Title June 2023

Petro na Adrea waliitwa na Bwana wakati gani?

Swali: Katika kitabu cha Luka 5:1-7 tunaona kuwa Bwana Yesu aliwakuta Petro na Andrea ufukweni na akawaita, lakini tukirejea kwenye Yohana 1:35-42 tunasoma kuwa aliwaita wakati wapo kwa Yohana Mbatizaji?.. Je biblia inajichanganya?

Jibu: La! Biblia haijichanganyi hata kidogo, vinginevyo kitabu chote kitakuwa cha uongo!.. Lakini kwasababu ni kitabu cha kweli,  basi kamwe hakiwezi kujichanganya!.

Kabla ya kuichambua mistari hiyo hebu tuisome kwanza..

Luka 5:1 “Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,

2  akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, lakini wavuvi wametoka, wanaosha nyavu zao.

3  Akaingia katika chombo kimoja, NDICHO CHAKE SIMONI, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni.

4  Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.

5  Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, TUMEFANYA KAZI YA KUCHOSHA USIKU KUCHA, TUSIPATE KITU; LAKINI KWA NENO LAKO NITAZISHUSHA NYAVU.

6  Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika”

Hapa ni kweli Bwana aliwakuta Andrea na Petro baharini wakivua samaki.. Lakini katika kitabu cha Yohana tunasoma habari nyingine tofauti kidogo..

Yohana 1:35 “Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake.

36  Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!

37  Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.

38  Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?

39  Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi.

40  ANDREA, NDUGUYE SIMONI PETRO, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.

41  HUYO AKAMWONA KWANZA SIMONI, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo).

42  Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe)”.

Uhalisia ni kwamba Bwana Yesu alikutana na Adrea na Petro kwa mara ya kwanza kipindi wanatoka kwa Yohana Mbatizaji, lakini Bwana Yesu hakuwaambia wamfuate, (yaani wawe wanafunzi wake)!.. Lakini kwa tukio lile tayari walikuwa wameshafahamiana na Bwana.

Sasa tunapokuja katika tukio la kule baharini, ndipo Kristo anawaambia waache Nyavu zao wamfuate na yeye atawafanya kuwa wavuvi wa watu badala ya kuwa wavuvi wa samaki.

Kwahiyo  katika tukio hili la pili ni wazi kuwa tayari Petro na Andrea walikuwa wanamjua Bwana, Ndio maana tunaona hata haikuwa ngumu kwa Petro kumkubalia Bwana akitumie chombo chake katika kuwafundisha makutano (Na Bwana anaonyesha kama kuwa na ujasiri wote katika kutumia chombo cha Petro na kumpa maagizo kana kwamba tayari wanajuana).. na ndio maana pia tunaona haikuwa ngumu kwa Petro kumwamini Bwana na kwenda kushusha nyavu kwa neon la Bwana.. kwasababu tayari alikuwa anamjua, walishakutana huko nyuma..

Kwahiyo hakuna mkanganyiko katika habari hizo, isipokuwa ni waandishi wawili wamenukuu matukio mawili tofauti.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Yakobo na Yohana waliitwa “Wana wa Ngurumo”?

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?

Je Bwana Yesu aliruhusu wanafunzi wake kubeba Fimbo au hakuwaruhusu? (Marko 6:8 na Mathayo 10:10).

Rudi nyumbani

Print this post

Manyoyota ni nini (Ayubu 37:6)

Manyoyota ni neno lingine la “manyunyu”. Manyunyu ya mvua kwa lugha nyingine yanaitwa “manyoyota”

Ayubu 37:6 “Kwani huiambia theluji, Anguka juu ya nchi; Na vivyo manyonyota ya mvua, Na hayo maji ya mvua yake kubwa”.

Baraka za Bwana zinafananishwa na manyunyu ya mvua..

Ezekieli 34:26 “Nami nitawafanya wao, na mahali palipo pande zote za mlima wangu, kuwa baraka, nami nitaleta manyunyu kwa wakati wake; yatakuwako manyunyu ya Baraka”

Tunapoenda katika njia zake Bwana atatunyeshea manyunyu ya Baraka.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

IJUE HEKIMA YA MUNGU KATIKA KUKUINUA KIMAISHA.

Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote

Wakolosai 3:5 inamaana gani?

Kwanini mtu afanye miujiza na bado asiende mbinguni?

Rudi nyumbani

Print this post

Kuguguna maana yake nini? (Ayubu 30:3 )

Neno “kuguguna” linapatikana mara moja tu katika kitabu cha Ayubu 30:3 na maana yake ni “kutafuna”

Ayubu 30: 2 “Naam, uwezo wa mikono yao utanifaa nini? Watu ambao nguvu zao zimekoma. 

3 Wamekonda kwa uhitaji na njaa; HUGUGUNA NCHI KAVU, penye giza la ukiwa na uharibifu”

Hapa maandiko yanalizungumzia kundi la watu ambao ni maskini, wasio na nguvu, huguguna (hutafuna) riziki zao mahali pakame, penye giza na uharibifu.

Ufunuo kamili kwa mtu yule anayemtegemea mwanadamu.. Maandiko yanasema atakaa mahali pakame, katika nchi ya chumvi..

Yeremia 17:5 “ Bwana asema hivi, AMELAANIWA MTU YULE AMTEGEMEAYE MWANADAMU, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.

 6 Maana atakuwa kama FUKARA NYIKANI, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani PALIPO UKAME, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.”

Bwana atusaidie tumtegemee yeye siku zote, na kumfanya yeye kuwa kinga yetu.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Hazama ni nini katika biblia?(Ezekieli 16:12, Kutoka 24:47)

RACA

HAMA KUTOKA GIZANI

Bwana alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto”

Mapooza ni nini? Na je! Twawezaje kuepukana nayo?

Rudi nyumbani

Print this post

NI INJILI GANI UNAHUBIRI?

Masomo maalumu kwa watumishi wa Mungu (Wahubiri).

Je umebeba ushuhuda gani katika injili yako?.

Tujifunze jambo kwa Yohana Mbatizaji..

Yohana 10:40 “Akaenda zake tena ng’ambo ya Yordani, mpaka mahali pale alipokuwapo Yohana akibatiza hapo kwanza, akakaa huko.

41  Na watu wengi wakamwendea, wakasema, yohana kweli hakufanya ishara yo yote, LAKINI YOTE ALIYOYASEMA YOHANA KATIKA HABARI ZAKE HUYU YALIKUWA KWELI.

42  Nao wengi wakamwamini huko”.

Hapo maandiko yanasema Yohana hakufanya ishara yoyote kama alivyofanya Musa katika hatua ya kuwahubiria ukombozi wana wa Israeli, au kama alivyofanya Eliya aliposhusha moto, au kama alivyofanya Eliya na manabii wengine..

Lakini Yohana yeye tunasona alibeba kitu kingine cha ziada.. Na kitu hicho ni “USHUHUDA WA KWELI WA YESU”. Na ndicho kilichomfanya aonekane mbele za Mungu kuwa mkuu kuliko manabii wote waliotangulia..

Mathayo 11:9  “Lakini kwa nini mlitoka? Ni kuona nabii? Naam, nawaambia, na ALIYE MKUU ZAIDI YA NABII.……

11  Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa WANAWAKE ALIYE MKUU KULIKO YOHANA MBATIZAJI; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye”.

Kwahiyo kumbe kinachojalisha si miujiza?, si ishara, si maajabu tunayoyatenda.. bali ni kile tunachokihubiri kumhusu Yesu?.. Je kina ukweli?.. na kama kina ukweli, je ni katika kiwango gani?

Yohana alianza kuhubiri habari za Toba na ondoleo la dhambi na kusema Ufalme wa Mungu umekaribia wamwamini yeye ajaye.

Mathayo 3:1 “Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema,

Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Injili ya namna hii ndiyo Bwana Yesu aliyoanza kuihubiri pia…

Mathayo 4:17 “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia”.

Umeona injili ya Yohana iliyovyofanana na ya Bwana?..Yohana aliuona ushuhuda wa Yesu na akauhubiri kabla hajaja, aliona hizi ni nyakati za kutubu na kumrudia Mungu, kwasababu ufalme wa Mungu umekaribia!!.. .

Vile vile hakuanza kuwaambia watu watubu halafu baadaye waendelee na dhambi zao, bali aliwaambia watubu na baada ya hapo wazae matunda yapatanayo  na toba zao, wala wasijisifie dini, wala madhehebu.. Maana yake baada ya kutubia uzinzi ni lazima waishi maisha ya usafi baada ya hapo, kama umetubia ulevi ni lazima wauache ulevi, kama wametubia ukahaba ni lazima wauache ukahaba na vifaa vyote vya ukahaba, ikiwemo mavazi!..(hiyo ndio maana ya kuzaa matunda yapatanayo na toba).

Luka 3:7 “Basi, aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?

8  Basi, TOENI MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto.

9  Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; BASI KILA MTI USIOZAA MATUNDA MAZURI HUKATWA NA KUTUPWA MOTONI”.

Injili ya namna hii ndiyo iliyobarikiwa na Bwana Yesu, na ndiyo iliyochaguliwa kuwa NJIA KWAAJILI YA BWANA!, Na ndiyo  iliyomfanya Yohana awe mkuu kuliko manabii wote ingawa hakufanya muujiza wowote.

Je! Na wewe kama mtumishi wa Mungu unahubiri nini? Je unahubiri mambo ya ulimwengu huu au injili ya ufalme wa Mbinguni??..  Injili yako ni ya magari na majumba na pesa?..

Kumbuka Injili ya ufalme wa mbinguni ni ile ile haijabadilika ambayo ni “kutubu na kuzaa matunda yapatanayo na toba kwamaana ufalme wa mbinguni umekaribia” Huo ndio ushuhuda wa Yesu na ndio roho ya unabii.

Ufunuo 19:10b “….. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii”.

Vile vile usikimbilia kutafuta au kutengeneza miujiza, usitumie nguvu nyingi kutafuta maajabu… bali tafuta kwanza Ushuhuda wa Yesu, ukiupata huo utakuwa umepata muujiza mkubwa sana katika utumishi wako!.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

WAKO WATATU WASHUHUDIAO MBINGUNI NA DUNIANI.

IJUE HEKIMA YA MUNGU KATIKA KUKUINUA KIMAISHA.

JE UMEKUFA PAMOJA NA NANI?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Wagalatia 6:1 inaposema ‘ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe’

Wagalatia 6:1 ‘Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe’.

JIBU: Hapa biblia inatupa mwongozo sahihi wa jinsi ya kuwavuta upya ndugu ambao walianguka katika dhambi. 

Tunafundishwa tuwarejeshe katika Roho ya upole, maana yake sio ya kulaumu au ya ukali. Kwamfano utakuta mtu karudi nyuma katika ulevi wake aliokuwa nao mwanzoni.  hapo yakupasa utumie busara kumrejesha upya ili iwe  rahisi tena mtu huyo kugeuka na kutubu, kuliko kutumia ukali mfano kumkaripia au vinginevyo. Ukitumia kauli za lawama au mashtumu, si rahisi kumvuta, kinyume chake zitamfanya achukie zaidi au akasirike.

Lakini pia sehemu ya pili anasema..ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.

. Maana yake ni kwamba hata wewe mwenyewe Unaweza ukajaribiwa na shetani uwapo katika kazi hii ya kuwavuta wengine waliokengeuka katika wokovu. Kwamfano huyo mlevi anaweza akakutukana, halafu wewe ukakasirika, ukaanza kurejesha lugha za matusi kwake kwasababu ya hasira, hapo tayari umeshaanguka katika dhambi.

Baadhi ya watu wa Mungu wamejaribiwa na kuanguka  katika uzinzi walipokuwa wanafanya huduma Kwa watu walio wa jinsia tofauti na wao. Wengine katika anasa waliposhirikiana  na watu wa kidunia waliowashuhudia habari za Yesu.

Hivyo tunapaswa tujichunge nafsi zetu sana tuwapo katika kuipeleka habari njema kwa makundi ya watu tofauti tofauti. Kwasababu na sisi pia shetani anatuwinda. Lakini Tukiwa watu wa maombi na kuliishi Neno tutajilinda sana  nafsi zetu na mitego hiyo ya shetani. Ndio maana ya hilo Neno ‘ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe’.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo

Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?

Waliouawa Shitimu kwa pigo walikuwa ni watu Elfu 23 au elfu 24?.

NINYI AKINA BABA MSIWACHOKOZE WATOTO WENU

Rudi Nyumbani

Print this post

DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.

Hizi ni dalili 9 za mtu mwenye pepo.

1.Hofu.

Ukiona kuna hofu ndani yako isiyoisha, kila wakati unaishi katika hali ya  wasiwasi wa kitu usichokijua wala usichokiona, kila wakati unapata mshtuko na mkandamizo mkubwa wa mawazo, furaha inakuwa haidumu ndani yako, dakika yoyote unaona au unahisi kama utapoteza maisha..hizo ni roho chafu za mapepo zimekuingia, hivyo tafuta msaada wa maombezi haraka sana.

Warumi 8:15 “Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba”.

2. Ndoto zinazojirudia rudia.

Ukiona unaota Ndoto zinazojirudia rudia, ndani ya kipindi kifupi… na zote zina maudhui ya kishetani ikiwemo vifo, uzinzi, mauaji, au vitisho. Tafuta msaada wa maombezi.

3. Sauti.

Ikiwa unasikia sauti zinakuita jina lako au zinakupa taarifa Fulani au maagizo fulani na zinajirudia mara kwa mara, (tofauti na ukiwa katika mazingira ya kusali au katika nyumba ya ibada), Tafuta msaada wa maombezi.

4. Kiburi

Ukiona una kiburi kilichopitiliza kilichoshuhudiwa na watu wengi pamoja na chuki nyingi na vinyongo na hasira zilizopitiliza, hiyo sio hali ya kawaida…katafute msaada wa maombezi haraka sana.

5. Nguvu za Ajabu

Ukiona una nguvu za ajabu katika mwili wako, ambazo chanzo chake hukielewi katafute msaada wa maombezi.

6. Kufanya vitu pasipo kujitambua

Ukiona unafanya vitu pasipo kujitambua, (pasipo kuwa na habari)… baada ya muda kupita ndio unakuja kuambiwa kuwa ulifanya hiki au kile, au wewe mwenyewe ndio unakuja kugundua ulifanya hiko kitu pasipo kujitambua.. Katafute msaada wa maombezi.

7. Tabia chafu

Ukiona unaendeshwa na tabia chafu usiyoweza kujizuia, tafuta msaada wa maombezi.

8. Magonjwa yasiyoeleweka

Ukiona unapata ugonjwa au magonjwa yanayoonyesha tabia zisizo za kawaida, (maana yake yana badilika badilika), leo utaumwa hiki kesho kingine tofauti kabisa na cha jana, tafuta msaada wa maombezi..

9. Hamu ya kusoma Neno na kufanya Maombi

Ukiona Hamu ya kusoma Neno na kufanya maombi imepungua ndani yako kwa kiwango kikubwa, tafuta msaada wa maombezi.

Kumbuka!…Mtu mwenye pepo ndani yake kamwe hawezi kumtumikia Mungu, kwani roho hizo siku zote zinapingana na roho wa Mungu. Mtu anaweza kweli kutamani kumtumikia Mungu, lakini roho hizo zitamvunja moyo na kupingana naye na kumtesa na kumletea kukata tamaa na mateso. Hivyo ni lazima zitoke kwanza na kuwa huru ndipo aweze kumtumikia Mungu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TABIA KUU TATU ZA WAHUBIRI WALIORUDI NYUMA NA KUMWACHA MUNGU.

KWANINI MITUME WAMUULIZE BWANA FARAGHANI?

KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

EPUKA KUUNDA MATARAJIO YAKO, KWENYE AHADI ZA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

ZIJUE TABIA ZA AHADI ZA MUNGU KWA MWAMINIO.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima.

Leo tutaona Tabia Moja ya ahadi za Mungu, na Kwa kuijua hiyo basi itakutia moyo wewe ambaye upo katika matarajio ya kuzipokea ahadi timilifu za Mungu.

Nataka tujifunze Kwa Ibrahimu. Kama tunavyojua Mungu alimwahidia kuwa atakuwa na uzao mkubwa kama nyota za mbinguni kwa idadi yake jinsi zisivyoweza kuhesabika. (Mwanzo 15:5).

Lakini katika kuzipokea haikuwa sawa na matarajio yake, Bali zilikuwa za kukwama kwama sana. Utaona Sara alikuwa mgumba, mpaka Ibrahimu anakufa aliambulia mtoto mmoja tu kutoka Kwake mwanamke aliyeitwa mama wa mataifa mengi..Lakini heri ingekuwa Kwa Ibrahimu tu, lakini bado tunaona Kwa Isaka,. Rebeka naye alikuwa na shida katika uzazi, mpaka kuwazaa wale watoto wawili yaani Esau na Yakobo, lilikuwa ni jambo la kulisumbukia sana.. Vivyo hivyo hata Kwa Yakobo, mke wake kipenzi Raheli alikutwa na matatizo hayo hayo…

Hawa wote ndio watu ambao waliahidiwa na Mungu kuwa uzao wao utaongezeka Kwa wingi Kwa mfano wa nyota za mbinguni…lakini tunaona Kila wanapotaka kuongezeka walikwama kwama.

Utajiuliza ni kwanini? 

Sio kwamba walikuwa na shida au laana za ki-ukoo kama wengi wanavyodhani..au kwasababu ya majina yao yamefungwa,  Jibu ni hapana.. kwasababu Mungu tayari alishambariki Ibrahimu kwa kumwambia atakuwa baba wa mataifa mengi, alishabarikiwa,  lakini Mungu anataka kutufundisha sisi Tabia za ahadi zake jinsi zilivyo katika baadhi ya majira.

Sasa tunaona wakati wa Mungu ilipofika  jambo hili lilikuja kugeuka ghafla. Na watu Hawa ambao walionekana ni wenye wagumba wengi.. walianza kuzaliana Kwa wingi ambao uliushtusha ulimwengu. Pindi walipoenda Misri, walianza kuzaa, Kwa kasi hata ya kulipitia taifa la Misri   ndani ya wakati mfupi sana .walienda watu sabini tu lakini Kwa muda mfupi walikaribia kulizidi taifa la mamilioni ya watu.

Ikawa tishio kubwa Kwa Wamisri, mpaka wakabuni mpango wa kuwauwa watoto wote wa kiume watakaozaliwa..lakini bado hilo halikuzuia kitu. Wakati familia Moja ya Wamisri inazaa watoto wawili, familia Moja ya kiisraeli inazaa watoto kumi na Tano. ..

Kutoka 1:8-22

[8]Basi akainuka mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu.

[9]Akawaambia watu wake, Angalieni, watu wa wana wa Israeli ni wengi tena wana nguvu kuliko sisi.

[10]Haya! Na tuwatendee kwa akili, wasije wakaongezeka; tena, ikitokea vita, wao nao wasije wakashikamana na adui zetu na kupigana nasi, na kutoka katika nchi hii.

[11]Basi wakaweka wasimamizi juu yao wawatese kwa mizigo yao. Nao wakamjengea Farao miji ya kuwekea akiba, Pithomu na Ramesesi.

[12]Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea. Nao walichukiwa kwa sababu ya wana wa Israeli.

[13]Wamisri wakawatumikisha wana wa Israeli kwa ukali;

[14]wakafanya maisha yao kuwa uchungu kwa kazi ngumu; kazi ya chokaa na ya matofali, na kila namna ya kazi ya mashamba; kwa kazi zao zote walizowatumikisha kwa ukali.

[15]Kisha mfalme wa Misri akasema na wazalisha wa Waebrania, mmoja jina lake aliitwa Shifra, na wa pili jina lake aliitwa Pua;

[16]akasema, Wakati mwazalishapo wanawake wa Kiebrania na kuwaona wa katika kuzaa, ikiwa ni mtoto mwanamume, basi mwueni, bali ikiwa ni mtoto mwanamke, na aishi.

[17]Lakini wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, wasifanye kama walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri, lakini wakawahifadhi hai wale wanaume.

[18]Basi mfalme wa Misri akawaita wale wazalisha na kuwauliza, Kwa nini kufanya jambo hili, na kuwahifadhi watoto waume wawe hai?

[19]Wazalisha wakamwambia Farao, Ni kwa sababu hao wanawake wa Kiebrania si kama wanawake wa Kimisri; kwa kuwa ni hodari hao, nao huzaa kabla mzalisha hajapata kuwafikilia.

[20]Basi Mungu akawatendea mema wale wazalisha; na hao watu wakaongezeka sana, wakaendelea na kuzidi kuwa na nguvu nyingi.

[21]Ilikuwa kwa sababu wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, akawasimamishia nyumba.

[22]Kisha huyo Farao akawaagiza watu wake, akisema, Kila mtoto mwanamume atakayezaliwa mtamtupa mtoni, na kila mtoto mwanamke mtamhifadhi hai.

Lakini ongezeko hilo.kubwa, halikuanza hivyo.. uhodari huo wa Waisraeli kuzaliana Kwa kasi vile haikuwa kipaji, au Hali waliyokuwa nayo tangu mwanzo, Bali walianza kama Kwa kusua-sua sana..Lakini mwisho wa siku ahadi ilipokomaa ule uwingi kama nyota za mbinguni waliuona, hakukuwa na mgumba.

Ni Nini nataka tuone?

Sikuzote jambo lolote ambalo Mungu anatuahidia, ni kawaida katika hatua za mwanzo kuenda kama Kwa kusua sua hivi, SI vyepesi kuona vikitirika Moja Kwa Moja kama wengi tunavyotarajia..Kitaanza kidogo kama unaona mwanga Fulani hivi, halafu kitasimama, baadaye Kitaanza Tena, Kisha kitasimama, kitaonyesha dalili zote za kuongezeka, Kisha hakitaendelea Tena..hivyo hivyo kinaweza pita kipindi Fulani. Sasa ukijikuta katika Mazingira kama hayo hupaswi kuvunjika Moja na kujiona kama utakuwa na makosa Fulani, au Mungu ameghahiri ahadi zake..Jibu ni hapana. Hupaswi kukata tamaa, shikilia ahadi ya Mungu, ukiamini kuwa yeye ni mwaminifu lazima atimize ahadi zake kwako, kukuongeza.

Moja siku isiyokuwa na jina. Utaona mtiririko ambao haujautarajia, itakuwa siku baada ya siku ni kuongezeka tu, Wala hakuna kupungua. Wala kukwama-kwama kama mwanzo. Lakini hiyo yote hutegemea kung’ang’ana kwako na ahadi za Mungu sasa.

Jambo hili linasimama Mahali popote pale Mungu alipoweka maono yake moyoni mwako. Iwe ni katika huduma, kazi, uzao.n.k. Usiache tu kushikilia ahadi za Mungu, Tena ufurahi kwasababu maandiko yanasema hivyo, kwani uwingi wako upo karibuni.

Isaya 54:1

[1]Imba, wewe uliye tasa, wewe usiyezaa; paza sauti yako kwa kuimba, piga kelele, wewe usiyekuwa na utungu; maana watoto wake aliyeachwa ni wengi kuliko watoto wake yeye aliyeolewa, asema BWANA.

Shalom.

Je umeokoka? Je unamtambua kuwa Yesu yupo mlangoni kurudi? Ikiwa bado unasubiri nini? Tubu dhambi zako ukabatizwe katika jina la Bwana Yesu Kristo upokee ondoleo la dhambi zako. 

Kumbuka: UNYAKUO UPO KARIBU.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?

PALE AHADI ZA MUNGU ZINAPOKUJARIBU.

Tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu.

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

WEWE U MUNGU UONAYE.

Dina akatoka kuwaona binti za nchi. (Mwanzo 34:1)

MAJARIBU 10 WANA WA ISRAELI WALIYOMJARIBU MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)

Swali: Maandiko yanasema Mungu anaketi katika Nuru (1Timotheo 6:16 na Yohana 1:5) lakini yanasema tena Mungu anakaa kwenye giza (1Wafalme 8:12) Je yanajichanganya?.

Jibu: Tuisome mistari hiyo kwanza kabla ya kuingia katika ufafanuzi.

1Timetheo 6:16 “ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, AMEKAA KATIKA NURU ISIYOWEZA KUKARIBIWA; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina”

Tusome tena kitabu cha Wafalme..

1Wafalme 8:12 “Ndipo Sulemani akanena, Bwana alisema ya kwamba ATAKAA KATIKA GIZA NENE. 

13 Hakika nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako milele”

Je biblia inajichanganya?..

Jibu ni La! Biblia haijichanganyi mahali popote kwasababu ni Neno la Mungu lililojaa nguvu na Uweza na kweli.

Tukirudi katika mistari hiyo, ukweli ni kwamba Mungu juu mbinguni aliko, hayupo katika giza wala hakai katika giza, bali yupo katika Nuru kuu isiyoweza kukaribiwa sawasawa na andiko hilo la 1Timotheo 6:16 “…ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, AMEKAA KATIKA NURU ISIYOWEZA KUKARIBIWA”.

Ni sawasawa na jinsi tunavyomtolea matoleo yetu… Si kwamba yeye ana uhitaji na kwamba sisi tunaweza kumwongezea kitu, au tunaweza kumwibia, kiuhalisia sisi hatuwezi kumpa kitu Mungu, kwasababu vyote tutakavyompa ni vya kwake yeye, ndiye kaviumba… vile vile hatuwezi kusema tunamwibia Mungu kwasababu vyote yeye ni vya kwake..

Lakini linapokuja suala la mahusiano yake na sisi, Mungu aliye Mkuu na mweza huwa anajishusha na wakati mwingine kujifananisha na sisi, ndio maana utaona anajiweka na yeye kama mwanadamu mwenye kuhitaji kuhudumiwa kuhudumiwa, mwenye kuhitaji kupendwa, mwenye kujengewa nyumba n.k

Sasa katika hali hiyo ya kujishusha ili kujenga mahusiano yetu sisi na yeye, huwa anahitaji kufanyiwa vitu vilivyo bora kama tu sisi tunavyoweza kuwafanyia wale tunaowaheshimu vitu vilivyo bora, ndio hapo anaagiza tumtolee vile vinavyotugharimu sadaka zisizo kilema, vile vile na tumjengee Nyumba zilizo bora kuliko zetu tunazoishi.

Sasa Mfalme Daudi pamoja na Sulemani mwanae, kwa kutambua hilo waliwaza kumjengea Mungu nyumba yenye utukufu kuliko zao walizoishi. Waliona kule Sanduku la Mungu lilipo ni kwenye “giza nene” ndani ya Mapazia (yaani mahema).. Na wakati wenyewe wanakaa kwenye nyumba za Mierezi zilizojaa marumaru na mwangaza pande zote.

Hivyo dhamiri zao zikawagusa na kusema Mungu hatakaa kwenye “mapazia kule” bali atakaa kwenye nyumba kubwa yenye utukufu na mwangaza mwingi kuliko walizokuwa wanaishi wao, Ingawa walijua kabisa kuwa Mungu kwa ukuu wake na uweza wake hawezi kujengewa nyumba na wanadamu.. lakini waliadhimia kumjengea hivyo hivyo kwasababu walimjua Mungu katika viwango vingine tofauti na wengine walivyomjua.

1Wafalme 8:26 “Sasa, Ee Mungu wa Israeli, nakusihi, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako, Daudi, baba yangu. 

27 Lakini Mungu je? Atakaa kweli kweli juu ya nchi? Tazama, mbingu hazikutoshi, wala mbingu za mbingu; sembuse nyumba hii niliyoijenga!

28 Walakini uyaelekee maombi ya mtumwa wako, na dua yake, Ee Bwana, Mungu wangu, uisikilize sauti na maombi ya mtumwa wako, aombayo mbele zako leo”.

2Samweli 7:1 “Ikawa, mfalme alipokuwa akikaa katika nyumba yake, hapo Bwana alipomstarehesha, asiudhiwe na adui zake waliomzunguka pande zote,

2 mfalme akamwambia Nathani, nabii, Angalia sasa, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi, bali sanduku la Mungu linakaa ndani ya mapazia.

3 Nathani akamwambia mfalme, Haya, fanya yote yaliyomo moyoni mwako; maana Bwana yu pamoja nawe. 

4 Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema,

5 Enenda, ukamwambie mtumishi wangu, Daudi, Bwana asema hivi, Je! Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake?

 6 Kwa maana mimi sikukaa ndani ya nyumba, tangu siku ile niliyowatoa wana wa Israeli katika Misri, hata leo, lakini nimekaa katika hema na maskani.

7 Mahali mwote nilimokwenda na wana wa Israeli wote, je! Nimesema neno lo lote na mtu ye yote wa waamuzi wa Israeli, niliyemwagiza kuwalisha watu wangu Israeli, nikisema, Mbona hamkunijengea nyumba ya mierezi? 

8 Basi, sasa, mwambie mtumishi wangu, Daudi, maneno haya, Bwana wa majeshi asema hivi, Nalikutwaa katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo, ili uwe mkuu juu ya watu wangu, juu ya Israeli;

9 nami nimekuwa pamoja nawe kila ulikokwenda, na kuwakatilia mbali adui zako wote mbele yako; nami nitakufanyia jina kuu, kama jina la wakuu walioko duniani.

 10 Tena nitawaagizia mahali watu wangu Israeli, nami nitawapanda, wapate kukaa mahali pao wenyewe, wasiondolewe tena; wala wana wa uovu hawatawatesa tena, kama hapo kwanza; 

11 naam, kama vilivyokuwa tangu siku ile nilipowaamuru waamuzi, wawe juu ya watu wangu Israeli; nami nitakustarehesha mbele ya adui zako wote. Tena Bwana anakuambia ya kwamba Bwana atakujengea nyumba. 

12 Nawe siku zako zitakapotimia, ukalala na baba zako, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayetoka viunoni mwako, nami nitaufanya imara ufalme wake”

Ni nini tunachoweza kujifunza katika habari hii?.

Mungu ni mkuu lakini linapokuja suala la mahusiano yetu na yake anajiweka katika nafasi kama ya Mtu, Ikiwa unaishi katika nyumba nzuri yenye marumaru na Nuru kila mahali, lakini nyumba ya Mungu kule unakoabudu ni giza jitafakari mara mbili, (hapo ni sawa na umemweka Mungu kwenye giza) usiseme Mungu ni mkuu hawezi kujengewa nyumba.. ni kweli ni mkuu lakini anawivu kama wa mwanadamu wa kawaida (Kumbukumbu 4:24).

Kama humtolei Mungu vile vinavyopendeza, ukiwaza kwamba yeye ni tajiri kaumba vyote, na hana haja na chochote, tafakari mara mbili, hata Daudi aliwaza hivyo lakini bado aliwaza kumjengea Bwana Nyumba na Mungu akambariki na kumpa jina.

Kama Kitabu chako cha kumbukumbu za kazi ni kizuri lakini biblia yako ni makaratasi yaliyo chanika chanika, tafakari mara mbili.

Kama vitabu vyako na nyaraka zako zipo sehemu safi na katika hali nzuri lakini kitabu chako cha uzima (biblia) kipo makabatini na kwenye mikoba michafu, hapo umemwekea Mungu kwenye giza nene!! Na ni dharau za hali ya juu, tafakari mara mbili. Haya ni mambo madogo tu! Lakini yanatupunguzia utukufu mwingi sana na heshima yetu nyingi sana kwa Mungu

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?

HAMA KUTOKA GIZANI

MKUU WA ANGA.

Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo

Rudi nyumbani

Print this post

Yesu alipopanda kuomba kwanini atokewe na Musa na Eliya na sio manabii wengine?

SWALI: Katika ule mlima mrefu, aliopanda Yesu na wanafunzi wake kuomba, kwanini atokewe na Musa na Eliya na sio manabii wengine? Mfano wa Isaya au Samweli?


JIBU: Awali ya yote yeye kutokewa na wale watu halikuwa Kwa lengo lake. Bali Kwa lengo la wale wanafunzi aliokuwa nao,  Ili kutimizi mambo yafuatayo.

1 ) Kutimiza unabii mkuu uliomuhusu yeye.

a) Unabii wa kwanza ni ule alioutoa Musa kuwa atakuja Nabii mwingine kama yeye na kwamba watu wamsikilize..

Kumbukumbu la Torati 18:15

[15]BWANA, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye.

Soma pia Matendo 3:22-25,. Hivyo wayahudi walikuwa na matarajio ya kuona mtu anayefanana  na Musa atakayeleta Sheria mpya  akija duniani, lakini akiwa na nguvu na uweza mwingi mfano wa Musa..

Ndio sababu ya Musa kutokea mbele ya wanafunzi wake, ili Mungu awathibitishie huyu ndio yule Musa aliyemnenea habari zake.

b) Lakini pia unabii uliohusu kutangulia Kwa Eliya kabla ya Kuja kwake duniani.

Wanafunzi walikuwa na dukuduku kama huyu, ndiye Kristo aliyetabiriwa au sio, na kama ndio mbona Eliya hajatangulia mbele yake tukamwona? Kwasababu waliambiwa hivyo na waandishi. Lakini sasa walipomwona Eliya mwenyewe amesimama mbele ya Yesu wakaamini lakini bado hawakuelewa..Sasa walipokuwa wanashuka ndio wakapata nguvu ya kumuulizia hilo swali.. Na hili ndio likawa jibu lake.

Mathayo 17:9-13

[9]Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu.

[10]Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza?

[11]Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote,

[12]ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao.

[13]Ndipo wale wanafunzi walipofahamu ya kuwa amesema nao habari za Yohana Mbatizaji.

2) Na Pili ni Kutoa utata Kuwa yeye sio mmojawapo wa manabii wakubwa wa kale wanaodhaniwa.

Utakumbuka kabla ya kupanda mlimani aliwaliza watu kuwa wanamzungumzia kuwa yeye ni nani? Wanafunzi wakamjibu kuwa wanasema yeye ni Eliya, wengine mmojawapo wa manabii wa Kale.n.k. Hivyo kulikuwa na utata mwingi. Lakini siku hiyo alitoa utata huo Soma.Mathayo 16:13-18. 

Mitume walipoona sura za manabii wao wa kale wamesimama mbele ya Yesu, mwenye utukufu mwingi sana kupitia wao. Wakaamini yeye ni zaidi ya manabii wote wakubwa Kwa wadogo waliowahi kutokea katika historia.

3) Lakini pia alikuwa na Lengo la kuwafunulia kuwa atakufa kama mmojawapo wa manabii wakubwa, lakini pia atapaa kama mmojawapo wa manabii wakubwa.

Musa alikufa, lakini Eliya alipaa.

Yesu ndio mtu pekee miongoni mwa wanadamu, aliyekufa, Kisha akazikwa, kisha akafufuka.na mwisho akapaa. Kwa hiyo Ile ilikuwa ni lugha ya kinabii, kueleza hatma yake na ndio maana hata manabii Hao walikuwa wakizungumza mambo yahusuyo kufa kwake na kufufuka.(Luka 9:31).  

Hizo ndio zilikuwa sababu kuu za Bwana kutokewa na manabii wale wawili na sio wengine. Na walipokuwa wanashuka Akawaambia wanafunzi wake wasimwambie mtu mpaka atakapofufuka katika wafu.

Kufunua nini?

SI wote watamwona Yesu katika kilele Cha utukufu wake, isipokuwa wale tu walio na kiu na yeye. Ambao watakuwa tayari kuwa karibu naye wakati wote mfano wa Hawa wanafunzi watatu yaani Yohana, Petro na Yakobo.

Ukimpenda Yesu tumia muda mwingi kuwepo uweponi mwake. Utamjua sana Kwa mapana na marefu yake.

Je! Umeokoka? Je unatambua kuwa hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi? Dalili zote zimeshatimia, unasubiri nini usimpe Bwana maisha yako, embu fanya uamuzi leo. Tubu dhambi zako, mgeukie Yesu, Unyakuo usikupite. Ikiwa utapenda upate mwongozo huo, wasiliana nasi kwa namba zetu hizi bure +255693036618 /+255789001312

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

LAKINI MAKINDA WAWEZA KUYATWAA UWE NAYO.

Rudi nyumbani

Print this post

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

Jina la Bwana Yesu litukuzwe Daima. Nakukaribisha katika kuyatafakari maneno ya Mungu.

Lipo andiko ambalo tunaweza kuona ni la kinyonge lakini linatiba kubwa sana kama tukilitumia. Embu tuone ni nini mwandishi huyu mwenye hekima  aliomba Kwa Bwana 

Mithali 30:7-9

[7]Mambo haya mawili nimekuomba;  Usininyime [matatu] kabla sijafa. [8]Uniondolee ubatili na uongo;  Usinipe umaskini wala utajiri;  Unilishe chakula kilicho kadiri yangu. [9]Nisije nikashiba nikakukana,  Nikasema, BWANA ni nani?  Wala nisiwe maskini sana nikaiba,  Na kulitaja bure jina la Mungu wangu.

Nataka uone hapo aliposema..

“Usinipe umaskini wala utajiri;”

Katika maombi yetu ni rahisi sana kumwomba Mungu asitupe Umaskini, lakini ni ngumu sana kumwomba Mungu  asitupe “UTAJIRI”.. Nadhani huo ndio ukweli..

Utajiri ni Ile Hali ya kuwa na uwezo wa kumiliki au kuwa na vitu vingi.

Lakini huyu mtu hapa anamwekea Mungu mipaka katika maeneo hayo mawili, yaani Utajiri na Umaskini, Kwa lugha nyingine anamwambia Mungu sitaki UTAJIRI.. na sababu anaitoa pale “Nisije nikashiba nikakukana, Nikasema, BWANA ni nani?”

Alijua Kuna madhara ya kuwa na tamaa ya kutaka vitu vingi, mfano kuwa na mabilioni ya pesa kwenye akaunti, kuwa na mahekari ya mashamba mengi, kuwa na nyumba nyingi za kuishi na za kupanga, kuwa na magari mengi n.k. Alijua hayo ni matamanio ya Kila mwanadamu lakini alikataa kuyaomba kabisa.

Lakini Watu wengi tunaposoma huu mstari tunaelekeza mawazo yetu kwenye mambo ya Mali tu. Lakini Bwana anamaanisha pia utajiri wa kiroho.

Uchu huu wa kupata Kila kitu, kuwa na Kila kitu, umewavaa watu wengi hata watumishi wa Mungu. Labda utaona anakwenda mbele za Mungu, maombi yake na matazamio yake ni kuwa na upako kuliko watu wote, anachotaka ni Mungu ampe karama zote za Roho. Yeye naye awe Nabii, awe Mchungaji, awe mwinjilisti, awe mwalimu, awe mtume, awe  na karama zote 9 za Roho. Yaani atakaposimama mimbarani watu wamwone yeye ni kama Yesu. Awe mhubiri wa Dunia nzima wa kimataifa, mwenye mafunuo mengi kuliko wote duniani, mwenye kanisa kubwa kuliko yote duniani.

Maombi ya namna hii ni maombi ya utajiri. Na mara nyingi tunapoomba hivi Bwana Huwa hatupi, kwasababu si mapenzi ya Mungu kuomba vitu vilivyo zaidi ya uwezo wetu alivyotukirimia. Kila mmoja kawekewa kipimo chake na Mungu. Na katika hicho ndio tunaomba Mungu akibariki. Lakini si kila huduma Kila karama itakuwa ni yako.

1 Wakorintho 12:28-30

[28]Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.

[29]Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza?

[30]Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri?

Hivyo pale tunapokuwa na Nia ya kiasi, ndipo Mungu anapotuongezea  neema, na ndio tutakapomtumikia Mungu vizuri. Hekima inatufundisha tubadilishe matamanio. Yetu kutoka katika UCHU, mpaka “kutosheka na mishahara yetu”. Na hivyo tutafanya vizuri zaidi katika huduma, karama, na utumishi wetu Kwa ujumla. Watu watasaidika na kile ulichonacho sasa, kuliko kile usichokuwa nacho unakingoja.

Nabii Eliya ambaye alikuwa ni mkuu Kwa nguvu za Mungu, lakini pamoja na hayo hata katika maombi yake alisema “Mimi SI mwema kuliko Baba zangu (1Wafalme 19:4)”akataka Bwana asitishe huduma yake. Kwasababu aliona kama kipimo kile hakustahili kupimiwa.. Hakuwa na uchu wa kiroho. Si ajabu Kwanini Mungu akamtumia Kwa viwango vikubwa namna Ile.

Bwana atusaidie tuonyeshe sasa bidii katika nafasi zetu alizotukirimia leo, zaidi vile ambavyo tunavitazamia kesho. Tutumike Kwa kadiri ya alivyotujalia.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

Aibusu midomo atoaye jawabu la haki (Mithali 24:26)

Bilauri ni nini kibiblia?(Ufunuo 21:11,22:1)

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.

Biblia inasema askofu anapaswa awe mume wa mke mmoja! Je! Wale wasiooa kwa ajili ya injili hawawezi kuwa maaskofu?

Rudi nyumbani

Print this post