Jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, Nakukaribisha katika kuyachunguze maandiko nilipokuwa ninautafakari huu mstari, picha iliyojitengeneza moja kwa moja katika kichwani kwangu ni sawa mtu mwenye Hoteli maarufu ya 5 STAR Dubai, ambayo kifungua kinywa chake tu asubuhi gharama zake ni sh laki 3, mbali na gharama za chakula cha mchana na jioni, na zile za kulala..halafu leo hii unamwona anajitokeza hadharani anawakaribisha watu wote waje kula na kunywa katika hoteli ile bure, pasipo gharama yoyote…
Na cha kushangaza zaidi anatoa kauli hii “njoo UNUNUE bure”, hakwambii njoo nikupe bure, hapana bali anasema njoo “UNUNUE” bure, hii ikiwa na maana,utakapofika pale utaandikiwa risiti ya ununuzi kama tu vile mtu aliyelipia gharama zote, na hiyo inakupa uhalali wa kuhudumiwa kwa viwango vile vile bila upendeleo sawa tu na mtu Yule ambaye ametoa pesa yote mfukoni.