SIKU ZA MAPATILIZO.

SIKU ZA MAPATILIZO.

Zamani ilikuwa watu wakihadithiwa habari za siku za mwisho, walikuwa wanatetemeka na machozi yakiwatoka, lakini sasahivi Watu wanapuuzia, watu hawana hofu tena wakidhani kuwa yale mapigo yaliyoandikwa katika kitabu cha ufunuo ni kama hadithi ambazo hazitakuja kutokea duniani siku za hivi karibuni, wanaona kama mambo yale hayatauhusu sisi kabisa,ni ya watu wa vizazi vingine vya mbeleni sana vitakavyokuja, hivyo hawana haja ya kuyafuatilia sana, wengine wanayachukulia kiwepesi wepesi, wengine wanafanyia mizaha pale biblia inaposema siku hiyo watu wote, wakiwemo wafalme, majemedari, wakuu wa nchi, matajiri, watumwa, watu wa kila namna watakapojificha chini ya mapango na miamba na kuiomba iwaangukie ili tu wajisitiri na hiyo hasira kali ya mwana-kondoo ambayo inakwenda kumwaga juu yao (Ufunuo 6:12).

Hicho sio kipindi cha kukitamani kabisa, na ndio maana Bwana anatupa tahadhari mapema, akituonya tangu zamani tusitamani kuwepo huko, kwasababu pindi utakapojikuta tu umeingia katika hasira kali ya mwana-kondoo, huko ujue neema ya Kristo ilishaondoka siku nyingi. Mungu ni Mungu wa kisasi, biblia inasema kile apandacho mtu ndicho atakachovuna. Sasa siku hizo ndizo Bwana alizozitenga KUPATILIZA maovu ya ulimwengu wote. Ni kipindi maalumu ambacho Bwana amekiandaa kwa wale ambao wanaukataa wokovu sasa hivi na wanaoipinga kweli. Kwa watu wote wanaofanya maovu sasa hivi kwa siri, wakidhani kuwa Mungu hawaoni. Wakati wa Nuhu Mungu aliwapatiliza watu wa kipindi kile kwa adhabu moja yaani gharika, watu wa Sodoma kwa adhabu moja yaani moto, lakini watu tunaoisha sasahivi ambao tumeshaona mifano yote hiyo lakini hatutaki kutubu biblia inasema, kizazi hiki kimeandaliwa, dhiki, mapigo, pamoja na moto.

Hii ikiwa na maana kabla ya watu kuteketezwa kabisa ni lazima Bwana kwanza APATILIZE maovu yao yote waliyoyatenda, siku zote za maisha yao walizoishi hapa duniani, kwa dhiki na kwa mapigo ya vile vitasa 7 kisha waangamizwe halafu baada ya hapo kitakachofuata ni kutupwa katika lile ziwa la moto.

Ni lazima kwanza Bwana alipe kisasi kwa maovu yote yanayoendelea duniani sasa hivi. Siku hizo za kutisha Bwana Yesu aliziita siku za mapatilizo, alipokuwa pale katika milima ya Mizeituni akiwaleza wanafunzi wake mambo yatakayotokea katika siku za mwisho.

Luka 21:22 “Kwa kuwa siku hizo ndizo za mapatilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa.”.

Unaona? Yote yaliyoandikwa ni lazima yatimie, kisasi Bwana alichosema atalipa ni lazima kije tu, maovu yanayoendelea sasa hivi duniani, mauaji, ubakaji, uabuduji sanamu, uchawi, uzinzi, n.k. yote Bwana ni lazima ayapatilize kabla ule mwisho haujafika.

Ezekieli 7: 5 “Bwana MUNGU asema hivi; Ni jambo baya, JAMBO BAYA LA NAMNA YA PEKE YAKE; ANGALIA, LINAKUJA.

6 Mwisho umekuja, mwisho huu umekuja; unaamka ukupate; angalia, unakuja.

7 Ajali yako imekujia, wewe ukaaye katika nchi hii; majira yamewadia, siku ile inakaribia; siku ya fujo, wala si ya shangwe milimani.

8 BASI HIVI KARIBU NITAMWAGA GHADHABU YANGU JUU YAKO, nitazitimiza hasira zangu juu yako, nami nitakuhukumu sawasawa na njia zako; NAMI NITAKUPATILIZA MACHUKIZO YAKO YOTE.

9 Jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma; nitakupatiliza njia zako na machukizo yako yote yatakuwa katikati yako; nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, napiga”.

Siku hizo Bwana anasema hakutakuwa na huruma, watu watalia na kujutia na kutubu lakini hakuna atakayesikia, mpaka ghadhabu ya Mungu ya mwisho itakapomalizwa kumwagwa duniani. Na Bwana anasema ni HIVI KARIBUNI. Wapo watu wanadhani mwisho bado siku nyingi. Ni jambo la kutisha sana kujikuta umebaki siku ile, kwasababu ni lazima Mungu apatilize uovu wote, kwa watu wote wanaokufuru leo, na kuutukana msalaba.

Waebrania 10:28 “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?

30 Maana twamjua yeye aliyesema, KUPATILIZA KISASI NI JUU YANGU, MIMI NITALIPA. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.

31 NI JAMBO LA KUTISHA KUANGUKA KATIKA MIKONO YA MUNGU ALIYE HAI.”

Ndugu kanisa tulilopo ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama LAODIKIA (Ufunuo 3 ). Na makanisa mengine 6 yalishapita, na hili tulilopo ndilo la 7 na la mwisho, kama hujui hilo basi jaribu kufuatilia utalifahamu hilo. Kanisa lile la sita lijulikanalo kama FILADELFIA, kutokana na kumpendeza Mungu kwao, Mungu aliliahidia kuliepusha na ILE SAA YA KUJARIBIWA iliyokuwa imewekwa tayari kuujilia ulimwengu mzima (Ufunuo 3:10). Hivyo hiyo saa ni lazima ije katika kanisa letu hili, la Laodikia. Ni siku za mapatilizo ya ouvu wote. Siku ambayo dunia itajaribiwa.

Siku hizo za hatari, hata manabii wote wa uongo, pamoja na yule mpinga-kristo, ambaye atatokea Taifa la RUMI, Kanisa Katoliki, kulingana na unabii wa kibiblia, na wachungaji wote wa uongo, na waalimu wote wa uongo, na wote wanaojiita watumishi wa Mungu ila wa uongo, Hukumu zao zote zitapatilizwa pia katika hicho kipindi.

Yeremia 23: 1 “Ole wao wachungaji, wanaoharibu kondoo za malisho yangu na kuwatawanya! Asema Bwana.

2 Kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, juu ya wachungaji wanaowalisha watu wangu, Mmetawanya kundi langu, na kuwafukuza, wala hamkwenda kuwatazama; ANGALIENI, NITAWAPATILIZA UOVU WA MATENDO YENU, ASEMA BWANA”.

Ezekieli 13:6-11 “ Wameona ubatili, na uganga wa uongo, hao wasemao, Bwana asema; lakini Bwana hakuwatuma; nao wamewatumainisha watu ya kuwa neno lile litatimizwa.

7 Je! Hamkuona maono ya bure, hamkunena mabashiri ya uongo? Nanyi mwasema, Bwana asema; ila mimi sikusema neno.

8 Basi tazama, Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu mmenena ubatili, na kuona uongo, basi, kwa sababu hiyo, mimi ni juu yenu, asema Bwana MUNGU.

9 Na mkono wangu utakuwa juu ya MANABII WANAOONA UBATILI, na KUTABIRI UONGO; hawatakuwa katika mashauri ya watu wangu, wala hawataandikwa katika maandiko ya nyumba ya Israeli, wala hawataingia katika nchi ya Israeli; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU.

10 Kwa sababu hiyo, KWA SABABU WAMESHAWISHI WATU WANGU, WAKISEMA, AMANI; WALA HAPANA AMANI; na mtu mmoja ajengapo ukuta, tazama, waupaka chokaa isiyokorogwa vema;

11 basi waambie hao wanaoupaka ukuta chokaa isiyokorogwa vema, ya kwamba utaanguka; kutakuwa mvua ya kufurika;”

Unaona hapo! Biblia inasema manabii hawa wa Uongo wanawashawishi watu wakiwaambia AMANI,kuna amani na wakati hakuna amani, ndugu yangu epuka injili za faraja, injili ambazo huambiwi madhara ya dhambi zako, wala madhara ya hukumu ya milele, wewe ni kutiwa moyo tu na maisha yako unayoishi hata kama ni machafu kiasi gani..

Siku hizo utawala mbovu wa Roma chini ya kanisa Katoliki lililohusika kuua watakatifu wa Mungu zaidi ya milioni 68, katika kipindi cha Giza, na kumwaga damu zisizo na hatia katika vipindi vyote vya kanisa, Bwana atalihukumu nalo pia, biblia inasema hivyo. Ndio yule Babeli mkuu, mama wa makahaba na machukizo ya nchi,anayezungumziwa katika kitabu cha ufunuo

sura ya 17. Mungu atapatiliza damu za watakatifu wake juu yao.

Ufunuo 19:1 “Baada ya hayo nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, sauti kubwa mbinguni, ikisema, Haleluya; wokovu na utukufu na nguvu zina BWANA MUNGU wetu.

2 kwa kuwa hukumu zake ni za kweli na za haki; maana amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uasherati wake, na KUIPATILIZA damu ya watumwa wake mkononi mwake.

Hivyo huu sio wakati wa kuzisubiria siku hizo, neema bado ipo

Yeremia 5: 7 “Nawezaje kukusamehe? Watoto wako wameniacha mimi, na kuapa kwa hao ambao si miungu; nilipokuwa nimewashibisha chakula, walizini, wakakutana wengi pamoja katika nyumba za makahaba.

8 Walikuwa kama farasi walioshiba wakati wa asubuhi; kila mmoja akalia kwa kutamani mke wa mwenzake.

9 Je! Nisiwapatilize kwa sababu ya mambo hayo? Asema Bwana; na nafsi yangu, je! Nisijilipize kisasi juuya taifa la namna hii?”

Biblia inasema “Tokeni kwake enyi watu wangu Ufunuo 18:4”..tutoke katika mambo ya ulimwengu huu, tujiepushe na kizazi kilichomkataa Bwana, tujiokoe nafsi zetu, maana siku ya Bwana inayowaka kama moto inakuja.

Mtume Petro baada ya kuwahubiria watu maneno ya uzima ya Yesu Kristo, walimwuliza wakisema

Matendo 2: 37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.

40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, JIOKOENI NA KIZAZI HIKI CHENYE UKAIDI.

41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.

42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali”.

Na wewe leo unayesikia maneno haya, Roho anakuonya vile vile, tubu leo ukabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo, kama hujafanya hivyo, upokee kipawa cha Roho Mtakatifu na ujiepushe na KIZAZI HIKI CHENYE UKAIDI.

Tafadhali “share” kwa wengine.Na Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

TUSIFUNGWE NIRA PAMOJA NA WASIOAMINI.

KWANINI TUWE WENYE BUSARA KAMA NYOKA?

DHAMBI YA ULIMWENGU.

NADHIRI


Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments