Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?

Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?

Kumbukumbu 23:24 Uingiapo katika shamba la mizabibu la jirani yako, utaweza kula zabibu za kukushibisha, kama upendavyo; ila usitie katika chombo chako. 25 Uingiapo katika mmea wa jirani yako waweza kuyapurura masuke kwa mkono wako; ila usisongeze mundu katika mmea wa jirani yako.

Kwa hio nikiingia katika shamba la jirani yangu, napaswa kula matunda na kushiba, bila, ila nisiweke katika kapu?


JIBU: Hapo unapaswa uelewe haizungumzii tu kuingia katika shamba la mtu mwingine wakati wowote unaojisikia wewe na kuanza kula kwasababu tu maandiko yamesema tule ila tusibebe chochote hapana!!.. Jambo kama hilo linakuja pale unapokuwa katika mazingira ambayo umeshikwa na njaa, na hauna chakula, na ukiangalia hauna chochote mfukoni kwa wakati huo, na mfano ukiendelea mbele katika hali hiyo unaweza ukazimia kwa njaa njiani…Sasa katika mazingira kama hayo hapo mbele za Mungu unaweza kuingia kwenye shamba la mwingine na kula pasipo kuhesabiwa hatia yoyote mbele za Mungu..isipokuwa usijifungashie mazao yake na kuondoka nayo.

Lakini pia jambo la kukumbuka ni hili, sheria hizo walipewa wayahudi , hivyo utamaduni kama huo ulikuwa kwa wayahudi tu peke yao, kwasababu hiyo basi ilikuwa hata mtu akimwona mgeni kaingia katika shamba lake kwa dharura na kuanza kula, hamfanyi chochote kwasababu anajua agizo la Mungu juu ya masuala kama hayo. Lakini kwa mazingira ya watu wa mataifa kama sisi tuliyopo, huwezi tu kuingia katika shamba la mtu asiyemjua Mungu na kuanza kula mazao yake pasipo hata idhini yake, vinginevyo itakuwa ni kujitafutia tu matatizo..Ni rahisi kuingia katika shamba la mtu wa imani moja na wewe(Ndugu yako katika Kristo) kuliko la mtu asiyemjua Mungu,cha msingi ni kutumia hekima ya kwenda kuomba. Na ukikatazwa ondoka utafute pengine.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

JE! NI VEMA KWA MKRISTO KWENDA HOSPITALI AU KUTUMIA MITI SHAMBA ANAPOUGUA?

KANUNI JUU YA KANUNI.

NAOMBA KUJUA WATAKAOENDA MBINGUNI JE! NI WENGI AU WACHACHE?

JE! KUNA DHAMBI KUBWA NA NDOGO?

JE! INAWEZEKANA MTU AKAWA ANAFANYA MIUJIZA NA KUTOA PEPO NA BADO ASINYAKULIWE?

JE! UNAMPENDA BWANA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments