Mungu Hataki tuwe kama wanafki kama mafarisayo, ambao kwa nje, tunaonekana ni wakidini lakini kwa ndani ni wachafu. Malkia Esta hakubeba Torati na kuingia nayo kwa Mfalme ndipo akubalike, hakujidhihirisha kwamba yeye ni Myahudi, mwana wa Ibrahimu, na kwamba anamwabudu Mungu wa aliyeziumba Mbingu na nchi..hakufanya hayo yote, yeye aliingia tu mbele ya mfalme na barua ya maisha yake, na utii wake, unyenyekevu wake, upole wake, usikivu wake, na utulivu wake, na tabia yake njema, aliingia na tabia yake ya kuwa na kiasi, ya mtu asiye na majivuno, asiye na kiburi, asiyekuwa na tamaa, aliingia na tabia yake ya kuridhika, na kutotamani mambo makubwa, aliingia na tabia yake ya kutokusengenya, ya kutokuwa mwashetati, hiyo ndiyo iliyomfanya apendwe na Mfalme, hiyo ndiyo iliyomfanya akubalike..Hiyo ndiyo iliyomfanya Barua yake isomeke vyema mbele za Mfalme, na Ufalme wa Uajemi wote, na hiyo ndiyo iliyomfanya KITABU CHAKE JAPOKUWA HAKINA JINA LA BWANA MAHALI POPOTE LAKINI KIMEINGIA KATI YA VITABU 66 VYA BIBLIA.