Ni kwa jinsi gani Mungu anapatiliza maovu ya baba zetu sawasawa na Kutoka 20:5-6?

Ni kwa jinsi gani Mungu anapatiliza maovu ya baba zetu sawasawa na Kutoka 20:5-6?

SWALI:Kule katika kitabu cha KUTOKA 20:5-6.Mungu alisema”NAWAPATILIZA WANA MAOVU YA BABA ZAO.. Sasa hivi Baba wa Fulani akimwiba mke wa jirani yake na kumwua..Mungu Atawapatiliza adhabu hao watoto wa baba Fulani Kwa huo wizi na uuaji wake?? Shalom.


JIBU: Ukisoma mistari yote inasema hivi 

Kutoka 20:4“Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia”.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, HATA KIZAZI CHA TATU NA CHA NNE CHA WANICHUKIAO,

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.

Mwishoni mwa mstari wa 5 inasema hata kizazi cha tatu na cha nne cha “wanichukiao”. Kumbe cha hao wamchukiao, na sio cha wampendao, kama baba yako alikuwa ni mwovu anaabudu sanamu, halafu na wewe mtoto kwa kulijua hilo unafanya yale yale ambayo baba yako alikuwa anayafanya, hapo laana ya baba yako pamoja na yako mwenyewe itakupata…

Na ndivyo ilivyokuwa kwa wana wa Israeli, enzi zile za wafalme, jambo kuu lililowafanya wachukuliwe utumwani, kupelekwa Ashuru na Babeli ni kutokana na kuwa walikuwa hawampendi Mungu, Kwani baada ya kuona Baba zao na wafalme wao wanatenda maovu wanasimamisha maashera na kuabudu miungu mingine, wao badala ya kutubu wakayaiga yale yale waliyokuwa wanayafanya, hivyo Mungu alikasirika akayaketa maovu ya Baba zao wote yakawapata hao, mpaka walipotawanywa katika mataifa yote..

 Lakini pia ukisoma mstari wa 6 anasema “nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”. Ikiwa na maana kuwa hata kama Baba zako walikuwa ni waovu vipi, Hivyo Mungu akakusudia kuulaani uzao wao wote, ikatokea wewe (mtoto) anampenda Mungu na kumcha, basi rehema zake zinakuwa juu yake, kana kwamba hujazaliwa katika kizazi chenye laana. Hapo linatimia hili neno.

Ezekieli 18: 20 “Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake”.

Ubarikiwe.


SIKU ZA MAPATILIZO.

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA.

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

UNYAKUO.

LILE TUMAINI LILILO NDANI YETU LINAPOULIZIWA.

JE! VIUMBE VINATAZAMIAJE KWA SHAUKU KUFUNULIWA KWA MWANA WA MUNGU?


Rudi Nyumbani:

 

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Sumamwakalukwa
Sumamwakalukwa
2 years ago

Amina Asante tunabarikiwa sana