SWALI: Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? Yeremia 17:9
Yeremia 17:9 “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua”?
Kufisha; maana yake ni kusababisha kitu kife.
Hivyo hapo anaposema..moyo una ugonjwa wa kufisha.. Maana yake ni kuwa una ugonjwa wa kupelekea mauti, yaani ugonjwa usioponyeka.
Akiwa na maana kuwa, udanganyifu wa moyo ni mbaya sana, unaweza kukupeleka sio tu mauti ya mwili wako, bali mpaka roho yako pia. Kwamfano waweza kujiuliza shetani alidanganywa na nani kule mbinguni?. Jibu ni kuwa hakudanganywa na mtu yeyote, bali alidanganywa na moyo wake mwenyewe kwamba na yeye anaweza kuwa kama Mungu.
Na mwisho wa siku akapata hasara ambayo mpaka leo hii anaijutia ndani ya moyo wake. Hata sasa udanganyifu wa kwanza hautoki kwa shetani, bali unatoka ndani yetu wenyewe. Baadaye tukishadanganyika, ndipo shetani anapata nafasi ya kuuchochoa udanganyifu huo.
Biblia inasema,
Mithali 14:12 “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”.
Unaweza kuona kuvaa vimini na kujichubua ni sawa kwasababu moyo wako unakuambia hivyo, lakini kumbe ndio unakwenda kujiangamiza mwenyewe. Unaweza kudhani kumwabudu Mungu kwa kupitia chochote ni sawa tu kumbe, mwisho wake ni mauti.
Njia ni moja tu, nayo ni Yesu Kristo.
Hivyo andiko hilo, linatupa tahadhari kuwa, tumsikilize Mungu, kuliko mioyo yetu. Kwasababu wengi wamepotea, kwa kutii tamaa za mioyo yao, na sio Neno la Mungu.
Bwana atusaidie sana.
Neno “kufisha” utalisoma pia katika vifungu hivi;
Luka 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.
Zaburi 7:13 “Naye amemtengenezea silaha za kufisha, Akifanya mishale yake kuwa ya moto”.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?
Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?
Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?
VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.
Kiasi kama tafsiri yake ilivyo ni kuwa na uwezo wa kudhibiti jambo/tendo lisipitilize mipaka yake, yaani litendeke kwa sehemu tu.
Katika Ukristo, kiasi ni moja ya matunda tisa (9), ya Roho Mtakatifu.
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23 upole, KIASI; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
Ikiwa na maana ukipungukiwa nacho (kiasi), ni uthibitisho mojawapo kuwa Roho wa Mungu hayupo ndani yako.
Kwasababu huu ulimwengu una mambo mengi, ambayo, pengine sio mabaya, lakini yakipitiliza matumizi yake, yanabadilika na kuwa mabaya na sumu kubwa sana, kuliko hata matendo yenyewe mabaya.
Zifuatazo ni sehemu muhimu, ambazo, Roho Mtakatifu anataka sisi tuwe nazo na kiasi.
1Wakorintho 7:4 “Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.
5 Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu”.
Kukosa kiasi katika tendo la ndoa, hupelekea watu wengi sana kumtenda Mungu dhambi, wengine wanatenda mambo hayo hata kinyume na maumbile, wengine kutafuta njia za visaidizi n.k. wengine muda wao wote wanachowaza ni tendo lile tu, akili zao zote zinafikiria humo, mpaka inawapelekea kukosa muda kusali. Hivyo kiroho chao kinapungua sana kwasababu ya kuendekeza tamaa za mwili.
Biblia inasema..
1Wakorintho 7:29 “Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana;
Ikiwa na maana, tuishi kama vile, hakuna jambo jipya tumeongeza, pale tulipooa au kuolewa, hiyo itatusaidia sana, kuishi Maisha ya utakatifu na kumcha Mungu, katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho duniani.
Bwana ametuweka duniani tufanye kazi, pia tujitafutie rizki, lakini anatutahadharisha, tusipitilize, mpaka kufikia hatua ya mioyo yetu kuzama huko moja kwa moja tukamsahau yeye, hata muda wa ibada, au kuomba au kuwaeleza wengine Habari njema tukakosa..Hiyo ni hatari kubwa sana.
1Wakorintho 7:31 “Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita”.
Yaani fanyakazi huku ukijua mahusiano yako, au ratiba yako na Mungu haivurugwi hata kidogo.. Kwasababu ukiupeleka moja kwa moja moyo wako huko, ni lazima tu ulale kiroho, na matokeo yake, utakufa na bado hujayatengeneza mambo yako vizuri na Mungu.
1Wathesalonike 5:6 “Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, NA KUWA NA KIASI.
7 Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.
8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu”.
Usihangaishwe sana na shughuli za dunia hii.. Kuwa na kiasi katika hayo, ili mbegu yako imee vizuri. Zingatia sana hilo. Kama unatingwa na mihangaiko ya duniani, na moyoni mwako unaona ni sawa, basi ujue moyoni mwako Roho Mtakatifu hayupo.
Mungu anataka watumishi wake pia wawe na kiasi.. Hamaanishi kiasi katika kumtumikia hapana, anataka sana tuzidi kumtimika kwa bidii, bali anamaanisha kiasi katika karama.
Anasema..
Warumi 12:3 “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; BALI AWE NA NIA YA KIASI, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.
4 Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;
5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.
Hii ni kutuonyesha kuwa hakuna hata mmoja wetu mwenye karama zote, Ni YESU tu peke yake. Hivyo ridhika, na ulichokirimiwa, ukiwa ni mchungaji, usitake wewe wewe ndio uwe ni nabii, na mwalimu, na mwimbaji, na mwinjilisti, na mtume n.k. Huwezi kuwa Yesu.
Jifunze kuwapa wengine nafasi, na kunyanyua karama zao, pia fahamu kuwa wapo watakaokuwa na karama bora kukuzidi wewe. Ukilijua hilo utajifunza kuwa mnyenyekevu, na ndivyo Mungu atakavyokutumia Zaidi.
Mhubiri 7:16 “Usiwe na haki kupita kiasi; Wala usijiongezee hekima mno; Kwani kujiangamiza mwenyewe?
Hapa pia Mungu hamaanishi kwamba tusiwe na haki nyingi kupitiliza hapana, anapenda sana tuwe hivyo. Lakini anachomaanisha hapo ni kuwa tusiwe watu wa kujihesabia haki kupitiliza,(yaani kujisifia) kwani matokeo yake ni kujiangamiza wenyewe.
Bwana Yesu alitoa mfano wa yule Farisayo na mtoza ushuru waliokwenda kusali kule hekaluni, lakini yule Farisayo akaanza kumwambia Mungu mimi ni mkamilifu kuliko huyu mtoza ushuru, mimi ninafunga mara mbili kwa juma, mimi natoa zaka, mimi nahudhuria mikesha kila wiki, mimi nahubiri sana n.k. Lakini yule mtoza ushuru akasema Bwana nirehemu mimi ni mwenye dhambi..Matokeo yake yakawa yule mtoza ushuru akahesabiwa haki kuliko yule Farisayo..
Ndipo Yesu akasema..
Luka 18: 14 “…kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa”.
Uendapo mbele za Mungu, au mbele za wanadamu kuwa na kiasi.. Mwache Mungu akuhesabie haki mwenyewe. Usijifisie kwa lolote.
Biblia inasema..
Mithali 10:19 “Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili”.
Kwanini haisemi, katika Uchache wa maneno, hapakosi kuwa na maovu?..Ni kuonyesha kuwa, unapokuwa mzungumzaji kupitiliza, ni rahisi sana kujikwaa ulimi, lakini ukiwa si mwepesi wa kuzungumza zungumza, yaani kila Habari au kila jambo unachangia, basi utajiepusha na maovu mengi.
Mhubiri 5:2 “Usiseme maneno ya ujinga kwa kinywa chako, wala moyo wako usiwe na haraka kunena mbele za Mungu; kwa maana, Mungu yuko mbinguni, na wewe upo chini, Kwa hiyo maneno yako na yawe machache”.
Vinywaji kama divai, vilikuwa ni vya kitamaduni Israeli, wakati ule, kwasababu pia ndani yake waliamini kuna tiba, (1Timotheo 5:23) hivyo vilikuwa vinanyweka kwa kiasi sana, kwasababu vilikuwa na kiwango cha kileo ndani yake.
Paulo akamwagiza Timotheo kuhusiana na Mashemasi na wazee wa kike katika makanisa, akamwambia.
1Timotheo 3:8 “Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu.
Lakini sasa kwa watu kukosa kiasi, leo hii, wanakwenda kunywa pombe ambayo haiwasaidii chochote, wala haina umuhimu wowote katika mwili, Wakati wa sasa tunazo dawa, kwanini ukanywe divai.
Na biblia imeweka wazi kabisa, walevi wote sehemu yao itakuwa katika lile ziwa la moto (1Wakorintho 6:10).
Sio kila kitu ule, au unywe. Zuia koo lako, zuia tumbo lako. Wakati mwingine funga, Litunze hekalu la Mungu. Utaona faida yake
Hapa anatoa angalizo, katika mienendo yetu na mionekano. Hususani kwa vijana.
Tito 2:6 “Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi”;
Jiulize kwanini hasemi, wazee au Watoto? Anasema vijana kwasababu Anajua kabisa vijana wengi wakike na wakiume waliokoka wanakosa, kiasi katika ujana wao.
Hakuna sababu ya kukesha katika muvi au magemu, au mipira kutwa kuchwa. Ukiwa umeokoka, ili hali unajua kabisa kusoma biblia, kuomba na kuhubiri kunakusubiria.
Hakuna sababu ya binti wa Mungu avae/ aonekane kama mabinti wa ulimwengu huu. Unaweka mawigi, unavaa suruali, uweka kucha za bandia, n.k. Kuwa “natural”..
1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, NA MOYO WA KIASI; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani”;
Soma pia (1Timotheo 3:11)
Kijana, huna sababu ya kunyoa kiduku, uonekane kama msanii fulani, kwenye tv. Kumbuka Mwonekano wako unakupunguzia utukufu wako.
Kwahiyo, kwa kuhitimisha ni kuwa KIASI katika mambo yote ni muhimu sana. Hivyo tujitahidi kwa upande wetu kila mmoja aangalie ni wapi amekosa kiasi, basi arekebishe mapema, na Roho Mtakatifu atajaa tena ndani yetu kutusaidia kuushinda ulimwengu.
Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho, Biblia inasema..
1Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze”.
Umeona! Ibilisi anawatufuta watu wanaokosa kiasi ili awemeze, Usiwe mmojawapo!
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je ushabiki wa mpira ni dhambi?
Wibari ni nani?(Mithali 30:26)
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)
Je! Mtu ambaye hajaoa anaruhusiwa kulichunga kundi?
“Vya Kaisari mpeni kaisari” ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?
Yeremia 48:10 “Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu; NA ALAANIWE AUZUIAYE UPANGA WAKE USIMWAGE DAMU”.
Je kufuatia mstari huo, Mungu anahimiza mauaji?
Jibu: Awali ya yote ni muhimu kuelewa tofauti ya Amri, Sheria na Hukumu za Mungu, sasa kuelewa juu ya mambo hayo, na tofauti zao kwa mapana, unaweza kufungua hapa >>>Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?
Lakini kwa ufupi ni kwamba, sheria zote na amri zote zilizotolewa katika agano la kale, zilikuwa na hukumu.. Maana yake ni kwamba, ikitokea mtu kavunja sheria au amri mojawapo basi alistahili hukumu. Na hukumu hiyo ilikuwa ni lazima itekelezwe…isipotekelezwa ilikuwa ni dhambi mbele za Mungu kama tu ilivyo dhambi ya kuvunja amri.
Mfano mmojawapo wa hukumu ni ile hukumu ya mtu kupigwa mawe mpaka afe anapokamatwa katika uzinzi..
Mfano wa hukumu nyingine ni hii..
Kutoka 21:15 “Ampigaye baba yake au mama yake, sharti atauawa”.
Kwahiyo mtu yeyote aliyeonekana akimpiga mzazi wake, hukumu ilikuwa ni kifo..wasipomuua mtu huyo, Mungu alikuwa anawaadhibu!..kwahiyo ili waendelee kukaa salama, Bwana Mungu asiwapige, ilikuwa ni lazima wamuue huyo kijana aliyempiga mzazi wake.
Hali kadhalika ilikuwepo hukumu nyingine ya mtu yeyote anayekwenda kuabudu miungu mingine.. ilikuwa ni sheria kwamba mtu akienda kuabudu miungu mingine sharti auawe, haijalishi ni mzazi wako au ndugu yako, ni lazima utamwua aidha kwa kumpiga mawe au kwa upanga.. Usipomwua ulikuwa unalaaniwa na Mungu.
Kumbukumbu 13:6 “Atakapokushawishi kwa siri ndugu yako, mwana wa mamaako, au mwana wako, au binti yako, au mke wa kifuani mwako, au rafiki yako aliye kama moyo wako, akikuambia, Twende tukaabudu miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako;
7 katika miungu ya mataifa yaliyo kando-kando yenu karibu nawe au mbali nawe, tokea ncha moja ya dunia hata ncha ya pili ya dunia;
8 USIMKUBALIE WALA USIMSIKIZE; WALA JICHO LAKO LISIMWONEE HURUMA, WALA USIMWACHE, WALA USIMFICHE;
9 MWUE KWELI; MKONO WAKO NA UWE WA KWANZA JUU YAKE KATIKA KUMWUA, NA BAADAYE MIKONO YA WATU WOTE.
10 Nawe mtupie mawe hata afe; kwa kuwa alitaka kukupotoa na Bwana, Mungu wako aliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
11 Na Israeli wote watasikia na kuogopa, wasifanye tena uovu mfano wa huo katikati yako”.
Vile vile ilikuwepo hukumu ya kwamba, mtu yeyote au kikundi chochote kikizuka katikati ya jamii ya Israeli, ambacho kinawashawishi watu kuabudu miungu mingine mbali na Mungu wa Israeli. Bwana Mungu alitoa ruhusa ya watu hao kuuliwa kwa makali ya upanga.
Kumbukumbu 13:12 “Ukisikia yasemwa habari ya miji yako mmojawapo, akupayo Bwana, Mungu wako, ukae humo, ukiambiwa,
13 KUMETOKA KATIKATI YAKO MABARADHULI KADHA WA KADHA, WAMEWAPOTOA WENYEJI WA MJI WAO, WAKISEMA, TWENDENI TUKAABUDU MIUNGU MINGINE MSIYOIJUA;
14 ndipo nawe uulize na kutafuta, ukiuliza kwa bidii; nawe angalia, ikiwa kweli, na jambo lile halina shaka, kwamba machukizo mfano wa haya yafanyika katikati yako;
15 HAKIKA YAKO UWAPIGE WENYEJI WA MJI ULE KWA MAKALI YA UPANGA, KWA KUWAANGAMIZA KABISA, PAMOJA NA VITU VYOTE VILIVYOMO, NA WANYAMA WALIO HUMO, KWA MAKALI YA UPANGA”
Umeona?.. Hiyo ndio sababu Bwana kasema hapo kwenye Yeremia 48:10 “..ALAANIWE AUZUIAYE UPANGA WAKE USIMWAGE DAMU”.
Damu inayomwagwa ni ya watu waliomwacha Mungu wa Israeli na sheria zake kwa makusudi.
Lakini swali ni je!.. Hata sasa katika agano jipya hii sheria ipo??.
Jibu ni la!. Katika agano jipya hatuna hiyo amri!..haturuhusiwi kumwua mzinzi, wala mlevi, wala mwizi.. bali tunapaswa tuziue zile roho zilizopo ndani yao, zinazowashawishi wao kufanya mambo hayo.. na roho hizo ni roho za mapepo..hizo ndio tunazozipiga kwa Upanga wa Roho, huku na sisi tukiwa tumejivika silaha zote za roho.
Waefeso 6:11 “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, JUU YA MAJESHI YA PEPO WABAYA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO.
13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;
16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;
18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote”.
Tukiweza kuzivaa hizi silaha na kuutumia vizuri upanga wa roho, ndipo tutakapoweza kuziadhibu roho zote, zilizopo ndani ya watu na kuwaacha watu huru.
2Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;
4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.
Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.
KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.
Kwanini Bwana Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wakanunue upanga?
NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.
Jibu: Ndio ni jambo la kimaandiko kabisa kupiga kura kuchagua viongozi wa kanisa!.
Lakini ni lazima kuzingatia wanaopiga kura na anayepigiwa kura. Wanaopaswa kupiga kura kuchagua viongozi ni lazima wawe viongozi au watu waliodumu muda mrefu katika Imani (yaani watu ambao hawajaongoka hivi karibuni).. Kwasababu watu waliookoka hivi karibuni bado hawajajua imani vizuri, na sifa za viongozi wa kiimani, vile vile bado hawajazijua hila za shetani, na bado hawajui mambo mengi ya kiimani, hivyo endapo wakipewa nafasi hiyo wanaweza kuchagua watu kutokana na hisia zao tu!, au mitazamo yao tu, na si sawasawa na Neno!.
Vile vile mtu anayepigiwa kura ni lazima awe Mkristo aliyedumu muda mrefu katika Imani na aliyesifika kwa sifa njema, na sio mtu aliyeokoka hivi karibu, ambaye bado hajajua mbinu na hila za shetani.
Katika biblia utaona mtume wa 12, aliyechukua nafasi ya Yuda, aliteuliwa kwa kupigiwa Kura!.
Matendo 1:21 “Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu,
22 kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, INAPASA MMOJA WAO AWE SHAHIDI WA KUFUFUKA KWAKE PAMOJA NASI.
23 WAKAWEKA WAWILI, YUSUFU, AITWAYE BARSABA, ALIYEKUWA NA JINA LA PILI YUSTO, NA MATHIYA.
24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,
25 ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.
26 WAKAWAPIGIA KURA; KURA IKAMWANGUKIA MATHIYA; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja”.
Umeona hapo?..Mathiya alichaguliwa kwa Kura!.. na alichaguliwa na Mitume 11, ambao wana uzoefu wa kutosha wa kimaandiko kujua kiongozi bora anapaswa aweje, hawakuhusishwa waamini wote wa Yerusalemu waje kupiga kura!..bali walipiga kura wao viongozi tu! (ili kuzuia upenyo wa shetani)..
Vile vile aliyepigiwa kura, hakuwa mtu aliyekuwa maarufu au mwenye pesa, au mwenye ushawishi.. utaona sifa ya aliyetuliwa ni “mtu aliyefuatana nao mitume tangu wakati wa Yohana hadi wakati wa kuchukuliwa kwa Bwana juu mbinguni”..jumla miaka mitatu na nusu. Kwahiyo walimchagua mtu aliyekuwa mkongwe katika Imani na vile vile aliyekuwa mwaminifu.. Ndio maana utaona Yusufu na Mathiya wote walikuwa wakongwe, lakini Mathiya alikuwa mwaminifu Zaidi ya Yusufu ndio maana alichaguliwa.
Vile vile na sisi tunajifunza namna ya kuchagua viongozi wa kanisa kama Mashemasi, wazee wa kanisa, waangalizi wa Watoto, waweka hazina, waalimu wa vijana n.k kutumia kanuni hiyo.. Kwamba baada ya kusali na kufunga, basi wawekwe wanaostahili kupigiwa kura yule anayestahili, aliye mwamifinu na ateuliwe. Kwa sisi kumteua, basi ni Bwana kamteua..kwasababu sisi tuliomchagua tumetumia vigezo vya Neno kumchagua anayestahili na si macho yetu, Ndio maana na yeye anakuwa ni chaguo la Bwana.
Huo ndio ulikuwa utaratibu wa kanisa la kwanza..Ndio maana utaona Paulo kuna mahali anawaagiza akina Tito na Timotheo vigezo vya kuchagua viongozi..
Tito 1:4 “kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tuishirikiyo. Neema na iwe kwako na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
5 Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;
6 ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii”.
Je umeokoka?.. je una uhakika KRISTO akirudi leo unakwenda naye mawinguni?, kama huna huo uhakika basi ni uthibitisho kuwa atakapokuja utaachwa!.. Tubu leo kwa kudhamiria kuacha dhambi zako na tafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu, na upokee Roho Mtakatifu.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?
Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?
Nini maana ya kupiga Kite! Katika biblia.
Je ni tunaruhusiwa kunywa dawa wakati wa kufunga, au kuonja chakula wakati wa kupika kwaajili ya wengine?
Jibu: Unapofunga unakuwa unajizuia kula chakula au kunywa chochote, kwa lengo Fulani la kiroho. Lakini hatufungi kwa sheria au kanuni Fulani maalumu (biblia haijatupa kanuni yoyote maalumu), wala agizo la Sharti ya kufunga. Isipokuwa imesema tu “mambo mengine hayatoki isipokuwa kwa kufunga na kuomba”.
Mathayo 17: 21 “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga”
Lakini tukirudi kwenye swali, je tunaruhusiwa kunywa dawa wakati wa kufunga?
Jibu ni NDIO! Kama kuna ulazima huo, kwasababu “Vidonge sio chakula” huwezi kula vidonge ukashiba, au ukakata njaa. Vidonge kazi yake ni kutibu tatizo Fulani lililopo ndani ya mwili (yaani vimetengenezwa kwa lengo la matibabu). Kwahiyo mtu anaweza kuwa amefunga na huku anatumia dawa.
Vile vile kuonja ladha ya chakula, kama kimekolea chumvi, au viungo hakubatilishi mfungo!..Kwamfano unaweza kuwa umefunga, lakini unalo jukumu la kupika chakula kwa wengine ambao hawajafunga! Mf.watoto, katika mazingira kama hayo, unalazimika kuonja chakula kama kimeiva, au kimekolea chumvi..(lakini kwa kiwango kidogo tu! Cha kuishia kwenye ulimi).
Ukionja kwa namna hiyo hufanyi dhambi, wala hakuharibu mfungo wako.. Kwasababu hapo umeonja na hujala. Lengo lako ni kuonja kama chakula hicho kipo sawa au la!.. Ungekuwa umeonja kwasababu unayo njaa, hapo ingekuwa ni tatizo, lakini hujaonja kwa lengo hilo.
Kwasababu ingekuwa hilo ni tatizo, basi hata mswaki asuhuhi, ingekuwa si ruhusa kupiga!..kwa maana ile dawa ya meno, tunapoiweka mdomoni, tayari tunaionja, hata kama hatutaki, vile vile tusingepaswa tusikie hata harufu ya chakula, lakini hayo mazingira hatuwezi kuyaishi.. Ni lazima tusafishe vinywa vyetu kila siku, na pia tutakutana na mazingira tofauti tofauti mahali tunapoishi..
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba kutumia dawa wakati wa mfungo si kosa, wala kuonja chakula kwakiwango kidogo kinachoishia ulimini si dhambi.
Lakini Zaidi ya yote, mfungo kwa mkristo unapaswa uwe ni jambo la mara kwa mara, inasikitisha mtu anayejiita ni mkisto lakini hana rekodi yoyote ya kungunga angalau wiki moja mfululizo.
Mkristo wa namna hii nguvu zake za kiroho zipo chini sana, kuna mambo katika Maisha yake, hawezi kuyapokea kwasababu Bwana Yesu mwenyewe alisema “kuna mambo hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kuomba”.
Bwana atusaidie tuwe waombaji na vile vile wafungaji!
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je mama mjamzito anaruhusiwa kufunga?
Je! ni halali kwa mtu wa Mungu kutumia njia za uzazi wa mpango,ikiwamo mipira?
Je sisi wakristo tunaruhusiwa kufanya 40 za marehemu?
SWALI: Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu na sio mtu wa kuomba omba tu, ilimradi?
JIBU: Katika vita lazima ujue adui wako mkuu ni nani.. Bwana Yesu alisema maneno haya;
Mathayo 26:40-41
[40]Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
[41]Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.
Hapa Bwana alitarajia, wakeshe, Yaani waombe naye masafa marefu, (kama vile wewe unavyotamani uwe na nguvu hata ya kukesha katika maombi mpaka asubuhi), lakini kinyume chake, hawakuweza kumaliza hata Saa moja..matumaini yao yaliishia katikati..
Lakini Bwana Yesu alipowakuta wamelala hakuwaambia kemea pepo hilo la uchovu, au wachawi hao waliotumwa kuwafanya mpige pige miayo ya usingizi, muda wote muombapo..
Bali aliwaambia maneno haya “ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU”..Akiwa na maana roho zao kweli zilikuwa zinatamani kukesha naye kule bustanini…na ndio maana walitii wito wa kwenda kuomba..kama roho zao zisingekuwa radhi kufanya vile muda ule wangekuwa vitandani mwao wamelala..
Lakini Bwana anawaambia kikwazo ni nini.? Kikwazo ni MIILI yao.. Huyo ndio adui wao wa kwanza wanapaswa wamuangalie, sana
Tunashindwa kuomba, hata wakati mwingine kusoma Neno,..kwasababu ya mwili,..Lakini kama tukishindana na mwili ipasavyo basi tutaweza fungua milango mingi ya rohoni.
Sasa tutawezaje kuwa hivyo?
Ni kujitengenezea ”pumzi ya kiroho”..Kama vile wanariadha wafanyavyo katika mwili, kwa kawaida yule anayefanya mazoezi sana, huwa anajiongezea pumzi ya kukimbia umbali mrefu zaidi kuliko yule asiyefanya mazoezi yoyote, Atakimbia mzunguko mmoja tayari hoi.
Unapotaka uwe mwombaji mzuri, hata wa masafa marefu, ni lazima uanze kidogo kidogo, ukikumbuka kuwa adui wako wa kwanza sio shetani bali ni mwili wako..
Hivyo unaanza siku ya kwanza kuomba dakika 15, kesho huna budi kuongezea nyingine 5, kesho kutwa yake nyingine 5, hivyo hivyo, bila kurudi nyuma, Sasa kwa jinsi utakavyozidi kuongeza muda wako katika maombi ndivyo utakavyoona wepesi wa kuomba..
Kipindi cha mwanzoni utaona ni shida kumaliza saa moja katika maombi…lakini kama utakuwa ni mtu wa kuomba kila siku, utaona ni jepesi sana kama tu vile unavyoomba dakika 10..
Hautatumia nguvu kufikia huo muda, kwasababu tayari pumzi ya maombi ipo ndani yako.
Pengine jambo usilolijua ni kuwa wewe usiyeomba unaweza kudhani yule anayeweza kukesha saa nyingi katika kuomba, anapata shida sana..lakini ukweli ni kwamba wewe ambaye unasali dakika chache, ndio unayechoka sana kuliko yule..kwasababu kuna kilele fulani mtu anayeomba huwa anakifikia ile raha ya maombi inaingia ndani yake..wala haoni ugumu wa kuendelea mbele.
Hivyo jitahidi sana..Kushindana na mwili wako, ondoa mawazo yako sana kwa shetani, ni kweli upo wasaa ibilisi atataka kuvuruga ratiba zetu za maombi, lakini si jambo la kila siku…pindi unaposikia tu kuomba unalala, halafu unasema ni shetani…Ni huo mwili wako ndugu..
Anza leo kujizoeza kuomba. Shindana na usingizi, shindana na uchovu, shindana na uvivu.
Na hatimaye utakuwa mwombaji bora..Pia usingoje kuombewa, ombewa tu muda wote, vilevile usiseme Namwachia Mungu mwenyewe afanye, na ilihali hutaki kuomba..utapata hasara..Muda mwingine Kristo anasimama kutuombea..lakini wakati mwingine anataka kusimama na sisi kuomba, Kama alivyowaambia mitume wake hapo. Kesheni pamoja nami.
Mambo muhimu yatakayoweza kukupeleka rohoni haraka sana katika uombaji wako, Ni yapi?
Kisha baada ya hapo ndio uingie moja kwa moja katika vipengele vyako vya maombi.
Zingatia hayo, na Mungu atakutia nguvu, katika hatua zako za maombi.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?
YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.
Kuna tofauti gani kati ya SALA na DUA?
Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
Ijumaa kuu ni nini? Na kwanini iitwe kuu?
Midiani kwasasa ni eneo la Mashariki mwa nchi ya Saudi-Arabia, Kusini mwa nchi ya Yordani. Asili ya waMidiani ni Ibrahimu.
Maandiko yanaonyesha baada ya Sara kufa, Ibrahimu alimwoa mwanamke mwingine aliyeitwa Ketura, na huyu Ketura, alikuja kuzaa Watoto 6 wa kiume , na mmojawapo wa Watoto hao aliitwa Midiani, ambaye ndiye Baba wa wa-Midiani.
Mwanzo 25:1 “Ibrahimu alioa mke mwingine jina lake akiitwa Ketura.
2 Akamzalia Zimrani, na Yokshani, na Medani, na MIDIANI, na Ishbaki, na Sua”.
Wamidiani walikuwa wanamwabudu Mungu wa Ibrahimu isipokuwa si katika sheria za Musa kama Israeli walivyofanya, kwasababu Torati ilikuja miaka mingi baada ya Midiani kuwa Taifa kubwa.
Wamidiani walimtumikia Mungu katika mfumo wa sadaka za kafara kama alivyofanya Ibrahimu, hawakumjua Mungu kwa mapana ( yaani katika sheria kama Israeli walivyomjua walipokuwa jangwani). Na hiyo ni kwasababu ahadi ya agano Mungu aliyompa Ibrahimu, ilikuwa ni kwa Ibrahimu na mwanaye Isaka mwana wa Sara na si kwa wana wa Ketura.
Hivyo wamidiani walimtumikia Mungu wa Ibrahimu lakini si kwa usahihi wote. Ndio maana tunakuja kumwona Mkwewe Musa aliyeitwa Yethro (au Reuli) ambaye alikuwa ni Mmidiani kwa asili, maandiko yanasema alikuwa ni “kuhani” wa nchi hiyo ya Midiani (soma Kutoka 2:16).
Ikiwa na maana kuwa alikuwa anafanya kazi za kikuhani kama Haruni lakini si katika ukamilifu wote kama walivyokuwa wanafanya akina Haruni na wanawe.
Hivyo kwaasili waMidiani walikuwa ni ndugu ya Israeli kupitia Ibrahimu. Lakini baadaye tunakuja kusoma wamidiani waligeuka na kuwa madui wa kubwa wa Israeli, kipindi Israeli wanatoka Misri kuelekea Kaanani hawa wamidiani walijiunga na WaMoabu na kumwajiri mtu aliyeitwa Balaamu ambaye alikuwa ni mchawi kutoka Midiani kuja kuwalaani, jambo ambalo lilimchukiza sana Mungu, na kufanya Mungu awalipize kisasi wamidiani kwa kosa hilo.
Hesabu 31:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
2 Walipize kisasi wana wa Israeli juu ya Wamidiani; kisha baadaye utakusanywa uwe pamoja na watu wako.
3 Basi Musa akanena na watu, na kuwaambia, Wavikeni silaha watu miongoni mwenu waende vitani, ili waende kupigana na Midiani, wapate kumlipiza kisasi Bwana, juu ya Midiani”.
Lakini Ijapokuwa Mungu aliwapiga waMidiani karibia wote, lakini hawakuisha wote.. Wamidiani walikuja kunyanyuka tena na kuwa Taifa kubwa, na lenye nguvu kuliko hata Israeli.
Na miaka kadhaa baadaye Israeli walipomwacha Mungu, na kwenda kuabudu miungu mingine, Mungu aliwatia waisraeli mikononi mwa hawa Wamidiani wawatese, na Waisraeli wakateswa miaka 7 na waMidiani, mpaka walipomlilia Bwana, na kupelekewa mwokozi awaokoe (ambaye alikuwa ni Gideoni).
Waamuzi 6:1 “Kisha wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu mbele za macho ya Bwana; Bwana akawatia mikononi mwa Midiani muda wa miaka saba
2 Mkono wa Midiani ulikuwa na nguvu juu ya Israeli; tena kwa sababu ya Midiani wana wa Israeli walijifanyia hayo mashimo yaliyo milimani, na hayo mapango, na hizo ngome.
3 Basi ikawa, hapo Israeli walipokuwa wamepanda mashamba, Wamidiani wakakwea, na Waamaleki, na hao wana wa mashariki; wakakwea juu yao;
4 wakapanga marago juu yao, na kuyaharibu hayo maongeo ya nchi, hata ufikapo Gaza, wala hawakuacha katika Israeli riziki ziwazo zote; kondoo, wala ng’ombe, wala punda.
5 Kwa maana walikwea na ng’ombe zao na hema zao, wakaja mfano wa nzige kwa wingi; wao na ngamia zao pia walikuwa hawana hesabu; nao waliingia katika hiyo nchi ili kuiharibu.
6 Israeli walitwezwa sana kwa sababu ya Wamidiani; nao wana wa Israeli wakamlilia Bwana.
7 Kisha ikawa, hapo wana wa Israeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Midiani,
8 Bwana akamtuma nabii aende kwa hao wana wa Israeli; naye akawaambia, Bwana, yeye Mungu wa Israeli, asema hivi, Mimi niliwaleta ninyi mkwee kutoka Misri, nikawatoa katika nyumba ya utumwa;
9 nami niliwaokoa na mikono ya Wamisri, na mikono ya wote waliokuwa wakiwaonea, nami niliwafukuza watoke mbele zenu, nami niliwapa ninyi nchi yao;
10 kisha niliwaambia, Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu; msiiche miungu ya Waamori, ambayo mwaketi katika nchi yao; lakini hamkuitii sauti yangu.
11 Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani.
12 Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa”.
Jamii ya Wamidiani kwasasa haipo, bali imemezwa na jamii nyingine za Arabia na Yordani na Misri, kiasi kwamba kwasasa hakuna ajijuaye kama yeye ni mmidiani au la!.
Lakini tunachoweza kujifunza kwa Habari ya Wamidiani ambao walikuwa ni maadui wa Israeli kwa kipindi chote, ni kuwa “maadui wanatabia ya kuchipuka tena”.
Wamidiani waliuawa karibia wote na mali zao kutekwa nyara na wa Israeli, kwaufupi ni kama vile walifutwa juu ya uso wa nchi, lakini tunaona walikuja kuchipuka tena na kuwa Taifa kubwa tena lenye nguvu kuliko Israeli, na tena likawatawala Israeli. Lakini hiyo yote ni matokeo ya Waisraeli kumwacha Mungu.
Vile vile na sisi tukimwacha Mungu, haijalishi yale magonjwa ambayo yalikuwa yameondoka miaka mingi na hatuyaoni tena, yatarudi tena na kuchipuka kwa nguvu na kutuangamiza!.
Tukimwacha Mungu haijalishi tulikuwa na ushindi mkubwa kiasi gani dhidi ya mapepo na wachawi!, tukimwacha Mungu Watanyanyuka tena na kutudhuru na kututesa!.
Tukimwacha Mungu na kurudia ulevu, uzinzi, wizi, uvaaji mbaya, utukanaji…haijalishi tulikuwa na ushindi mkubwa dhidi ya shetani hapo kabla…atanyanyuka tena na jeshi lake kwa nguvu na kuteka nyara… Israeli hawakutegemea kama Taifa walilopiga na karibia kulitowesha kabisa, leo lingekuja kuwatawala kwa miaka 7 tena kwa utumwa mkali.
Na sisi hatuna budi kujifunza katika haya, ili tusifanya makosa waliyofanya Israeli.
1Wakorintho 10:11 “Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.
12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.
Bwana atusaidie nasi pia tusirudi nyuma.. kusudi tusije tukampa nguvu adui yetu shetani.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je ni kweli Musa alikuwa mtu mpole kuliko wote duniani?
Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.
Marago ni mahali ambapo watu wanaweka makao ya muda kwa makusudi maalumu.
Kwamfano watu zamani walipokuwa wanakwenda vitani, waliweka makempu au makambi au mahema mahali mahali…hayo ndio yaliitwa marago..
Kwamfano ukisoma..
Waamuzi 10:17-18 inasema..
[17]Wakati huo wana wa Amoni walikutana pamoja, wakapanga marago huko Gileadi. Wana wa Israeli nao wakajikusanya wakapanga marago Mispa.
[18]Na hao watu, wakuu wa Gileadi, wakaambiana wao kwa wao, Je! Ni mtu yupi atakayeanza kupigana na wana wa Amoni? Yeye atakuwa ni kichwa juu ya wenyeji wote wa Gileadi.
Ikiwa na maana wote waliweka kambi zao za kijeshi huko Mispa.
Hali kadhalika Wana wa Israeli walipokuwa katika safari yao ya kuelekea nchi ya ahadi waliweka makazi ya muda sehemu kadha wa kadha..
Kwamfano ukisoma..
Kutoka 29:13-14
[13]Kisha twaa mafuta yote yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo juu yake, uyateketeze yote juu ya madhabahu.
[14]Lakini nyama yake huyo ng’ombe, na ngozi yake, na mavi yake, utayachoma kwa moto nje ya marago; ni sadaka kwa ajili ya dhambi.
Akiwa na maana hivyo viungo vya ndani watavichoma mbali na pale wana wa Israeli walipoweka makambi..
Neno hilo italisoma pia katika vifungu hivi;
Kutoka 36:6, Walawi 4:21, 10:5, Waamuzi 21:12.
Hata sisi hapa duniani ni kama tupo maragoni..Hatuna makazi ya kudumu..tumewekwa kwa makusudi maalumu..kusudi hilo likiisha..hakuna kukutanika tena..
Ibrahimu alilijua hilo..Kiasi kwamba japokuwa alikuwa na tajiri na mwenye mali nyingi..Moyo wake hakuuweka hapa duniani, hata kidogo..Bali kule kwenye mbingu mpya na nchi mpya(YERUSALEMU MPYA)..Na hiyo ndio ilikuwa sababu ya kuitwa Baba wa imani..Aliishi kama mpitaji hapa duniani..
Waebrania 11:9-10
[9]Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
[10]Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu….
[14]Maana hao wasemao maneno kama hayo waonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
[15]Na kama wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea.
[16]Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana amewatengenezea mji.
Je na sisi twaweza fanana na Ibrahimu?
Je tunaweza kuwa kama Ayubu ambaye japo alipoteza kila kila hakutetereka katika imani yake..kinyume chake ndio analibariki jina la Bwana.?
Hivyo nasi tuishi kama wapitaji. Kwasababu tukiwa ni watu wa namna hii, tunapata faida zote mbili kwanza ulimwengu hauwezi kutuzomba tukamsahau Mungu. Na pili Bwana atatubariki hata kwa hivyo tusivyovitazama..Kwasababu mioyo yetu haipo huko.
Bwana atusaidie.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Shetri ni nini kama tunavyosoma katika Marko 3:38?
Neno Buruji lina maana gani katika biblia?
Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)
Gumegume ni nini? (Isaya 50:7)
HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU
Easter ni nini?..Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?
Jibu: Tusome,
Marko 4:35 “Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.
36 Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye
37 Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.
38 Naye mwenyewe alikuwapo katika SHETRI, amelala JUU YA MTO; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?”.
Katika kisa hicho tunaona Wanafunzi walimchukua Bwana Yesu kama alivyo (yaani bila ya kitu chochote cha njiani kama vile chakula, au mavazi). Walimchukua kama alivyo..Na kumchukua kunakozungumziwa hapo ni kumchukua, kama vile mtu anavyomchukua mwenzake na kumpa lifti ya gari, ndivyo wanafunzi walivyomchukua Bwana Yesu..
Lakini tunaona walipokuwa njiani ndani ya ile Merikebu, Bwana Yesu alienda kulala katika Shetri ya Merikebu.
Sasa “SHETRI” au kwa lugha nyingine “TEZI”, ni sehemu ya Nyuma ya Meli au Merikebu, ambayo ni pana, na ndiyo iliyotumika katika kuwekea mizigo, na pia ndipo palipotengenezewa vyumba vya kulala watu. Sehemu ya mbele ya Meli au Merikebu inaitwa “OMO”, ambayo ni nyembamba ili kuisiaidia meli kukata mawimbi.
Sasa Bwana Yesu alienda kulala kwenye Shetri, mahali ambapo kulikuwa na nafasi ya kulala, na akawa amelala juu ya mto! (Mto unaozungumziwa hapa sio mto wa kutiririsha maji, bali ni ule mto wa kulalia kitandani, kuupatia shingo egemeo bora). Na akiwa Dhoruba ikaanza, na chombo kikakaribia kuzama..na Baadaye wanafunzi wakamwamsha Bwana na Bwana Yesu akaikemea ile Dhoruba ikatulia.
Sasa kikubwa tunachoweza kujifunza katika tukio hilo ni kuwa, Bwana Yesu anaweza kuwa yupo ndani yetu lakini amelala!. Tusipopaza sauti zetu kwa nguvu kwa maombi, basi tutahangaika na Dhoruba zilizopo nje, na wala yeye hatasema chochote.
Hii inatukumbusha kuwa waombaji, na si waombaji tu, bali waombaji wenye bidii, wenye kupaza sauti mpaka majibu ya maombi yatokee.
Bwana atusaidie katika hayo.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!
Bustani ya Edeni ipo nchi gani?
MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.
Swali: Je Ni sahihi kimaandiko kwa mwimbaji wa nyimbo za injili kufanya collaboration na wasanii wa kidunia?..
Kabla ya kujibu swali hili, hebu tujiulize kwanza swali lifuatalo!. Je ni sahihi Mchungaji kumwalika mtu wa kidunia ambaye hajaokoka kabisa aje kuhubiri madhabahuni?. Kama jibu ni Ndio!, basi pia ni sahihi Mwimbaji wa nyimbo ya Injili kushirikiana na msanii wa kidunia katika kuimba, lakini kama jibu ni hapana!! basi pia si sahihi mwimbaji wa nyimbo za injili kushirikiana na mwimbaji wa nyimbo za kidunia kumwimbia Mungu.
Jambo moja lisilofahamika na wengi, hususani waimbaji wa nyimbo za Injili, ni kwamba hawajui kuwa Huduma ya kumwimbia Mungu, ni huduma kama ya Uchungaji tu!..Unaposimama kumwimbia Mungu, ni sawasawa na umesimama madhahabuni unahubiri, na unaonya na unawajenga watu kiroho, sawasawa na uchungaji tu, au uinjilisti….
Sasa Unaposhirikiana na mtu ambaye hajaokoka utakuwa unaiharibu kazi ya Mungu, badala ya kuijenga, umempandisha shetani madhabahuni ahubiri..kwasababu yule mtu ambaye hajaokoka anazo roho ndani yake, ambazo ni za mashetani…maisha yake yanaongozwa na shetani, aidha kwa kujua au kwa kutokujua..kama ni hivyo atawezaje kusimama kuwahubiria wengine waokoke, wakati yeye mwenyewe hajaokoka, atawashaurije wengine waache ulevi wakati yeye mwenyewe ni mlevi na mzinzi, atawaambiaje watu wawe wasafi mwilini wakati yeye mwenye mwili mzima umejaa tattoo?.
Umeona? Tunaweza kushirikiana na watu ambao hawajaokoka katika kufanya mambo mengine ya kimaisha kama kazi (ukiwa ofisini au shuleni, utashirikiana na watu ambao hawajaamini, haina madhara), au unaweza kuishi nao, au kula nao… lakini SI KUFANYA NAO KAZI ZA MADHABAHUNI!!!.
Bwana Yesu alikuwa anakula na watoza Ushuru, na makahaba na wenye dhambi wote… lakini hakuwahi kuwatuma Pamoja na wakina Petro wakahubiri Injili!!.. Hakuna mahali Bwana Yesu kamtupa Adrea na Farisayo mmoja au kahaba wakafanye collaboration katika kuhubiri Injili!.. Kwasababu hilo kundi bado lilikuwa linahitaji kwanza kuhubiriwa liokoke na si kwenda kufanya huduma!.
Kwahiyo na sisi kama Watumishi tulioitwa katika kuutangaza ufalme wa Mungu kwa njia ya nyimbo na nyinginezo.. na kama tunataka kushirikiana Pamoja na watu wengine ambao kwasasa ni wa kidunia, (bado hawajaokoka)..Sharti kwanza TUWABADILISHE WAOKOKE!!!, watubu dhambi zao na kubadilisha Maisha yao, na baada ya kuokoka na kupata wokovu kamili, wakae kwenye madarasa ya kumjua Mungu kwa kitambo Fulani, na wakishafikia kiwango Fulani cha ufahamu wa kumjua Mungu, ndipo tushiriki nao katika kufanya huduma ya kumwimbia Mungu au uinjilisti, Ili kazi ya Mungu isiharibike wala kutukanwa!!.
Kwahiyo kwa hitimisho, ni kwamba sio sahihi kushiriki Pamoja na wasio amini kutangaza Habari za ufalme wa mbinguni..
Bwana atubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je ni sahihi kusikiliza miziki ya kidunia?.
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
Je! Ni kanisa lipi sahihi kumuabudia Mungu?