Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? (Yeremia 17:9)

by Admin | 18 May 2022 08:46 am05

SWALI: Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? Yeremia 17:9

Yeremia 17:9 “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua”?


Kufisha; maana yake ni kusababisha kitu kife.

Hivyo hapo anaposema..moyo una ugonjwa wa kufisha.. Maana yake ni kuwa una ugonjwa wa kupelekea mauti, yaani ugonjwa usioponyeka.

Akiwa na maana kuwa, udanganyifu wa moyo ni mbaya sana, unaweza kukupeleka sio tu mauti ya mwili wako, bali mpaka roho yako pia. Kwamfano waweza kujiuliza shetani alidanganywa na nani kule mbinguni?. Jibu ni kuwa hakudanganywa na mtu yeyote, bali alidanganywa na moyo wake mwenyewe kwamba na yeye anaweza kuwa kama Mungu.

Na mwisho wa siku akapata hasara ambayo mpaka leo hii anaijutia ndani ya moyo wake. Hata sasa udanganyifu wa kwanza hautoki kwa shetani, bali unatoka ndani yetu wenyewe. Baadaye tukishadanganyika, ndipo shetani anapata nafasi ya kuuchochoa udanganyifu huo.

Biblia inasema,

Mithali 14:12 “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti”.

Unaweza kuona kuvaa vimini na kujichubua ni sawa kwasababu moyo wako unakuambia hivyo, lakini kumbe ndio unakwenda kujiangamiza mwenyewe. Unaweza kudhani kumwabudu Mungu kwa kupitia chochote ni sawa tu kumbe, mwisho wake ni mauti.

Njia ni moja tu, nayo ni Yesu Kristo.

Hivyo andiko hilo, linatupa tahadhari kuwa, tumsikilize Mungu, kuliko mioyo yetu. Kwasababu wengi wamepotea, kwa kutii tamaa za mioyo yao, na sio Neno la Mungu.

Bwana atusaidie sana.

Neno “kufisha” utalisoma pia katika vifungu hivi;

Luka 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.

Zaburi 7:13 “Naye amemtengenezea silaha za kufisha, Akifanya mishale yake kuwa ya moto”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

Jehanamu ni nini?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

JIWE LILILO HAI.

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/05/18/nini-maana-ya-ugonjwa-wa-kufisha-yeremia-179/