Ni mlima gani Yule Mwanamke Msamaria aliokuwa anaumaanisha? (Yohana 4:19)

Ni mlima gani Yule Mwanamke Msamaria aliokuwa anaumaanisha? (Yohana 4:19)

Jibu: Tusome,

Yohana 4:19 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

20 BABA ZETU WALIABUDU KATIKA MLIMA HUU, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia”.

Mlima Mwanamke Msamaria aliokuwa anaumaanisha ni MLIMA GERIZIMU.

Katika Mji wa Samaria kulikuwa na milima mikuu miwili mikubwa iliyokuwa inaangaliana, ambapo katikati ya milima hiyo kulikuwa na bonde.. Na milima hiyo ndio Mlima Gerizimu, na Mlima Ebali.

Mwanzo wa milima hii kutajwa katika biblia, ilikuwa ni kipindi wana wa Israeli wanatoka Misri kuelekea Kaanani, ambapo Mungu alimpa Musa maagizo na kumwambia atakapovuka mto Yordani, Nusu ya kabila ya Israeli (Yaani kabila 6) wapande juu ya mlima Gerizimu, kwaajili ya kuitikia Baraka na nusu nyingine iliyobakia (yaani kabila 6), zipande juu ya mlima Ebali kwaajili ya kuitikia laana.

Na katikati ya milima hiyo miwili, (yaani katika lile bonde lililokuwepo katikati) makuhali walisimama na kusoma Baraka na Laana kama zilivyoandikwa katika Torati ya Musa.. Ziliposomwa laana wale waliokuwa juu ya Mlima Ebali waliitika kwa sauti, AMEN!.. Na ziliposomwa baraka wale waliokuwa juu ya mlima Gerizimu waliitika AMEN kwa sauti!

Kumbukumbu 27:11 “Musa akawaagiza wale watu siku iyo hiyo, akasema,

12 Hawa na wasimame juu ya MLIMA WA GERIZIMU kwa kuwabarikia watu, mkiisha vuka Yordani; Simeoni, na Lawi, na Yuda, na Isakari, na Yusufu, na Benyamini;

13 na hawa na wasimame juu ya mlima wa Ebali kwa laana; Reubeni, na Gadi, na Asheri, na Zabuloni, na Dani, na Naftali.

14 Kisha Walawi na wajibu, wawaambie watu wote wa Israeli kwa sauti kuu,

15 Na alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. Na watu wote wajibu, waseme, Amina.

16 Na alaaniwe amdharauye baba yake au mama yake. Na watu wote waseme, Amina.

17 Na alaaniwe aondoaye mpaka wa jirani yake. Na watu wote waseme, Amina”.

Unaweza kulisoma jambo hilo hilo tena katika kile kitabu cha Yoshua 8:33-34

Hivyo mlima Gerizimu, ukajulikana na Wasamaria kama mlima wa Baraka, na Ebali Mlima wa laana.

Kumbukumbu 11: 29 “Tena itakuwa, atakapokuleta Bwana, Mungu wako, na kukutia katika nchi uendeayo kuimiliki, ndipo uiweke baraka juu ya mlima wa Gerizimu, na laana uiweke juu ya mlima wa Ebali”.

Kwa maelezo marefu kuhusu milima hii na ujumbe iliyoubeba katika roho unaweza kufungua hapa >>> MLIMA GERIZIMU NA EBALI

Kwahiyo Wasamaria wakaamini huo mlima GERIZIMU ndio MLIMA WA MUNGU, ambao Bwana ataliweka jina lake, jambo ambalo linapishana na Imani ya kiyahudi, inayoamini kuwa mlima wa Bwana ni MLIMA MORIA ulipo Yerusalemu, mahali pale Ibrahimu alipotaka kumtoa sadaka mwanawe, na ndipo Mfalme Daudi alipomwona Yule malaika wa uharibifu, na ndipo ambapo mwanae Sulemani alikuja kutengeneza Hekalu la Mungu.

Kwahiyo huyu mwanamke Msamaria alipokutana na Bwana Yesu kisimani, alijaribu kumweleza kuwa wao (yaani Bwana Yesu na wayahudi wengine) wanaamini kuwa sehemu ya kuabudia ni katika ule mlima Moria kule Yerusalemu, pale palipojengwa hekalu… Na wakati wao Wasamaria wanaamini ni katika mlima Gerizimu ambapo Mungu alipaagiza kuwa watu Wabarikiwe.

Lakini katika hayo yote tunaona jibu la Bwana Yesu lilikuwaje..

Yohana 4:20 “Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.

21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo HAMTAMWABUDU BABA KATIKA MLIMA HUU, WALA KULE YERUSALEMU.

22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23 LAKINI SAA INAKUJA, NAYO SASA IPO, AMBAYO WAABUDUO HALISI WATAMWABUDU BABA KATIKA ROHO NA KWELI. KWA MAANA BABA AWATAFUTA WATU KAMA HAO WAMWABUDU”.

Ikimaanisha kuwa Mungu haabudiwi tena katika vilele vya milima ya damu na nyama.. bali katika vilele vya milima ya Roho zetu.

Tunapomwamini Yesu, na kujazwa Roho wake Mtakatifu.. na kuifahamu kweli hiyo..Basi tunapokwenda kumfanyia Mungu ibada, tunakuwa tunamwabudu katika Roho na Kweli.

Je na wewe leo unamwabudu Baba katika roho na kweli?.. au katika Uzuri wa Kanisa lako na Mapokeo yako?.. au katika dini yako na dhehebu lako?..

Kumbuka maandiko yanasema wale wote wasio na Roho wake hao sio wake (Warumi 8:9), na hakusema wale wote wasio na dhehebu, au dini ndio sio wake..

Swali ni je!, unaye umempata huyo Roho?..Kama bado basi ni rahisi sana kumpata kama unamhitaji katika maisha yako, kwasababu yeye ndio muhuri wa Mungu kwetu.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.

40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.

Marana atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

Wasamaria walikuwa ni watu gani?

KATIKA MLIMA WA BWANA ITAPATIKANA.

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Bundala jumanne ramadhan
Bundala jumanne ramadhan
1 year ago

Namebarikiwa na mafundisho haya.

Aggrey Nyarigoti
Aggrey Nyarigoti
1 year ago

Nimebalikiwa sana naningependa kuendelea kusoma