JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 5)

Bwana Yesu asifiwe, nakukaribisha katika Makala zinazoeleza juu ya thawabu mbalimbali za Mungu, na vigezo ambavyo Mungu atavitumia kuzitoa thawabu hizo. Tumeshatazama vigezo vya thawabu kadha wa kadha huko nyuma, na sasa, tutaendelea na sehemu yetu ya tano (5)

5) Zipo thawabu za kumiliki miji mingi Zaidi katika ule ufalme wa Mungu.

Mungu ameahidi,kuwapa utawala mkubwa, wale watu ambao watatumika kwa uaminifu wakiwa hapa duniani.

Tuupitie mfano huu tutaelewa zaidi;

Luka 19:12 “Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.

13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja.

14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.

15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.

16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.

17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.

18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.

19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.

20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.

21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.

22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;

23 basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?

24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.

25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.

26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho”.

Mfano huo unajieleza wenyewe.. Ikiwa Bwana amekupa kiwango Fulani cha neema umtumikie hapa duniani, anatarajia kuona umekizalisha kwa wingi kwa jinsi uwezavyo. Mfano amekupa neema ya kufagia uwanja wa kanisa, anatarajia, kuona na vyoo pia, ni visafi, na madirisha na viti vinakaa katika hali ya usafi siku zote.

Kwasababu siku atakayokuja, atatazama, kama kile alichokupa mwanzo, na utawajibikaji wako je! vinaendana, lakini ikiwa utaona kazi ya kufagia kanisa, haina maana yoyote, ukaendelea na shughuli zako, atakuja kukuambia kama uliona uvivu kufagia basi si ungemwajiri mtu akusaidie kuifanya hiyo kazi umlipe, kuliko kuuacha uwanja wangu ukiwa na vichaka na matakataka namna ile? Unaona Kama tu alivyomwambia yule aliyepewa fungu moja, si ungeweka kwa watoa riba, ili nijapo nikute na faida yangu?. Ndivyo atakavyotuambia na sisi!

Lakini kama tutakuwa waaminifu wa kile alichotupa, tukazalisha na Zaidi ya  pale, tujue kuwa, uaminifu wetu, utaamua umiliki wetu katika ufalme ule…Kama ni miji basi tutamiliki hiyo miji kulingana na uaminifu wetu sasa.

Hivyo hiyo inatupa hamasa, tuitende kazi ya Bwana bila kutoa visingizio, bila kudharau, tena tutende Zaidi ya pale kwa kadiri tuwezavyo, kwasababu hivyo hivyo vidogo ndivyo vitakavyopima utajiri wetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments