Je vazi alilovikwa Bwana Yesu lilikuwa la Zambarau au Jekundu?

Je vazi alilovikwa Bwana Yesu lilikuwa la Zambarau au Jekundu?

Swali: Tunasoma katika Marko 15:17,na Yohana 19:2  kuwa Bwana alivikwa Vazi la rangi ya Zambarau, lakini tukirudi kwenye Mathayo 27:28 tunaona ni vazi Jekundu, Sasa vazi lipi ni sahihi hapo?.

Jibu: Tusome,

Marko 15:16 “Nao askari wakamchukua ndani ya behewa, ndiyo Praitorio (yaani, nyumba ya uliwali), wakakusanya pamoja kikosi kizima.

17 Wakamvika VAZI LA RANGI YA ZAMBARAU, wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani;

18 wakaanza kumsalimu, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”.

Tusome tena..

Mathayo 27:27 “Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima.

28 WAKAMVUA NGUO, WAKAMVIKA VAZI JEKUNDU.

29 Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!”

Sasa kwa mistari hii miwili ni rahisi kusema kuwa biblia inajichangaya.. lakini biblia kamwe haijichanganyi, kinachojichanganya ni fahamu zetu.

Sasa tukirudi kwenye hiyo mistari ni kwamba zamani mavazi waliyokuwa wanavaa watu wenye heshima, au mamlaka Fulani, yalikuwa ni ya rangi ya zambarau iliyochanganyikana na rangi nyekundu. Sehemu kubwa ilikuwa ni rangi ya Zambarau na sehemu ndogo ni nyekundu. Hivyo mtu atakayelitaja kama vazi la Zambarau au kama vazi jekundu, anakuwa hajakosea..

Kwa mfano unaweza kusoma…

Ufunuo 17:4 “Na mwanamke yule alikuwa AMEVIKWA NGUO YA RANGI YA ZAMBARAU, NA NYEKUNDU, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake”.

Pia unaweza kusoma Ufunuo 18:16, Luka 16:19.

Kwahiyo Marko na Mathayo…wote walikuwa sahihi..isipokuwa kila mmoja kaelezea rangi, iliyokuja ya kwanza kichwani mwake.

Lakini Zaidi sana tunachoweza kujiuliza ni kwanini Bwana wamvike vazi lile la Zambarau na nyekundu? Na si la rangi nyingine?.. Jibu ni kama tulivyojifunza hapo juu kuwa mavazi hayo yalivaliwa na watu wenye cheo au wafalme au mamalkia.. Kwahiyo walipomvika vazi hilo lengo lake ni ili wamdhihaki “mfalme wa wayahudi”..kwahiyo ni vazi kama la kumdhihaki ndio maana wakamvika na taji ya miiba, kwasababu watu wanaovaa mavazi kama hayo wanakuwa pia na taji za utukufu!.. Lakini Bwana Yesu walimvika Taji ya miiba.

Sasa kwa urefu juu ya Taji ya miiba, unaweza kufungua hapa >> Taji ya Miiba.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

AKAJIFUNGA VAZI LAKE, AKAJITUPA BAHARINI.

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments