Title June 2023

JE UTII WAKO KWA MUNGU UMETIMIA?.

Je unajua kuwa kama utii wako haujatimia mbele za Mungu, kuna mambo utashindwa kuyafanya?? Kama utiifu wako kwake ni mdogo basi upo hatarini sana, Kama ulikuwa hulijui hili, basi ni vizuri ukalijua leo.

Hebu tusome maandiko yafuatayo..

2Wakorintho 10:3  “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4  (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;

6  tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, KUTII KWENU KUTAKAPOTIMIA

Hapo mwishoni anamalizia kwa kusema “KUTII KWENU KUTAKAPOTIMIA”. Ni wengi wanalisoma hili andiko lakini hawafiki hapo mwisho, au hata wakifika hapo mwisho basi hawatafakari vizuri maana ya maneno hayo “Kutii kwenu kutakapotimia”.

Maana yake ni kwamba kama kutii kwako mbele za Mungu hakujatimia basi HUTAWEZA KUANGUSHA NGOME, hutaweza KUANGUSHA MAWAZO YALIYOINUKA juu yako na juu ya maisha yako na familia yako na shughuli zako… kama kutii kwako hakujatimia mbele za Mungu vile vile HUTAWEZA KUTEKA NYARA, wala hutaweza KUPATILIZA MAASI yoyote yaliyoinuka kinyume chako… Kwaufupi hutaweza  kabisa kushindana vita vya kiroho!!..utaishia kusumbuliwa tu na shetani na wanadamu.

Mungu anapenda UTII, Na Utii una nguvu nyingi.. Kwa jinsi tunavyoongeza viwango vyetu vya kumtii Mungu ndivyo NGUVU ZETU ZA KIROHO ZINAVYOONGEZEKA.. Na hivyo tunakuwa na uwezo mkubwa wa kumshinda Adui na hila zake na njama zake.

Lakini leo hii kama Mungu anakuambia uache dhambi hutaki kumtii unategemea vipi Uwe na Nguvu za kuangusha Ngome ndani yako?, kama Ukiambiwa ukabatizwe hutaki kutii unategemea vipi uweze kuangusha ngome za mizimu ya ukoo wenu na mababu?.

Kama unaambiwa tu uache kuvaa mavazi hayo yasiyokupasa hutaki kutii, unategemea vipi hayo maradhi ya muda mrefu na hizo shida zikuondoke????.. Kama tu kumtii Mungu ni shida utawezaje kutiisha fikra nyingine imtii Kristo? Sawasawa na hilo andiko??.

Mtii Mungu kwanza ndipo uwe na nguvu za kuwafanya wengine wamtii Kristo…Ukikosa utii kwa Mungu ndivyo unavyojimaliza mwenyewe…

Na si kumtii Mungu leo na kesho kuendelea na mambo mengine… Hapana! Bali biblia inatufundisha kuwa utii wetu unapaswa uwe endelevu ndipo tufikie kiwango cha “kutimia” kule biblia unakokusema, ndipo matokeo yatakapoonekana.

Yakobo 4:7 “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. 4.8  Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”.

Je umeitii Injili?, Je umeitii kazi ya Mungu na maagizo yake yote?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.

Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.

SWALI: Mstari huu unamaana gani? Mithali 19:21 Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.


JIBU: Kila moyo wa mwanadamu, unamatamainio mengi, lakini uhalisia ni kwamba sio matamanio yote ni ya ukweli au yanania nzuri baadaye, kwamfano mtu atataka mali nyingi, lakini moyo wake unasema atakapopata nyumba kubwa na gari atawakomoa waliomdharau, atalipiza kisasi, atafanya anasa ,atatembea kwa majigambo, ataongeza Masuria.

Na  ndio maana mengi ya malengo kama haya yawezi kusimama kwa watoto wa Mungu, kwasababu yana hila nyingi nyuma yake. Mtume Yakobo aliliweka wazi jambo hili, ni kwanini wakati mwingine hatupokei majibu ya maombi yetu alisema..

Yakobo 4:2  “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! 3  Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”

Lakini kinyume chake anasema Shauri la Bwana ndilo litakalosimama. Maana yake ni kuwa Hekima ya Bwana inayopima  haya yote imaamua cha kutoa na kutokutoa. Hivyo si matamainio yako yote unayoyaona ni mema, basi yatakuwa mema pia mbele za Mungu, mengine yana udaganyifu mwingi. Ndio maana Yeremia 17: 9 inasema “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua”?

Hivyo tuombapo jambo ni busara kumalizia na kusema “Bwana mapenzi yako yatimizwe”.

Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala Mwangalie sana

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)

JIFUNZE KUDUMU UWEPONI MWA MUNGU.

Je ni kweli Yuda hakuwa na dhambi kwa kumsaliti Bwana, kwasababu tayari ilikuwa imeshatabiriwa?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Abramu aliondoka Harani kabla au baada ya kifo cha baba yake?.

Swali: Maandiko yanatuonyesha Tera, baba yake Abramu aliishi jumla ya miaka 205 (Mwanzo 11:32) na tena yanaonyesha kuwa Tera alimzaa Abramu akiwa na miaka 70 (Mwanzo 11:26), na ukirudi kwenye Mwanzo 12:4 biblia inatuonyesha tena Abramu alitoka nchi ya Harani alipofikisha miaka 75.

Sasa ukipiga mahesabu vizuri utaona miaka aliyoishi Tera baba yake Abramu isingepaswa iwe 205, bali iwe miaka 145 yaani (70+75=145) kama Abramu aliondoka kwelii Harani baada ya kifo cha babaye! , Lakini tunaona biblia inatuambia umri wa Tera ulikuwa ni miaka 205. (Je biblia inajichanganya!)

Jibu: Jibu ni kwamba Biblia haijichanganyi na wala haijawahi kujichanganya, vinginevyo ingekuwa ni kitabu cha uongo!. Lakini tunaona maneno yaliyomo ndani ya biblia ni ya uzima tena yenye Nguvu.

Sasa tukirudi kwenye swali letu, je! Abramu alitoka Nchi ya Harani kabla au baada ya kufa baba yake? Jibu ni kwamba alitoka BAADA YA BABA YAKE KUFA!, Na si kabla!. Tunalithibitisho hilo Zaidi katika kitabu cha Matendo ya Mitume..

Matendo 7:2 “Naye akasema, Ndugu zangu na baba zangu, sikilizeni: Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Ibrahimu, alipokuwa katika Mesopotamia, kabla hajakaa Harani,

3  akamwambia, Toka katika nchi yako na katika jamaa zako, ukaende hata nchi nitakayokuonyesha.

4  Ndipo alipotoka katika nchi ya Wakaldayo, AKAKAA HARANI, AKATOKA HUKO BAADA YA KUFA BABAYE, Mungu akamhamisha mpaka nchi hii mnayokaa ninyi sasa.

Sasa kama ni hivyo kwanini hesabu ya miaka haikai sawa..badala ya  miaka 145 anaonekana kufa akiwa na miaka 205?.

Jibu ni kwamba Tera hakumzaa Abramu akiwa na miaka 70, bali maandiko yanasema alipofikisha umri wa miaka 70 akamzaa Abramu, Nahori na Harani. (watoto watatu).

Mwanzo 11:26 “Tera akaishi miaka sabini, akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani”. 

Maana yake ni kwamba watoto hawa watatu walianza kuzaliwa  baada ya Tera kufikisha miaka 70, na si kwamba wote watatu walizaliwa ndani ya mwaka mmoja, bali walizaliwa katika vipindi tofauti tofauti pengine walipishana miaka mitano mitano au hata kumi kumi au hata Zaidi ya hapo, lakini Tera alipofikisha miaka 70 ndipo alipoanza kuzaa!

Sasa swali la msingi hapa ni mtoto yupi aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa na yupi aliyekuwa wa mwisho kati ya hao watatu..

Katika hiyo Mwanzo 11:26 tunaona Abramu akitajwa wa kwanza, sasa hiyo haimaanishi kuwa yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa!!.. Orodha hiyo imetajwa kufuatia heshima ya watu hao na si ukubwa!.. Abramu ndiye aliyetukuka mbele za Mungu Zaidi ya hao ndugu zake wawili ndio maana kawekwa hapo wa kwanza..kwasababu habari inayoendelea itamhusu yeye yeye na uzao wake.. hiyo ndio sababu ya yeye kutajwa wa kwanza na si nyingine.. Lakini kuhalisia aliyekuwa mkubwa kuliko wote pale ni Harani.

Tunajuaje Harani ndiye aliyekuwa mkubwa kuliko Abramu na Nahori?…

Kwanza Abramu alisafiri na Lutu, ambaye alikuwa ni mtoto wa Harani kaka yake.. Na wakati huo tayari Lutu alikuwa mtu mzima kipindi anasafiri na Abramu (Mwanzo 12:5)… Pili Abramu na Nahori aliyetajwa wa pili kwenye orodha alimwoa mtoto wa Harani kaka yake.

Mwanzo 11:29 “Abramu na Nahori wakajitwalia wake. Jina la mkewe Abramu aliitwa Sarai, na jina la mkewe Nahori ALIITWA MILKA, BINTI HARANI, ambaye alikuwa baba wa Milka na wa Iska”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Abramu hakuwa mtoto wa kwanza wa Tera bali huenda alikuwa wa pili au wa tatu, Harani ndiye aliyekuwa wa kwanza ingawa kwenye orodha ameonekana wa mwisho…na Tera hakumzaa Abramu akiwa na miaka 70 bali akiwa na miaka 130. Na Abramu aliondoka Harani alipofikisha miaka 75 baada ya kifo cha baba yake, ambaye alikufa akiwa na miaka 205.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! biblia inajichanganya katika 1Petro 2:13 na Matendo 5:29.

Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)

WEWE U MUNGU UONAYE.

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

Je Ni kweli haturuhusiwi kula nyama kulingana na Isaya 66:3?

Rudi nyumbani

Print this post

Waliouawa Shitimu kwa pigo walikuwa ni watu Elfu 23 au elfu 24?.

Swali: Napenda kujua je!, idadi ya Wana wa Israeli waliouawa kwa pigo kule Shitimu ilikuwa ni Elfu 23 au elfu 24?..maana sehemu moja tunaona biblia inataja watu elfu 23 (1Wakorintho 10:8) na sehemu nyingine Elfu 24, (Hesabu 25:9) je biblia inajichanganya?.

Jibu: Biblia haijichanganyi sehemu yoyote kwasababu sio kitabu cha Uongo, bali ni kitabu kilichojaa maneno ya uzima wa Mungu, na ya kweli.

Sasa ili tuielewe vizuri tuisome habari yenyewe kuanzia ule mstari wa kwanza wa kitabu hicho cha Hesabu 25

Hesabu 25:1 “Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu; 2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.

3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.

4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.

5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal peori.

6 Na tazama, mtu mmoja miongoni mwa wana wa Israeli akaja na kuwaletea nduguze mwanamke Mmidiani mbele ya macho ya Musa, na mbele ya macho ya mkutano wote wa wana wa Israeli, hapo walipokuwa walia mbele ya mlango wa hema ya kukutania.

7 Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake;

8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli.

9 Nao waliokufa kwa hilo pigo walikuwa WATU ELFU ISHIRINI NA NNE HESABU YAO

Hapa tunaona ni watu elfu 24 waliokufa kwa pigo hilo… lakini tunaona idadi nyingine tofauti ikitajwa katika kitabu cha Waraka kwa wakorintho.

1Wakorintho 10:8  “Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, WAKAANGUKA SIKU MOJA WATU ISHIRINI NA TATU ELFU”.

Sasa je! Biblia inajichanganya? Jibu ni La!

Ukweli ni kwamba idadi ya waliokufa kwa pigo ni watu elfu 24 na si elfu 23 lakini kwanini Paulo katika hiyo 1Wakorintho 10:8 aseme ni elfu 23?

Ni lazima uangalie ni nini Paulo alichokuwa anajaribu kukupitisha kwa watu wa wakorintho, Lengo na Nia ya Paulo ilikuwa ni kuwaonyesha madhara ya Uasherati, jinsi unavyoweza kuleta madhara makubwa ndani ya kipindi kifupi!.

Sasa hapa Paulo anasema walianguka watu elfu 23 “KATIKA  SIKU MOJA”. Ikiwa na maana kuwa huwenda lile pigo lilienda Zaidi ya “siku moja” . Huwenda lilidumu siku mbili au Zaidi ya hapo! Ndipo likakoma!.. lakini katika ile siku moja tu ya kwanza walianguka watu elfu 23 (hiyo ni idadi kubwa sana)…na idadi ya wote waliokufa mpaka siku ya mwisho pigo lilipokoma ilikuwa ni watu elfu 24.

Sasa Paulo anajaribu kuwaonya Wakorintho jinsi uasherati unavyoweza kuleta madhara makubwa ndani ya kipindi kifupi kuliko wanavyodhania, kama ilivyokuwa kwa hawa wana wa Israeli walivyozini na wanawake wa Moabu..

Ndio maana tukirudi nyuma kidogo kwenye kitabu hicho hicho, mlango ule wa 6 utaona jinsi Paulo anavyoelezea ubaya wa dhambi ya uasherati..kwamba ni mbaya  Zaidi ya dhambi zote mtu anazoweza kuzifanya katika mwili…

1Wakorintho 6:15 “Je! Hamjui ya kuwa MIILI YENU NI VIUNGO VYA KRISTO? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!

16  Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.

17  Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye.

18  Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ILA YEYE AFANYAYE ZINAA HUTENDA DHAMBI JUU YA MWILI WAKE MWENYEWE.

19  Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

20  maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.

Ni nini tunajifunza?

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni madhara ya Uasherati, wengi wanasema nikishafanya uasherati nitatubu tu!..pasipo kujua kuwa uasherati wa mara moja unaweza kuleta madhara makubwa ndani ya muda mfupi!ll…Wana wa Israeli walipomaliza kufanya dhambi hiyo ndani ya siku moja walikufa watu elfu23, nafasi ya kutubu hawakuiona..

Vile vile dhambi ya uasherati inaweza kukuharibia mambo yako mengi ndani ya siku moja. Inaweza kukuharibia maisha yako moja kwa moja ndani ya siku moja, inaweza kukupeleka kuzimu ndani ya siku moja, na inaweza kukuletea majuto makubwa ndani ya siku moja, Zaidi sana biblia inasema mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa.

Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.

Itaishindaje dhambi ya Uasherati?.. Je kwa kuomba tu? Jibu ni La!..bali kwa kuikimbia kama Yusufu alivyoikimbia..

1Wakorintho 6:18  “Ikimbieni zinaa..”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)

Kipaku ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Mhubiri 10:16 “Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana, Na wakuu wako hula asubuhi!”


Mstari huu umegawanyika katika sehemu mbili;

  1. Sehemu ya kwanza ya huu mstari inasema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana.
  2. Na ya pili ni hiyo, ikiwa wakuu wako hula asubuhi.

Tuitazame sehemu ya kwanza: mfalme kijana.

Hapo mhubiri anajaribu kueleza uhusiano uliopo kati ya uongozi na ukomavu wa mtu. Akatumia mfano wa kijana, kwasababu mara nyingi ni ngumu sana kuipata busara kwa vijana,  kutokana na kuwa hawana uzoefu mwingi wa maisha na pia hawajaandaliwa vya kutosha, kumudu nafasi za uongozi, kinyume chake kitakachowaongoza ni hisia tu za ujana na si vinginevyo. Na ndio maana mtu kama Sulemani alilitambua hilo alipotawadhwa tu mfalme akiwa bado kijana mdogo, alimwomba Mungu ampe hekima ya namna ya kuwaongoza watu wake. Na Bwana akamjalia.

1Wafalme 3:7 “Na sasa, Ee Bwana, Mungu wangu, umenitawaza niwe mfalme mimi mtumwa wako badala ya Daudi baba yangu; nami ni mtoto mdogo tu; sijui jinsi inipasavyo kutoka wala kuingia. 

8 Na mtumwa wako yu katikati ya watu wako uliowachagua, watu wengi wasioweza kuhesabiwa, wala kufahamiwa idadi yao, kwa kuwa ni wengi. 

9 Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?  10 Neno hili likawa jema machoni pa Bwana, ya kuwa Sulemani ameomba neno hili”

Walikuwepo pia wafalme wengine waliotawadhwa wakiwa wadogo kama Yoashi, lakini akasaidiwa na kuhani Yehoyada katika ufalme wake, na ukawa bora (2Wafalme 11-12)

 Lakini tunakuja kuona kwa mwanawe Sulemani aliyeitwa Rehoboamu. Yeye naye alikuwa ni kijana lakini hakutaka mashauri kwa wazee waliomtangulia, kinyume chake, akasikiliza mashauri ya vijana wenzake Hivyo ikapelekea ufalme wake kugawanyika, na kupoteza makabila kumi kati ya kumi na mbili ya Israeli.(Soma 1Wafalme 12:1-16)

Lakini sehemu ya pili ya mstari huu inasema Ole wako nchi ikiwa wakuu wako hula asubuhi.

Maana yake kwamba kuwa na viongozi ambao wanatanguliza maslahi yao kabla ya kazi, nchi hiyo sikuzote huishia pabaya. Sikuzote watu wanakwenda kufanya kazi asubuhi, wakitarajia kile walichokihangaikia kutwa nzima ndio wakifaidi jioni, lakini hapa tunaona ni kinyume chake. Na jambo hili ni kweli, Tunaona katika baadhi ya mataifa yanayoendelea, wananchi wao wanapitia katika taabu, na umaskini wa hali ya juu, kutokana na kuwa viongozi wao, wanatazama maslahi yao binafsi wanapoingia madarakani na sio maslahi ya taifa.. Uchu wa madaraka na ukuu, ndio wanachokitazama lakini sio kujenga mataifa yao.

Hii inafunua nini rohoni?

Neno hili linawahusu, watumishi wote wa Mungu wanaosimama katika ngazi za uongozi. Ikiwa wewe bado ni kijana au mchanga katika huduma(hata kama una-mvi) na umepewa kundi ulichunge, Omba sana hekima kwa Mungu, pia kuwa tayari kujifunza kwa waliokutangulia, Sikuzote viongozi-wachanga, katika hatua za awali wanajiamini kuwa wanajua kila kitu, lakini kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda ndivyo wanavyotambua kasoro zao nyingi. Hivyo ili kuepuka, kufanya makosa ya kiutumishi, tafuta sana msaada kwa Mungu katika hekima na mashauri.

Lakini pia, ikiwa wewe ni mchungaji, askofu, mtume, mwalimu, au unatumika katika huduma yoyote, epuka tamaa hususani ya mali. Si kila shilingi unayoipata uipeleke tumboni, au kujijengea majumba na biashara. Ni heri ukatazama kwanza hali ya kanisa la Kristo. Kama mchungaji mwema yakupasa kuipendezesha kwanza nyumba ya Bwana, kisha Baadaye Bwana mwenyewe ndio akupendezeshe wewe. Unatembelea gari ya Tsh milioni 40, halafu kanisa ni la makuti, Hapo ni nini unategemea kama sio ufukara wa kiroho hadi kimwili baadaye.

Kwahiyo hekima hizi zinatuonya, ili uongozi wetu usianguke mbeleni, hivyo tuzingatie sana maneno haya ya hekima. Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP

Mada Nyinginezo:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?

VIJANA NA MAHUSIANO.

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.

NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Bwana Yesu aliruhusu wanafunzi wake kubeba Fimbo au hakuwaruhusu? (Marko 6:8 na Mathayo 10:10).

Swali: Tukisoma Marko 6:8, tunaona Bwana Yesu anawaruhusu wanafunzi wake “wabebe fimbo”, lakini tukirejea katika Mathayo 10:10 tunasoma habari tofauti, Bwana Yesu anawakataza wasibebe chochote hata fimbo..sasa mwandishi yupi yupo sahihi na yupi hayupo sahihi? Je biblia inajichanganya yenyewe?.

Jibu: Biblia kamwe haijichanganya mahali popote, vinginevyo kitabu kizima kitakuwa ni cha uongo!. Lakini kama ni kitabu cha kweli kilichojaa maneno ya kweli ya uzima, na Roho Mtakatifu basi hakiwezi kuwa kitabu cha ushuhuda wa uongo!, au unaochanganya!..kinachochanganyikiwa ni fahamu zetu katika kukielewa kitabu hicho, lakini chenyewe kama chenyewe hakina kasoro yoyote.

Awali ya yote tuisome mistari hiyo…

Marko 6:7 “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu;

8  akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;

9  lakini wajifungie viatu; akasema, Msivae kanzu mbili”.

Hapa ni kweli tunaona Bwana anawaambia wasibebe chochote ila Fimbo tu!… Tusome tena habari hiyo katika kitabu cha Mathayo..

Mathayo 10:7 “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.

8  Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.

9  Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;

10  wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, WALA FIMBO; maana mtenda kazi astahili posho lake”.

Hapa tunaona Bwana anawakataza hata Fimbo wasibebe, na ilihali kule kwenye kitabu cha Marko tunaona anawaambia wasibebe kitu kingine chochote isipokuwa Fimbo tu!.. Sasa mwandishi yupi ni wa kweli na yupi ni wa uongo?.

Jibu ni kwamba waandishi wote ni wa kweli hakuna aliye mwongo!,

Katika Marko Bwana anawaambia wasibebe vitu vya njiani isipikuwa FIMBO TU!.. Sasa fimbo hakikuwa chakula bali ni kifaa kinachomwezesha mtu kutembea katika milima na mabonde! Ni kama tu kiatu kilivyo msaada kwa miguu katika safari ndefu za miiba na mavumbi.. Fimbo na yenyewe ilikuwa ni hivyo hivyo..

Kwahiyo fimbo ilikuwa ni sehemu ya kitu cha msingi mtu anachoweza kuwa nacho kwa safari kama tu vile mtu alivyo na kanzu au kiatu au nguo.

Lakini sasa Bwana alichowakataza ni wao kubeba fimbo ya pili au ya tatu, kana Kamba moja ikivunjika basi kutakuwepo na akiba. Hicho ndicho kitu Bwana alichowakataza akawaambia wabebe fimbo moja tu!. Wasihofie endapo hiyo waliyonayo itapata itilafu, kwani huko wanakokwenda Mungu wa mbinguni atawafungulia mlango watapata nyingine.

Lakini pia sio Fimbo tu!, bali hata kanzu!.. wasibebe na kujifungasha mizigo ya kanzu nyingi, waende na hiyo moja tu iliyopo mwilini kwasababu huko waendako Baba yao wa mbinguni anajua kuwa wana haja na nazo, hivyo wasitie wasiwasi kwasababu mtenda kazi amestahili posho yake (watapata huko waendako). Ndio maana akawakataza wasibebe kanzu mbili…

Marko 6:8 “akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;

9  lakini wajifungie viatu; akasema, MSIVAE KANZU MBILI”.

Hapo mwisho anasema “msivae kanzu mbili” maana yake ile moja waliyonayo mwilini inatosha.. vile vile wasibebe fimbo nyingine ya pili, hiyo moja watakayokuwa nayo inatosha!..sawasawa na hiyo Mathayo 10:10..

Kwahiyo biblia haijichanganyi, bali shetani ndiye anayetuchanganya….

Sasa kufahamu ni somo gani tunaloweza kujifunza nyuma ya hii habari fungua hapa>>> Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?

Je suruali ni vazi la kiume tu?

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

Je! habari ya muda aliotawala Mfalme Yekonia inajichanganya? (2Wafalme 24:8 na 2Nyakati 36:9).

Rudi nyumbani

Print this post