Title May 2022

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

SWALI: Je? Daudi na Yonathani walikua wanashiriki mapenzi ya jinsia moja?

Kufuatana na vifungu hivi;

1 Samweli 20:30

[30]Basi hasira yake Sauli ikawaka juu ya Yonathani, akamwambia, Wewe, mwana wa mke mkaidi, asi, je! Mimi sijui ya kuwa umemchagua huyo mwana wa Yese, kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.


JIBU: Andiko hilo halina uhusiano wowote wa Yonathani na Daudi kuwa na mahusiano ya jinsia moja..

Wazo kama hilo linakuja kichwani mwa watu kufuatana na lile andiko linalosema upendo wa Jonathan kwa Daudi ulikuwa zaidi ya upendo wa mwanamke (2Samweli 1:26).Ambalo nalo halihusiani na jambo hilo kabisa.

Katika andiko hilo tunaona Sauli alipoona kwamba mwanawe Jonathani anashikamana sana na Daudi na kwamba yupo tayari hata kumwachia ufalme wake ambao alistahili yeye kuumiliki..ilimfanya Sauli aghadhibike sana juu yake ndipo akamwambia maneno hayo..

1 Samweli 20:30 “… je! Mimi sijui ya kuwa umemchagua huyo mwana wa Yese, kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako”.

“Aibu ya uchi wa mama yake”..Akiwa na maana “aibu ya mama yake aliyemzaa” na si vinginevyo .

Yaani kwa tendo lile la kumruhusu Daudi aje kuwa mfalme wa Israeli badala yake italeta aibu kubwa na fedheha kwa mama yake, kwa kuzaa mtoto ambaye haendelezi ufalme katika familia

Na ikumbukwe kuwa wa-mama wa wafalme enzi zile walikuwa wanapewa heshima kubwa kiasi cha kuwekewa kiti cha enzi pembezoni mwa wafalme . Na ndio maana utaona sehemu nyingi mfalme mpya atajwapo huwa anaambatanishwa na jina la mama yake, na sio mke au mtoto kwasababu walipewa heshima yao, kipekee. ( soma 2Wafalme 21:19, 22:1).

Sasa hapa inapotokea Yonathani hapiganii kiti chake cha ufalme kinyume chake ndio yupo tayari kumpa Daudi ufalme wote..Ndio maana Sauli akamwambia tendo analolifanya ni aibu kubwa sana kwa mama yake.

Hii inatufundisha nini?

Upendo usio wa kinafki unakuwa tayari kujishusha pale panapostahili kufanya hivyo.

Hautafuti mambo yake wenyewe..sawasawa na 1Wakorintho 13:5

Unawatanguliza wengine mbele..

Si ajabu ni kwanini Daudi hakuufananisha upendo ule na wa mwanamke yeyote duniani.

Na sisi pia tupendane, kwa kuwa tayari kutangulizana. Kumuhesabu mwingine ni bora zaidi yetu sisi wenyewe, Hiyo itatupa kibali kikubwa sana kwa Mungu. Kama vile Yonathani ambaye hadi leo hii tunazisoma habari zake kwa mema.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAMA, TAZAMA, MWANAO.

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Upole ni nini?

Unyenyekevu ni nini?

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1).

Kiyama ni nini?

YESU NDIYE ATAKAYEKURUSHIA MAWE, USIPOTUBU.

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

Rudi nyumbani

Print this post

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

Tusome,

Yohana 8:56 “Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi”.

Jibu: Siku aliyoiiona Ibrahimu sio siku Kristo anamwaga damu yake pale Kalvari, kwaajili ya ondoleo la dhambi ya ulimwengu..

Sasa ni lini Ibrahimu aliiona hiyo siku?

Aliiona hiyo siku wakati anakutana na Melkizedeki, mfalme wa Salemu. Melkizedeki  maandiko yanasema alikuwa KUHANI WA MUNGU ALIYE JUU. (Hapa ndipo siri ya furaha ya Ibrahimu ilipokuwepo).

Melkizedeki alimjia Ibrahimu kama mtu, akiwa na mkate na Divai mkononi mwake, na akampatia Ibrahimu mkate ule na divai ile. Sasa Melkizedeki alikuwa ni Bwana Yesu Mwenyewe, aliyemtokea Ibrahimu kwa sura nyingine, na kwa umbile lingine, kabla ya wakati..

Waebrania 6:20 “alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki”.

Ndio maana, Bwana Yesu aliwaambia Wayahudi, kwamba kabla ya Ibrahimu kuwapo yeye (Yesu) alikuwapo..

Yohana 8:57 “Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?

58 YESU AKAWAAMBIA, AMIN, AMIN, NAWAAMBIA, YEYE IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NIKO.

59 Basi wakaokota mawe ili wamtupie; lakini Yesu akajificha, akatoka hekaluni”

Kwahiyo tumeshaona kuwa aliyekutana na Ibrahimu alikuwa ni Bwana Yesu mwenyewe katika mwili. Lakini utaona huyu Melkizedeki (Kristo), alipokutana na Ibrahimu, hakumpa nyumba, wala mali, wala fedha, wala kingine chochote, bali alimpa MKATE na DIVAI.

Sasa huo Mkate na Divai Ibrahimu aliopewa na Melkizedeki.. ulikuwa ni ufunuo wa Mwili na Damu ya Yesu ambao atakuja kuutoa baadaye kwaajili ya uzima wa ulimwengu..

Yohana 6:51 “Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.

52 Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sisi mwili wake ili tuule?

53 Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.

54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.

55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.

56 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake ”.

Hiyo ndiyo sababu kwanini Bwana Yesu siku ile ya pasaka alitwaa Mkate na Divai na kuwapatia wanafunzi wake, na akaagiza tendo lile la kushiriki Mwili wake na damu yake liwe endelevu.

Kwahiyo Ibrahimu alipata ufunuo wa Melkizedeki, kuwa ni Melkizedeki ni Kuhani wa Mungu ambaye atakuja kuleta upatanisho kupitia Mwili wake na Damu yake, ambao unafananishwa na ule Mkate na Divai.

Kwahiyo kitendo hicho cha Ibrahimu kupata ufunuo wa ukuhani wa Melkizedeki, atakaokuja kuufanya siku za mbeleni, ndicho kilichomfanya ashangilie.

Na alishangilia kwasababu aliona Ulimwengu unakwenda kupatanishwa, unakwenda kuokolewa na Kuhani Mkuu, unakwenda kumkaribia Mungu kupitia huyu Melkizedeki..

Ndio maana utaona Ibrahimu hakumwona Melkizedeki kama Mfalme tu!, bali alimwona kama Kuhani Mkuu..

Sasa kabla ya kuendelea mbele hebu tujikumbushe kwa ufupi kuhani ni nani na kazi ya kuhani ni ipi?

Kuhani ni mtu Maalumu aliyeteuliwa na Mungu, kuwaunganisha watu na Mungu wao. Kwasababu katika kumkaribia Mungu kuna kanuni.. katika kumtolea kuna kanuni, vile vile katika kumwomba au kupeleka haja zetu kwake kuna kanuni. Sasa Mtu asipozijua hizi kanuni na akamwendea Mungu hataambulia chochote, au hata anaweza kujitia katika laana badala ya baraka kutokana na kutokujua kanuni.

Hivyo Makuhani ni watu maalumu waliokuwa wanazijua kanuni za kusogelea Mungu na kumsogeza Mtu kwa Mungu.. Ndio maana utaona wana wa Israeli walipotaka kumtolea Mungu, kulikuwa na taratibu za Namna ya kumtolea Mungu ili sadaka hiyo ikubalike, kwamba ilikuwa ni lazima Mwanakondoo achinjwe ipatikane damu, na kupitia ile damu kuhani anaingia nayo ndani ya hema na kufanya upatanisho wa yule mtu na muumba wake..

Sasa Ibrahimu alikuwa anajua umuhimu wa Ukuhani na Makuhani. Ndio maana siku hii alipokutana na Melkizedeki alifurahi.

Sasa kwanini alifurahi?.. Ni kwasababu huyu aliyekutana naye..alikuwa ni KUHANI, na sio kuhani tu!, bali kuhani MKUU!, na sio kuhani mkuu tu!, bali kuhani mkuu wa MILELE wa Mungu aliye juu. (Zaburi 110:4).

Mwanzo 14:18 “Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa KUHANI WA MUNGU ALIYE JUU SANA”

Ibrahimu alipojua kuwa Melkizedeki ni kuhani Milele, maana yake alijua kuwa hata siku yeye atakapokufa!, bado huyu kuhani atakuwepo..kwahiyo alimuona Melkizedeki akija tena miaka mingi baadaye akiwa na Mkate na Divai na kuupa ulimwengu mzima….

Alimuona Melkizedeki akija tena duniani, Pamoja na damu, ili kuwapatanisha watu na Mungu wao..Alimuona akiingia kwenye hema ya kimbinguni akifanya upatanisho, na aliona kupitia damu yake mwenyewe watu wanapatanishwa na Mungu. Hivyo alifurahi na kushangilia..

Waebrania 6:20 “alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki”.

Waebrania 5:9 “naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;

10 kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki”.

Hadi leo hii, huyu Kuhani Mkuu, Yesu.. yupo anaishi na ndiye mpatanishi wetu sisi na Baba. Wala hakuna wokovu kwa mwingine yeyote, wala hakuna njia nyingine yeyote ya kufika mbinguni isipokuwa kwa njia yake yeye.

Waebrania 8:1 “Basi, katika hayo tunayosema, neno lililo kuu ndilo hili: Tunaye kuhani mkuu wa namna hii, aliyeketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Ukuu mbinguni,

2 mhudumu wa patakatifu, na wa ile hema ya kweli, ambayo Bwana aliiweka wala si mwanadamu”.

Je umemwamini na kuoshwa dhambi zako naye?..kumbuka dini yako, tabia yako nzuri, sifa zako nzuri, dhehebu lako, na matendo yako havitakufikisha mbinguni kama utakuwa hujamwamini na kufuata kanuni zake za wokovu. Na kanuni yake ni kuamini, kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, kubatizwa ubatizo sahihi na kupokea Roho Mtakatifu. Kama umeikosa hii kanuni basi wewe upo mbali na Mungu, haijalishi unaona mambo yako yanaenda sawa..

Mkaribie leo Yesu kuhani Mkuu upate wokovu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

NI NINI BWANA ANATAZAMIA KILA TUNAPOSHIRIKI MEZA YAKE.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

KATIKA MLIMA WA BWANA ITAPATIKANA.

Je ni sahihi kumwita mtu “Mkuu”?

TUSIWE WAVIVU WA KUSIKIA.

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Swali: Tunasoma katika Warumi 11:4, Mungu anasema kuwa “nimejisazia” lakini katika Wafalme tunasoma Mungu anasema “nitajisazia” kana kwamba ni kitendo kinachokuja mbeleni.. Je hapo mwandishi gani yupo sahihi?

Tusome:

Warumi 11:4 “Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? “NIMEJISAZIA WATU ELFU SABA” wasiopiga goti mbele ya Baali”.

1Wafalme 19:18 “Pamoja na hayo NITAJISAZIA katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia Baali, na kila kinywa kisichombusu”.

Jibu: Ni muhimu kufahamu kuwa siku zote biblia haijichanganyi.. isipokuwa fahamu zetu ndizo zinazojichanganya..

Ili kuelewa vizuri labda tuanze kusoma juu kidogo katika mstari huo 1Wafalme 19 ila tuanzie juu kidogo..

1Wafalme 19:14 “Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana, Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu waiondoe.

15 Bwana akamwambia, Enenda, urudi njia ya jangwa la Dameski; ukifika, mtie mafuta Hazaeli awe mfalme wa Shamu.

16 Na Yehu mwana wa Nimshi mtie mafuta awe mfalme wa Israeli; na Elisha mwana wa Shafati wa Abel-Mehola mtie mafuta awe nabii mahali pako.

17 NA ITAKUWA ATAKAYEOKOKA NA UPANGA WA HAZAELI, YEHU ATAMWUA; NA ATAKAYEOKOKA NA UPANGA WA YEHU, ELISHA ATAMWUA.

18 Pamoja na hayo NITAJISAZIA katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia “baali”, na kila kinywa kisichombusu”.

Katika Habari hiyo tunaona kuwa kumbe Mungu alikuwa amekusudia kuwaangamiza watu wote wanaobudu na kumsujudia baali. Lakini utaona wakati anataka kupitisha hukumu hiyo, akasema ATAJISAZIA yaani (atawabakisha) watu elfu 7 ambao hawamsujudii baali TANGU SASA.. yaani wakati wengine wote watakufa kwa upanga wa Hazaeli, Yehu au Elisha, Ambao utakuja baadaye.. hili kundi la watu elfu 7 lililopo sasa, litakuwa salama kwasababu halimsujudii Baali..

Kwahiyo Mwandishi wa Kitabu cha Warumi hajichanganyi na wa kitabu cha Wafalme, wote wapo sahihi

Ili tuelewe Zaidi labda tutafakari mfano huu.

“Umetenga magunia 10 ya makapi, na magunia 7 ya ngano.. na ukamwambia mtu mmoja kuwa “wiki ijayo utayachoma magunia yote ya makapi, na utabakiwa na magunia 7 ya ngano”. Na wakati wakati huo huo ukampa taarifa hiyo hiyo mtu mwingine kwa kusema “umejibakishia magunia 7 ya ngano ambayo hutayachoma moto wakati utakapoteketeza makapi”. Je! Kwa kauli hizo mbili utakuwa umejichanganya?.. jibu ni la!.. utakuwa umeelezea jambo lile lile ila kwa namna nyingine.. Ndicho Mwandishi wa kitabu cha Wafalme na Warumi walichoandika, kauli zao hazijakinzana bali zote zimelenga kitu kimoja na maana ile ile moja.

Lakini nini tunachoweza kujifunza hapo katika Habari hiyo?.. Tunachoweza kujifunza ni kuwa Mungu analitimiza neno lake na wala hasemi uongo.. aliwaondoa wote wanaoabudu baali na kuwasaza watu elfu 7 kama alivyosema..wasiopigia goti baali.

Na zama hizi za mwisho, unabii unasema Kristo atarudi kwaajili ya hukumu ya ulimwengu kwa wote wanaotenda maovu. Na neno lake kama alivyosema litatimia. Hivyo ni wajibu wetu sisi kusimama katika Imani kama tumeshampokea Yesu, na kama bado ni wakati wa kumpokea na kuiamini injili yake.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Baali alikuwa nani?

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

Ni kiumbe gani kinachosujudiwa hapo katika Warumi 1:25?

Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze maneno ya Uzima wa Mungu wetu..

Yapo maswali kadhaa ambayo tunaweza kujiuliza, juu ya tukio la Bwana Yesu kutokewa na Musa na Eliya siku ile alipopanda mlimani kuomba pamoja na wale wanafunzi wake watatu (Petro, Yohana na Yakobo)..

Na maswali yenyewe ni haya..

 1) Iweje Bwana Yesu atokewe na Musa ambaye tayari alishakufa miaka mingi?, na Zaidi ya yote maandiko yanasema alizikwa, tena na Mungu mwenyewe?..

2) Kwanini Musa na Eliya wamtokee?.. kulikuwa na umuhimu gani wa wao kumtokea Bwana?

Sasa ili tupate majibu ya maswali hayo vizuri, Labda tusome habari yenyewe kwa ufupi kisha tuendelee

Luka 9:28 “Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba.

29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.

30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni MUSA NA ELIYA;

31 walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”

Kiini cha majibu ya maswali yetu tutakipata katika huu mstari wa 31.. “walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”

Kumbe Sababu ya Musa na Eliya kumtokea Bwana, ilikuwa ni kuzungumza kuhusu Kufa kwake Bwana Yesu, ambako atakutimiza Yerusalemu.

Sasa swali linakuja?, je ni kwamba Bwana Yesu alikuwa hajui kwamba atakwenda kufa mpaka atokewe na watu hao wawili, wamweleze kuhusu kufa kwake?.. Jibu ni la!.. alikuwa anajua, lakini zipo siri nyingine zihusuzo kufa kwake na kufufuka kwake na kupaa kwake, ambazo hizo Baba alimfunulia siku hiyo kupitia manabii hao wawili.

Kumbuka kabla ya Kristo kufa, roho za watakatifu zilikuwa chini, na shetani alikuwa na uwezo wa kuzileta juu, kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka lile tukio la Samweli kuletwa juu ya yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi, na baada ya kuletwa juu, Samweli aliweza kutoa unabii wa mambo yajayo, ijapokuwa alikuwa ameshakufa na kuzikwa, kwani tunasoma, alimtolewa Unabii Mfalme Sauli kuhusu KUFA KWAKWE, AMBAKO KUTAKWENDA KUTIMIA KIPINDI SI KIREFU KUTOKA PALE. Unaweza kusoma Habari hiyo kwa urefu katika kitabu cha 1Samweli 28:1-19.

Sasa Biblia haijaeleza Musa alikuwa anamweleza nini Bwana Yesu, lakini tunajua kabisa ni kuhusu Habari za kufunguliwa kwao wafu, na kwamba Bwana Yesu atakwenda kusulibiwa na kushuka sehemu ya wafu wao (akina Musa na wengine walipo na kuwaweka huru, na kwamba siku ya tatu atafufuka).

Kwahiyo kumbe kabla ya Bwana Yesu kufa, Wafu waliendelea kuishi, na pia iliwezekana kuwaleta baadhi yao juu na kutoa unabii, kwa njia yoyote ile!..

Kwasababu hiyo basi tumeshapata jibu ni kwanini MUSA, aliletwa juu na Mungu, ili kutoa unabii (Habari za kufa kwake Bwana Yesu, ijapokuwa Musa alikuwa ameshakufa kitambo na kuzikwa)…Ni kama tu vile, Nabii Samweli alivyoletwa juu na yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi. (Kumbuka jambo hilo liliwezekana tu kipindi kabla ya Bwana Yesu kufa, lakini baada ya Bwana Yesu kufa na kufufuka, hakuna mchawi yeyote anayeweza kumleta juu mtu aliyekufa, kwasababu Kristo alizichukua funguo za Mauti na kuzimu).

Hapo tumepata jibu kuhusu Musa, sasa vipi kuhusu ELIYA?

Tunajua kabisa Eliya hakufa, bali alipaa..Maana yake Eliya anayajua yaliyo ya Mbinguni.. kama Nabii, Bwana alimtoa huko na kuja kumpasha Habari Bwana Yesu, kuhusu kupaa kwake, na enzi na mamlaka zinazomngojea Mbinguni (labda na siku hiyo alimpa na tarehe ya kupaa kwake, hatujui).

Kwasababu ijapokuwa Eliya alikuwa amepaa mbinguni, lakini bado alikuwa ni Nabii. Kwahiyo ujio wa Eliya ulikuwa ni wa muhimu sana kwa Bwana, kupata taarifa kuhusu kupaa kwake.

Kwahiyo kwaufupi ni kwamba Mungu aliwatumia manabii hawa wawili kama Manabii wa Ushahidi. Na Ushahidi huo ni wa KUFA kupitia Musa, na Kupaa kupitia ELIYA. Kwasababu Kristo naye atakufa kama Musa aliye nabii mkuu, na vile vile atapaa mbinguni kama ELIYA.

Kwahiyo baada ya tukio lile, Bwana Yesu alipokea Ufunuo mkuu kuhusu Mauti yake na kufufuka kwake, na kupaa kwake.. Zaidi sana na kurudi kwake kutakavyokuwa..ndio maana tunaona pia Uso wake uling’aa kama jua, kuashiria siku ya kurudi kwake kutakavyokuwa.

Na wakati ulipofika kweli Bwana Yesu, alikufa, akafufuka, na akapaa mbinguni.. imesalia hatua moja tu!.. nayo ni KURUDI KWAKE KUTUCHUKUA!..

Je! Umejiandaaje?.. Kama Nabii hizo mbili za kufa na kufufuka kwake na kupaa kwake zilitimia.. Basi hata kurudi kwake kutatimia. Na tupo katika majira ya kurudi kwake, dalili zote zimeshaonekana, muda wowote mambo yanakwisha, Kristo anakuja kuwachukua watakatifu wake, na kitakachokuwa kimesalia kwa wale watakaobaki ni majuto na dhiki kuu.

Je umejiandaaje? Je umemwamini Yesu na kutubu dhambi zako? Je umebatizwa katika ubatizo sahihi?…kama bado unangoja nini?.. Ukiikataa leo injili siku hiyo hutakuwa na la kujitetea. Mpokee Yesu leo, na ukabatizwe na kujazwa Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

Rudi nyumbani

Print this post

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Unajua ni kwasababu gani Bwana Yesu aliitwa Mwana wa Mungu? ..Mungu kukuona wewe kama  mwana wake kweli kweli sio tu uwe umezaliwa na yeye kwa kumkiri na kubatizwa, hapana bali pia kuwa na huduma ya upatanisho ndani yako….

Biblia inasema..

Mathayo 5:9

[9]Heri wapatanishi;

Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

Jiulize Kwanini isiseme wataitwa watakatifu, au wataitwa wafalme, au wataitwa makuhani wa Mungu..bali wana wa Mungu.

Hilo jambo ambalo Yesu Kristo alilijua ndio maana kusudi lake kubwa la yeye kuja duniani, lilikuwa ni kutupatanisha sisi na Mungu..Yaani sisi tuliokuwa tumefarakana na Mungu kwasababi ya dhambi, sasa tunawasiliana naye kwa kupitia Yesu Kristo mwana wake..

Tunalithibitisha hilo katika mistari hii..

2 Wakorintho 5:18-19

[18]Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho;

[19]yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.

Umeona? Tendo la Yesu kuacha enzi na mamlaka, na kuja duniani ili kutupatanisha tu sisi hilo ndio lililomfanya Mungu amwone kuwa ni mwana  bora kuliko wana wake wote aliokuwa nao.

Ndio maana akamshuhudia  mwenyewe..Huyu ni mwana wangu, mpendwa wangu, niliyependezwa naye. (Mathayo 3:17)

Akampa kibali cha kipekee kuliko wanadamu wote walioko ulimwenguni.

Hata sisi ili  Mungu atuone ni wana wake kwelikweli hatuna budi kuwa na huduma hii ya upatanisho ndani yetu.

Tuulete ulimwengu kwa Kristo. Lakini jambo ambalo hatujui ni kuwa kuwapatanisha watu waliogombana si jambo rahisi..la kwenda kuwashikanisha mikono tu halafu basi.. Hapana..lina gharama kubwa sana..kama ulishawahi kujaribu utalithibitisha hilo.

Ilimlazimu Yesu aache enzi na mamlaka, aje duniani, na kama hiyo haitoshi akataliwe kwanza na wale anaowapatanisha, (yaani sisi), na bado autoe uhai wake pia kwa ajili wao.

Kwa ufupi ni kwamba alikuwa anafosi upatanisho ambao ulikuwa hauwezekani kwa namna yoyote ile, ni uadui uliokuwa umekomaa..lakini hakukata tamaa, hadi mwisho wa siku ukatokea tu wenyewe.

Na sisi vivyo hivyo anasema ametupa huduma ya upatanisho. Yaani na sisi tukaupatanishe ulimwengu na Mungu kwa kupitia yeye.

Hivyo tufahamu kuwa tunapowahubiria watu, hadi kuokoka halitakuwa jambo rahisi kama sisi tunavyodhani..Watu wengi wamekatishwa tamaa  kuhubiri habari njema..kisa watu wanaowahubiria hawana geuko au badiliko, lolote..wengine ndio wanawatukana na kuwapiga

Hatuna budi kuendelea..kwasababu hakuna upatanisho ulio mwepesi. Ni unajitoa sadaka kwa vita ambayo si yako. Leo atakupuuzia, kesho atakutukana, lakini kesho kutwa ataokoka.

Ukifanikiwa kwa jambo hilo moja. Utajiongezea daraja la juu zaidi mbinguni..La kuwa mwana mpendwa wa Mungu. Na kwa jinsi unavyoendelea kufanya ndivyo kubali chako kinavyoongozeka kwa Mungu, hatimaye..kufikia kilele cha kufanana na Yesu Kristo..Ukimwomba Mungu lolote atakupa, na kazi zake zote utazifanya..Kama yeye alivyosema maneno haya..

Yohana 5:20-21

[20]Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizo atamwonyesha, ili ninyi mpate kustaajabu.

[21]Maana kama Baba awafufuavyo wafu na kuwahuisha, vivyo hivyo na Mwana awahuisha wale awatakao.

Umeona hiyo ndio faida za kuwa mwana wa Mungu kwelikweli.

Nasi pia tuanze kwa kuthamini wengine, kwa kuwahubiri habari njema, hapo tutakuwa tunaukiri UWANA wetu kwa Mungu..Ukimwona jirani yako amepotea basi pambana naye kwa hali na mali mpaka amgeukie Kristo kama wewe…wakati mwingine ugumu utakuwepo japo si kwa wote..

Ukifahamu kuwa hakuna upatanisho usiokuwa na gharama, basi utakuwa na uvumilivu na amani kwa yote utakayokutana nayo.

Bwana akubariki.

Uwe na utumishi mwema wa upatanisho.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MJUE SANA YESU KRISTO.

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Heri maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Kwanini, tuimbe, je! kuna ulazima wowote wa kufanya hivyo?

Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Kiyama ni nini?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

Daudi anapomwambia Mungu, kuwa GONGO LAKE na FIMBO YAKE vinamfariji, alikuwa anamaanisha nini?..

Jibu: Tusome,

Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, GONGO LAKO NA FIMBO YAKO VYANIFARIJI”.

Zamani wachungaji wa kondoo na Mbuzi, walikuwa wanatembea na Zana hizo mbili (Gongo na Fimbo), zilizokuwa zinazowasaidia katika shughuli zao uchungaji. Na kila zana likuwa na kazi yake.

GONGO: Hii ilikuwa ni kipande cha kifupi cha fimbo maalum, iliyonyooka, ambayo ilikuwa Nene kidogo na fupi, Na kazi ya Gongo, ilikuwa si nyingine Zaidi ya kupiga maadui wa mifugo kama Mbwa mwitu, dubu, Mbweha, fisi n.k Kwahiyo wachugaji walitembea nayo wakiwa katika uchungaji, ili kundi liwe salama..Fisi walipotokea kutaka kukamata kondoo, wachungaji waliwapiga kwa gongo hilo.

FIMBO: Hii ni Zana ya pili, ambayo haikuwa kwa lengo la kudhuru maadui, bali kwa lengo la kuwaongoza kondoo. Fimbo ya Mchungaji ilikuwa ni ndefu na yenye mkunjo mwishoni, na lengo la mkunjo huo ni kumvuta kondoo anapokuwa kwenye hatari au anapoelekea kwenye hatari, mkunjo ule unasaidia kuishika shingo ya kondoo au mguu wa kondoo na kumvuta kutoka kwenye hatari.. vile vile, kazi nyingine ya fimbo hiyo ni kuwaongoza kondoo wakae kwenye mstari, wasitoke.

Sasa swali ni kwanini Daudi aseme Fimbo ya Bwana na Gongo lake vinamfariji?

Ni kwasababu yeye (Daudi) anajifananisha na kondoo na Mungu anamfananisha na Mchungaji aliyeshika Fimbo na Gongo, kwamba kondoo anapoona kuwa mchungaji wake kashika Gongo, basi anakuwa hana wasiwasi kwasababu anajua gongo lile kazi yake ni kuwapiga maadui zake.. Hivyo Daudi hakuogopa maadui kwasababu Bwana ndiye mchungaji wake, hivyo gongo lile lilikuwa Faraja kwake.

Vile vile, Fimbo ya Bwana, ambayo ina mkunjo mwishoni, ilimfariji kwasababu yeye kama kondoo alijua hawezi kupotea, kwasababu ile Fimbo itamwongoza katika njia iliyonyooka, Zaidi sana hata atakapopita kando ya bonde la Mauti, Fimbo ile itamwongoza katika njia iliyonyooka, na hatapotea kamwe.

Na sisi katika roho ni kondoo na Yesu ni Mchungaji, Mkuu.. Ambaye naye pia ameshika Gongo na Fimbo, kutulinda na kutuchunga.

Waebrania 13:20 “Basi, Mungu wa amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu MCHUNGAJI MKUU WA KONDOO, kwa damu ya agano la milele, yeye BWANA WETU YESU”

Umeona?..Bwana Yesu ni Mchungaji Mkuu wa Kondoo.. wengine ni wachungaji, lakini si wachungaji wakuu.., hali kadhalika wengine ni wachungaji, lakini si wachungaji wema… Lakini Bwana Yesu ni mchungaji Mkuu, na Mchungaji mwema.., anawachunga kondoo katika njia iliyo nyooka kwa fimbo yake, wala hakuna hata mmoja atapotea akiwa kwake, vile vile anaweza kutoa uhai wake kwaajili ya kuwaokoa kondoo..

Yohana 10:11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.

12 Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwakamata na kuwatawanya.

13 Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake”.

Je! Umempokea Yesu leo?.. Je Bwana Yesu ni mchungaji wako?.. kama hujampokea Yesu, bado wewe ni kondoo uliyepotea,  ambaye Bwana Yesu, mchungaji mwema ANAKUTAFUTA!!!, kwasababu hapo ulipo haupo salama, mbwa-mwitu wanasikia harufu yako toka mbali na wanakusogelea kwa kasi, fisi na dubu, wanasikia harufu yako na wanakukaribia ili wakudhuru, wakufanye kitoweo… Leo hii umemwona Mchungaji mwema Yesu Kristo, mkimbilie huyo uwe salama, ili hatimaye useme kama Daudi.. “Bwana ndiye Mchungaji wangu, sitapungukiwa na chochote, gongo lake na fimbo yake vyanifariji”.

Huko kwenye ulevi ulipo, umepotea, huko kwenye uzinzi, na uasherati ulipo umepotea, huko kwenye dansi ulipo na kwenye miziki, fasheni, na anasa za kidunia umepotea!.. haupo salama!.. Maisha yako yapo hatarini, wewe ni windo bora la mapepo yote, ni windo bora la wachawi, ni windo bora la mauti. Na vyote hivyo vinakutafuta.. Haupo salama kabisa!..kimbilia kwa Yesu…

Kama bado hujaokoka na unahitaji kuokoka ili uwe salama ndani ya Mchungaji mwema Yesu, basi wasiliana nasi inbox tuweze kuomba nawe, sala fupi ya kumkaribisha Bwana Yesu, maishani mwako.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?

Kwa namna gani mauti hufanya kazi ndani yetu na uzima kwa wengine? (2Wakorintho 4:12).

JAWABU LA MAISHA YA MTU.

Rudi nyumbani

Print this post

NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

Nakusalimu katika jina kuu la Yesu Kristo Bwana, nakukaribisha tena, katika kuyatafakari maneno ya uzima, maadamu siku ile inakaribia.

Bwana wetu Yesu Kristo alipokuja hapa duniani, dira yake ya kwanza haikuwa kwa kila mtu duniani, bali ilikuwa kwanza kwa Wayahudi, kisha watu wengine baadaye, ndio maana hata watu wa mataifa walipomfuata awaponye aliweka ugumu mkubwa kidogo kwao, na aliwaeleza waziwazi kabisa kuwa sikutumwa kwa ajili yenu bali kwa wayahudi.( Soma Mathayo 15:22-28),

Hata kipindi kingine, alipowatuma wanafunzi kuhubiri, aliwakataza kabisa wasiwafuate mataifa ikiwemo wasamaria, waliokuwa Israeli wakati huo, bali wayahudi tu.

Mathayo 10:5 “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie.

6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli”.

Umeona, kwahiyo kusudi la awali la Kristo lilikuwa ni kumalizana kwanza na wayahudi.. Lakini kuna wakati, ratiba zake zilivurugwa, Hivyo akalazimika tu kutumiza kusudi lake la kuokoa kwa muda kwa watu wa mataifa aliokutana nao..

Embu tusome..

Yohana 4:3 “aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya.

4 NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

5 Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.

6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.

7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe”.

Umeona hapo, tafakari vizuri, Bwana hakuwa na lengo la kuzungumza chochote pale Samaria, bali, mawazo yake yalikuwa ni kwenda Galilaya kwa wayahudi..Lakini sasa ili kufika Galilaya ilimlazimu apitie Samaria., Hakuna namna.. Samaria ilikuwa ni njia panda ya kufika Galilaya..

Na alipofika pale biblia inatuambia, alikuwa amechoka sana, lakini je! Alale tu? Kisa hakutumwa kwao? Au akae tu apumzikie, huku akitazama roho za makafiri zikipotea?.. Ni wazi kuwa hata kama ni mimi, ningekuwa sijatumwa mahali Fulani, halafu nimechoka, ya nini kujisumbua kufanya nisiyoagizwa? Ningelala zangu..

Lakini kinyume chake, ilimpasa aghahiri hata kula chakula, aghahiri hata uchovu wake, aanzane na yule mwanamke mwenye dhambi pale kisimani, jambo lililomfanya sio tu yule mwanamke mwenyewe kumshangaa, bali pia mitume wake paliporudi, kumwona anawahubiria mataifa tena mwanamke jambo ambalo yeye mwenyewe alilikataza, huko nyuma.

Yohana 4:9 “Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)

10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai”.

Ni nini Bwana anataka tujifunze?

Ili ufikie Galilaya yako, huna budi kupitia Samaria, Ni Mungu mwenyewe ndio anayeruhusu hiyo hali, unasema nina mipango ya kwenda kuhubiri injili kwa watu Fulani mijini au vijijini, malengo ambayo ni mazuri, lakini leo hii unajikuta upo katika mazingira ya shule, ambayo hayatimizi malengo yako, Hapo hapo shuleni, kuwa muhubiri wa Injili, wahubirie wanafunzi wenzako, kwasababu imekupasa kwanza upitie hapo ndipo ufikie kule Mungu alikokuonyesha, au unakokutazamia.

Leo umejikuta katika mazingira ya kazini, usisubirie tu wakati Fulani kufika, ukasema bado bado. Kristo hakuwa na mawazo hayo. Alijua kabisa Samaria ni anapita tu, hana kusudi lolote pale, lakini aliwashuhudia Habari za wokovu, na hadi mwisho watu wengi wakamwamini hadi wakataka kumfanya awe mfalme wao, akakataa.

Kwahiyo wakristo wengi, sasa tumekuwa ni wa kusubiri suburi, tukisema ngoja kwanza nitoke hapa, au ngoja kwanza nimalize hiki au kile, ndio nitaanza kuifanya kazi ya Mungu.. Hujui ni kwanini Mungu kakupitisha hapo, tumia nafasi hiyo kumuhubiri Kristo,

Tumeambiwa, tuwe tayari wakati wote..ufaao na usiofaa.

2Timotheo 4:2 “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.

Halikadhalika Bwana Yesu mwenyewe  alituambia tujifunze kwake,(Mathayo 11:29)..Na hili ni somo mojawapo tunapaswa tulitafakari kutoka kwake, ili mahali popote tulipo tuwe watu wa kumzalia matunda, bila kungojea tufike Galilaya yetu.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?

OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!

JE MGOGORO WA URUSI NA UKRAINE,UMETABIRIWA KIBIBLIA?

Ni mlima gani Yule Mwanamke Msamaria aliokuwa anaumaanisha? (Yohana 4:19)

Ayari ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Kiburi cha Uzima ni nini? (1Yohana 2:16)

Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Rudi nyumbani

Print this post

HUANGUA MAYAI YA FIRA, NA KUSUKA WAVU WA BUIBUI;

SWALI: Isaya 59:5 ina maana gani?

Isaya 59:5 Huangua mayai ya fira, na kusuka wavu wa buibui; yeye alaye mayai yao hufa, na hilo livunjwalo hutoka nyoka.


JIBU: Ni mstari unaoeleza asili  ya watu waovu.

Anasema huangua mayai ya fira. Fira ni aina ya nyoka wenye sumu kali sana, ambao kwa kawaida mtu akikutana nao, ni lazima awaue, au akikuta mayai yao ni lazima ayakanyage, kwasababu, asipofanya hivyo yakitotolewa wataleta madhara, Lakini mtu mwovu biblia inasema ni kinyume chake huyatotoa. Ikiwa na maana ni mtu ambaye anaona madhara Fulani yanakuja mbele kwa wengine badala ayaangamize, yeye ndio anayekuwa wa kwanza kuyakumbatia.

Mfano mmojawapo wa hawa ni manabii wa uongo, wanaojua kabisa, dhambi ina madhara, na mtu asipoishi katika utakatifu hawezi kumwona Mungu (Waebrania 12:14), lakini kwasababu hawataki kupoteza watu, kwa  tamaa za pesa, hawawaonyi juu ya mambo kama hayo, kinyume chake ndio wanawasogeza kabisa kwenye mambo ya mwilini, biashara na mali, wanamsahau Mungu. Halafu wanakufa katika dhambi zao na kwenda kuzimu.

Vilevile anasema husuka wavu wa buibui. Kama vile tunavyojua buibui anaposuka wavu wake, ni kwa lengo la kunasa wadudu awale. Halikadhalika asili ya watu wa waovu ndivyo ilivyo, huandaa mazingira yote, ya wenzao kunaswa katika mambo maovu na kuangamia.

Kwamfano unapomwombea adui yako afe, ni sawa na mtu anayeunda wavu wa uangamivu. Bwana alisema tuwaombee, lakini sisi tunawatakia mauti, tena katika maombi.

Kwa ufupi, hii ni tabia ya kutengeneza kama sio kufurahia anguko la wengine.

Hivyo biblia inatuonyesha pia tukiwa na tabia kama hizo, zinatufanya na sisi Mungu asitutee na kutupa haki zetu kwa vile tumwombavyo, nasi majibu yanakuja kinyume chake.. Pale tunapotazamia jema linakuja ovu,na  tunapotazamia nuru linakuja giza, tunalithitibitisha hilo katika vifungu vinavyofuata..

Isaya 59:6-9

6 Nyavu zao hazitakuwa mavazi, wala hawatajifunika kwa kazi zao; kazi zao ni kazi za uovu, na vitendo vya udhalimu vimo mikononi mwao.

7 Miguu yao hukimbilia mabaya, nao hufanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia; mawazo yao ni mawazo ya uovu; ukiwa na uharibifu zaonekana katika njia kuu zao.

8 Njia ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika miendo yao; wamejifanyizia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hajui amani.

9 KWA SABABU HIYO HUKUMU YA HAKI I MBALI NASI, WALA HAKI HAITUFIKILII; TWATAZAMIA NURU, NA KUMBE! LATOKEA GIZA; TWATAZAMIA MWANGA, LAKINI TWAENDA KATIKA GIZA KUU.

Hivyo tupambane, kwa bidii zote tusiwe vyombo vya shetani vya kuunda mabaya kwa wengine.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Lumbwi ni nini katika biblia?

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Donda-Ndugu ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Ipo tofauti ya “Uzima” na “Uzima wa milele”.

Uzima, kila mwanadamu anao, na si wanadamu tu peke yao wenye uzima, bali hata Wanyama wanao uzima, na hata ndege na mimea. Lakini Pamoja na kwamba Uzima upo kwa viumbe vingi, lakini Uzima wa milele haupo kwa wote.

Uzima wa Milele ni kitu kingine kabisa…ambacho Mtu hana budi kukitafuta.. Na asipokitafuta na kukipata ataishia kuwa na uzima tu wa kitambo, ambao hautadumu sana, kwasababu wote wasio na uzima wa milele ndani yao, wakishakufa hawatafufuliwa na kuendelea kuishi, badala yake wataangamizwa katika ziwa la moto.

Na Uzima wa milele (ambao kwa lugha nyingine unaitwa “UZIMA TELE”), Unapatikana kwa mmoja tu ambaye ni Yesu.

Yohana 10:10 “…mimi nalikuja ili WAWE NA UZIMA, KISHA WAWE NAO TELE”.

Umeona?..Bwana Yesu amekuja ili tuwe na UZIMA, yaani tuwe na Afya, tuishi Maisha ya heri katika mwili, lakini hajaishia hapo, bali pia tuwe na UZIMA TELE, (Yaani tuwe Uzima wa Milele).

SASA SWALI NI JE TUTAUPATAJE UZIMA WA MILELE?

Jambo moja linalowachanganya wengi, ni kudhani kuwa kuwa na maadili mazuri au kuwa na dini nzuri, au KUSHIKA AMRI 10, ndio kupata Uzima wa milele, pasipo kujua kuwa kuzishika amri 10, au kuwa na dini nzuri, au dhehebu zuri, kama mtu “hajaamua kujikana nafsi ya kumfuata Bwana Yesu” ni kazi bure.. Dini yake nzuri huyo mtu, au maadili yake mazuri, au sifa yake nzuri bado, hakutampa uzima wa milele.

Hebu tusome kisa kifuatacho.. (Zingatia vipengele vilivyoanishwa kwa herufi kubwa).

Mathayo 19:16 “Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate UZIMA WA MILELE?

17 Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. LAKINI UKITAKA KUINGIA KATIKA UZIMA, zishike amri.

18 Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo,

19 Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.

20 Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?

21 Yesu akamwambia, UKITAKA KUWA MKAMILIFU, ENENDA UKAUZE ULIVYO NAVYO, UWAPE MASKINI, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI; KISHA NJOO UNIFUATE”.

Hapo nataka uone maswali, huyu mtu aliyomwuliza Bwana na Majibu Bwana aliyompa.. Swali la kwanza huyu mtu alitaka kujua jinsi ya kuupata UZIMA WA MILELE. Lakini utaona Bwana Yesu alimwambia akitaka KUUPATA UZIMA, (Zingatia; sio uzima wa milele, bali Uzima tu), azishike amri.

Ikiwa na maana kuwa Kuzishika amri 10 peke yake hazimpi mtu UZIMA WA MILELE, bali zinampa tu UZIMA. (aishi Maisha marefu hapa duniani na ya heri) Sawasawa na Walawi 18:5.

Walawi 18:5 “Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo MTU AKIZITUMIA ATAISHI KWA HIZO; mimi ndimi Bwana”.

Lakini swali la pili, huyu mtu alilomwuliza Bwana Yesu ni kwamba, tayari ameshazishika hizo amri, ni kitu gani alichopungukiwa Zaidi?.

Na Bwana Yesu alipoona kuwa anauhitaji UZIMA WA MILELE na si UZIMA TU!. Ndipo akamwambia “akauze kila kitu alichonacho kisha amfuate” kwa ufupi, ajikane nafsi yake ajitwike msalaba wake na kumfuata.

Lakini kwasababu yule mtu alikuwa anautaka Uzima na si Uzima wa milele, hakutaka kufanya vile, akaondoka!.. Na akaondoka akiwa na Uzima, na heri katika Maisha, lakini hana Uzima wa milele, jambo la kuhuzunisha sana.

Ndugu unayesoma ujumbe huu, maandiko yanasema kuwa Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele, habadiliki (kasome Waebrania 13:8), Maana yake ni kuwa vigezo vyake ni vile vile, kwa jinsi alivyomwambia huyu bwana, kwamba akauze vyote amfuate ndipo apate uzima wa milele, ndivyo anavyotuambia hata watu wa leo.

Sio kwamba huyu ndugu, alikuwa na bahati mbaya mpaka aambiwe vile na Bwana Yesu. Hapana!. Maneno hayo hayo aliwaambia pia wanafunzi wake kabla ya kumfuata..

Luka 14:33 “Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Sasa kuacha vyote kunakozungumziwa hapo ni kukitoa kitu katika moyo wako moja kwa moja, kama ni mali, Rafiki, ndugu, au chochote kile, unakitoa moyoni mwako na kuwa tayari kuyafanya mapenzi ya Mungu..Kama kimeondoka kweli moyoni mwako, basi hata ukiwa nacho kimwili hakina madhara yoyote, kwasababu kiwepo au kisiwepo, hakikusumbui kwasababu huna muunganiko nacho kiroho.. Lakini kama umekiondoa kimwili lakini moyoni mwako bado kipo, bado utakuwa hujafanya chochote..

Hivyo hiyo ni kanuni KUU sana, ambayo sote tunapaswa tujifunze. Gharama za kuupata uzima wa milele si ndogo. Zinahitaji kujikana nafsi kweli kweli, na kubeba msalaba na kumfuata Yesu.

Hebu kwa kumalizia tuisome faida hiyo ya kujikana nafsi na kumfuata Yesu kwa kumalizia mistari ya chini..

Mathayo 19:22 “Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

23 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.

24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.

25 Wanafunzi waliposikia, walishangaa mno, wakisema, Ni nani basi awezaye kuokoka?

26 Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.

27 Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?

28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele”.

Je! Umejikana nafsi na kumfuata Yesu? Au unajitumainia dini yako?, huyu kijana alikuwa na dini na ameshika amri zote lakini hakuwa na uzima wa milele ndani yake?, unadhani wewe na dhehebu lako utautolea wapi?..

Maadili yako yatakupa Uzima tu!, ni kweli utabarikiwa kwa kuishi vizuri duniani, kwa kuwa na moyo mzuri, lakini kama Yesu hajaingia ndani yako, huna uzima wa milele.

Ukitaka uzima wa milele weka dhehebu lako pembeni, weka dini yako pembeni, weka mali zako pembeni, weka uzuri wako pembeni, weka umaarufu wako pembeni,  weka sifa zako pembeni, na kila kitu chako, weka kando nenda kama mshamba mbele zake Bwana Yesu, kama asiyejua chochote, kama mtu aliyezaliwa leo, kama vile kondoo aliyetayari kuchungwa…Bwana Yesu anataka moyo uliojiachia kwake, moyo wa unyenyekevu..hapo ndipo atakapokuonyesha njia na kukupa uzima wa milele?.

Kama hujaokoka basi hakikisha siku ya leo haipiti bila kuokoka, kwasababu hujui ni nini kitatokea kesho, tafuta mtu aliye mkristo, aombe Pamoja na wewe katika sala fupi ya kumkaribisha Bwana Yesu maishani mwako, au wasaliana nasi kwa namba zilizopo chini ya somo, tutakusaidia kwa hilo.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

NUNUA MAJI YA UZIMA.

NUNUA MAJI YA UZIMA.

MFALME ANAKUJA.

OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

SWALI: Kwanini watu watakaohukumiwa siku ile ya mwisho, wanaonekana kutofautishwa katika sehemu mbili, wengine watatokea “baharini”, na wengine katika “mauti na kuzimu”. Kwanini iwe hivyo na tofauti ya maeneo hayo ni ipi?

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.

12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.

13 BAHARI IKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE; NA MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.

15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.


JIBU: Hukumu ya mwisho kabisa ni hukumu ijulikanayo kama “hukumu ya kiti cheupe cha enzi cha mwanakondoo”. Ni hukumu inayokamilisha wafu wote walioko makaburini, mbali na watakatifu.

Haitachagua wakubwa, wala wadogo, vijana au wazee. Waovu wote watafufuliwa wakati huu na kila mmoja atahukumiwa sawasawa na matendo  yake, kisha atatupwa katika lile ziwa la moto, aangamie huko milele.

Lakini biblia inatuonyesha siku hiyo waovu hao watatoka sehemu kuu mbili,

  1. ya kwanza, ni habarini,
  2. na ya pili ni Mauti na Kuzimu.

Kumbuka, lugha iliyotumika hapo ni lugha ya kinabii, na sio halisi kabisa kwamba bahari inayo wafu wake. Hapana.

Je Bahari ikawatoa wafu waliokuwa ndani yake, kunamaanisha nini?.

Tukianzana na wafu waliokuwa baharini. Tabia ya bahari sikuzote ni kubwa, haina mwisho, ukipotea humo, umepotea moja kwa moja. Na kibiblia maji mengi(bahari) inamaanisha ulimwengu.

Ufunuo 17:15 “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha”.

Hii ikiwa na maana sikuile ya mwisho, wafu wote, yaani waovu wa mataifa yote, wa lugha zote, waliokufa tangu Adamu, hadi wakati wa kurudi kwa Bwana Yesu kulinyakuwa kanisa lake (siku ya unyakuo). Wote hao watakuwa katika kundi la wafu watokao baharini. Watafufuliwa na kuhukumiwa.

Mauti na kuzimu kulifunua nini?

Lakini mara baada ya unyakuo kupita. Kuna tukio lingine litafuata, ambalo linajulikana kama dhiki kuu.

Kipindi  hichi kinajulikana kama kipindi cha utawala wa shetani(mpinga-kristo), watu wengi sana watauliwa, kutokana na dhiki ambayo Mungu ataruhusu shetani aisababishe, kwa waovu wote, watakaobakia duniani. (Tukiachia mbali wale ambao watakataa chapa ya mnyama). watauawa.

Ukisoma Ufunuo 6:8 inasema.

“Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda JINA LAKE NI MAUTI, NA KUZIMU AKAFUATANA NAYE. Nao wakapewa mamlaka juu ya robo ya nchi, waue kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni na kwa hayawani wa nchi”.

Umeona huyu farasi wa kijivujivu anaitwa mauti, akiambatana na kuzimu. Ambaye ni ibilisi akifanya kazi yake wakati huo. Naye atasababisha vifo vya robo ya watu waliopo duniani wakati huo. Kwamfano kwa dunia ya sasa ni Zaidi ya watu BILIONI 2, watauawa, na hiyo itakuwa ni katika mapigo ya ghadhabu ya Mungu, na vita vya Harmagedoni, na magonjwa, na wote hawa watakaokufa  moja kwa moja watakuwa chini ya “Mauti na kuzimu”.

Sasa biblia inaposema Mauti na Kuzimu ikatoa wafu wake, umeshaelewa kuwa ni wafu waliokufa katika hichi kipindi cha Dhiki kuu, ambao kimsingi walikuwa chini ya mpanda farasi wanne, aliyeitwa mauti na kuzimu.

Sasa kwanini sehemu zote mbili zitajwe?

Ni kuonyesha kuwa hukumu hiyo haitambakisha mfu hata mmoja. Itakuwa ni hukumu ya ulimwengu mzima kwa wale ambao hawakunyakuliwa, Au kuikataa cha ya mnyama.

Ikiwa leo hii umekufa kama mlevi, au fisadi, au kihaba, utakapokufa utakwenda katika Habari la kiroho. Lakini ikiwa utakufa katika dhiki kuu, vilevile utakwenda katika katika mauti na kuzimu. Na wote siku ya mwisho mtafufuliwa. Na kuhukumiwa, kila mmoja kwa kipimo chake. Kisha mtatupwa katika ziwa la moto.

Ndugu, hukumu ya Mungu ni ya kuiogopa sana, kwasababu hakuna nafasi ya pili baada ya kifo. Ukifa leo ghafla, ni moja kwa moja jehanamu ukisubiria siku hiyo ya ufufuo ifike, Kwanini hayo yote yatukute? Watu walio kuzimu leo hii Ni kilio na majuto ndivyo vinavyoendelea, wanatamani wangepata hata dakika 2 za kutubu lakini hawana. Wewe muda unao. Lakini unafurahia ulimwengu.

Mgeukie Kristo, leo akusamehe dhambi zako. Tubu kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu na tamaa zake zote. Dhamiria kumfuata Yesu, naye atakuokoa, katika dakika hizi za majeruhi. Kumbuka Unyakuo ni wakati wowote, hilo linafahamika. Muda umeisha, dalili zote zimeshatimia. Mlango wa neema kwa mataifa hivi karibuni utafungwa.

Bwana atusaidie.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.

MPINGA-KRISTO

UTAWALA WA MIAKA 1000.

JE MGOGORO WA URUSI NA UKRAINE,UMETABIRIWA KIBIBLIA?

Rudi nyumbani

Print this post