Je ni sahihi kusikiliza miziki ya kidunia?.

Je ni sahihi kusikiliza miziki ya kidunia?.

Jibu: Mpaka imeitwa miziki ya kidunia maana yake imebeba maudhui ya kidunia: Na biblia inasema yeye aliye rafiki wa dunia ni adui wa Mungu.

1Yohana 2:15  “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16  Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17  Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”

Miziki yote ya kidunia inahubiri au kutangaza mojawapo ya vitu vifuatavyo: uasherati, vurugu, kiburi, kutukuza vitu vya ulimwengu huu kama mali na fahari zake, na kilicho kikuu Miziki hii inachokihubiri ni UVUGUVUGU.

Sasa kwanini uvuguvugu?

Utakuta wimbo una beti moja au mbili zinazotangaza kupendana, au zinazotaja uweza wa Mungu, na kumsifia Mungu, lakini ina beti sita za matusi, au beti 4 zinazotangaza uasherati na anasa za ulimwengu huu, Hivyo zinatangaza uvuguvugu asilimia mia moja!..na Mtu anapoisikiliza, na yeye ile roho ya uvuguvugu, ni lazima imwingie…na  Bwana Yesu aliukataa na kuulani uvuguvugu!.

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16  Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu”

Mungu anauchukia uvuguvugu kuliko hata kuwa baridi!..yaani kwa Mungu ni heri mtu awe baridi kabisa lakini si vuguvugu.

Hivyo si sahihi kabisa kwa Mkristo kusikiliza miziki ya kidunia. Kwasababu inatangaza mambo ya kidunia.

Na mtu anayeokoka ni lazima aifute miziki hiyo na kuacha kuisikiliza kabisa.. na kuanza kuujaza moyo wake mambo ya kiMungu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

Je watu ambao hawajasikia kabisa injili watahukumiwa?

WAOMBEENI WANAOWAUDHI.

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

Ukweli dhidi ya uongo.

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
1 year ago

Je, ni sahihi mkristo kuvalia shanga mkononi