Kuapiza ni nini? (Mathayo 5:21-22)

Kuapiza ni nini? (Mathayo 5:21-22)

Mathayo 5:21  Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu. 22  Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto.

JIBU: Katika vifungu hivi tunaona Bwana Yesu anatoa mtazamo mpya kuhusiana na dhambi ya uuaji. Hapo mwanzo ilidhaniwa kuwa pale mtu anapochukua hatua ya kumchinja ndugu yake, au kumpiga mpaka kufa kama alivyofanya Kaini, ndio umehitimu kuwa muuaji. Lakini Bwana Yesu anasema..

Kitendo  tu cha kumwonea hasira ndugu yako, kumfyolea, na kumwapiza, tayari ni kosa la uuaji.

Sasa alikuwa na maana gani kwa maneno hayo matatu. “Hasira, kufyolea na kuapiza?”

Hasira kwa ndugu, huzaa mambo kama kinyongo, uchungu, na wivu. Kwahiyo kama mtu akiwa na mambo kama hayo  kwa ndugu yake, mbele ya Kristo amestahili kuhukumiwa.

Lakini pia akimfyolea. Kumfyolea ni kumwita mwenzako mjinga wewe, au mpumbavu wewe. Ukilenga mtu asiye na akili, Kwa urefu wa tafsiri hii fungua hapa>> RACA Hilo nao ni kosa lililostahili kuketishwa kwenye mabaraza ya wazee, utoe hesabu.

Lakini mbaya zaidi kumwapiza. Hichi ni kitendo cha kumtamkia kabisa maneno ya  laana. Kana kwamba ni mtu mwovu sana aliyepindukia. Kwamfano kumwita ndugu yako mwana-haramu wewe, au kumwita ‘shoga wewe’, kumwita msenge(neno lenye maana mtu anayeshiriki uovu kinyume na jinsia yake), kumwita pepo, kafiri wewe, n.k. maneno ambayo hayawezi kutamkika, ni sawa na tusi kwa mwenzako. Huko ndio kuapiza.

Adhabu yake Kristo anaifananisha na kutupwa katika jehanamu ya moto.

Hivyo hatupaswi kudhani kuwa, kuua ni mpaka tumwage damu, lakini twaweza kufanya hivyo tokea moyoni mwetu hadi vinywani mwetu, kabla hata hatujafikia kwenye kitendo chenyewe.

Tujazwe Roho Mtakatifu, tuwezi kuzishinda tabia hizi mbaya za mwili.

Katika agano la kale ilikuwa sio tu kumpiga mzazi wako, ilikupasa kifo (Kutoka 21:15), lakini pia kumwapiza huku, adhabu yake ilikuwa ni moja tu na hilo kosa la kwanza yaani kifo.

Kutoka 21:17 “Yeye amwapizaye baba yake au mama yake, sharti atauawa”

Shalom.

Je! Umeokoka? Fahamu kuwa usipomwamini Kristo, na kupokea msamaha wake wa dhambi, hauna uzima wa milele ndani yako. Kwasababu kamwe hutakaa umpendeze Mungu kwa nguvu zako au matendo yako mwenyewe. Na sababu ya Yesu kufa msalabani kwa ajili yako kukusaidia, kupokea msamaha wa dhambi, lakini pia nguvu ya kushinda mambo mabaya kwa Roho wake Mtakatifu tuliopewa. Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu akuokoe leo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo ya wokovu, Bwana akubariki >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Amen

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bwana alimaanisha nini kusema “atazamaye mwanamke kwa kumtamani” amezini naye?

Je ni sahihi kumwita mtu “Mkuu”?

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

UFANYE MOYO WA MUNGU UWAELEKEE WATU WAKE.

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments