Wasamaria walikuwa ni watu gani?

Wasamaria walikuwa ni watu gani?

Baada ya Israeli kuondolewa na Waashuru kutoka katika nchi yao, Mfalme wa Ashuru aliwaleta watu wengine, wakakae katika nchi hiyo,waliyoondolewa.. ili kwamba nchi hiyo , isibakie mapori.

Watu hao walioletwa kukaa katika nchi ya Israeli, hawakuwa Wayahudi bali walikuwa ni wapagani, wanaoabudu miungu yao.
Na walipoletwa walienda kukaa mahali pajulikanapo kama Samaria, huku wakiwa bado na miungu yao.

Lakini maandiko yanasema walipofika katika nchi takatifu, walisumbuliwa sana na simba (simba walikuwa wanaua watu sana).

Mpaka Mfalme wa Ashuru alipotuma kuhani mmoja wa kiyahudi kwenda kuwafundisha desturi za hiyo nchi..kwamba ni nchi takatifu hivyo hawana budi kuishi kulingana na kanuni za Mungu wa Israeli na si kulingana na kanuni za miungu yao.
Hivyo walupopelekewa Kuhani walivipokea vitabu vitano tu vya Musa, pamoja na kitabu cha Yoshua, lakini vitabu vingine vilivyosalia vya manabii hawakuviamini wala kuvipokea.

Hivyo wakawa ni jamii ya watu wanaozishika sheria za Mungu wa Israeli nusu..na nusu wanaitumikia miungu yao.

2 Wafalme 17:24
“Naye mfalme wa Ashuru akaleta watu kutoka Babeli, na Kutha, na Ava, na Hamathi, na Sefarvaimu, akawaweka katika miji ya Samaria badala ya wana wa Israeli; wakaumiliki Samaria, wakakaa katika miji yake.

25 Basi ikawa, wakati ule walipoanza kukaa huko, hawakumcha BWANA; kwa hiyo BWANA akapeleka simba kati yao, nao wakawaua baadhi yao.

26 Kwa hiyo wakamwambia mfalme wa Ashuru, wakasema, Wale wa mataifa uliowahamisha, na kuwaweka katika MIJI YA SAMARIA, hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi; kwa hiyo amepeleka simba kati yao, na tazama, wanawaua, kwa sababu hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi.

27 Ndipo mfalme wa Ashuru akatoa amri, akasema, Mpelekeni mmojawapo wa makuhani, mliowachukua kutoka huko; aende akakae huko, akawafundishe kawaida ya Mungu wa nchi.

28 Basi mmoja wa makuhani waliochukuliwa kutoka Samaria akaenda akakaa katika Betheli, akawafundisha jinsi ilivyowapasa kumcha BWANA.

29 Lakini pamoja na hayo watu wa kila taifa wakajifanyia miungu yao wenyewe, wakaiweka katika nyumba za mahali pa juu, walipopafanya Wasamaria, kila taifa katika miji yao walimokaa.

30 Watu wa Babeli wakafanya Sukoth-benothi kuwa mungu wao, watu wa Kutha wakafanya Nergali, watu wa Hamathi wakafanya Ashima,

31 Waavi wakafanya Nibhazi na Tartaki; nao Wasefarvi wakawaunguza wana wao katika moto kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.

32 Basi hivyo wakamcha BWANA, nao wakijifanyia wengine wao kuwa makuhani wa mahali pa juu, ambao waliwafanyia dhabihu katika nyumba za mahali pa juu.

33 WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA miungu YAO WENYEWE, sawasawa na kawaida za mataifa ambao wao walihamishwa kutoka kwao.

34 Hata siku hii ya leo hufanya sawasawa na kawaida za kwanza; wala hawamwogopi BWANA, wala hawazifuati sheria zao, wala hukumu zao, wala ile torati, wala ile amri BWANA aliyowaamuru wana wa Yakobo, ambaye alimpa jina la Israeli”

Umeona hapo, mstari wa 33..maandiko yanasema wakamca Bwana na kuitumikia miungu yao wenyewe..

Yaani walifanya mambo mawili kwa wakati mmoja..

Kwa tabia hiyo basi wayahudi ambao walikuwa wanaishika sheria ya Mungu wa Israeli kwa ukamilifu wote,..wakawa hawachangamani na hawa Wasamaria.

Mpaka wakati wa kuja kwa Bwana, Wayahudi walikuwa bado hawachangamani na Wasamaria (Yohana 4:9).

Lakini Bwana Yesu alipokuja, alikiondoa hicho kiambaza cha kati,

Hata mahali pa kuabudia pakawa si tena Yerusalemu katika mlima Moria (katika hekalu la Sulemani) wala si Samaria katika mlima Gerizimu, ambao Wasamaria ndio waliamini mahali oanapowapasa wao kuabudia..bali pakawa ni KATIKA ROHO NA KWELI.. Hapo ndipo mlimani pa Bwana alipopachagua.

Yohana 4:21 “Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, AMBAYO WAABUDUO HALISI WATAMWABUDU BABA KATIKA ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.

Je na wewe leo unamwabudu Baba katika Roho na Kweli? Yaani katika Roho Mtakatifu na katika Neno lake?

Kama bado mpokee leo Kristo, na ukabatizwe ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu, upate ondoleo la dhambi na upokee kipawa cha Roho Mtakatifu.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MSAMARIA MWEMA.

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments