Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;

Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;

SWALI: Kwanini Biblia inakataza kula asali nyingi, nini maana ya mstari huu kiroho?

Mithali 25:16 “Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha; Usije ukashiba na kuitapika”.

Pia sehemu nyingine inasema..

Mithali 25:27 Haifai kula asali nyingi mno; Vile vile mtu kutafuta utukufu wake mwenyewe si utukufu.


JIBU: Asali hufananishwa na Neno la Mungu,

Ezekieli 3:1 Akaniambia, Mwanadamu, kula uonacho; kula gombo hili, kisha enenda ukaseme na wana wa Israeli.  2 Basi nikafunua kinywa changu, naye akanilisha lile gombo.  3 Akaniambia, Mwanadamu, lisha tumbo lako, ulijaze tumbo lako kwa hili gombo nikupalo. Ndipo nikalila, nalo kinywani mwangu lilikuwa tamu, kama utamu wa asali.

Soma pia Ufunuo 10:10. Utalithibitisha hilo.

Na kila mmoja wetu anashauriwa alisome Neno la Mungu (alile) sana kwasababu ndio uzima wetu (Mathayo 4:4).

Mithali 24:13 Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema, Na sega la asali lililo tamu ulionjapo

 Lakini katika maandiko hayo tunaona tena biblia inatuasa tusile nyingi mno kupita kiasi, ikaja kutuletea madhara..Sasa maana yake ni nini? Je! Tulipende Neno la Mungu kwa kiasi au la?

Jibu ni kwamba hapo haimaanishi tulisome/ tujifunze neno la Mungu kwa kiasi hapana.. Bali analenga katika Suala la NIA zetu.. Ni kawaida yetu sisi watoto wa Mungu, kuwa na NIA inayopitiliza hususani pale tunapolifahamu sana Neno la Mungu.

Kwamfano, tunaposoma juu ya neema ya Mungu iliyokuwa inatembea  juu ya Eliya, Kisha tunaposoma kitabu cha Malaki4:4-5, kwamba ahadi imetolewa kuwa Roho ya Elia itarudi tena katika siku za mwisho. Baadhi ya watu wanajiweka katika nafasi hizo, na wanaamini kuwa Mungu anakwenda kuwaandaa kwa roho hiyo ili waje kuionya dunia kwa mapigo na ishara kama za kwake.

Au Musa kafunga siku 40 bila kunywa wala kula, akaongeza na nyingine 40 na yeye bila uongozi wa Roho Mtakatifu anasema na mimi lazima nifunge hivyo.

Wapo wengine wanasema na mimi nisipotokewa na Yesu kama Paulo alivyotokewa kule Dameski, bado sitakwenda kuhubiri injili, hivyo wanasubiriwa kwa miaka watokewe wapewe maagizo, kwa kufunga na kuomba.  Sasa Hali kama hizi zina hatari kwasababu mwisho wa siku zinamfanya asiwe mtu wa matunda kwa kungojea jambo ambalo huwenda Mungu hajalikusudia katika maisha yao, kwasababu   amenia makuu kuliko kipimo kile alichopimiwa na Mungu.

Mtume Paulo aliyasisitiza sana makanisa juu ya jambo hilo akasema..

Warumi 12:16b  “.. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili

Na hapa pia anasema..

1Wakorintho 7:17  “Lakini kama Bwana alivyomgawia kila mtu, kama Mungu alivyomwita kila mtu, na aenende vivyo hivyo. Ndivyo ninavyoagiza katika makanisa yote. 18  Je! Mtu fulani ameitwa hali amekwisha kutahiriwa? Asijifanye kana kwamba hakutahiriwa. Mtu fulani ameitwa hali hajatahiriwa bado? Basi asitahiriwe. 19  Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu bali kuzihifadhi amri za Mungu. 20  Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa. 21  Je! Uliitwa u mtumwa? Usione ni vibaya lakini kama ukiweza kuwa na uhuru, afadhali kuutumia. 22  Kwa maana yeye aliyeitwa katika Bwana hali ya utumwa, ni huru wa Bwana. Vivyo hivyo yeye naye aliyeitwa hali ya uhuru, ni mtumwa wa Kristo.

Ikiwa Bwana kakupa kipimo cha ushemasi, tembea katika hicho kwa uaminifu usilazimishe uwe nabii wa mataifa yote kama Yeremia. Bwana amekuokoa, tumika katika kipimo hicho hicho, ikiwa itampendeza kukunyanyua juu zaidi, basi atafanya kwa wakati wake, lakini kwasasa tujishughulishe na mambo manyonge,

Lakini si hayo tu, wakati mwingine katika kufahamu sana maandiko, hupelekea tabia za majivuno, kujiona unafahamu, kukataa kushauriwa kunazalika ndani ya mtu. Hivyo hupelekea kujifungia mwenyewe milango ya Mungu kuendelea kusema naye. Hivyo ili kuepuka kuitapika asali iliyo nzuri na njema, ni vizuri haya yote tukajiepusha nayo, tunapojifunza kwa bidii Neno la Mungu kila siku.

Tule asali kwa kadiri ya kututosha tusije tukashiba tukaitapika, kwa kukosa shabaha ya maandiko.

Maran Atha.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NJAA IPO?, USIACHE KULA ASALI.

Kwanini iwe ni nchi ibubujikayo maziwa na asali?

Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Aibusu midomo atoaye jawabu la haki (Mithali 24:26)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments