuwa anaisema mbele ya umati. Isipokuwa wanafunzi wake tu, pamoja na wachache waliomfuata baada ya pale kutaka kufafanuliwa.

Ndugu ikiwa leo unakwenda kanisani kutimiza tu ratiba, kutazama kwaya, kuangalia watu wamevaaje, hata ukiwepo humo unasinzia, unaangalia muda utatoka saa ngapi, ni kweli utakutana na Mungu, atasema na wewe, utamwona, utahisi uwepo wake, utanena hata kwa lugha, utasisimka moyo. Lakini kumwelewa, haitakaa iwezekane. Kwasababu Mungu hajifunui kwa watu ambao  mioyo yao haipo kwake.Hana utaratibu huo.

Na sio tu kanisani, hata mahali popote pale, iwe ni shuleni, kazini, nyumbani, barabarani, Mungu huwa anazungumza, anasema kwa njia mbalimbali tena kirahisi sana, Lakini hutaelewa ikiwa huna moyo wa dhati kwa Mungu wako.

Alisema hivi;;

2Nyakati 16:9 “Kwa maana macho ya Bwana hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, WALIOKAMILIKA MOYO KUELEKEA KWAKE…”

Alisema pia..

Mathayo 15:7  “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, 8  Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami”.

Yatupasa sasa tuondoe unafiki wa ndani, kwa kumaanisha kweli kweli kumpenda Mungu kwa moyo, ili sasa aanze kutufunulia sauti yake na kazi zake. Tukimfuata Kristo tujue kinachotupeleka kule ni Utakatifu na haki, na sio kwasababu tunashida tutimiziwe mahitaji yetu, hapo ndipo atapendezwa na sisi, na hatimaye, tutamwona kila inapoitwa leo.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

NIFANYE NINI ILI NIKUBALIWE NA YESU?

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Kristo aitwe Mwana-kondoo. (Yohana 1:29)

Yohana 1:29 “Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!”.

Bwana Yesu sehemu nyingine anajulikana hivi kama Mwana-kondoo kufuatia tabia ya kondoo ilivyo.

Kondoo ni mnyama mpole sana na mnyenyekevu, tofauti na Mbuzi.. Kondoo Anapokatwa manyoya yake huwa hajigusi anatulia sana, na pia hawezi kujichunga mwenyewe huwa anamtegemea mchungaji asilimia mia. Tofauti na mbuzi au Ng’ombe.

Lakini pamoja na hayo kondoo aliyekomaa ambaye tayari kashaota pembe ijapokuwa ni mpole lakini kuna vipindi vichache vichache anakuwa na hasira hususani wakati wa mvua, na pia anapokutana na kondoo mwingine aliye wajinsia kama yake. Hivyo Bwana Yesu hajajifananisha na kondoo aliyekomaa, kwasababu anazo kasoro nyingi.. bali anajifananisha na kondoo mchanga, (mwana-kondoo) ambaye bado hata hajaota pembe, ambaye hawezi kupambana, aliye mnyenyekevu na mpole.

Bwana Yesu naye ni mpole mfano wa huyo.. Maandiko yanamshuhudia hivyo..

Mathayo 21:5  “Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, MPOLE, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda”.

Na yeye mwenyewe anajishuhudia hivyo  katika Mathayo 11:28.

Mathayo 11:28  “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29  Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; KWA KUWA MIMI NI MPOLE na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30  kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Je umemfuata Yesu aliye mpole?..yeye anayeongea nawe kwa sauti ya upole moyoni mwako, kwamba utubu dhambi?.

Kama bado unasubiri nini?

Okoka leo na ukabatizwe na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu nawe utapata ondoleo la dhambi…na jina lako litaandikwa katika kitabu cha uzima cha mwanakondoo na utakuwa na nafasi katika mji ule, mbingu mpya na nchi mpya.

Ufunuo 21:27 “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Upole ni nini?

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

Je ni kweli Musa alikuwa mtu mpole kuliko wote duniani?

JE! UNAMPENDA BWANA?

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Rudi nyumbani

Print this post

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

Masomo maalumu kwa watumishi wa Mungu,

Je kibiblia ni jukumu la wachungaji peke yao kulichunga kundi? Na mitume na manabii hiyo si kazi yao??….. kama ndio basi huenda Bwana Yesu alikosea alipomwambia Petro ambaye ni Mtume, alichunga kundi lake..

Tusome,

Yohana 21:15  “Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia , Naam ,Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

16  Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, CHUNGA KONDOO ZANGU.

17  Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, LISHA KONDOO ZANGU”.

Kumbe kazi ya kuchunga, na kulisha kondoo si ya mchungaji peke yake, bali hata ya mitume, na waalimu na manabii na wainjilisti… Ikiwa na maana kama Bwana amekupa watu chini yako ni lazima ujue kuwa unawajibu wa kuwachunga na kuwalisha…pasipo kuweka visababu sababu.

Sasa leo hatutazungumzia sana kuhusiana na KUCHUNGA kondoo.. lakini tutalitazama jukumu la KULISHA KONDOO ulilopewa wewe kama mtumishi wa Mungu.

Awali ya yote ni muhimu kujua kondoo ni nani?

Kondoo ni mnyama asiyeweza kujiongoza mwenyewe na Bwana Yesu anao watu ambao siku zote hawataweza kusimama wenyewe (maana yake siku zote watahitaji msaada tu ili waendelee kudumu katika Imani na katika kuifanya kazi ya Mungu). Na kundi hili ni kubwa kuliko lile kundi la watumishi wa Mungu.

Kundi la hili lisipochungwa vizuri na kulishwa ipasavyo linaharibika na kupotea kabisa, na shetani ndilo analolitafuta sana….

Sasa Bwana alimpa jukumu Petro, na anakupa jukumu wewe kama mtumishi wa Mungu, pasipo kujali karama yako, kuwa LISHA KONDOO WAKE lakini si tu kondoo bali pia WANA-KONDOO, Haya ni makundi mawili ambayo ni lazima ujifunze kuyatofautisha.

Tofauti ya kondoo na Mwana kondoo, ni hii; Kondoo aliyekomaa anajulikana kwa jina hilo la “Kondoo” na kondoo aliye chini ya umri wa mwaka mmoja anaitwa “mwana-kondoo”. Sasa Bwana alimwambia Petro alishe makundi hayo yote mawili, na anatuambia pia sisi..

Chakula cha kondoo aliyekomaa ni tofauti na cha yule mchanga.. huwezi kuwalisha wote chakula kinachofanana, kwani kundi moja litadhoofika.. ukimpa maziwa kondoo aliyekomaa, atadhoofika, vile vile ukimpa chakula kigumu kondoo mchanga ataathirika.. kwahiyo ni lazima ujifunze kukigawanya chakula kulingana na makundi ya watu walio chini yako.

Ni lazima uwe na chakula cha waongofu wapya, na chakula cha waliokomaa kiimani, na ni  sharti lazima Makundi yote yale chakula cha kushiba..

Ni lazima chakula chako kilenge kuwakuza wale kondoo wachanga (maana yake wakue kiroho) na kuwanenepesha wale kondoo waliokomaa (maana yake wajae maarifa). Tukiwa watumishi wa aina hiyo basi mbele zake Bwana tutaonekana tunampenda lakini kama hatuwalishi inavyopaswa na huku tunajivuna kuwa sisi ni watumishi wa Mungu, basi bado hatujalijua pendo la Kristo?.

Hivyo Kama Mtumishi wa Mungu jenga tabia ya kulitazama kundi lako (Sawasawa na Mithali 27:23)..usisieme mimi ni Mtume sina karama hiyo?, na huku unawalisha watu mambo yasiyowajenga, hata Petro alikuwa ni Mtume na si mchungaji lakini alipewa hilo jukumu na Bwana la kulisha vizuri kondoo watakaokuwa chini yake, usiseme mimi ni Nabii sina wito huo na huku unawalisha watu maono ya uongo na mafundisho manyonge…hata Musa alikuwa ni nabii lakini alibeba jukumu hilo la kuwalisha watu amri, na sheria za Mungu.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! UNAMPENDA BWANA?

“Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika”,Maana yake nini?

Nitajuaje kuwa nimesamehewa dhambi zangu?

NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)

Jibu: Turejee,

Mwanzo 4: 16 “Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni.

17 Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe”.

Henoko aliyeenda na Mungu hakuwa mwana wa Kaini, kwasababu Uzao wa Kaini wote ulilaaniwa, na hivyo hakutoka nabii yeyote wala mtu yeyote mwenye rekodi ya kumpendeza Mungu katika huo uzao, bali uzao wote uligharikishwa na ile gharika.

Swali kama ni hivyo kwanini Henoko aonekane hapa kama ni uzao wa Kaini?.

Jibu ni kwamba Huyu Henoko anayetajwa hapa katika (Mwanzo 4:16) sio yule aliyeenda na Mungu, bali alikuwa ni Henoko mwingine, kwasababu jina hilo ‘Henoko’ hakuwa nalo mtu mmoja tu!, bali ni wengi waliitwa kwa jina hilo, kama tu leo majina yetu yanavyoweza kuwa ya watu wengine mahali pengine.

Lakini yule Henoko, aliyekuwa mtumishi wa Mungu, na aliyempendeza Mungu alitokea Uzao wa Sethi na habari zake tunazosoma katika Mwanzo mlango wa 5.

Mwanzo 5:18 “Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko. 

19 Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.

20 Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa. 

21 Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. 

22 Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake.

23 Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano.

24 Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa”.

Huyo ndio Henoko aliyeenda na Mungu, ambaye alikuwa mwana wa Yaredi wa uzao wa Sethi, na alikuwa ni mtu wa saba kutoka kwa Adamu (Yuda 1:14). Lakini yule mwingine alikuwa mwana wa Kaini.

 Ni sawa Lameki aliyetajwa katika Mwanzo 4:18-19, ambaye alioa wake wawili, na yule aliyetajwa katika Mwanzo 5:28-31 ambaye alikuwa ni baba yake Nuhu… Hawa walikuwa ni Lameki wawili tofauti wenye tabia mbili tofauti, ingawa majina yao yalifanana…ndivyo ilivyo pia kwa hawa Henoko wawili tuliojifunza habari zao.

Sasa Ni jambo gani tunaloweza kujifunza kwa Henoko aliyeenda na Mungu?

Alikuwa ni mtu aliyeenda na Mungu; Maana yake Njia zake zilimpendeza Mungu mpaka kufikia hatua ya Mungu kumtwaa, na kabla ya Mungu kumtwaa biblia inasema alionyeshwa ujio wa Bwana, siku ile atakayokuja na watakatifu wake kwaajili ya vita vya Harmagedon na utawala wa miaka 1000 duniani.

Yuda 1:14  “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,

15  ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake”

Bwana atusaidie na sisi tuwe watu wa kwenda  na Bwana katika njia zake kama alivyokuwa Henoko.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! tunapaswa kukiamini Kitabu cha Henoko?

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

Wanefili walikuwa ni watu gani?

EPUKA MAKUNDI ILI UTAKATIFU WAKO UDUMU!.

Rudi nyumbani

Print this post

IPENDE BUSTANI YAKO.(Ilime, itunze)

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima.

Ipo tabia ambayo tunapaswa tujifunze kuhusu Mungu. Kama tunavyojua, alipomaliza kuumba vitu vyote ndani ya zile siku saba, zoezi la mwisho kabisa lilikuwa ni Mungu kupanda bustani mashariki mwa Edeni. Tengeneza picha, bustani hiyo ilikuwaje! Bila shaka ilikuwa ni nzuri sana. Mungu alifanya kazi ya kuchukua Ua hili, Ua lile, ukoka huu, ukoka ule, mti huu wa kivuli, mti ule wa matunda kila moja mahali pake stahiki.. Yaani kwa ufupi Edeni ni bustani ambayo iliundwa kwa kila aina ya mmea, lakini katika mpangilio bora. Jambo lililoifanya bustani ile kuwa tofauti na maeneo mengine yote duniani.

Kwani huko kwingine kulijiotea otea, bila mpangilio maalumu. Japo pia napo kulikuwa pazuri lakini sio kama Edeni, kwasababu ile ni bustani iliyopandwa sio kujiotea. Lakini tunaona, asili ya ile Bustani. Ni kwamba ilihitaji kulimwa na matunzo baada ya pale ili iendelee kuwepo vilevile katika ubora wake. Hii ikiwa na maana kama isingetunzwa na kulimwa, ingepotea kabisa, na kufanana tu na sehemu nyingine yoyote ya dunia.

Mwanzo 2:8 “Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya…15 Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.

Watunza bustani wanaelewa jambo hili, mahali ambapo wanazipanda, huwa ni lazima mara kwa mara, wawepo kung’oa majani-shambulizi yanayojitokeza, wanafyeka ukoka unapozidi kimo, wanatia mbolea panaposua sua, na wanainyeshea bustani kila siku, na wakati mwingine kuiwekea uvuli. Hivyo ni kazi ambayo inamgharimu mtunza bustani kuwepo pale wakati mwingi.

Ndivyo ambavyo Mungu alimpa jukumu hilo Adamu, kwamba aitunze bustani na kuilima, kwasababu hilo halikuwa jukumu lake tena. Tafsiri yake ni kwamba ili aendelee kukaa katika mahali pazuri pa nchi. Hana budi kupalima na kupatunza. Asipofanya hivyo pataendelea kuwa kama sehemu nyingine tu ya dunia.

Lakini Adamu, hakuweza kudumu katika bustani ile kwasababu aliyakaidi maagizo ya Mungu.

Hii ikifunua nini?

Kila mtu ameandaliwa Edeni yake hapa duniani, ambayo atamfurahia Mungu wake katika hiyo. Si kila mazingira Mungu amekuwekea wewe kumfurahia yeye, si kila mahali ni Edeni yako. Ipo sehemu maalumu, ambapo hapo Mungu anakuundia kisha wewe unapatunza baada ya hapo.

Na sehemu yenyewe ni ndani ya Kristo.

 Maana yake ni kuwa ukishaokoka, tayari Mungu amekuwekea mema yako mbeleni. Hivyo kuanzia huo wakati huna budi kuanza kuistawisha bustani yako kwa kuitilia mbolea mara kwa mara, kuinyeshea maji, kuipalilia, kuichonga n.k.. Ndio hapo, linakuja suala la Maombi ya mara kwa mara, mikesha, mifungo, kutafakari Neno, kufanya ibada za sifa,  kutoa sadaka, kujitenga na dhambi, na kushuhudia.

Unapokuwa mtu wa namna hii ndivyo unavyoifanya bustani yako kupendeza siku baada ya siku rohoni, ndivyo inavyojitofautisha na sehemu nyingine za dunia, kwa uzuri wake. Matokeo yake ni kuwa Dunia yako itakuwa ya neema sikuzote yenye furaha, Amani na mafanikio, yenye kububujika maziwa na asali. Lakini ukikaa tu ukasubiri, ukasema Mungu atatenda, huku huyatunzi  maneno ya Mungu ndani yako, sahau kuona mabadaliko yoyote maisha yako yatakuwa hayana tofauti na yale ya kale, kwasababu kazi ya utunzaji sio ya Mungu bali ni yako. Wewe umemsubiria Mungu, wakati Mungu alishamaliza kazi yake.

Litunze sana Neno la Mungu, kwa kuliishi sio kulisikia tu. Kwani wanaofanya hivyo wanafungua milango mingi sana ya kiroho, Kanisa la Filadelfia ndio kanisa pekee lililopendwa na Kristo kwasababu liliyatunza maneno yake, na matokeo yake likafunguliwa mlango wa mafanikio mbele yake.

Ufunuo 3:8  “Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe UMELITUNZA NENO LANGU, wala hukulikana jina langu”.

Hivyo anza sasa kujibidiisha kulitendea kazi Neno la Mungu. Kwa jinsi unavyolitunza ndivyo utakavyoona mabadiliko yako.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je, unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Tunaishi katika dakika za nyongeza tu? Dalili zote zilizotabiriwa kuhusiana na kurudi kwa pili kwa Yesu zimeshatimia?. Wasubiri nini? Ukifa leo utajibu nini mbele ya kiti cha enzi cha Mungu?  Tubu sasa ukabatizwe, upokee ondoleo la dhambi zako. Ikiwa bado hujafanya hivyo, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo; +255693036618/+255789001312

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

EDENI YA SHETANI.

SISI TU MANUKATO YA KRISTO.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.

AKAPITA KATIKA LILE SHAMBA AMBALO YAKOBO ALIMPA YUSUFU MWANAWE

Rudi nyumbani

Print this post

AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia!.

Usipoujua ufunuo umhusuyo Yesu hutaona sababu ya kumwamini wala kumfuata, vile vile usipopata ufunuo wa kutosha uhusuo ubatizo hutaona umuhimu wa kubatizwa! (utaona ni habari tu ya kawaida, kwamba ukibatizwa au usipobatizwa vyote ni sawa tu).

Nataka nikuambie ndugu, ubatizo ni tendo la muhimu sana kuliko wengi tunavyodhani. Na leo nataka tuone ni jinsi gani agizo la Ubatizo lilivyoambata na Toba, kwamba baada ya kutubu ni lazima kubatizwa.

Hebu tuyasome maneno yafuatayo ya Bwana Yesu..

Luka 24:46  “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

47  na kwamba mataifa yote “WATAHUBIRIWA KWA JINA LAKE HABARI YA TOBA NA ONDOLEO LA DHAMBI, kuanza tangu Yerusalemu”.

Nataka tuone na kuutafakari kwa kina huo mstari wa 47 unaosema kuwa mataifa yote watahubiriwa “KWA JINA LAKE HABARI YA TOBA NA ONDOLEO LA DHAMBI”

Hili ni agizo ambalo Bwana Yesu aliwapa wanafunzi wake kwamba watu wote ni lazima wahubiriwe habari ya toba na ondoleo la dhambi kwa jina lake.

Mitume walilisikia hili agizo la Bwana, na walilishika  sasa hebu tuangalie ni kwa namna gani walilitekeleza,..je walikwenda kuwaambia tu watu “watubu waondolewe dhambi zao au kuna la ziada walilifanya ”

Tusome kitabu cha Matendo 2:36-38

Matendo 2:36  “Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Umeona hapa! Petro anawaambia watu “watubu na kubatizwa kwa jina lake Yesu, wapate ondoleo la dhambi zao”.. na sio tu “Tubuni mpate ondoleo la dhambi”….. sasa linganisha na yale maagizo Bwana aliyowapa akina Petro kuwa “wakawahubirie watu wote kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi”.

Kumbe kuhubiriwa habari ya Toba na ondoleo la dhambi ni pamoja na ubatizo!.. Maana yake ili mtu apate ondoleo kamili la dhambi zake ni lazima pia akabatizwe (Katikati ya Toba na ondoleo la dhambi, kuna ubatizo ambao shetani kawafumba watu macho wasiuone)..Ndio maana ni ngumu leo hii wengi kushinda dhambi, kwasababu mzizi wa dhambi katika maisha yao haujaondolewa, kwasababu wameukosa ubatizo sahihi.

Mitume sehemu zote walihubiri hivi, kwamba watu baada ya kutubu ni lazima wakabatizwe ili dhambi zao ziondolewe… na mitume kamwe wasingeweza kufanya kitu chochote kilicho kinyume na maagizo ya Bwana Yesu…ikiwa na maana kuwa walimwelewa sana Bwana pale aliposema kuwa wakawahubirie mataifa yote kwa jina lake, kwamba ubatizo pia kwa jina lake ni sehemu ya mahubiri yao.

Swali ni je!, na wewe umebatizwa kwa maji mengi na  katika ubatizo sahihi wa jina la Bwana Yesu?.. Kumbuka, kama ulibatizwa utotoni basi fahamu kuwa watoto wachanga hawabatizwi kwasababu bado hawajatubu, (kujitambua hawajajitambua watawezaje kutubu?) ni sharti kwanza wahubiriwe wamwamini Mwokozi na kujijua kuwa wao ni wenye dhambi ndipo watubu na kubatizwa.  Bwana akubariki.

Tafuta ubatizo sahihi kama bado hujabatizwa, na kama utahitaji msaada Zaidi wa namna ya kupata ubatizo karibu na mahali ulipo basi utawasiliana nasi kupitia namba zetu hapa chini.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

HUNA SHIRIKA NAMI.

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

Rudi nyumbani

Print this post