MSAMARIA MWEMA.

MSAMARIA MWEMA.

Msamaria mwema ni mtu wa nanma gani?


Ni kauli ambayo tunaisikia katika jamii yetu mara kwa mara. Na hiyo inatokea pale mtu mfano amekumbana na matatizo au shida Fulani halafu akakutana na mtu asiyemfahamu kisha akamsaidia kutatua tatizo hilo. Sasa mtu kama huyo baadaye akija kuulizwa ilikuwaje ukafanikiwa au ukafanikisha kitu kile katika yale mazingira? ..Ndio hapo utamsikia anasema nilikutana na msamaria mwema akanisaidia…

Lakini baadhi ya watu hawajui chanzo cha msamaria mwema ni nini?..

Habari yake tunaipata kutoka katika biblia, tusome,

Luka 10:25  “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?

26  Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?

27  Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.

28  Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.

29  Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?

30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.

31  Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.

32  Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.

33  Lakini, MSAMARIA MMOJA katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,

34  akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.

35  Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.

36  Waonaje wewe, katika hao watatu, ni yupi aliyekuwa jirani yake yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?

37  Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.

Ni yapi tunajifunza katika Habari ya msamaria mwema?

  • Ili na wewe ufanyike msamaria mema, ni sharti uwe moyo wa huruma.
  • Ni sharti, uwe mwepesi kumsaidia mtu, ambaye hata haonyeshi dalili ya kuomba msaada kwako, lakini unajua kabisa yupo katika hali ya kuhitaji msaada.
  • Upo tayari kutoa hata mali zako, au vitu vyako vya thamani kwa ajili ya kumsaidia tu mtu

Sasa ukizingatia hayo, Basi mbele za Mungu utakuwa umekidhi vigezo vya kumpenda jirani yako kama nafsi yako.. Hapo utakuwa umeshida amri ya pili iliyo kuu kuliko zote, kama yule msamaria mwema.

Kumbuka  tendo hilo lina thawabu kubwa sana mbele za Mungu.

Hivyo ni wajibu wetu sote, kulikumbuka hilo wakati wote tunapoishi humu duniani, ili na sisi Mungu atuhurumie siku ile tuurithi uzima wa milele..

Mada Nyinginezo:

JIRANI YANGU NI NANI?

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
ROLANDY
ROLANDY
1 year ago

nini maana ya
1 kuposwa
2 dada poa