Uchunguzi huu wa Sulemani tunaweza kuusoma katika kitabu cha Mhubiri tukianzia mwanzoni kabisa tunaona Sulemani akieleza jinsi alivyoutia moyo wake kutafuta na kuchunguza hekima ili kupata jawabu hilo moja, hivyo ilimgharimu kujaribu kitu kimoja kimoja kinachoweza kutamanika hapa duniani, na kila alichokijaribu na kuona sio chenyewe chenye ufunguo wa maisha kwa kwa mwanadamu alisema ni UBATILI, hivyo akaendelea na kingine, kadhalika alipoona hicho nacho hakiwezi kumsaidia mwanadamu alisema ni UBATILI..hivyo akakiacha akaendelea na kingine, hivyo hivyo mpaka alipofanikiwa kujaribu kila kitu unachoweza kukifahamu hapa chini ya jua, hakuna ambacho hakukijaribu, mpaka kwa wachawi na miungu migeni alifika, hakuna kitu ambacho hakukijaribu Sulemani, alijaribu vyote, lakini vyote aliona ni ubatili na upotevu ni sawa na kuufuata na kujilisha Upepo, mpaka tunapokuja kusoma sasa kwenye sura ya mwisho kabisa ya kitabu cha Mhubiri baada ya Sulemani kwenda huku na kule, kufanya hichi na kile, kujaribu hichi na kile, ndipo mwisho wa siku anakuja kulipata JAWABU lenyewe alilokuwa analitafuta kwa muda mrefu, tangu ujana wake, lililomgharimu hata kuipoteza nafsi yake katika mambo yasiyompasa kuyafanya ili tu alipate na hatimaye akalipata jawabu hilo..Haikuwa kazi rahisi..