Tuchukue mfano mwepesi, kuna kichaa mahali Fulani, kaonekana akivunja vioo vya magari ya watu, na kupiga watu barabarani, na kaharibu mali, na kisha wakamkamata na kumfunga kamba! Je! wale waliomfunga kamba watamhukumu kwanza kwa kuanza kumuuliza kwanini amevunja vioo vya magari?, au kwanini anapiga watu, au kwanini ni mwaribifu…utagundua kwamba! Hawataweza kufanya hivyo…watajua tatizo halipo katika matendo anayoyafanya, bali tatizo lipo katika akili zake nalo ni ile hali ya ukichaa iliyondani yake!!…Hivyo wakitaka wapate ufumbuzi wa tatizo lao, watashughulika kwanza na tiba ya akili yake, zaidi ya tiba ya mambo anayoyafanya, hawawezi kumshauri aache uaribifu, au aache kupiga watu katika hali yake ya ukichaa aliyokuwepo, ni sawa na kupaka rangi upepo.. sharti wamtibu kwanza tatizo lake hilo moja!..Na mengine yatatibika yenyewe.