Kama kichwa cha waraka Huu kinavyosema… “Waraka wa pili wa Paulo Mtume kwa Wakorintho”
Kutuonyesha kuwa Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hichi..
Tunaweza kukigawanya katika sehemu kuu tatu (3)
1) Utendaji kazi wa Mungu, na wajibu wa watakatifu katika huduma na maisha yao ( sura ya 1-7)
2) Utoaji bora kwa mkristo.(Sura ya 8-9)
3) Utetezi wa huduma ya Paulo (10-13)
1) Utendaji kazi wa Mungu, na wajibu wa watakatifu katika huduma na maisha yao ( sura ya 1-7)
Katika sura hizi, Mtume anagusia maeneo kadha wa kadha, kama ifuatavyo.
i) Faraja ya Mungu
Paulo anatoa shukrani zake kwa jinsi Mungu anavyoweza kuwafariji watu wake katikati na dhiki na majaribu mazito. Akimtaja Mungu kama ni ndio mtoa faraja yote, katika dhiki zetu. (1-3-7)
2 Wakorintho 1:3-4
[3]Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote;
[4]atufarijiye katika dhiki zetu zote ili nasi tupate kuwafariji wale walio katika dhiki za namna zote, kwa faraja hizo, tunazofarijiwa na Mungu.
ii) Nafasi ya kutubu.
Sehemu inayofuata Paulo anaeleza sababu ya kutofika Korintho haraka, kama ilivyodhaniwa. Ni ili asilete tena huzuni zaidi kama akiwakuta bado hawajakamilika. Na hiyo ni kutokana na kuwa hawakuwa na mabadiliko ya haraka kwa agizo lake la kwanza, hivyo hakutaka afanye ziara ya ghafla bali wayatengeneze kwanza wao wenyewe ili ziara yake kwao, safari hii iwe ya raha na sio ya hukumu.(1:23-2:4)
iii) Wajibu wa kusamehe. (2:5-11)
Paulo anawahimiza wakorintho kusamehe kwa wale watu wanaoleta huzuni ndani ya kanisa, Hususani waliomnenea vibaya utume wake. Anahimiza kuliko kusimamia adhabu ziwapasazo ambazo wana haki kweli ya kuzipokea. Kinyume chake wawasamehe ili wawapate tena wasipotee kabisa katika huzuni zao.
IV) Utukufu wa agano jipya.(sura ya 3-5)
Paulo Anaeleza jinsi gani, agano jipya utukufu wake ulivyo mbali na ule wa agano la kale. Kwasababu utukufu wa agano jipya umekuja Katika Roho atoaye uhuru.
Paulo anaeleza kwasababu hiyo hatupaswi kulegea kwa kuenenda kwa hila au kulichanganya Neno la Mungu na uongo. Au kwa kutohubiri injili. Bali kufanya yote bila kujali utu wetu wa nje kuchakaa. Tukijua kuwa ule wa ndani unafanywa upya siku baada ya siku na kwamba ipo siku tutasimama mbele ya kiti hukumu kutoa Hesabu ya mambo yetu yote tuliyoyatenda katika mwili.
Paulo anaeleza kwamba kama Kristo alivyopewa huduma ya upatanisho sisi pia tumepewa Neno Hilo hilo ndani yetu. Kuupatanisha ulimwengu na Mungu kupitia Yesu Kristo. Akionyesha kuwa ni wajibu wetu sote kuhubiri injili.
V) Maisha ya ukamilifu (sura ya 6-7)
Paulo anawasihi Wakoritho waikunjue mioyo yao na waishi maisha ya ukamilifu na ya uangalifu wasiwe kwazo la namna yoyote ili utumishi wao usije laumiwa siku ile ya Bwana
Lakini pia anawapa onyo wasiwe na ushirika na wasioamini.
Pamoja na hilo katika sura ya saba, Paulo anaeleza furaha yake kwa Wakorintho Kwa kuitii toba..kufuatana na waraka aliowaandikia hapo kabla wa huzuni ( Ambao haupo miongoni mwa nyaraka hizi zilizo kwenye biblia). Ambapo walipousoma walitubu na kugeuka, kwelikweli. Kuonyesha utii wa toba. Ambao unapaswa uonekane ndani ya makanisa hata sasa.
2) Utoaji bora kwa mkristo.(8-9)
Katika sura ya 8-9
Paulo anahimiza michango kwa ajili ya watakatifu walio Yerusalemu, Akitolea mfano watakatifu wa Makedonia jinsi walivyoweza kutoa kwa ukarimu hata katika umaskini wao, vivyo hivyo na wao anawahimiza wawe na moyo huo huo. Akiwaonyesha jinsi Bwana wetu Yesu alivyotupa kielelezo cha kukubali kuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.
2 Wakorintho 8:9
[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.
Kwasababu utumishi wa namna hiyo sio tu unawapata watakatifu rizki lakini pia huleta matunda ya shukrani kwa Mungu.
2 Wakorintho 9:12
[12]Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu;
3) Utetezi wa huduma yake (Paulo). Sura ya 10-13
Katika sura hizi Paulo anaitetea Huduma yake dhidi ya watu wengine wanaojitukuza mbele za watu, kana kwamba ni mtume wa kweli kumbe ni mitume wa uongo, ambao huwashawishi watu kwa majivuno ya nje na ukali, lakini si ya kazi.
2 Wakorintho 11:20
[20]Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.
Hivyo Paulo anawaeleza kwa upana uthabiti wa huduma yake, tangu asili ya kabila lake, mateso aliyopitia, akionyesha mpaka kusimama vile, hakukutokea hivi hivi tu, bali katika masumbufu mengi, anawaeleza pia maono aliyoyafikia mpaka kunyakuliwa mbingu ya tatu, hiyo yote ni kuwaonyesha wakorintho kama wanataka kuamini kwa watu wanaojisifia basi yeye anawazidi wao, lakini hatumii njia hiyo, bali ya udhaifu ili asihesabiwe zaidi ya vile watu wavionavyo Kwake.
Salamu za mwisho.
Anahimiza wakoritho wanie Mamoja, watimilike na wafarijike.
Hivyo kwa ufupi mambo haya makuu tunaweza kuyapata katika waraka huu;
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)
Fahamu maana ya 2 Wakorintho 8:9 alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.
Rudi Nyumbani
About the author