Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

Je! Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?.

Jibu: Kulingana na maandiko mtu wa kwanza kufa alikuwa ni HABILI, mwana wa ADAMU.

Mwanzo 4:8 “Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani].

Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua”.

Sababu ya Kaini kumuua Habili ndugu yake ilikuwa ni wivu. Kwani sadaka yake haikukubaliwa na Mungu lakini ya ndugu yake Mungu aliikubali kwasababu aliitoa katika vitu vilivyonona..na kutoka kwa wazaliwa wa kwanza.

Mwanzo 4:3 “Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa BWANA.

4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. BWANA akamtakabali Habili na sadaka yake;

5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.

6 BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?

7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde”.

Roho ya Habili, ipo peponi sasa, yaani paradiso sehemu ya watakatifu..akingoja ufufuo wa watakatifu, utakaotokea katika siku za mwisho, wakati parapanda ya mwisho itakapolia.

Na pia tunajifunza  tusiwe watu wasiomjali Bwana, kimatoleo kama Kaini, yeye alitoa tu ilimradi…lakini mwenzake alitoa katika vitu vilivyonona na katika wazao wa kwanza, pia tusiwe watu, wenye wivu kama Kaini.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

SISI NI WINDO BORA SANA, LA DHAMBI.

MUNGU ATAKUUA UKIWA MBAYA MACHONI PAKE.

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

USIRUHUSU MUNGU AWEKE UADUI KATI YAKO NA WATU WAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

1 comment so far

Friedrich a son of JESUS%Posted on5:56 pm - Nov 8, 2021

God bless u!

Leave a Reply

UTAPENDA KUCHANGIA HUDUMA HII?

Tutamshukuru Mungu kwa ajili yako, kwa mchango wako, ili kuifanya injili hii isonge mbele Tuma sadaka yako kwa namba hizi:
Airtel:+255789001312 -Devis Magembe
Mpesa: +255767992434-Denis Magembe