Hadhari ni nini kibiblia? (Mithali 1:4)

Hadhari ni nini kibiblia? (Mithali 1:4)

Hadhari ni nomino ya kitenzi tahadhari. Neno Lenye maana ya “uangalifu”.

>Kwamfano mwalimu anayesahisha mitihani ya wanafunzi tunasema huwa na hadhari kubwa katika usahishaji.

  • Kula bila hadhari ya usafi huweza sababisha magonjwa.

Katika biblia neno hili utalisoma kwenye vifungu hivi;

Danieli  2:13 Basi ile amri ikatangazwa, na hao wenye hekima walikuwa karibu na kuuawa; watu wakamtafuta Danielii na wenzake ili wauawe.  14 Ndipo Danieli kwa busara na HADHARI akamjibu Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, aliyekuwa ametoka ili kuwaua wenye hekima wa Babeli;  15 alijibu, akamwambia Arioko, akida wa walinzi wa mfalme, Mbona amri hii ya mfalme ina ukali namna hii? Ndipo Arioko akamwarifu Danielii habari ile

Mithali 1: 1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.  2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu;  3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili.  4 Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na HADHARI;

Yoshua 22:24 au kama sisi tumefanya jambo hili kwa HADHARI sana, tena makusudi, huku tukisema, Katika siku zijazo wana wenu yamkini wakanena na wana wetu, na kusema, Ninyi mna nini na Bwana, yeye Mungu wa Israeli?

Sisi pia kama watakatifu, tuwe na hadhari, katika maisha ya ulimwenguni. Tunaishi ulimwenguni lakini hatupaswi kufungwa nira na huo kwa jinsi isivyo sawasawa. Kwasababu watu wanaokosa jambo hili husongwa na anasa, udanganyifu wa mali na shughuli za ulimwengu huu, na tamaa ya mambo mengine hatimaye hawazalishi kitu.

Shalom.

Je! Umeokoka? Unatamani leo kupokea msamaha wa dhambi? Ikiwa jibu ni ndio basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya kumkaribisha Yesu moyoni mwako.>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Akida ni nani kibiblia, na kazi yake ni ipi? (Mathayo 8:5)

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

AGANO LA MOYO LENYE NGUVU

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments