Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)

Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 8 ili tuweze kuelewa vizuri..


Mathayo 22:8 “Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.
9 Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.
10 Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.
11 Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.
12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? NAYE AKATEKEWA”.


“Kutekewa” kunakozungumziwa hapo si Kutekewa maji au kinywaji fulani, hapana!…Bali maana yake Ni “KUKOSA MANENO”


Mtu anayekosa Neno la kujibu pale anapoulizwa, mtu huyo Ndio katekewa..
Katika habari hiyo Bwana Yesu anatoa mfano wa mtu aliyeishiwa maneno baada ya kukutwa hana vazi la harusi.


Hali itakayokuwa kwa wengi katika Ile siku ya mwisho. Maandiko yanaonyesha kuwa katika siku ya mwisho, Bwana atawakataa watu wengi, ambao hawakuwa na vazi la Harusi walipokuwa duniani.
Na vazi la harusi maandiko yameweka wazi kuwa Ni “Matendo ya haki ya watakatifu”.


Ufunuo 19:8 “Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu”


Katika siku ile wengi watadhani Ni dini zao zintakazowapa kibali Cha kuingia uzimani, wengine watadhani Ni Imani zao n.k. pasipo kujua kuwa bila utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu.


Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”


Na Utakatifu hatuupati kwa nguvu zetu, Bali kwa msaada wa Bwana.


Tunapotubu kwa kudhamiria kabisa kuacha dhambi zetu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi Kama bado hatujabatizwa Basi Bwana anatupa Roho wake mtakatifu ambaye huyo ndiye atakayetusaidia sisi kuweza kuwa wakamilifu na watakatifu.


Hivyo tukiupata utakatifu katika maisha yetu, Basi katika Roho tutaonekana mbele zake tumevaa vazi la harusi na hivyo siku Ile hatutatekewa mbele zake, hatutaishiwa maneno.


Lakini tukiyakosa hayo, huku tukitumainia dini zetu, na madhehebu yetu, na theologia zetu… basi tujue kuwa tutakosa cha kujibu mbele zake siku Ile..


Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

BALI WANA WA UFALME WATATUPWA NJE!.

TAFUTA KWA BIDII KUWA MTAKATIFU.

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments