Wahiti ni watu gani?

Wahiti ni watu gani?

Wahiti ni watu gani, na wa Taifa gani kwa sasa?

Biblia haijaeleza kwa urefu, Habari ya Wahiti, lakini kulingana na maandiko, walikuwa ni watu Hodari na waliotawala sehemu ya nchi ya Israeli, katika upande wa kaskazini. Kumbuka Nchi ya Israeli hapo kwanza ilikuwa inakaliwa na watu wa mataifa, ambao ndio hao Wahiti, wengine ni Wayebusi, Wahivi, waperizi na Wakaanani.

Kulingana na historia, Wahiti, hawakumiliki tu sehemu ya nchi ya Israeli, enzi za zamani, bali pia historia inaonyesha walimiliki sehemu ya nchi ya Syria kwa sasa na mashariki mwa nchi ya Uturuki, ambayo zamani ilijulikana kama Asia ndogo.

Wahiti hawakuwa watu waliomwabudu Mungu wa Israeli, bali walikuwa wanaabudu miungu na walikuwa wanaishi katika desturi za kipagani; Na katika biblia kipindi cha Ibrahimu na Isaka, Wahiti walikuwepo tayari katika nchi ile, wanamiliki sehemu ya ardhi, ndio maana utaona Esau mwana wa Isaka alikwenda kujitwalia wake kutoka kwa hawa Wahiti.

Mwanzo 26:34 “Esau alipokuwa mwenye miaka arobaini, akamwoa Yudithi, binti Beeri, MHITI, na Basemathi, binti Eloni, Mhiti.

35 Roho zao Isaka na Rebeka zikajaa uchungu kwa ajili yao”.

Wahiti Pamoja na kwamba waliondolewa katika nchi ya Israeli, wakati waisraeli wanaingia katika nchi hiyo ya ahadi, lakini bado waliendelea kuwepo na kumiliki sehemu nyingine za dunia, na ndio maana utaona wakitajwa hata baada ya wana wa Israeli kurudi kutoka katika uhamisho wa Babeli.

Ezra 9:1 “Na mambo hayo yalipokwisha kutendeka, wakuu wakanikaribia, wakisema, Watu wa Israeli, na makuhani, na Walawi, hawakujitenga na watu wa nchi hizi, wamefanya sawasawa na machukizo yao, yaani, ya Wakanaani, na WAHITI, na Waperizi, na Wayebusi, na Waamoni, na Wamoabi, na Wamisri, na Waamori.

2 Maana wametwaa binti zao kuwa wake zao, na wake za watoto wao; basi mbegu takatifu wamejichanganya na watu wa nchi hizi; naam, mkono wa wakuu na mashehe umetangulia katika kosa hili”.

Wahiti waliondolewa katika nchi ya ahadi na Mungu, kwasababu ya matendo yao ya kipagani, ambayo yalikuwa kinyume na mapenzi ya Mungu.

Kumbukumbu 9:4 “Usiseme moyoni mwako, Bwana, Mungu wako, atakapokwisha kuwasukumia nje mbele yako, ukasema, Ni kwa haki yangu alivyonitia Bwana niimiliki nchi hii; KWANI NI KWA AJILI YA UOVU WA MATAIFA HAYA BWANA AWAFUKUZA NJE MBELE YAKO.

5 Si kwa haki yako, wala kwa unyofu wa moyo wako, hivi uingiavyo kuimiliki nchi yao; LAKINI NI KWA UOVU WA MATAIFA HAYA BWANA, MUNGU WAKO, AWAFUKUZA NJE MBELE YAKO; tena apate kuliweka imara hilo neno Bwana alilowaapia baba zako Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo”.

Wahiti, waliendelea kuwepo miaka mingi, lakini nyakati za agano jipya hatuwaoni wakitajwa tena, ni wazi kuwa jamii hiyo ya watu ilipotea kabisa, mpaka leo hakuna jamii ya Wahiti duniani, kama vile walivyo Israeli.

Ikifunua kuwa wote wasiomcha Mungu, watapotea lakini wote wamtumainio Bwana watadumu milele.

Zaburi 125:5 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.

2 Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele”.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

SOMO no.02 (BINTI WA YEFTHA).

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Peter Mgaza
Peter Mgaza
1 year ago

Amen mtumishi ubarikiwe

Lucas mhula
Lucas mhula
1 year ago

Amen🙏🙏

Danieli
Danieli
1 year ago

Amina nashukuru kwa somo nzuri Mungu awabariki