Nyakati za kuburudishwa ni zipi? (Matendo 3:19).

Nyakati za kuburudishwa ni zipi? (Matendo 3:19).

Nyakati za kuburudishwa ni kile kipindi cha utawala wa miaka elfu moja.

Kipindi hicho ni kipindi ambacho dunia itarejeshwa na kuwa kuwa nzuri zaidi hata ya Edeni, ni kipindi ambacho tutatawala na Kristo kama wafalme baada ya kuonekana wadhaifu nyakati nyingi, ni kipindi ambacho tutaishi kama malaika wasioumwa wala wasiozeeka wala kufa.

Hicho kitakuwa ni kipindi cha kufutwa machozi kwa wateule, na kipindi cha kutawala pamoja na Kristo (kwa ufupi kitakuwa ni kipindi cha kuburudika).

Matendo 3:18 “Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo.

19 Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, ZIPATE KUJA NYAKATI ZA KUBURUDISHWA;

20 apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani;

21 ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu”.

Umeona?..Kristo sasahivi yupo juu mbinguni, lakini atakuja tena kutoka huko aje aifanye dunia kuwa kama Edeni na hata zaidi ya pale, na kuwaburudisha wato wote waliojikana nafsi sasa, wanaochekwa sasa kwaajili ya jina lake, walioua kuacha uzinzi, ulevi, uvaaji mbaya, utukanaji n.k kwaajili ya jina lake.

Na nyakati hizo zimekaribia sana, kinachosubiriwa ni kondoo wa mwisho kuingia ndani ya zizi, ili majira hayo yaanze.

Lakini swali jepesi ni je!.. Umempokea Yesu leo?..je utakuwepo katika hiyo miaka ya kuburudishwa au utakuwepo katikamahali pa mateso majira hayo yatakapoanza?.

Ni heri ukatubu leo, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu kama bado hujatubu wala kubatizwa ubatizo sahihi wala kupokea Roho.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:

Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Nini maana ya Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu;?

Nini maana ya Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu&?

NJIA MOJAWAPO YA KUPATA MSAADA KUTOKA KWA BWANA.

Rudi nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JOSIAH LLOYD MURUVE
JOSIAH LLOYD MURUVE
1 year ago

Mungu awabariki kwa kazi hii mnayoitenda