Ezekieli 13:6-11 “ Wameona ubatili, na uganga wa uongo, hao wasemao, Bwana asema; lakini Bwana hakuwatuma; nao wamewatumainisha watu ya kuwa neno lile litatimizwa.
7 Je! Hamkuona maono ya bure, hamkunena mabashiri ya uongo? Nanyi mwasema, Bwana asema; ila mimi sikusema neno.
8 Basi tazama, Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu mmenena ubatili, na kuona uongo, basi, kwa sababu hiyo, mimi ni juu yenu, asema Bwana MUNGU.
9 Na mkono wangu utakuwa juu ya MANABII WANAOONA UBATILI, na KUTABIRI UONGO; hawatakuwa katika mashauri ya watu wangu, wala hawataandikwa katika maandiko ya nyumba ya Israeli, wala hawataingia katika nchi ya Israeli; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU.
10 Kwa sababu hiyo, KWA SABABU WAMESHAWISHI WATU WANGU, WAKISEMA, AMANI; WALA HAPANA AMANI; na mtu mmoja ajengapo ukuta, tazama, waupaka chokaa isiyokorogwa vema;
11 basi waambie hao wanaoupaka ukuta chokaa isiyokorogwa vema, ya kwamba utaanguka; kutakuwa mvua ya kufurika;”