UWEZA WA MUNGU NJE YA WAKATI.

UWEZA WA MUNGU NJE YA WAKATI.

Tunaposikia kuhusu uweza wa Mungu wa kufanya mambo “nje ya wakati” moja kwa moja tunafikiria, juu wa wakati ambao umepitiliza muda wake. Lakini hatufikirii juu ya wakati ambao “bado haujafikiwa” ambao nao pia huitwa “nje ya wakati”.

Kwamfano Elisabethi alipokea ujauzito nje ya wakati, (yaani katika wakati uliopitiliza), wakati ambapo viungo vya uzazi havipo tena, mfano tu wa Sara. Lakini wakati huo huo Mariamu (mamaye Yesu), alipokea pia ujauzito nje ya wakati(Lakini wakati ambao haujafikiwa).

Ikiwa na maana kabla hata hajamkaribia mwanamume, alionekana tayari mimba imeshatungishwa tumboni. Huo ni uweza wa Mungu wa ajabu.

Ni lazima ufahamu kuwa katika maisha yako ya wokovu wewe kama mwaminio, majira yote mawili Bwana atakupitisha kwa mpigo. Fahamu kuwa kuna mahali utacheleweshwa kidogo,lakini pia kuna mahali utawahishwa haraka kabla ya wakati wake. Vyote viwili vitakwenda sambamba, Hivyo hupaswi kuwa na mashaka naye, kwasababu matokeo aliyoyatazamia Mungu juu ya maisha yako ya wokovu yatatokea tu.

Umtazamapo Mungu, usimweke kwenye kipimo tu cha “ndani ya wakati” ulichokizoea. Jiandae kwa lolote. Lakini mpango wake ni lazima utimie.

Maandiko yanasema..

Ayubu 22:21 Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia.

Na pia anasema..

Warumi 11:33  “Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani!”

Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

INJILI NI UWEZA WA MUNGU, UULETAO WOKOVU.

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments