Je ni sahihi kumwita mtu “Mkuu”?

Je ni sahihi kumwita mtu “Mkuu”?

Katika Mathayo 9:2 tunasoma Bwana anamwita “Mkuu” Yule mtu aliyepooza ?.. Je ni sahihi na sisi kuitana wakuu?


Jibu: Tusome,

Mathayo 9:2 “Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, ALIMWAMBIA YULE MWENYE KUPOOZA, JIPE MOYO MKUU, MWANANGU, umesamehewa dhambi zako”.

Hapo ukisoma vizuri utaona Bwana hakumwita Yule mtu “Mkuu”.. Bali alimaanisha “ajipe Moyo Mkuu” yaani “moyo ulio mkuu”. Kwahiyo ni moyo mkuu ndio uliotajwa hapo, na si Mkuu kama mtu. Kristo hana Mkuu juu yake zaidi ya Baba, hivyo hawezi kumwita mtu yeyote  duniani Mkuu,  zaidi sana anatuita sisi WANAWE,  kama mwishoni hapo alipomalizia.. “jipe moyo mkuu, MWANANGU, umesamehewa dhambi zako”

Kadhalika biblia haijaruhusu sisi kwa sisi kuitana “Wakuu”, kwasababu aliye Mkuu wetu sisi sote ni mmoja tu naye ni Kristo, (Soma Matendo 3:15 na Ufunuo 1:5). Sisi tukiitana majina yetu kama ndugu inatosha!..Vyeo vingine vya juu zaidi ya hivyo vinamhusu Bwana wetu Yesu peke yake (Mathayo 23:8-11).

Sasa hivi upo mtindo wa sisi kwa sisi kuitana “wakuu”, utaona mtu atazungumza maneno mawili matatu na mwenzie na katikati atataja neno “mkuu” kama kionjo cha kumpandisha hadhi Yule anayezungumza naye. Si sawa kufanya hivyo!.. Ni mtindo ambao chanzo chake ni kutoka kwa Yule adui yetu shetani.

Lakini pamoja na hayo, tunaweza kujifunza kitu kupitia hiyo habari!.. Bwana alimwambia Yule aliyepooza kwamba “jipe moyo mkuu ” na si “ajipe tu moyo”..bali “moyo mkuu”.. Maana yake tunapokuwa katika dhiki fulani, au tatizo fulani, au ugonjwa fulani.. Hatuna budi kujipa moyo mkuu wenyewe!.. Maana yake hatupaswi kukata tamaa.. Tunapaswa kuamini mpaka mwisho, ili tupokee uponyaji wetu, au Baraka zetu. Kama ni kuomba tunapaswa tuendelee kuomba kwa Moyo Mkuu, kama kutafuta tunapaswa tuendelee kutafuta kwa Moyo Mkuu, mpaka tukipate. Lakini tunapokata tamaa kirahisi ni ngumu kupokea au kupata kile tulichokuwa tunakitafuta.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini ndugu wanaokaa pamoja wawe kama mafuta ya Haruni?

Nini tofauti kati ya moyo na roho?

SHETANI ANAPOKUINGIA, ANATIA MOYO MGENI NDANI YAKO.

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments