Jibu: Tusome,
Matendo 13:42 “Na walipokuwa wakitoka, wakawasihi waambiwe maneno haya sabato ya pili.
43 SINAGOGI ILIPOFUMUKANA, Wayahudi na waongofu watauwa wengi wakashikamana na Paulo na Barnaba; ambao, wakisema nao, wakawatia moyo kudumu katika neema ya Mungu.
44 Hata sabato ya pili, watu wengi, karibu mji wote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu.
45 Bali Wayahudi, walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana”.
Maana ya Sinagogi KUFUMUKANA ni sinagogi Kutawanyika!.. Yaani Tendo la watu kutawanyika baada ya ibada, ndio KUFUMUKANA!. Hivyo mstari huo ili ueleweke vizuri tunaweza kuuweka hivi..
Matendo 13:42 “Na walipokuwa wakitoka, wakawasihi waambiwe maneno haya sabato ya pili.
43 WATU WALIPOTAWANYIKA Wayahudi na waongofu watauwa wengi wakashikamana na Paulo na Barnaba; ambao, wakisema nao, wakawatia moyo kudumu katika neema ya Mungu”.
Tunachoweza kujifunza katika Habari hiyo ni Utayari wa Mitume wa kanisa la kwanza katika kuhubiri injili. Waliweza kuingia kila mahali na kuwafanya watu wamgeukie Kristo kwa nguvu nyingi za Roho, hata kila mahali baada ya mahubiri yao, watu wengi waliungana nao.
Na sisi hatuna budi kuwa na bidii katika kuifanya kazi ya Mungu kama waliyokuwa nayo Mitume, ili Bwana atuongezee Neema yake.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
About the author