Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?

Wapelelezi wa uhuru wa wakristo ni watu gani (Wagalatia 2:4)?

Jibu: Tuanzie kusoma ule mstari wa 3

Wagalatia 2:3 “Lakini Tito aliyekuwa pamoja nami, naye ni Myunani, hakulazimishwa kutahiriwa.

4  BALI KWA AJILI YA NDUGU ZA UONGO WALIOINGIZWA KWA SIRI; AMBAO WALIINGIA KWA SIRI ILI KUUPELELEZA UHURU WETU TULIO NAO KATIKA KRISTO YESU, ILI WATUTIE UTUMWANI;

5  ambao hata saa moja hatukujitia chini yao, ili kwamba kweli ya Injili ikae pamoja nanyi.”

Hapo kuna mambo matatu (3).. NDUGU WA UONGO, 2) WALIINGIA KWA SIRI, na 3) KUUPELELEZA UHURU.

1.NDUGU WA UONGO.

Watu waliookoka waliitwa NDUGU, na hata leo wanaitwa hivyo hivyo “Ndugu”, lakini wapo Ndugu wa Kweli na pia wapo wa “Uongo”. Ndugu wa kweli ni wale waliookoka kikweli kweli, ambao wapo katika kundi au kusanyiko katika Nia ya KRISTO na si kwaajili ya kutafuta mambo yao wenyewe (1Wakorintho 16:20 na Wagalatia 1:2).

Lakini “Ndugu wa Uongo” Hao ni watu ambao wanajiingiza katika kanisa, ikiwa Nia yao si kumtafuta Kristo wala kumtumikia bali kutafuta mambo yao mengine kama Fedha, au Fursa Fulani, na wengine kuupeleleza uhuru wa wakristo na wengine ni mawakala kabisa wa Ibilisi, wanajiunga kwa lengo la kuliharibu kundi na kulisambaratisha. Mfano wa hao ndio wale Paulo aliwaozungumzia katika waraka kwa Wafilipi..

Wafilipi 3:17 “Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi.

18  Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;

19  mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.

20  Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo”.

Makundi haya ya Ndugu wa Uongo, yamesambaa katika nafasi zote, kuanzia Wachungaji, Mitume, manabii, waimbaji, mpaka washirika/waumini.

2. WANAJIINGIZA KWA SIRI

Kundi hili la Ndugu wa Uongo, huwa hawajiingizi kwa wazi bali kwa siri, maana yake ni kwamba wanajigeuza na kufanana na Ndugu wa kweli.. lakini ndani yao wanajua ni nini wanatafuta sawasawa na maandiko yanavyosema..

2Wakorintho 11:13  “Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.

14  Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.

15  Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”

3. KUUPELELEZA UHURU.

Sasa ni Uhuru gani ambao Wakristo wanao?.. Jibu: Ni uhuru unaotuweka mbali na utumwa wa Sheria… Katika Ukristo hatuna sheria za kutahiriwa, kwamba ni lazima mtu atahiriwe au asitahiriwe ndipo akubaliwe na Mungu, vile vile na sheria nyingine zote kama kushika sabato na kushika miezi na sikukuu, kuna aina fulani tu ya chakula n.k hizo zote maandiko yanasema tumewekwa huru nazo..

Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

17  mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo……………………..

20 Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani,

21  Msishike, msionje, msiguse;

22  (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu?

23  Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili”.

Sasa walikuwepo wayahudi ambao wanajiingiza katika kanisa la Kweli na Kristo, si kwa lengo la kumtumikia Bwana, bali kwa lengo la kuwatwika watu mzigo wa kushika sabato, na mwandamo wa mwezi na sikukuu za kiyahudi.

Hata sasa wapo watu baadhi ambao wengine wanatenda mfano wa hayo kwa kujua au kwa kutokujua, mfano mapokeo ya kushika sabato yanauua uhuru wetu katika Kristo, mapokeo ya kutahiriwa yanaua uhuru wetu katika Kristo n.k

Hivyo hatuna budi kuzipima roho, si kila pokeo ni la kupokea.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru

MWENGE WAKO WA UHURU UPO WAPI?

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments